Tuliowahi kuchukua mikopo tukafanya ndivyo sivyo

Tuliowahi kuchukua mikopo tukafanya ndivyo sivyo

Nimemaliza chuo mwaka jana imefika wakati n nimeamin mtaji ndo changamoto kwangu lkn nikahisi bank anaweza kuwa mkombozi wangu lkn kwa uzi huu nimekuwa mwoga ghafla mpaka kichwa kinaniuma dah
Sikushauri kuchukua mkopo kwajili ya kuanzisha biashara mfumo wa biashara kwa sasa si mzuri labdaniwe kwajili ya kuendeleza au kukuza
 
Huu uzi nimeuona punde tu ulivyo anzishwa lakin nilisita kuchangia kutokana na maswahibu yaliyo nipata...Mikopo ilinifanya mpaka nikaathirika kisaikolojia...ingawa bado sija recover....nimeona nisitia neno kwanza...nijipe mda kidogo niweze kusahau...nilichanganyikiwa kweli kweli...ilifikia hatua hata bara bara ya vumbi navushwa na watoto wadogo....Mweh..Ndugu zangu kuwen makini na mikopo...na hiz banks za Tz nyingi ni wafanya biashara sidhan kama zina malengo ya kumnufaisha mkopaji...zina interest kubwa...kiasi kwamba lazma uwe makin sna..
Mkuu stori yako unasikitisha, ila umetubania sisi tuweze jifunza.
Ila umenichekesha sana,
 
Nilichukua mkopo 2010, 2ml nmb kwa miaka mitatu. Nikaingiza shambani kule babati Manyara kilimo cha alizeti. Nikalima ekari 20. Nilipovuna nikakamua mafuta nikapata 450000. Tangu siku hiyo kilimo na mimi hapa dunia baibai, labda kama na mbinguni kipo itakuwa kesi nyingine.
 
sikushauri kuchukua mkopo kwajili ya kuanzisha biashara mfumo wa biashara kwa sasa si mzuri labdaniwe kwajili ya kuendeleza au kukuza
Acha kukata tamaa kama nao pambana na serekali upate chako huwezi kuishi good life na kujifunza mambo mengi ukijifungia chumban na serekali haiwez kukpa msamaha wa kodi hata siku moja
Uoga wako ndio umaskini wako
 
Na mwakani nachukua pesa nyingine kama 10 MLS. Hivi nifanye mambo coz nimeshajua wap nilikosea so i jst wanna correct my mistakes so tuzidi kuombeana ntawaletea feedback hapa hapa jukwani waoga endeleeni hivyo hivyo kujifungia chumbani
 
Nimepitia kwa makini sana michango ya wachangiaji wengi kwenye uzi huu.

Kutokana na uzoefu wangu na wachangiaji wengine, kukopa pesa ufanye biashara ikisimamiwa na ndugu au rafiki ni kujitakia kuishi kama shetani.

Watu hutofautiana uwezo na access ya kukopa. Wengine humu nimeona wanauwezo wa kukopeshwa million 10 wengine 20 na wengine mpaka million 200.

Kwenu nyinyi wenzangu tunaoweza kukopeshwa chini ya million 10, hakikisheni kama ndio kwanza tunanza kukopa kwa ajili ya kuanzisha biashara basi tubuni biashara inayoweza anza kwa mkopo ambao unaweza kuulipa kwa kipindi cha mwaka 1 tu deni liwe limeisha. Hii husaidia kupunguza ukubwa wa riba na hata ikitokea biashara imekufa muda wa kusota huwa mfupi sana.

Binafsi huwa na ndoto ya kuwa na mtaji wa hata million 50 lakini hujiambia biashara kubwa kiasi hicho sharti izaliwe na biashara nyingine ndogo niliyo ikopea kwa makato ya mwaka mmoja tu na si vinginevyo.

Kama hatuwezi kuanzisha biashara kwa makato ya mwaka mmoja tu basi hata tukikopa mapesa mengi ya kukatwa mika 4 biashara hiyo haiwezi fanikiwa.

Kama unataka kopa pesa kununua bodaboda ya biashara si kitu kibaya, ila jipime kwanza kama wewe mwenyewe utakuwa tayari kuipigia kazi in case madereva wanakusumbua alafu ukisha kuwa na bodaboda weka mashaliti magumu kwa dereva unayetaka kumkabidhi hasa juu ya upotevu kama itatokea.

Madereva wengi hupoteza bodaboda kizembe sana hivyo ni bora muandikishiane namna atakavyo wajibika kuilipa iwapo itatokea upotevu wowote ule na kama hajiwezi kabisa basi awe na mdhamini wake. Kumkabidhi mtu pikipiki bila mkataba ni sawa na kutupa pesa chooni.

Binasfi niko mbioni kwenda kopa pesa kununua bodaboda ya biashara lakini kama nitakosa dereva wa uhakika wa kumkabidhi mimi mwenyewe nitaingia barabarani kama ufanisi wangu wa kazi nilikoajiliwa utadhorota kutokana na mimi kwenda kazini nimechoka poa tu sito jali hilo maadam nisipopambana na hali yangu hakuna wa kunisaidia dunia hii.
Asante
 
Ila nimepitia post nzima naona kila aliyechukua kapata matatizo nataka kujua naomba je m50 wanataka ngapi kwa mwezi na kwa muda gani je wanamuda walioupanga mfano lazima miaka 5 tu au unaweza kuchukua muda mrefu nahitaji ufafanunuzi zaidi kabla sijaingia kwenye deni naogopa sana madeni
Kwa mwaka kwa huo mkopo utarudisha sio chini ya 6m kwa kila mwezi sasa wew kodi kwa mwak ni 2.5M utalipaje hilo deni kama sio kuja kuuza kabisa hiyo nyumba kwa bei ya hasara na ili kulipia deni lako
 
Ila mishahara wanaolipwa wachezaji hauna siri!hivi kwa nn?
Kumbuka teams ni brands na wanashindana na wengine kupata wachezaji bora hivyo kuitangaza mishahara ya play makers wao ikiwa mikubwa ni kujibrand kwa mashabiki na wawekezaji sasa mie mjasiriamali unataka ujue kipato changu eti nikuwekee wazi how come??!!
 
Nilichukua mkopo 2010, 2ml nmb kwa miaka mitatu. Nikaingiza shambani kule babati Manyara kilimo cha alizeti. Nikalima ekari 20. Nilipovuna nikakamua mafuta nikapata 450000. Tangu siku hiyo kilimo na mimi hapa dunia baibai, labda kama na mbinguni kipo itakuwa kesi nyingine.
Hahahahaaa mkuu nimecheka hadi watu wameniangalia kwenye mwendokac. Mie nilkopa 1.5m nikampadogo awe anatoa beg Uganda auze bukoba maana aliniambia inalipa sana. Mimi nikamwambiaje kwa mwez awe anantumia 100000 tu. Dah alintumia mwez mmojatu hadi saiv kuanzia mwaka2014 .
 
kwa mwaka kwa huo mkopo utarudisha sio chini ya 6m kwa kila mwezi sasa wew kodi kwa mwak ni 2.5M utalipaje hilo deni kama sio kuja kuuza kabisa hiyo nyumba kwa bei ya hasara na ili kulipia deni lako

So mwaka Ni Kwa mwezi Kodi m2.5 Ni gorofa Na like maeneo mazuri imefanywa ofisi Na wazungu Nataka kujua Kwa mwezi nalipia ngapi
 
Habar wapendwa humu Jf

Bila kupoteza muda katika pulukushan za maisha kuwa magumu kuna wakati unaona the only solutions ni kuchukua mkopo katika taasis za fedha mbalimbali ili kufungua ofisi nyingine itakayo kuingizia kipato zaidi
Ila cha kushangaza sasa unakuta tunaa ngukia pua na maisha kuwa tete zaidi ya hapo nyuma ilivyokuwa
Mfano ni mm
2013 nilikopa 5mls kwenye bank ya Nmb kwa muda wa miaka 4 ambapo nlipanga kufungua biashra zangu mjini ili sister angu ndio azisimamie huko town basi nkaongea nae akanipa michongo yake ya biashra za mahindi zinavyomlipa anatoa mahindi Dodoma anapeleka Dar.
Akaniambia mm ntakuwa napata laki 300000 kila atakapo uza Mzigo at the same time my capital remain costant mim nkachukulia kama biashara ndio hivyo basi ntatengeneza pesa ndefu fun ndani ya muda mfupi coz ndan ya mwezi anaenda kufunga Mzigo Mara 3
Nkamtumia 4.5mls kwa acc. Ile laki tano kama kawa nkaitia kibiriti na Toto's za mjini nkajua after 1 week ntaanza kupokea pesa zangu za faida
Hapo salary nlikuwa napokea 190000 net baada ya makato tote
Kumbe nae sister ndio kawa tycoon wa mjini anaztumbua pesa tu na vibwana vyake mpaka na kuja kumpigia simy vp mbona kimya hunitumii ile pesa yan amelewa haezi hata kuongea
Nkampigia Kesho yake eti akaniambia aliibiwa pesa yote na hapo alipo amebakiwa na lak3 tu na ndio anataka alipe kodi ili asifukuzwe kwenye chumba alichopanga
Nlikaaa chini bado nusu nilie ila nkajikaza kiume namshukuru mungu nlikuwa sina mke wala mtoto
Maisha yakawa magumu zaidi loan board walipo anza kunikata nkawa sasa kutoka 190000 nkawa napokea salary 135000 na madeni yalikuwa yameniabdama sana sikuona raha ya kufanya kazi coz nlishidwa kumsaidia MTU yeyote nyumban sio baba waka mama wala ndugu yeyote
Mungu sio wew wala mm mwaka huku deni likaisha na namshukuru mungu naishi maisha ya furaha na mwaka huu ntaenda nyumban kuwasalimia since 2012 sijawah kwenda kabisa .

Kwa wale mliochukua mikopo jaman kuweni makini na Yale mtakayoenda kufanya msije mkachanyikiwa mkatamani kujinyonga kama mm.
Wish u marry X-mas
And
Happy new year 2018
Mkuu,hayo yametokea wengi hasa kipindi hiki vyuma vikiendelea kukaza. Mmoja alinisimulia aifanya mchezo unafanana na huo. Huyu,alikimbia na hela,akatafutwa miezi minne ndo akapatikana. Duh,ilikuwa seleka acha kabisa. Alimtupa ndani,akampeleka kwa court,amefungwa mwaka na nusu,na akitoka alipe pesa zote.
 
Ila nimepitia post nzima naona kila aliyechukua kapata matatizo nataka kujua naomba je m50 wanataka ngapi kwa mwezi na kwa muda gani je wanamuda walioupanga mfano lazima miaka 5 tu au unaweza kuchukua muda mrefu nahitaji ufafanunuzi zaidi kabla sijaingia kwenye deni naogopa sana madeni
Mkuu mbali na hiyo nyumba kama dhamana,watataka uwe na biashara yenye mzunguko was kuonyesha unaweza kulipa hiyo mil 50,wanachoangalia sana sio dhamana,in uwezo wa biashara kuwalipa maana wao hawana nia ya kuuza mali yako.
 
Back
Top Bottom