Uchaguzi 2020 Tuliosimamia Uchaguzi tukiri kuwa tumewatendea dhambi Watanzania kwa sababu ya kutii Mamlaka

Uchaguzi 2020 Tuliosimamia Uchaguzi tukiri kuwa tumewatendea dhambi Watanzania kwa sababu ya kutii Mamlaka

Amewanyima tu hao wapinzani ajira ya ubunge, udiwani na hata huo Urais! Ila upinzani hauwezi kufa kamwe. Hata ndani ya hicho chama chake, upinzani na makundi yatendelea tu kushamiri.

Yaani tumerudishwa enzi za Mwalimu! Hovyo kabisa.
Maamuzi ya walio wengi yaheshimiwe. Wananchi ndio wametaka chama kimoja kitawale baada ya kugundua waliowaamini waliwageuka na kujali matumbo yao zaidi kuliko wao waliowachagua. Kwa mfano, ilifika mahali mbowe alijiona mungu mtu ndani ya CHADEMA ikifika kipindi kama hiki cha uchaguzi anajichagulia tu wanawake anawatumia kingono kama kigezo cha kuwapa viti maalum. Ruzuku ya chama alikua anaitafuna anavyotaka bila kuulizwa na mtu, ukihoji unaitwa msaliti unafukuzwa kwenye chama. Mpaka sasa chama hakijafanya jambo lolote la maendeleo kutokana na ruzuku waliyokua wanapokea. Sasa kiburi kitamuisha, hana ubunge, chama kimepoteza uwakilishi bungeni, ruzuku haipo tena au itapungua kwa kiasi kikubwa sana.

Halikadhalika wabunge wa upinzani, baada ya kuchaguliwa hakuna jambo walilokua wanawafanyia wananchi zaidi ya kujijenga kimaisha wao na familia zao. Wakiulizwa kuhusu maendeleo, wanadai hiyo ni kazi ya Serikali, lakini Serikali hiyo hiyo ikifanya wanaibeza. Wananchi walichoka huu ulaghai, wameamua kuwapa lesson. Ukitaka kujua kwamba haya ni maamuzi ya wananchi, utaona ngome nyingi za upinzani ambazo zimechukuliwa na CCM hakuna malalamiko wala wananchi kugomea matokeo ina maana wanajua walichokifanya.

Kwahiyo, walioturudisha nyuma ni Wapinzani wenyewe kwa kuwadharau wananchi waliowapa imani na kuwachagua.
 
Mimi nilitenda haki na CHADEMA /upinzani wameshindwa kwa haki mf kwenye kituo changu kura za urais ccm kura171,CHADEMA kura 36,ubunge CCM kura 151,CHADEMA kura 67 na vituo vya majirani zangu pia CCM imeongoza kwa gape kubwa tu nadhani kuna kitu upinzani wajipange vzr kukifanyia kazi hasa vijijini, wenzao ccm wanamtaji mkubwa sana huko, ukijumlisha na mbwembwe zingine kama TASAF na ugawaji wa nguo za chama yaani huwaambii kitu vijijini.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nikiona comments kama hizi huwa sishangai maana ndiyo aina ya watanzania tulionao kwa sasa, hata pale ambapo jamaa zake, ndugu zake na jirani zake wameumizwa, kuuawa na kutiwa vilema, yeye kwake hamhusu na wala hajali kwa sababu yuko na walioshika mpini. Yuko tayari aweke kila aina ya uwongo, fitina na kejeli kwa watanzania wenzake eti tuu kwa sababu wao ni wapinzani.
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Mkuu hukuwaona walivyokuwa wanatukana juzi kati hapa
Nikikumbuka yale matusi ndio huwa nachoka kabisaa wamevuna walichopanda.

Congratulations in advance President Magufuli
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Na wewe tunafatilia kura yako ulimpigia nani! Ili tujuwe u-pamoja nasi au niaje!
Usihangaike ndugu nilifanya hivi
Urais CCM [emoji736]
Ubunge CCM [emoji736]
Udiwani CCM [emoji736]

Hivyo ndivyo nilivyofanya na kura zangu zote zimetiki.

Hongera CCM

Congratulations in advance President Magufuli
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Nikiona comments kama hizi huwa sishangai maana ndiyo aina ya watanzania tulionao kwa sasa, hata pale ambapo jamaa zake, ndugu zake na jirani zake wameumizwa, kuuawa na kutiwa vilema, yeye kwake hamhusu na wala hajali kwa sababu yuko na walioshika mpini. Yuko tayari aweke kila aina ya uwongo, fitina na kejeli kwa watanzania wenzake eti tuu kwa sababu wao ni wapinzani.
Sawa huo ndio mtazamo wako,lakini nikuhakishie mimi nilipiga kura ya mbunge na Raisi kwa upinzani na nilichoandika hapo ni uhalisia na sijakingia kifua serikali wala tume,nilichoandika ni uhalisia wa kituo changu kama kuna uchakachuzi ulifanyika ni ngazi zingine, ambazo mimi sikubahatika kuona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usihangaike ndugu nilifanya hivi
Urais CCM [emoji736]
Ubunge CCM [emoji736]
Udiwani CCM [emoji736]

Hivyo ndivyo nilivyofanya na kura zangu zote zimetiki.

Hongera CCM

Congratulations in advance President Magufuli
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
Hayo tutayajua baada ya kufatilia karatasi zako! au hukuona kuwa tumenakili namba za kitambulisho chako?
 
Hayo tutayajua baada ya kufatilia karatasi zako! au hukuona kuwa tumenakili namba za kitambulisho chako?
Umeshapoa kwa maumivu kwanza maana isije ikawa bado unapovu la kugaragazwa vibaya. Kura ni kwenye box la kura jipangeni upyaaa then tukutane 2025.

Congratulations in advance President Magufuli
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Katiba iliyopo watu wameshindwa kuitumia.

Magufuli kapiga marufuku mikutqno kinyume na katiba.

Hiyo mpya mkipewa halafu akaivunja hivyo hivyo, mtafanya kipi cha tofauti?

Mimi naona katiba mpya ni muhimu, ila mara nyingi inafanywa kuwa kisingizio tu.

Katiba haileti mabadiliko. Watu ndiyo huleta mabadiliko.

Sasa kama watu hawana muamko, katiba mpya utasaidiaje?
Umeandika vyema. Tatizo si katiba tatizo watu. Leo kuna braza mmoja aliniambia kwa mara ya kwanza kaipigia kura CCM maana walimpa Pesa.Pesa yenyewe sidhani kama inazidi elfu 20.
 
Walijipanga Sana isipokuwa kama mtoa mada alivyoonesha masikitiko yake, ilibidi watii mamlaka. Huenda kuna namna Ya maandalizi yanapaswa kuanza kufanyika sasa kuelekea 2025
Jinsi inavyoonyesha ni kama CCM ndiyo yenye hati miliki ya nchi hii, hivyo ni vigumu kushindana kati ya wananchi na wenye nchi. Lakini ukiondoa paka nyumbani, subiri uharibifu wa panya ndani.
 
Umeshapoa kwa maumivu kwanza maana isije ikawa bado unapovu la kugaragazwa vibaya. Kura ni kwenye box la kura jipangeni upyaaa then tukutane 2025.

Congratulations in advance President Magufuli
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
Haahhahah hakuna povu! kwani mwenye kura nyingi asipotangazwa na tume huyo si mteule!! So haijalishi idadi ya kura ila atangazae ametimizaje maagizo toka juu
 
Hayo mliyoyafanya wala sio mapya ktk ulimwengu wa mashetani yamefanywa na wengi tu ila walivuna waliyopanda, subirini mavuno yenu mtalipwa hapa hapa duniani
Hatuna cha kueleza sisi tuliosimamia Uchaguzi tutabaki nafsi zikituuma lakini tulitii mamlaka zilizokuwa juu yetu.

Mkakati kuanzia juu mpaka chini kabisa kwenye ngazi ya mwisho mkakati ulitekelezwa na watendaji wakatimiza.

Narudia tena, ogopa mamlaka iliyoko juu yako. Tulifanya serikali za mitaa na tumemalizia uchaguzi mkuu.

Lazima kibaki chama kimoja kwa mujibu wa kauli za mamlaka, sasa wewe mtu mmoja unaanzaje kupinga?

Ili haya yote yaishe ni Katiba Mpya vingnevyo upinzani usahau kabisaaa uchaguzi huru.
 
Maafisa vipenyo walinikalia kooni nikakumbuka nina watoto wadogo bado wanamuhitaji baba yao ikabidi nibadilishe tarakaimu ya chini iende juu ya juu iende chini. Moyo unauma Ila hamna namna na nimefanya toba kwa Hilo.
Wewe ni mtu mzuri nami namsihi mungu wangu akusamehe
 
Naomba namba ya simu ya Mh. Hashim Rungwe aka mzee wa ubwabwa na kuku wa kienyeji nataka nimpongeze na nimchangie gunia moja la mpunga wa hapa Kyela. Alipotangaza wali na kuku wa kienyeji kasababisha kuku wa kienyeji wamepanda bei. Naombeni comedian mumshirikishe hata part moja tu katika filamu zenu.
Kwa hiyo kwio sasa wameshakuwa anasa?
 
Katiba iliyopo watu wameshindwa kuitumia.

Magufuli kapiga marufuku mikutqno kinyume na katiba.

Hiyo mpya mkipewa halafu akaivunja hivyo hivyo, mtafanya kipi cha tofauti?

Mimi naona katiba mpya ni muhimu, ila mara nyingi inafanywa kuwa kisingizio tu.

Katiba haileti mabadiliko. Watu ndiyo huleta mabadiliko.

Sasa kama watu hawana muamko, katiba mpya utasaidiaje?
Uko makini mkuu .kenya mwamko mkubwa balaa wanasiasa ndo wanaogopa wananchi
 
Back
Top Bottom