Tuliopitia Vita Na Chuki Makazini Tushirikishane Hapa

Kazini kuwa time taker, cheka na kila mtu, mpende kila mtu ila usimwamini mtu.
Workmates wakifahamu kuna hatua ya kimaendeleo unapiga chuki zitaanza , hapo jiandae kurogwa
 
Duh
 
Au Wana mchukia mwenye Boxer mpya wakati wao Wana pikipiki za zamani
 
Ni kweli tena ukute HR kutokea uko Kilimanjaro wanapenda kutetea wazungu kama ndugu zao, utakuta Mzungu kakubali kulipa pesa nyingi, HR ana mkataza husiwalipe hivi walipe hivi, Yani HR alitokea jamii ya kanda ya kaskazini tu ujue staff mme umia.
 
Ishi vizuri na hao maofisini. Toa lonja kwa Wana wageni hapo kazini. Siku moja moja hawawezi kukusahau kukutoa. Kumbuka maisha ni duara. Uaminifu na ustaarab ni kitu muhimu. Ukiweza kujiendeleza fanya hivyo.
Kuna jamaa alihadithia maskani kuwa kuna mwana alifukuzwa kazi kwa Faizar kiwanda Cha mikate Dar kisa kavaa sendo zile za 60,000 kama Mwarabu. Mwarab kumuona akakwambia kwa mshahara ninaokupa huwezi kuvaa sendo ya bei hii. Wewe unaniibia. Akamfuta kazi hapohapo. Hili ni funzo kuwa weka password ktk maendeleo yako kazini. Wengine si wazuri.
 
Safi sana piga kazi kiongozi
 
Ngoja nami niweke case yangu

Nliajiriwa taasisi flani ya elimu kubwa tu hapa Dar baada ya miezi mitatu tu mkuu wa taasisi akatokea kuniamini sana kutokana na ufanyaji wangu akaniita ofisini akanipiga brush ya maana juu ya kitengo kingine nyeti katika taasisi hiyo kabla ya kutoka ofisini akaniambia nipitie reception kuna barua nichukue. Kucheck kaniongezea majukumu mengine nyeti sana na wenye safari za kutosha nafika kwa boss wangu wa kitengo changu kashatumiwa ujumbe akaniweka kitimoto sema sana umekuja juzi tu unajifanya wewe ndo mfanyakazi bora sio tutaona. Bwana were

Picha linaanza naye akaniongezea majukumu ikawa nkiingia kazini asubuhi natoka saa nne usiku nkifika nyumbani sita usiku ikawa ni kawaida mwili ulikubali ila nlichakaa hatari. Nkarudi kwa mkuu kumwomba anitoe kwenye kitengo cha kwanza akaniambia nkikutoa huko hicho kitengo kitashindwa kuperfom aseee ile kazi ilinitesa nlishindwa kufanya mambo ya msingi ya kwangu binafsi ya maendeleo ndugu wakaniweka kando kwasababu muda wote ilikua ni kazi na mimi.

Baada ya miaka minne rasmi ikaanza vita ya kuniharibia aseee ombea hii kitu usiombe watu wakuamulue jambo nlipigwa vita ya kufa mtu ikawa ni mashtaka kila siku uzuri mkuu wa taasisi aliliona hilo akatuita akampa makavu boss wangu mbele yangu bwana weeeee ilitokea tu nkaanza kuichukia kazi mwenyewe nkawa siendi kazini sina sababu nkafatwa mpaka kwangu na mkuu wa taasisi akaniuluza kama kuna jambo haliko sawa nimweleze lakini sikuona tatizo lolote hatimaye nkaacha kazi mwenyewe ukiniuliza Leo kwanini nliacha sinaga sababu Ila sijawahi kujutia mpaka kesho huo uamuzi
 
Nilikuwa kwenye kampuni flani na wajinga flani mngoni na mfipa,wakapiga zenge kwa boss ili niondoke kibaruani.nikasema hawa hawanijui vizuri itakuwa.mbona tumepigwa wote termination letter,na hawakuwa wamejipanga na mtaa,wanaishi maisha ya hovyo kwelikweli.
 
Hahaaaaaa....
Walimwaga mboga ukatoboa sufuria hahaaa
Ulimwambiaje bosi hahaaa sipati picha yaani vile unaanza "...bosi ni kweli lakini na fulani na fulani'
Hahaaa
 
Ukamwaga mboga
Dadeki zao [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…