Tulikuwa tunaambiwa USA inaendeshwa kitaasisi na si maamuzi ya mtu mmoja. Mbona sasa tunashuhudia vituko?

Tulikuwa tunaambiwa USA inaendeshwa kitaasisi na si maamuzi ya mtu mmoja. Mbona sasa tunashuhudia vituko?

Mbona mi naona ni yaleyale isipokuwa ilikuwa inafanya vitu kwa kinyago cha mbuzi sasahivi inafanya vitu kwa kinyago cha chui ila simba ni yuleyule!, sikuzote marekani husimama upande wa faida haijalishi atakuja na sura gani!.
 
Huo hapo ndio ushahidi wenyewe , nimefanya inquiry juu ya sheria za Marekani na muktadha ambao Rais anakuwa kavunja sheria
Loophole anayotumia Trump ni hiyo ya kuwa na wabunge wengi ndani ya congress, tangu ameanza mpaka Sasa mambo yote ambayo ameruhusiwa kufanya kafanya kisheri na lolote lenye ukakasi au liko nje ya mipaka yake kama ulivyoona hapo congress imelipinga
Opinion zako sio ushahidi. Ulichoandika ni nafsi yako na sio Sheria yoyote ya Usa.

Mimi nimeweka kesi ya kwanza ambayo Tayari Trump Ameshashindwa, kama Alikua sahihi kwanini kashindwa? Na kesi sio moja zipo nyingi tu.


Hii nyengine.

So anachofanya Trump ni kutumia mabavu tu sasa hivi na kukiuka Amri za mahakama.
 
Si Kweli kavunja Katiba na sheria mara kibao, kuna kesi za kutosha tu ila hazina nguvu sababu yupo kwenye power.

Mfano
Kwenye Katiba ya Marekani Congress wana uwezo wa kulimit spending za Government, serikali hairuhusiwi kutumia ama kuzuia matumizi ambayo yamepitishwa na Bunge

Trump alivyoingia Madarakani kuna vitu kibao vilivyopitishwa na Bunge amevikataa kwa kisingizio haviendi na will of America

Mfano wa kesi

Sasa hivi Usa kuna Constitutional crisis
Duh!...kwamba Trump ni mvunjifu wa Katiba?...
 
Maslahi ya matajiri kama Musk, siku akitoa huduma za Afya, Elimu na vitu vingine vya msingi bure nishtue, Ulaya, Middle East na karibia Nchi zote Tajiri Duniani vitu kama Afya na Elimu si tatizo tena ila Nchi kubwa kama Usa bado wanajadili Bima za Afya kama Tanzania tu. Kupata Degree unaingia Deni unalolipa karibia maisha yote.
Duh.!.ubeberu wao ni kiwango cha juu mno....yaani wenye nguvu/fedha ndio wanafaidi.
 
Wakuu, kwa miaka mingi tuliambiwa maamuzi yoyote pale USA ni ya taasisi na si mtu mmoja. Kwamba katiba yao ndio inaamua, kwamba hata akija Rais kichaa anaongoza maana yeye si mtoa maamuzi pekeake.

Lakini hiki tunachoshuhudia sasa hivi mbona ni kama Afrika tu?

Yani Trump sasa hivi anaweza kuamka tu na kutoa tamko kwamba toa hiki weka pale, kile leta hapa.

Mfano mzuri ni ishu misaada kwa Afrika, na hili la kujitoa WHO na sasa eti anapanga kujitoa UN.

Mbona mimi naona kama US mfumo wao wa uongozi ni mbovu kuliko Afrika?
Mkuu wengi tuliaminishwa hivyo mpaka majuzi tulipoyaona haya.
 
Yani USA sasa haina tofauti na nchi za kiafrika maamuzi yanatolewa na mtu mmoja tu
Rais wa Ukraine kamtolea nje deal lake la kumsainisha kujichotea madini ya Ukraine, kamfanya adui na kuendesha kampeni ya kumwondoa madarakani. 😳
 
Maamuzi anayofanya Trump YAPO ndani ya mamlaka yake kama Rais, mimi na wewe pamoja na wamarekani Gen Z tunaona ajabu kwasababu ni kwa muda mrefu rais hajawahi kutumia mamlaka yake namna hii
Sawa kama ni hivyo lakini najiuliza ni kwa nini marais waliomtangulia hawakufanya anachofanya yeye leo hii? Walipotezea kwa ajili ya masilahi mapana ya marekani au ni kwa kutokujuwa?
Zamani nilifikiri kabla marais hawajakutana kwa ajili ya kukamilisha deal fulani kuna wasaidizi wao wanakuwa wameshakaa na kukubaliana kila kitu then marais ni showoff tu ya kukubaliana na kusaini, lakini sio nilichokiona juzi pale WH.
 
Wakuu, kwa miaka mingi tuliambiwa maamuzi yoyote pale USA ni ya taasisi na si mtu mmoja. Kwamba katiba yao ndio inaamua, kwamba hata akija Rais kichaa anaongoza maana yeye si mtoa maamuzi pekeake.

Lakini hiki tunachoshuhudia sasa hivi mbona ni kama Afrika tu?

Yani Trump sasa hivi anaweza kuamka tu na kutoa tamko kwamba toa hiki weka pale, kile leta hapa.

Mfano mzuri ni ishu misaada kwa Afrika, na hili la kujitoa WHO na sasa eti anapanga kujitoa UN.

Mbona mimi naona kama US mfumo wao wa uongozi ni mbovu kuliko Afrika?
Kila anachofanya Trump kiko ndani ya mamlaka yake....HAVUNJI SHERIA WALA HAKANYAGI KATIBA. Ni sawa tu leo hii mama Abdul asaini mfungwa kunyongwa,walio wengi watashangaa humu...
 
Wakuu, kwa miaka mingi tuliambiwa maamuzi yoyote pale USA ni ya taasisi na si mtu mmoja. Kwamba katiba yao ndio inaamua, kwamba hata akija Rais kichaa anaongoza maana yeye si mtoa maamuzi pekeake.

Lakini hiki tunachoshuhudia sasa hivi mbona ni kama Afrika tu?

Yani Trump sasa hivi anaweza kuamka tu na kutoa tamko kwamba toa hiki weka pale, kile leta hapa.

Mfano mzuri ni ishu misaada kwa Afrika, na hili la kujitoa WHO na sasa eti anapanga kujitoa UN.

Mbona mimi naona kama US mfumo wao wa uongozi ni mbovu kuliko Afrika?
Chadomo huwaga ni roporopo wanaweza kudanganya wajinga tuu.

Rais ndio Kila kitu kwenye Nchi yeyote hakuna Cha Katiba Mpya Wala ya zamani.
 
Trump is running America like it's his own house. Those who used to say America has strong institutions should come here and tell us what we're witnessing under Donald Trump's leadership. It's a total disaster for a nation that calls itself a first-world country.
But ataangukia pua very soon kama akiendelea na haya maamuzi yake, within 100 days but alot of disasters
 
Watashangaa vipi wakati sheria ya kunyongwa ipo?

Kila anachofanya Trump kiko ndani ya mamlaka yake....HAVUNJI SHERIA WALA HAKANYAGI KATIBA. Ni sawa tu leo hii mama Abdul asaini mfungwa kunyongwa,walio wengi watashangaa humu.
 
Kavizuia kwasababu katiba inamruhusu kuvizuia , angekuwa kavunja sheria kwa kufanya hivyo tayari wapinzani wangeanza zengwe la impeachment ili aondolewe
Nalo hilo la impeachment linawezekana kama ndani ya siku 100 tu za utawala wake ndio haya tunayoyashuhudia mbeleni tunaweza kuliona hilo la kumtaka aondoke madarakani.
 
Wakuu, kwa miaka mingi tuliambiwa maamuzi yoyote pale USA ni ya taasisi na si mtu mmoja. Kwamba katiba yao ndio inaamua, kwamba hata akija Rais kichaa anaongoza maana yeye si mtoa maamuzi pekeake.

Lakini hiki tunachoshuhudia sasa hivi mbona ni kama Afrika tu?

Yani Trump sasa hivi anaweza kuamka tu na kutoa tamko kwamba toa hiki weka pale, kile leta hapa.

Mfano mzuri ni ishu misaada kwa Afrika, na hili la kujitoa WHO na sasa eti anapanga kujitoa UN.

Mbona mimi naona kama US mfumo wao wa uongozi ni mbovu kuliko Afrika?
Kiranga Nguruvi3 Mag3 Nyani Ngabu
 
Wakuu, kwa miaka mingi tuliambiwa maamuzi yoyote pale USA ni ya taasisi na si mtu mmoja. Kwamba katiba yao ndio inaamua, kwamba hata akija Rais kichaa anaongoza maana yeye si mtoa maamuzi pekeake.

Lakini hiki tunachoshuhudia sasa hivi mbona ni kama Afrika tu?

Yani Trump sasa hivi anaweza kuamka tu na kutoa tamko kwamba toa hiki weka pale, kile leta hapa.

Mfano mzuri ni ishu misaada kwa Afrika, na hili la kujitoa WHO na sasa eti anapanga kujitoa UN.

Mbona mimi naona kama US mfumo wao wa uongozi ni mbovu kuliko Afrika?
Wewe unafikiri matamko ya trump yapo kikatiba na ni kwa maslahi ya marekani au anajitamkia tu kama huko kwenu kwa kusadikika?
 
Basi mfumo wao wa uongozi ni mbovu sana!

Kwahiyo pale alipo anaweza hata kuamuru kubonyezwa kitufe cha nyukilia kulipua nchi flani bila kuingiliwa na yeyote.
unataka Rais awe na madaraka sawa na mbunge??
ndivyo ulivyokuwa unaitafsiri demokrasia??
 
Lakini hiki tunachoshuhudia sasa hivi mbona ni kama Afrika tu?

Mfano mzuri ni ishu misaada kwa Afrika, na hili la kujitoa WHO na sasa eti anapanga kujitoa UN. Mbona mimi naona kama US mfumo wao wa uongozi ni mbovu kuliko Afrika?
Trump anawaumbua Wazungu kwa unafiki wao. Wakome sasa kutulecture sisi kuhusu democracy na waanzie kwako

Yaani mtu mmoja anaibuka na tamko tu au Executive Order moja tuu na kila Muhimili unaufyata kimyaaa

Sasa hivi amefuta msaada kwa nchi ya Ukraine kwa kutoa tamko tu wakati misaada mingine ilipitishwa Senate
 
Hizo zilikuwa ni propaganda za kumdidimiza Magufuli.
Ila utashi wa Rais ndio unaongoza nchi.
Huyu wetu kasema tule kwa urefu wa kamba.
Na tunakula kweli kwa urefu wa kamba, km angesema vinginevyo pia tungefuata tu.
 
Wakuu, kwa miaka mingi tuliambiwa maamuzi yoyote pale USA ni ya taasisi na si mtu mmoja. Kwamba katiba yao ndio inaamua, kwamba hata akija Rais kichaa anaongoza maana yeye si mtoa maamuzi pekeake.

Lakini hiki tunachoshuhudia sasa hivi mbona ni kama Afrika tu?

Yani Trump sasa hivi anaweza kuamka tu na kutoa tamko kwamba toa hiki weka pale, kile leta hapa.

Mfano mzuri ni ishu misaada kwa Afrika, na hili la kujitoa WHO na sasa eti anapanga kujitoa UN.

Mbona mimi naona kama US mfumo wao wa uongozi ni mbovu kuliko Afrika?
Mpaka sasa yote ambayo kayafanya yanaangukia kwenye mamlaka yake ya kiraisi.

Hajafanya jambo lolote lile lililo kinyume na katiba, kwa mfano, hajapiga marufuku vyama vya kisiasa kufanya shughuli zao kisa uchaguzi umeisha. Hajakataza watu kuamini wanachotaka kuamini.

Hajafungia chombo chochote kile cha habari, si gazeti, kituo cha runinga, redio, wala kumfunga mwandishi yeyote yule wa habari.

Hajaingilia taasisi zingine zozote zile zilizopo chini ya matawi ya serikali, i.e., bunge na mahakama.

Majuzi hapa kamwondoa mkuu wa majeshi pamoja na viongozi wengine waandamizi wa jeshi. Mamlaka hayo anayo kikatiba.

Hivyo hajavunja katiba.

Yeye ndiye mkuu wa tawi la utendaji [executive branch] na kwa msingi huo, anayo mamlaka kiutendaji.

Sasa akitenda, ni kipi ambacho anakiuka?

Labda ni uelewa mdogo wa jinsi ambavyo Marekani inaendeshwa ndo maana watu mnafikia mahitimisho kimakosa….
 
Back
Top Bottom