Tukutane tunaomiliki magofu kwa ajili ya kufarijiana

Tukutane tunaomiliki magofu kwa ajili ya kufarijiana

Wakuu habari za muda huu najua mko njema tunaendelea kupata pumzi ya bure na Mungu atubariki

Kama kawaida kuna wakati mtu unapambana na inafika hatua unatamani uwe na kwako uchomoke kwenye mambo za kupanga au tena ukahitaji kujiwekeza kwenye ujenzi kama biashara

Sasa kama ilivyo kawaida kujenga hakujawai kuwa rahisi, baada ya kupiga hesabu zangu nikaona nisimamishe kibanda cha vyumba vitatu na sebure nikiwa na uhakika na biashara yangu kuimarika kiasi kwamba kila mwezi ninaweza kusave 1ml nikaelekeza kwenye ujenzi

Doh! Najuta baada tu ya kuamsha boma upepo wa biashara ukabadirika na nisiweze kunyanyuka mwaka wa pili huu boma limekuwa gofu kila nikipiga ramani hazieleweki.

Je vipi kwako mdau nyumba yako imekamilika au umejiunga katika jumuia ya magofu tz? Unafanyaje kujiondoa katika hali hiyo?

Karibuni
Mngetupia walao tupicha picha ingekuwa bye
 
Niliiona juzi mitaa ya goba, kishapitisha umeme na kapiga plasta ila haijaezekwa....nikabaki nashangaa
Ela yako tu mkuu. Mimi tanesco waliniwekea nguzo na kuweka kabisa nyaya wakati hata wiring sijafunga. Fundi alifanya kufunga wiringa na kuunga tu
 
Anza na kununua material mkuu, kidogo kidogo mkuu
Utakuja kunishukuru
Hii ilikuwa formula yangu... nilikuwa nanunua material nayaacha dukani yakitimia ya stage fulani namshtua fundi anakuja analiendeleza.
Niko mbioni kuhamia mwezi huu japo finishing haijakamilika naenda kuhamia hivyo hivyo maana maji, umeme, skimming, gypsum grills, milango tayri, nataka nimalizie master bedroom kwa tiles na aluminum nihamie kwanza maana ni mimi pekee sina familia huku nikimalizia finishing taratibu.
Ila katika ujenzi nimegundua kama ela kama yangu ya kusanya sanya, ni kama unakwua unaukia pesa tu na vitu haviishi.
Mpaka sasa najiuliza watu wanaochukua mkopo sijui 20 mls wakajenge, naona kama ni kosa kubwa. Maana mtu unakuta mshahara milioni 1 anachukua mkopo 20 mls, anajenga nyumba haishi, kuhamia haamii na bado anakatwa, na kodi iko pale pale.
 
Kungekuwa hakuna wizi wa vifaa vya ujenzi kama mchanga, mawe, matofali etc Bunge kupa mbinu ya kusogeza ujenzi.
Hardware zipo na wanatunza risiti ukilipia sema hela haikai pia nilipofikia panataka hela cash approximation ni kama 3m- 4m
 
Nimechoka na kulimia
 

Attachments

  • IMG_20241130_085316_129.jpg
    IMG_20241130_085316_129.jpg
    753 KB · Views: 10
Ni hatari hii stage nimekwama kwenye tope nashukuru kwa hamasa mkuu
Mimi niliipiga kunzia mwaka jana mwezi wa tatu, nikakwamba baada ya kumalizia kozi zile tatu za juu baada ya lenta. ilikuwa mwez wa tisa mwaka jana. nikapumzika nikaja kuezeka mwaka huu mwezi wa nne. uzuri mashimo yachoo niliyajenga nilipomaliza kujenga msingi ili nipae kifusi cha kujazia msingi.
now imebaki kupiga rangi, tiles na aluminum. gypsum, skimming, mifumo ya maji, milango yoteya chuma na mbao, na frills za madirisha tayari.
Sema kujenga boma rahisi... kuanzia kwenye kuezeka ndipo unaanza sasa kuona uhalisia wa ujenzi.
 
Hii ilikuwa formula yangu... nilikuwa nanunua material nayaacha dukani yakitimia ya stage fulani namshtua fundi anakuja analiendeleza.
Niko mbioni kuhamia mwezi huu japo finishing haijakamilika naenda kuhamia hivyo hivyo maana maji, umeme, skimming, gypsum grills, milango tayri, nataka nimalizie master bedroom kwa tiles na aluminum nihamie kwanza maana ni mimi pekee sina familia huku nikimalizia finishing taratibu.
Ila katika ujenzi nimegundua kama ela kama yangu ya kusanya sanya, ni kama unakwua unaukia pesa tu na vitu haviishi.
Mpaka sasa najiuliza watu wanaochukua mkopo sijui 20 mls wakajenge, naona kama ni kosa kubwa. Maana mtu unakuta mshahara milioni 1 anachukua mkopo 20 mls, anajenga nyumba haishi, kuhamia haamii na bado anakatwa, na kodi iko pale pale.
Ukiona nyumba imeisha kila kitu na mwamba kaweka mpaka pavements na fence,mpe shkamoo...
 
Wakuu habari za muda huu najua mko njema tunaendelea kupata pumzi ya bure na Mungu atubariki

Kama kawaida kuna wakati mtu unapambana na inafika hatua unatamani uwe na kwako uchomoke kwenye mambo za kupanga au tena ukahitaji kujiwekeza kwenye ujenzi kama biashara

Sasa kama ilivyo kawaida kujenga hakujawai kuwa rahisi, baada ya kupiga hesabu zangu nikaona nisimamishe kibanda cha vyumba vitatu na sebure nikiwa na uhakika na biashara yangu kuimarika kiasi kwamba kila mwezi ninaweza kusave 1ml nikaelekeza kwenye ujenzi

Doh! Najuta baada tu ya kuamsha boma upepo wa biashara ukabadirika na nisiweze kunyanyuka mwaka wa pili huu boma limekuwa gofu kila nikipiga ramani hazieleweki.

Je vipi kwako mdau nyumba yako imekamilika au umejiunga katika jumuia ya magofu tz? Unafanyaje kujiondoa katika hali hiyo?

Karibuni
Ezeka chumba na sebule hamia.
 
kwenye kila hatua ya maendeleo unayopiga, tambua kuna vita ya nyama na kiroho itakuandama.

Jifunze kuweka GUARD kila mara na unatakiwa utambue ADUI yako ni nani ili upambane nae MAPEMA..

Mimi nilinunua kiwanja mwaka 2021 mwezi wa tano nakumbuka siku simba anacheza na mashujaa, simba akala chuma moja.

Nilikua na milioni 2 nawaza kuweka chumba kimoja cha SLOPE (msingi upo), lakini hadi leo kiwanja kimebaki Jina tu..

Vita niliyokutana nayo baada ya hapo kuanzia kwa ndugu zangu tu baada ya kujua nimenunua kiwanja ilikua balaa sana maana sikuwashirikisha chochote...

Ikawa ndio mwanzo wa ile mil 2 kumeguka na kuisha..

Ila naamini all is well one day Yes
Screenshot_20241130-115914.jpg
 
Mimi niliipiga kunzia mwaka jana mwezi wa tatu, nikakwamba baada ya kumalizia kozi zile tatu za juu baada ya lenta. ilikuwa mwez wa tisa mwaka jana. nikapumzika nikaja kuezeka mwaka huu mwezi wa nne. uzuri mashimo yachoo niliyajenga nilipomaliza kujenga msingi ili nipae kifusi cha kujazia msingi.
now imebaki kupiga rangi, tiles na aluminum. gypsum, skimming, mifumo ya maji, milango yoteya chuma na mbao, na frills za madirisha tayari.
Sema kujenga boma rahisi... kuanzia kwenye kuezeka ndipo unaanza sasa kuona uhalisia wa ujenzi.
Hongera sana mkuu hakika umejinyima vya kutosha mimi renta bado ndo napambana niondoke kwenye hii stage ya renta na bati
 
Hivi pagala linaweza kukaa miaka mingapi mpaka liwe gofu la kubomoa na kuanza upya?
 
Back
Top Bottom