Tukumbushane maisha ya UDSM enzi hizo, wazee wa Bibo na Main Campus

Tukumbushane maisha ya UDSM enzi hizo, wazee wa Bibo na Main Campus

Maisha yalikuwa na stress Sana pale kitivoni( sheria) wahuni tulikuwa tuna jibalance kwa kununua kuponi za RB 600, nimekaa mabibo hostel miaka minne , bila kunji ninge disco, nawakumbuka Prof majamba alikuwa anatupeleka mno, videmu vya education tumepiga Sana uwanjani mabibo, corner bar,Riverside nk kuangalia epl hapo kighorofani, club le mambo sijui Bado ipo, unaenda club unarudi unakula tikiti nk kifupi udsm Ni sehemu nzuri
 
Hiki ndicho kipindi ambacho na mimi nilipita udsm! Boom 2500! Rais wa Daruso akiwa ni Mwita Mwikabwe (Mwita Waitara MB)!!

Kwa mara ya kwanza niliishi kwenye nyumba ya ghorofa na yenye madirisha ya aluminium pale Mabibo Hostel!!
Kuna mwita mwingine alikuwa na upara hivi alikuwa engineering kule alikuwa president wa Daruso achana na huyu mbunge jina limenitoka. Janki flani mtaratiibu.
 
Ni kweli jamaa alikuwa na nyota ya kupendwa lakini pia mshindani wake aliyewekwa alikuwa dhaifu na alipata ufadhili wa chama cha majambazi. Sasa hii iliwaongezea watu monkari wa kumpa Odong kura. Kipindi hiki mlimani ilikuwa sifa sana kujitambulisha kama mwanaharakati na aibu kubwa kujihusisha na serikali kwa namna yoyote ile.
Shida kubwa ya huyu ndugu Odong aliupenda sana uraisi wa DARUSO. Na kwa sababu hiyo vijana wa system wakamdanganya kwamba ili aungwe mkono na serikali achukue kadi ya UVCCM. Baada ya kumpa tu, usiku wakamvamia na kesho yake akawa deported! Wana tulipopewa taarifa kwamba jamaa alikamatwa na kadi ya UVCCM hakuna aliyeangaika naye. Hata hivyo serikali iliyochaguliwa haikudumu, ilipinduliwa na wazee wa DARUSO board wakaongoza kwa mwaka mzima. Ni furaha yangu kwamba tuliwatendea haki wanamapinduzi na familia ya wanafunzi wa Udsm kwa ujumla.

Alikuwa anajua kiswahili ?
 
Haabari wadau..!
Maisha ya UDSM enzi hizo yalikuwa powa sana sijajua kwa sasa.

Tuanzie wapi ,ngoja tuanze na Boom enzi hizo lilikuwa 4000/= kwa siku ila tulivyoingia chuo ikabidi tufanye mgomo Boom liongezwe watoto wa mama hawataelewa.

Maandamano yalianzia Revo Square sijuhi kama watoto wa leo wanaijua Revo Square watu wakatolewa lecture room wajoin movement watoto wa mama wakakimbia ila watoto wa mbwa tukaingia mtaani tulivyofika Mlimani City mabomu yalipigwa kama yote vile tukapoteana.

Kipindi hicho kuna wale wajamaa ndio wakuu wa vyuo wanajiita Tripple M yaani Mkandala,Mgaya na Maboko.

Mgomo ulipoisha chuo kizima tulirudishwa nyumbani kwa mda usiojulikana,baada ya kurudishwa tena sisi waanzilishi wa mgomo tukafukuzwa ila mm nikafanya harakati sikufukuzwa.

Mwaka wa kwanza nilipata room mabibo hostel pale maisha yalikuwa powa sana wale wa mwaka wa pili na kuendelea tukawa tunawabeba yaani kitanda chembamba mnalala wawili kana mpo lupango vile ,usiombe umbebe mtu mrefu.

Mwaka wa pili inabidi huwai chuo kabla akijafunguliwa ukatafute mtu wa kukubeba (kushare naye kitanda).

Ukiwa mwaka wa kwanza ni ngumu sana kupata demu wengi wanadharau mwaka wa kwanza,ila mwaka wa pili ndio mwaka wa kupata demu inabidi uliwahi konteana jipya (first year),asikwambie mtu hapa watoto wa mwaka wa kwanza wanamegeka kiurahini sana .

Boom likiingia safari za mlimani City ,Survey ,Ambiace n.k ila boom likikata tunaanza kupiga pasi ndefu kama hatuna akili nzuri hata lectures hazipandi kipindi hiki mademu wasio na msimamo wanaanza kujiuza ili wapate pesa za kujikimu,yaani kama una demu anaweza kukusaliti boom likikata.

Kipindi cha boom likikata wahuni tunaanza kugonga RB (Rice Beens) wali maharage ambao bei yake ilikuwa 600/=Boom likikata watu wanaanza kusifia wali mahatagr wa Cafe 1 na Coet ndio mtamu.Wazee wa bibo wanapiga tu shato pori mwendo wa kutembea kwa mguu toka main campus aibu washikaji wakikuona wanajua umefua.

Kuishi mabibo ni mateso hakukuwa na Kijazi Flyover foleni mtindo mmoja usishangae kutoka bibo mpk campus ukamaliza masaa zaidi ya matatu ubungo mataa.kukosa lecture au kuchelewa test kawaida kisa foleni ya ubungo mataa.
Duuuh, ilikuwa nona sana!!
 
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2011 mwezi wa pili kulikuwa na mgomo tulipigwa mabomo siji sahau nilijikuta nipo kwenye mtalu wa maji taka Ila Kuna miamba sokwe mtu na alishababu aka mabilika sijui wako wapi Hawa miamba na kadada flani ka Arusha jina nimekasahau
 
Back
Top Bottom