Tuliopitia Vita Na Chuki Makazini Tushirikishane Hapa

Tuliopitia Vita Na Chuki Makazini Tushirikishane Hapa

Mkuu,unapoenda kufanya kazi kwenye ofisi yeyote ile,sikiliza tu maneno ya kuambiwa kua nani mbaya na nani mwema hapo kazini ila usichukulie serious au kumuhukumu mtu mpaka mtu huyo atakapokufanyia ubaya wewe au wema,sio rahisi kwa mtu kua mbaya kwa watu wote au kua mwema kwa watu wote,

Muhukumu mtu kwa jinsi atakavyo kutreat wewe kama wewe na sio kwa kusikia tu,mtu mbaya kwa wengine anaweza kua mwema kwako au mwema anaweza kua mbaya kwako,

Find the good in people and ignore the bad in them coz no one is perfect.
Nlikuwaga ofisi Moja hivi Ina wafanyakazi watano tu. Lakini wakitoka nje kula au kuwa field Kila mtu anamkandia mwenzake kuwa jau mara fitna. Mara mjuajiii. Nikachunguza sana nikagundua hapa ili uwe salama Bora uwe neutral.
Kuna kijamaa kikawa kinajifabza ndo kiongozi pale lakin mshahara ukitoka anaitwa mwingine kabisa kwenda kusaini na kuruhusu hela zitoke.
Nilichokuja kugundua kni kuwa binadamu tuna rangi nyingi sana. Sijui kama kinyonga anatufikia
 
Msala naopitia sasa hivi Mwenyezi Mungu ndio mjuzi wa yote
Don't give up mkuu ndio uanaume huo pendelea kusoma vitabu mkuu soma kiatabu kinaitwa the power of POSITIVE THINKING na the magic of THINKING big you will be fine mkuu nilishapitia huko kote mkuu ni kawaida hasa kwa wanaume.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm wakat naanza kazi nilikuwa namla bosi nlchokuja kukosea et nkaajatoka na Staffmates nkawa nkagonga wote,,, bhana bhn msijaribu hii michezo makazini... Nlchukiwa na bos na kunyimwa kla aina ya fursa mpk nliomba uhamisho mwenyewe
 
Tulikuwa tunadai mshahara meneja alikuwa rafiki yangu sana(kwa nilivoamini) akampigia mkurugenzi ili tusikie upande wake.

Mkurugenzi akatoa majibu hayaridhishi, meneja akakata simu huku analalamika mkurugenzi kuwa na mambo ya kisenge mi nikasema huyu mkurugenzi ana mambo ya kifala sana.

Dah kumbe yule meneja hakuwa amekata simu nikashangaa mkurugenzi kanipandia hewani anawaka mixa kunitishia kwenda polisi kwa kumdhalilisha ila kilichoniacha hoi ni meneja kutohusishwa kwa chochote katika ile issue pamoja na yeye kuwa muanzilishi wa kutukana.

Mkurugenzi akaanza kunitenga sana ofisini akishirikiana na meneja nikaona isiwe kesi Mungu sio muhaya nika resign baadae.

Nilimuachia Mungu na kujifunza kutomuamini mtu. Leo yule meneja ni wakili na mimi ndo nilimpa laki ya kulipia mihuri miwili maana baadae alikuja kupitia msoto usio wa kawaida
Believe believe believe guys we have to believe and working harder.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilifanya kazi na "WAPALE" kwenye ofisi Moja

Aiseee Hawa watu ni noma sana aisee

Sitakuja kusahau jamaa ni wanafki sana

Yaani ni hatari...Wana majungu sijwahi ona...
Ndicho kinachonikuta mimi kwenye hili kabila.Aisee kaa mbali nao na hili kabila kabisaaa
 
Nlikuwaga ofisi Moja hivi Ina wafanyakazi watano tu. Lakini wakitoka nje kula au kuwa field Kila mtu anamkandia mwenzake kuwa jau mara fitna. Mara mjuajiii. Nikachunguza sana nikagundua hapa ili uwe salama Bora uwe neutral.
Kuna kijamaa kikawa kinajifabza ndo kiongozi pale lakin mshahara ukitoka anaitwa mwingine kabisa kwenda kusaini na kuruhusu hela zitoke.
Nilichokuja kugundua kni kuwa binadamu tuna rangi nyingi sana. Sijui kama kinyonga anatufikia
Kiufupi waafrika hatupendani kuna ile story ya HR wa barrick gold mine kuwalipa pesa kiduchu wafanya kazi licha ya management kuidhinisha pesa kubwa ila HR alikataa akasema kama hawataki tutaleta wengine ndio utajua wabongo jinsi tulivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah! inasikitisha sana aisee,roho mbaya haijengi kabisa,kwa style hii,hayo maendeleo yatakujaje sasa?
Poleni sana mkuu.
We acha tu mkuu nilipoenda sehemu nyingine nikapewa nafasi ya assistant nikakataa nikapendekeza mtu mwingine management ikakataa na mpaka leo boss akiondoka ofisini ananiachia mimi na barua ya kuondoka nafanya hvyo hvyo japo kishingo upande kwasababu mimi napenda sana uhuru na nina experience mbaya sana na uongozi baada ya kumuona mtu anaacha kazi ya million 15 salary per month kwasababu ya fitna na majungu nachukia sana uongozi sema kuna mazingira hamna namna.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni stori ndefu, umeshawahi kuchukiwa bila sababu....basi from day one huyu HR alinichukia tu...Huyu HR wengi wanamwogopa,ana jina hapa,Neno lake ni sheria..akisema umekosa inatakiwa ukubali.
Sasa hapa staff wengi ni waoga,wanajipendekeza kwake mpaka na wazungu.
Mimi ni mtu ninayosimamia misimamo yangu siyumbishwi kabisa japo Corona imenitoa kwenye reli.
Baada ya miaka mingi kuona siingi 18 zake akajaribu kuunga urafiki baada ya miezi kadhaa nikaona haiwezi..nikaendelea na mfumo wangu wa mwanzo.
Nikaletewa boss,mapambano yakawa makubwa..Mwaka mimi na boss wangu hatuzungumzi...baadae tulimaliza tofauti zetu tukawa kitu kimoja...
Boss akanikubali sana,nikawa promoted
Miezi 7 sijaongezwa mshara wala sijapokea barua...
Nikaona wananitania,nikaanza tafuta kazi, simu zikapigwa kwa HR kama mimi ni staff wa hapa..
Akawa ananisiribia..mwezi wa nane nikaongezwa pesa na barua nikapewa.

Vita ikaanza upya kati yetu (mimi na boss wangu) na HR...

Tarehe 29 mwezi uliopita tukamfata mzungu,tukamweleza hali halisi...tukaona mzungu hana sauti.

Nikamwambia boss wangu hapa hamna kazi,na draft resignation letter, tarehe moja nawapa.

Usiku wake mzungu ananiita ananionesha boss wangu kashamtumia email ya ku-resign. Kaniwahi.

Leo hapa nimeshaandika yangu....
Nawaza ni wakati gani wa kuituma.

Nataka niondoke kwa wema tu,
Tuki-resign sote kwa pamoja itaonekana lengo ni kuikomoa kampuni.



Sent from my SM-G975U using JamiiForums mobile app
Skilizia. Kwa kuwa ashajua unataka kusepa atakuwekea mambo flan flan sawa ili ukae kama anakuhitaji. So jipe muda kidogo uangalie upepo.
 
Siku hiyo tupo kikaoni manager akasema 'Kuna laptops mbili zimeibiwa kuna mtu kaonekana, hizo ni tabia za kiswahili tafadhali rudisha kabla hatujakuweka wazi' kuna jamaa hua nataniana naye tukaanza tupiana vijembe juu ya huo wizi.

Ilikua Ijumaa, J3 kufika naitwa na administrator pembeni yupo manager jamaa akaniambia "Hii ni kazi na sijaenda polisi kwakua sitaki tuharibiane kazi, CCTV imeona unaingia humu ofisini siku ambayo naamini laptops zilipotea" nilishikwa na hasira ya ghafla kwa sababu kuu moja;

Mimi siyo mwizi.

Hata iweje mimi kuiba kwangu ni haiwezekani.

Nikamuambia "Bro hiki unachonihisi nacho kwangu mimi hiki is very low, tuendelee nakusikiliza" akaniuliza kwanini ulitoka floor yako ukaja hii? Now hiyo siku hiyo reception ya floor yao ilikua inawekwa stika kuna mdada akaniachia funguo akaniambia nimsaidie kufunga mlango fundi akimaliza.

Hiyo siku liva alikua anacheza na vila na alikua anaogozwa, so nikatoka kupanda hiyo floor. Nilivyofika sikuingia rooms zingine nikawa nimekaa juu ya meza ya reception napiga stori na yule fundi jinsi gani liva imeshuka kiwango.

Rooms zilizo around pale sikuingia kwakua sina haja ya kuingia. Kisha yule fundi akasema ameshamaliza ndani kabakisha nje so nifunge tu mlango nisepe. Nikafunga mlango nikamuacha jamaa anamalizia kazi zake.

Nikamuambia huyu administrator. Mpigie fundi ili athibitishe ninachosema, akasema hawezi kumpigia kwakua CCTV inaniona mimi nimeingia ofisini (CCTV inaishia kwenye kordo) nikamjibu sasa hiyo ndiyo legit reason ya kumcheki fundi ili akutajie kilichofuata baada ya CCTV ilipoishia. Akagoma.

Akaniuliza "Sasa kama CCTV ishakuona wewe ungekua mimi ungefanyaje?" Nikamuuliza "Lini ulithibitisha kwamba hazipo?" Akajibu J5 nikauliza lini ulithibitisha kwamba laptops zipo akajibu Jmosi ambayo wewe ulionekana umepanda huku.

Nikamjibu "Mimi ningekua wewe ningeanza kuangalia footages za Jmosi, J3, J4 na J5 yenyewe" akaniuliza sasa huo si mzigo nikamjibu ni kweli ila hizo zote ni siku zenye probability ya mashine kupotea. Nikanotice kinachomsumbua sasa hivi ni ameona footage hiyo moja na anataka hiyo hiyo iwe ndiyo uthibitisho, nikamuambia sijachukua nataka umpigie fundi hutaki akajibu nilishampigia nimeongea naye.

Akili ikaniambia ikiwa aliongea na jamaa this means jamaa kamuambia ilivyokua na kanotice haiwezekani niwe nimechukua so ni anajaribu tu kutafuta pa kupeleka lawama (ikiwa kweli zimeibiwa). Akamuambia manager hata hivyo kuna footage nyingine sijaiangalia twende tukaione kwanza. Akaniambia atanipa feedback.

Next day nikamuuliza manager ikiwa walienda akajibu hapana. A week later nikauliza ikiwa walienda akajibu hapana, a week later mkataba ukaisha na haujawa renewed.
Aisee pole sana.
 
Habari za muda huu

Haya yalinikuta kwenye kazi yangu ya kwanza nilipokuwa bado sijafunzwa na Ulimwengu

1. Chuki ya kwanza nilijisababishia mwenyewe baada ya kutongoza wafanyakazi watatu kwa nyakati tofauti wote walichomoa na kumbe walihadithiana ndipo nikaanza kupitia sarakasi na vitimbi hadi nikaona Ofisi Ni chungu.

2. Chuki ya pili nilikuwa na mshkaji alikuwa anapenda kunitembelea, siku moja alikuta kifaa kinachofanana sana na cha Mradi wa Taasisi, akauliza tu friendly umekitoa wapi, nikamjibu nilinunua dukani. Kumbe alienda kumuambia boss kuwa nimeiba kifaa Cha Mradi! Boss na yeye mwanamke, badala ya kuniita na kunihoji, akachukua uamuzi wa kunipunguzia 75% ya majukumu ikwemo ya site kwa hoja ya kwamba nimekosa uaminifu(japo hakuniamba directly, ila aliongea kwa mafumbo).

3. Nilifiwa, wakateuliwa wawakilishi wa taasisi wanisindikize msibani, baada ya msiba wakarudi kuhadithiana Hali ngumu ya kijijini kwetu. Niliposikia kuwa wamehadithia, nikachukua uamuzi wa kumpiga makofi yule dada. Kumbe ilikuwa ni Mali ya Boss, boss akazidisha vitimbi Hadi nikaona nikubali yaishe nikaacha kazi.

Namshukuru Mungu nilipata kazi Nyingine ambayo Ndiyo naifanya Hadi Sasa. Jambo la Msingi nililojifunza ni PRIVACY& CONFIDENTIALITY Ni muhimu Sana wakati wa kujumuika na workmates. Lingine ni KUTOKUMUAMINI YEYOTE KWA WAKATI WOWOTE kwani sehemu kubwa ya Chuki na vita makazini husababishwa na mtu kuwa na DETAILS zako.

Karibuni tushirikishane matukio ya Chuki na Vita tulivyowahi kupitia kazini.

Unapoenda officin kumbuka wale ni work mates sio friends. Nilijifunza hiki kitu mapema mno maana yalinikuta
 
Back
Top Bottom