Tukutane hapa tuliowahi kutoa na kupewa talaka, tujadili maisha baada ya talaka

Ni kuuza tu kabla ya kufikia mahakamani😂😂😂 yani maji yanapozidi unga tu kimya kimya unautia mjengo gengeni.

Ukilianzisha tu tayari hela iko kibindoni. Huyo mshenzi akitegemea mgao inakula kwake. Unamseti vizuri tu kuwa una nyingine umeijenga goba unataka uimalizie kwa finishing kali. Akijaa tu unavuta mpunga wako safi na kumpanga mteja wako hana haraka mpaka utakapoimaliza kabisa ndipo unahama kakupa miezi 6 mbele.

Yani ikifikia stage ya mgao mnagawana subwoofer na Tv tu pamoja na microwave na jiko la gas.😂 Wanaume wenzangu tuwe smart jamani
 
Faida si kwa mke hapo maana analishwa na kugongwa nje huko hana baya
 
Mali unaziandika majina ya watoto tu haina jinsi😂😂😂 kama ishu ni hio.
 
Mzee tz hakuna Vita Ila majeshi yetu kutwa kucha yapo kwenye mazoezi ....alafu mwanaume Kama wewe unaishije Kama funza
 
Sasa hizi mathematical probability na mbususu tena wapi na wapi wewe.
However, i do concur with u concerning the fact that side was an inane young man that knew little or nothing about women.

Kuingia kwenye ndoa na attitude ya kuwa mwanamke ni binadamu na ana matamanio kama mie mwanaume na kwamba anaweza gegegedwa any time ni kuwa mwenye busara. Wee kula mbususu ikiwepo hapo pembeni yako usitake kujua mengi sana maana kwanza wake wenyewe hawa tunaoanbreki pumbuz.

Nawashangaa sana wanaume wanao sema kuwa eti mkeo akikukamata unacheat ukatae. Wee wala usikatae kubali kabisa ndio nimecheat. Kutegemea kuwa mwenza hatacheat ni kusema kuwa umeoa au kuolewa na malaika....which is not the case. Mwenza sio malaika ni binadamu mwenye mapungufu.

Wanawake wenyewe hawa wakibongo ukikubaki umeacheat sana sana watakuitia kikao cha familia. Na wanakujaga na expectation ya kwamba utakataa. Sasa wee wakikuuliza unases ndio nimecheat. Kitakachotokea hapo ni mke kuulizwa tuu vipi huduma unapata hapo nyumbani? Akijibu ndio ataambiwa mama rudi nyumbani mkalee watoto wenu🤣🤣🤣🤣🤣
 
Na yeye ameolewa au bado yupo kitaa
Ameshaolewa, ila alianza kwanza kuzalishwa nje ya ndoa then jamaa nd kamuoa, after two years akampa talaka lkn wakarejeana so wapo wte na watoto wa 2,na mm pia nmepata watoto wa 2.hatuna mawasliano japo wte tunatoka kijiji kimoja
 
Kaka kwa jinsi ulivyo elezea nahisi ulisoma HKL,,kuna msamiati umeutumia hapo nmekumbuka mbali "I do concur"
 
Ndoa ni tumbo kaka
 
Nakataa dhana y kwamba kila mwanandoa anachapiwa
 
Kaka kwa jinsi ulivyo elezea nahisi ulisoma HKL,,kuna msamiati umeutumia hapo nmekumbuka mbali "I do concur"
🤣🤣🤣 Hamna bwana mie ni mtu wa namba, it just so happens that i have a facility with words.
 
Ndoa ni hiyari iliyo halalishwa na Mungu.
Tena ndoa ni kiapo mbele za Mungu.
Binadamu tumekuwa na kawaida ya kuvunja,
-- ndoa zetu,
--Ndoa za ndugu zetu,
--Ndoa za marafiki na jamaa zetu bila kujali.
Elewa tunafanya makosa makubwa sn mbele za Mungu.

Ni kweli kuwa ndoa inafika mahali inafifia na kukosa mapenzi ya mke na mume.
Lakini ni vizuri zaidi wahusika wakakaa na kujadili jinsi gn wataweza kurudisha mapenzi kwenye ndoa yao,
na sio kuvunja ndoa,
Tena bila sababu za msingi.,,

Talaka sio kitu kizuri ndg zangu,
Kitendo cha mwanaume kutoa talaka,
au mwanamke kuomba talaka,
Ni Sawa na kuvunja ahadi ambayo mliiweka mbele za Mungu kwamba mtapendana kwa shida na raha kwa maisha yenu yote.
Talaka huwa ina kawaida ya kurudi kwa wanandoa na kumuhukumu yule mkosefu,

Kuna mwanamke ambaye yeye ndy chanzo cha ndoa kuvunjika,
Lakini bado anadai talaka kwa nguvu zote,
tena kwa kashfa na vurugu.
Mwanamke huyu hatopata faraja ya ndoa huko aendako.,
Talaka itamrudia na kumchapa haswa.

Kuna mwanaume ambaye yeye ndy chanzo cha kuvunjika ndoa,
Na bado anatoa talaka kwa kosa alilofanya yeye.
Huyu mwanaume hatobaki salama huko aendako.
Talaka itamchapa haswa,
Mwishowe kujutia maamuzi ya talaka.

Talaka unatakiwa uitoe ukiwa upo very calm na sio hasira .
Unahitaji umakini Sana kwenye hili.
Talaka inaweza ikawa ndy mwanzo wa kuvurugikiwa maisha yako au mwanzo wa mafanikio,
Inategemea ni Kwa jinsi gani mmeachana.

Ushuhuda
Nilibahatika kuoa mwanamke fulani mrembo sn miaka 17 iliyopita.
Nikiwa bado kijana mdogo sikuwa na kipato kizuri ,
nilikuwa na kipato cha kawaida cha kuunga unga.
Yule binti alinisumbuwa sn sababu ya uzuri wake.

Nilijitahidi kumtunza kwa kadiri ninavyoweza,,
lakini mwisho wa siku alianza visa na kuomba talaka,
Tena kwa vurugu,
kashfa nyingi,
Alikwenda mbali zaidi na kusema mimi sio type yake,
ninamfuja na kumbana bana ili asiolewe na wanaume wenye pesa.

Alilazimisha talaka kwa matusi na kashfa ,
Alikuwa akitoka asubuhi na kurudi jioni tena amelewa na sijuwi pombe amenunuliwa na Nani,
Nikiuliza atajibu kashfa tupu,

"Nilishakwambiya niache na maisha yng wewe unaning'ang'ania nini?"

Aliponambiya maneno haya nilipata uchungu Sana moyoni
Nikiifikiria ndoa yng bado hata mwaka haijafikia,
Sababu nilikuwa na mapenzi mazito Sana kwake ,
nilishindwa kufanya maamuzi ya haraka,
Kwa kweli nilimpenda sn mke wangu.

Nilijitahidi kuwaeleza wazazi wake tatizo,
Lakini kwa majibu aliyonijibu mama mkwe nikagunduwa ,
hata mama mkwe pia hanitaki niishi na binti yake.
Sababu ya kipato changu duni ,,

Yaani mke wangu nimekuoa kwa mahari halafu Leo unambiye hunitaki?
Kwamba siyo type yako?
Hunipendi tena?

Niliitoa talaka kwa uchungu Sana.

Now ni miaka 17 ya talaka lakini still yupo mitaani anahangaika kupata Mwanaume hata wa kuishi nae store hamuoni.,
Hata mtoto wa dawa hana,
Kapauka kama mguu wa Teja.

Tusipende kutoa/ kuomba talaka kama wewe ndy mkosefu.
Jishushe/ omba msamaha maisha ya ndoa yaendelee..


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana. Ni kweli kabisa, kama wewe ndio chanzo cha kuvuruga mahusiano yenu mara nyingi utaharibikiwa huko mbeleni. Mimi wa kwangu alipata mchepuko , akawa anarudi asubuhi, akija ukimsemesha anasema bora tuachane. Baadae akahamia huko miezi 3 anasema yuko Msata kwenye shughuli zake, kumbe yuko kwa mchepuko hapa Dar. Bahati nzuri siku nikamuona anapita na gari, kumpigie anasema bado yuko huko. Nikavumilia nikaona huu ni ujinga. Kikaitwa kikao cha familia mara 2 hakutokea. Wazazi wake wakaniambia kwa uliyotueleza una haki ya kuondoka. Nikaanza mchakato wa talaka ndio ikawa hivyo tena. Kuona nimeondoka akapangisha nyumba akahamia kwa mwanamke. Baada ya miezi 6 akafukuzwa kwa mchepuko baada ya hela alizouza gari yangu kuisha. Yupo tu sasa hivi , baba yake kamuambia kama unataka amani ya hii dunia aniombe msamaha maana alifanya dhulma ya wazi. Ila Mungu ni mwema maisha yanasonga
 
Hakika mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakataa dhana y kwamba kila mwanandoa anachapiwa
Life is all composed of beliefs that we accumulated due to our own experience ama kusimuliwa ama kuwekewa kichwani due to our upbringing societies.
So sijakataa beliefs uliyo nayo kwa Jambo hili mkuu.
Do you believe kuwa wote wanandoa tokea wameoana wanaingiaga kaburini bila ya kuchepuka kweli yaani bila kuonja ladha nyingine.
Life is all about our beliefs, remember beliefs is the energy,do you know properties of the energy lakini.
Siku iyo beliefs zikitoka ndipo unashangaa.
 
Mali unaziandika majina ya watoto tu haina jinsi😂😂😂 kama ishu ni hio.
Bora ivo kuliko kuishi kwa shiiiida eti mke atafaidika mkiachana, mbona amekaa nawe miaka yote akikuzalia watoto ukaitwa baba? Akafanya na wewe ukawa na watu wako eti ile ni familia ya flani, lakini mali ambazo huja na kuondoka unaziona za thamani saaaana kuliko mke...sema mali yenye jina la mtoto ujue hukopei kama wewe ni hustler usiyechoka ila kama ni wale wa kujenga vinyumba viwili na gari ya kutembelea unaona umeyapatia maisha unaeza eka majina ya watoto
 
Mi hakikuwepo Cha kugawana coz ndo kwanza tulikuwa tuna miaka miwili na hatujawahi ishi pamoja....kwahiyo alikokuwa anaishi alikuwa na chake na ninapoishi nami Nina changu
Hii ni rahisi kwa kila mmoja wenu.

Kwa watu ambao wameishi kwa zaidi ya miaka 5 bila kuwa na migogoro ile kila siku, inapotokea kuachana, hakika nakuambia, sio mali zitakazomuuma MWANAUME. Mali ni nini bwana?

Kwa mwanaume, mwanamke alimuoa kwa kumpenda, humkabidhi maisha yake, mwanaume huanza kuishi kwa mujibu wa taratibu tu. Wanaosema wana-move on, ni waongo kama mazingira ya ndoa zao ni kama hii! Mwanamke anapenda kila mwanaume atakayeamua kumpenda, anasahau kila kitu akikutana na maisha bora!

Mwanaume hawezi kumsahau mwanamke aliyempenda na kumkabidhi maisha yake asilani.

Mwanaume atateseka na kutafuta kitu cha kumuondoa kwenye mateso ya fikra temporarily ambapo mara nyingi itakuwa ni kitu kinachomsogeza karibu na kifo chake.

Hakuna mwanaume aliyeshinda mbele ya mwanamke aliyempenda, rejea maandishi ya kiimani pia uone!
 
Na ndivyo wengi wanafanyiwa lakini bado hawajifunzi.....kuna dada mmoja jirani yangu yeye aliona hawara anafaa zaidi kuliko ata ndugu na watoto ukiachilia mume maana ni mke wa ndoa kabisa, katafuta kwa jasho anajenga kisirisiri eti mumewe asijue hati si akaandika jina la hawara, akanunua gari mnunuzi si jina la hawara, wakati huo kijana Mario hajaoa, amesubiri vimekamilika vizuuuuri kaoa nyumba anaishi yeye na mkewe, gari anatembelea yeye, kiujumla uyu mama amedhulumika kila kitu na biashara imekata saivi anauza mkaa wa mafungu gengeni nyieeeee kila nkimfikiria adi naogopa....usiishi na mtu unamuwazia negative tuuuu hata hajakuonesha ubaya wowote ila we unawaza mabaya tuu ndo hayo yanawakuta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…