Uchaguzi 2020 Tuliosimamia Uchaguzi tukiri kuwa tumewatendea dhambi Watanzania kwa sababu ya kutii Mamlaka

Uchaguzi 2020 Tuliosimamia Uchaguzi tukiri kuwa tumewatendea dhambi Watanzania kwa sababu ya kutii Mamlaka

Naomba namba ya simu ya Mh. Hashim Rungwe aka mzee wa ubwabwa na kuku wa kienyeji nataka nimpongeze na nimchangie gunia moja la mpunga wa hapa Kyela. Alipotangaza wali na kuku wa kienyeji kasababisha kuku wa kienyeji wamepanda bei. Naombeni comedian mumshirikishe hata part moja tu katika filamu zenu.
 
Hahahaaaaaa, kama ni utamu au uchungu tutausikia wote pasipo kujali kama ulimpigia kura nani. Dunia nzuri sana na tutaelewana. Hongera Mh. Rais wa JMT Dokta John Pombe Joseph Magufuli kwa ushindi wa kishindo.Hakuna ufalme na mamlaka itakayodumu milele, yote yana mwisho Duniani kote.
 
Hongera ndugu kwa kusema ukweli nakushauri pia uende kutubu kwa ajili yako ili usiwe mmoja wa washiriki wa hii dhambi na uovu huu mkubwa uliofanyika mbele ya uso wa Mungu.
Alisema alishatubu. Maisha yanaendelea
 
Katiba iliyopo watu wameshindwa kuitumia.

Magufuli kapiga marufuku mikutqno kinyume na katiba.

Hiyo mpya mkipewa halafu akaivunja hivyo hivyo, mtafanya kipi cha tofauti?

Mimi naona katiba mpya ni muhimu, ila mara nyingi inafanywa kuwa kisingizio tu.

Katiba haileti mabadiliko. Watu ndiyo huleta mabadiliko.

Sasa kama watu hawana muamko, katiba mpya utasaidiaje?
Watanzania wengi sana bado hawana akili na jana limenitokea na nimethibitisha kuwa wengi wetu hawana akili.
 
Majuto ni mjukuu. Sasa mmeturudisha kwenye utawala wa Chama Kimoja. Sio peke yenu. Hata mawakala wa vyama vya upinzani wamechangia haya

Magufuli atasema ameshinda ila CCM na TANZANIA kwa ujumla tumepoteza
KUHUSU mawakala waondolee dhambi kwani wengi walikuwa na akili ya Hali ya juu.
Baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika mawakala wengi walitaka wahesabu kwanza vibutu zilikochanwa kura ili wajue wapiga kura NI wangapi then ndo wahesabu kura msimamiz anakataa na kupiga simu police station eti kituo hiki kina fujo polisi wanakuja wanachukua msimamizi na mabox na kutokomea kusikojulikana na kumwacha wakala pale hajui la kufanya mbaya ZAIDI waliambiwa wasiwe na simu
 
Napata uchungu sana pale napokumbuka kuwa vyama vinatumia gharama kubwa sana kufanya kampeni, mfano kukodi chopa sio pesa ndogo! Pia gharama hizi kuna nyingine zinalipwa cash na nyingine yanakuwa ni makubaliano ya kuja kulipa baadae uchaguzi kupitia mafanikio ambayo chama kitayapata!
Sasa inapotokea mafanikio tarajiwa ya chama yakahujumiwa tena pakubwa kama hivi, kiukweli ni hasara sana!
Bora uingie hasara ambayo unajua kabisa kwamba umeisababisha mwenyewe lakini sio hasara ya kusababishiwa na mtu tena katika mazingira ya kulazmisha!
Mwenyezi Mungu akawafariji na kuwarudishia pale walipopungukiwa wale wote walioingizwa hasara za kulazmishwa!
Pia akawalipe mshahara wao wale wote waliohusika kuumiza wenzao! Naamini Mungu wetu ana macho anaona mpaka ya sirini!
 
CHADEMA kwishney
maneno ya Bashiru yakutumia dola kushinda uchaguzi yametimia
siku zote tumesema kuwa CCM ndiyo dola hamkuamini
 
Shida inaanzia hapo sasa. Kwanini hawakupewa barua? Kwanini walisubiri mpaka siku ya Uchaguzi then wakaibukia pale bila barua? Yaani sehemu nyingi Upinzani ulijiandaa/uliandaliwa kupigwa mapema.

Mambo ni mengi sana ya kujifunza na kuchukua hatua. 2025 sio mbali sana.
Mawakala waliambiwa hawatopewa barua za utambulisho baada ya kuapa bali tume yenyewe ndo itapeleka barua kwa wasimamizi wa vituo. Kua sehemu nyingine tume ilipeleka na sehemu nyingine haikupeleka kabisa. Na huwezi kuipangia tume
 
Watanzania tunajua CCM imeshinda kwa kishindo, hayo mengine mtajua wenyewe na mtahukumiwa kila mtu kwa wakati wake.
 
Hatuna cha kueleza sisi tuliosimamia Uchaguzi tutabaki nafsi zikituuma lakini tulitii mamlaka zilizokuwa juu yetu.

Mkakati kuanzia juu mpaka chini kabisaa kwenye ngazi ya mwisho mkakati ulitekelezwa na watendaji wakatimiza.

Narudia tena, ogopa mamlaka iliyoko juu yako. Tulifanya serikali za mitaa na tumemalizia uchaguzi mkuu.

Lazima kibaki chama kimoja kwa mujibu wa kauli za mamlaka, sasa wewe mtu mmoja unaanzaje kupinga?

Ili haya yote yaishe ni Katiba Mpya vingnevyo upinzani usahau kabisaaa uchaguzi huru.

Ndio maana wazungu wanatufananisha na wanyama sisi Wafrika

Ishu ilikuwa ndogo Sana, pale pale bungeni wangechange tu inchi ikawa ya chama kimoja, why tumetumia mapesa kibaaaaaaaaaao kwa kitu ambacho majibu yake tayari yalikuwa yamepatikana

No wonder hata wenyewe CCM wako kimya usikii hata kelele
 
Back
Top Bottom