Tulifika Pabaya: Mwenyekiti Ulinzi na Usalama Wilaya eti ni Jambazi?


Mpendwa Sky, sio CCM hii ya sasa. Unajua kuwa Sabaya alikuwa mmoja wa wateule wa jiwe ambaye alikuwa anamdharau mama kama VP kwa kiburi cha ukaribu na mwendazake?
Na hiyo habari ya kumvimbia mkuu wa gereza umeipata ndivyo sivyo, habari za ndani ni kuwa siku yake ya kwanza jela hataisahau maishani mwake.
 
Sabaya alikuwa na kesi ya kujifanya ofisa usalama wa taifa....baadae tunaona anakuwa mkuu wa Wilaya, nini kilitokea, alisingiziwa ile kesi? Kama alisingiziwa, nani alichukuliwa hatua? Kama hakusingiziwa na alishinda kesi, kwanini serikali hiyo hiyo iliyomtuhumu leo inamteua.

Tuna tatizo kubwa kuliko Sabaya. Hamad Masauni alijiuzulu uenyekiti UVCCM kosa la kughushi umri, inakuwaje bado yupo serikalini? Hakuna integrity test huko, hivi Nyerere angekubali viongozi wa aina hii kwenye serikali yake?

 
Asante sana mkuu, nitaanza kurudisha uzalendo kwa nchi yangu kama haya usemayo ni ya kweli.
 
Sabaya alikuwa ni TRA hivi?
 
Mataga hutawaona hapa.
 
yaani hawata baki salama kwenye maisha yao yote hapa Dunia kuna siku watu watajtolea kupambana nao!
Me binafsi kwa matendo ya ole sabaya ata nyama yake ninaweza kula bila kupikwa maana yule kafanya mambo ambayo hata shetani pengine hafanyi!
 
Then anapewa na askari kabisa wakafanye nae uhalifu.Kamati za ulinzi na usalama za wilaya na mkoa zipo tu kimya,kwann wasiwajibishwe nao?
 
Asante sana mkuu, nitaanza kurudisha uzalendo kwa nchi yangu kama haya usemayo ni ya kweli.
Mm mm! Don't quote me wrong, CCM ninayosema utofauti wa ile na hii ni katika kumshughulikia Sabaya kwani ziko sababu ambazo pengine Sabaya mwenyewe kawatibua.
Kwangu mengine bado ccm ni ile ile labda ijirekebishe na mwenendo unaonekana maana tabia za kishenzi zinaachwa zife na kuondoka na aliyrondoka
 

You are a fool! Eti watu wa kaskazini? Ukimaanisha kabila au eneo?? Hivi ni kweli hujui kuwa matendo yote aliyafanyia ndani au karibu na eneo lake la kazi kaskazini??

Wewe ulikuwa-brainwashed na “upendo” na “uzalendo” wa mwendazake! Katika mengi aliyofanya mazuri, kulikuwa na mabaya pia!! Uonevu. Dhulma. Kuonesha hayo ndio maana mnasema tena “msiwabambikie watu makosa”, “wafungulieni watu akaunti zako” na “wafungulie watu viwanda na mashamba yao”. Hata hao nao wamehongwa na matajiri ili waende kombo na mwendazake??

Unaweza kuwa hukuguswa na mambo ya Sabaya. Ni kwa kuwa labda hauko kaskazini au hata kama ungekuwa - asingekuwa na ishu na wewe. Tuache wahanga wathibitishe madhila yao mahakamani. Kama hakutenda mabaya, atakuwa mtaani na wewe.
 
Hiyo kusema marehemu alipendwa na 85%, labda hapo kijijini penu.

Nenda mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na mikoa ya Kusini, tena nenda vijijini, kawaulize wanavijiji wakulima wa mahindi, wakukima wa korosho, wakulima wa tumbaku, wakulima wa miti ya mbao, wafanyabiashara wa mbao, wakulima wa viazi, tena watafute wanaCCM, nina hakika utarudi na fikra tofauti.
 
Hivi kumbe Sabaya yeye katokea kanda ya magharibi. Hawa jamaa wa kaskazini wabaya sana. Hawataki kabisa mtu mwingine tokea kanda nyingine aongoze, huu ndio ugomvi wao kwa Sabaya
 
Udikteta ulikuwa unapeleka mizizi yake chini ingelifikia hadi Balozi wa Nyumba kumi angeweza kupiga simu Ikulu usiku wa manane ili apongezwe kwa 'Kushughulikia' Wananchi kwa kuwakomesha Chadema.

Kwa hilo tunamshukuru mtoa Roho Mungu.
 
Usihofu sasa wanaondoka watumishi majambaazi wanarudi watumishi wazee wa vijicent

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niliwahi kusema humu kwamba sio busara kwa RC na DC kuwa wenyeviti wa kamati za usalama mkoa na wilaya. Kwasababu hawa ni makada wa chama wanaoteuliwa kisiasa.

Tukiendelea na MFUMO huu vyombo vya usalama (polisi, takukuru na tiss havitafanya kazi zao kitaalamu na kwa ufanisi.

Kumbuka kwamba hata Uhamiaji, NIDA, TCRA na Tume ya Uchaguzi ni vyombo vya usalama pia. Kufanya chama cha siasa kiwe na ukiritimba kwenye vyombo au taasisi hizi ni hatari kwa maslahi ya nchi.

Ingeleta maana kama RAS na DAS ndiyo washiriki ktk kamati hizi kama makatibu/waratibu (coordinating secretaries) na kuripoti kwa Katibu Mkuu Kiongozi.

Awali baada ya UHURU Mwalimu J. K. Nyerere aliwaita RC na DC Makatibu wa TANU/CCM Mkoa na Wilaya. Lakini baadae ghafla wakapewa ugavana!

Sasa fikiria kama chama kingine cha siasa kikishika dola, halafu makada wake wawe wenyeviti wa kamati za usalama, CCM itakuwa salama?

Kwa MFUMO huu ni dhahiri hatuwezi kuwa na utawala wa demokrasia na haki. Kwasababu CCM itaendelea kutumia taasisi hizi kama vyombo vyake vya kujilinda dhidi ya upinzani.

Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
 
Hata kabla hajateuliwa Sabaya alikuwa jambazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…