Tulioangalia Kombe la Dunia mwaka 1986 nyumbani kwa Sheikh Yahya Magomeni tukutane hapa

Tulioangalia Kombe la Dunia mwaka 1986 nyumbani kwa Sheikh Yahya Magomeni tukutane hapa

Huu uzi kuna watu watapita kama hawaoni maana wengi mwaka huo walikuwa viunoni mwa wazazi wao, wengine mlikuwa Sitimbi huko hamjui hata video ni mdudu gani.

Mwaka 1986 kulikuwa na fainali za Kombe la Dunia nchini Mexico, Germany Magharibi anapigwa 3-2 na Argentina, Argentina anachukua ubingwa. Bonge moja la mechi haijawahi tokea ila imefunikwa na mechi ya jana achana na Messi kuna mtu akiitwa Zicco unamkumbuka.

Kuna timu ya Uruguay walikuwa wanasifika kwa kucheza rafu mbaya hadi huku mtaani timu ikicheza rafu ikawa inaitwa Uruguay.

Kipindi hicho Dar nzima tunaenda Magomeni Mikumi kwa sheikh Yahya ndio alikuwa na hiyo video big screen mithili ya ukubwa wa kioo cha fuso.

Hii screen iliwekwa nje ya nyumba yake sehemu ya wazi watu tulijazana kama tuko Uwanja wa Taifa
pembeni amepaki range rover milango sita.

Huyu ndiyo alikuwa Don Dar nzima, Bakhresa kipindi hicho hajaanza hata kuuza mikate anauza icecream tu.

Mwaka huo Tabata nzima bar ziko mbili tu,Camp bar na Hai bar
Hongera Sana kwako mkongwe. Nakiri kwamba umenizidi fainali moja tu katika maisha yangu. Mungu kanijalia kuangalia Kombe la Dunia Tangu fainali za 1990, Argentina ikifungwa na German Kwa penalty ya dakika za mwisho iliyopigwa na Andreas Brehme. Argentina wakipinga penati hiyo Kwa Muda mrefu wakiongozwa na Maradona. Watu wengi wakiamini kocha atamteua Lothar Matheus kupiga penalty ile, ghafla kocha anamwita pembeni wakati Argentina wakiendelea na ubishi na kumwagiza penalty ipigwe na Brehme.
 
Ile Argentina ya kina batista, huyu alikuepo jana
Maradona aliibuka mchezaji Bora 1986
Kuna mwamba anaitwa Gary lineker wa uingereza[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
Gary Lineker, a fair play player ever.
 
Sisi wengine tuliangalia majumbani mwetu fainali ya 1978 kupitia TVZ (Television Zanzibar) ambapo Argentina ilikuwa ni mwenyeji na ndio iliyoibuka bingwa. Huku washabiki wao waki chant " AARGENTINAAA AARGENTINAAA AARGENTINAAA"
Baada ya Kum bamiza Uholanzi 3-1
Hata mitaani watoto wakishinda kwenye chandimu ndio ilikuwa chant yao hiyo.
Nakumbuka mwaka huo na Wasomali walitunga wimbo kuwasifu Argentina
Zamani mpira ulikuwa ni Hamasa haswa dunia nzima haijalishi ni nani ili mradi wanacheza vizuri
 
Mwaka 1990 luninga zilishaanza kuwa nyingi, halafu anaibuka mjinga mmoja anasema Mzee Ruksa hakufanya kitu.

Mwaka 1986 hata mwaka ulikuwa haujatimia tangu Mwinyi aingie madarakani ndio maana hali ilikuwa hivyo.

Tumetoka mbali

Wacha uongo wako, zilikuwa nyingi aapi? Usitukuze vitu vya kijinga na ambavyo havikuwepo!
 
Hongera Sana kwako mkongwe. Nakiri kwamba umenizidi fainali moja tu katika maisha yangu. Mungu kanijalia kuangalia Kombe la Dunia Tangu fainali za 1990, Argentina ikifungwa na German Kwa penalty ya dakika za mwisho iliyopigwa na Andreas Brehme. Argentina wakipinga penati hiyo Kwa Muda mrefu wakiongozwa na Maradona. Watu wengi wakiamini kocha atamteua Lothar Matheus kupiga penalty ile, ghafla kocha anamwita pembeni wakati Argentina wakiendelea na ubishi na kumwagiza penalty ipigwe na Brehme.
Hiyo mechi naikumbuka ilikuwa ni kama kipindi cha pili cha fainali ya 1986 maana final contenders walikutana tena.enzi hizo mechi zilikuwa wa msisimko wa aina yake
 
Hiyo mechi naikumbuka ilikuwa ni kama kipindi cha pili cha fainali ya 1986 maana final contenders walikutana tena.enzi hizo mechi zilikuwa wa msisimko wa aina yake
Uko sahihi. Ilikuwa ni kama marudio ya 1986 Mexico.
 
Ujerumani ya Magharibi kipindi hiko ilikuwa na mchezaji hatari sana Matthaus.

Alimkaba sana Maradona, hivyo Barrachugga ndiyo akawa hatari sana upande wa Argentina, fainali.
 
Back
Top Bottom