Tuliowahi kuchukua mikopo tukafanya ndivyo sivyo

Tuliowahi kuchukua mikopo tukafanya ndivyo sivyo

Mimi nilikopa mwaka jana NMB Mi. 9 kwa miaka mitano. Nikachukua pikipiki mbili. Moja ya bodaboda na nyingine ya kwangu kutembelea. Mil.4 nikachukua kiwanja na shamba kwa ajili ya kilimo. Laki 5 nikalimisha shmaba na kupanda mahindi na laki tano nikafanyia mambo yangu menginene. Mshahara nikabaki 247,000

Matokeo yake;

i)Bodaboda ilidumu miezi sita ikaibiwa.
ii) mahindi sikupata hata nusu gunia,kwa sababu ya ukame.
iii)mipango yangu ilikuwa mwaka huu nioe kama mambo yangeenda vizur kinyume chake nimeshindwa,mchumba wangu alipoona hali imekuwa tete akaanza visa kumbe kashaanza mahusiano na mwanaume mwingine,nikabaki mimi kama mimi.
iv)Baada ya bodi ya mkopo kuanza kukata 15% nikaanza kuchukua 197,000/= kwa mwezi
v) kwa sasa siwezi saidia chochote kwa mama na ndugu zangu kibaya zaidi mdogo wangu kachaguliwa chuo cha afya diploma ada mil.2. 5 sijaweza kumpa hata mia.

Sina bahati kabisa
Pole sana.
 
Mimi nilikopa mwaka jana NMB Mi. 9 kwa miaka mitano. Nikachukua pikipiki mbili. Moja ya bodaboda na nyingine ya kwangu kutembelea. Mil.4 nikachukua kiwanja na shamba kwa ajili ya kilimo. Laki 5 nikalimisha shmaba na kupanda mahindi na laki tano nikafanyia mambo yangu menginene. Mshahara nikabaki 247,000

Matokeo yake;

i)Bodaboda ilidumu miezi sita ikaibiwa.
ii) mahindi sikupata hata nusu gunia,kwa sababu ya ukame.
iii)mipango yangu ilikuwa mwaka huu nioe kama mambo yangeenda vizur kinyume chake nimeshindwa,mchumba wangu alipoona hali imekuwa tete akaanza visa kumbe kashaanza mahusiano na mwanaume mwingine,nikabaki mimi kama mimi.
iv)Baada ya bodi ya mkopo kuanza kukata 15% nikaanza kuchukua 197,000/= kwa mwezi
v) kwa sasa siwezi saidia chochote kwa mama na ndugu zangu kibaya zaidi mdogo wangu kachaguliwa chuo cha afya diploma ada mil.2. 5 sijaweza kumpa hata mia.

Sina bahati kabisa
Pole sana.
 
Mimi nimechukua mwaka huu, lakini ni wa mwaka mmoja. Mwezi wa tatu namaliza deni. Nilichukua ninunue boda boda lakini huyu jamaa niliyempa boda boda badala ya kuleta hela analeta stories. Yaani najuta kwanini nilichukua. Kuna wakati natamani niichukue halafu nipige bei ili nikalipe deni lililosalia lakini nahofia jamaa ni Kachawi kweli na baba yake nadhani ni msaidizi wa Lucifer mwenyewe, asije akanifanya mbaya bure! Basi najikaza kiume hivyo hivyo
Haah unaogopa nn wakati ni pikipiki yako.
 
Mwenzenu mi kabla sijachukua mkopo baba alinishauri niwe natuma pesa kwa ajili ya kupata kiwanja na ujenzi baadae, sasa kidume nikajipinda, kila mwezi nilikua natuma laki mbili na yeye aliniambia kiwanja kinauzwa M2. Sasa miezi ilikatika naulizia kiwanja najibiwa pesa hazijatimia hahaha ikabidi nimuulize mama, jibu ni kwamba "Pesa zinatafutiwa mchele ila kapanga akipata pesa atakuja kukufanyia maarifa" duh! Nilikata tamaa ya kiwanja ilikua mwaka 2013. Hiyo ya kwanza;

Ya pili, ilikua mwaka 2015 nilichukua mkopo wa M13, milioni 6 nilizivuruga sikujua hata nilitumia nini, zilizobakia nilimtumie baba aninunulie kiwanja na kupiga japo foundation. Na hapa niliula na chuya, alinunua kiwanja chenye foundation zilizobakia akamalizia nyumba yake nikaahidiwa deni kwamba atakuja kunilipa, ila baba ni baba siwezi kumdai tena na najua silipwi kala mali yake mwenyewe.

Mwisho kuna mpango mwengine nataka nije nifanye kwa siri halafu nine nikwambie, mpango wenyewe ni kuja kununua japo banda la M25 maana nikimshirikisha atakuja kunilamba tena.
 
Alikili zako pia haziwez kukusaidia asa sijui iyo kaz unafanyaje, toka lini na wapi umeona biashara binafsi unafanyiwa na mtu haupo makini wewe ni mzembe.
 
Nilichojifunza mimi,usikope ili kununua kiwanja au kujenga nyumba ambayo haizalishi bali kopa na wekeza kwenye kitu kitakachokuwa kinazalisha ili mkopo ujilipe wenyewe
Ndo hapo sasa kwakuwa ni mtumishi unawekeza unamuweka msimamizi anakuingiza mjini mchana kweupeee
 
Nimepitia kwa makini sana michango ya wachangiaji wengi kwenye uzi huu.

Kutokana na uzoefu wangu na wachangiaji wengine, kukopa pesa ufanye biashara ikisimamiwa na ndugu au rafiki ni kujitakia kuishi kama shetani.

Watu hutofautiana uwezo na access ya kukopa. Wengine humu nimeona wanauwezo wa kukopeshwa million 10 wengine 20 na wengine mpaka million 200.

Kwenu nyinyi wenzangu tunaoweza kukopeshwa chini ya million 10, hakikisheni kama ndio kwanza tunanza kukopa kwa ajili ya kuanzisha biashara basi tubuni biashara inayoweza anza kwa mkopo ambao unaweza kuulipa kwa kipindi cha mwaka 1 tu deni liwe limeisha. Hii husaidia kupunguza ukubwa wa riba na hata ikitokea biashara imekufa muda wa kusota huwa mfupi sana.

Binafsi huwa na ndoto ya kuwa na mtaji wa hata million 50 lakini hujiambia biashara kubwa kiasi hicho sharti izaliwe na biashara nyingine ndogo niliyo ikopea kwa makato ya mwaka mmoja tu na si vinginevyo.

Kama hatuwezi kuanzisha biashara kwa makato ya mwaka mmoja tu basi hata tukikopa mapesa mengi ya kukatwa mika 4 biashara hiyo haiwezi fanikiwa.

Kama unataka kopa pesa kununua bodaboda ya biashara si kitu kibaya, ila jipime kwanza kama wewe mwenyewe utakuwa tayari kuipigia kazi in case madereva wanakusumbua alafu ukisha kuwa na bodaboda weka mashaliti magumu kwa dereva unayetaka kumkabidhi hasa juu ya upotevu kama itatokea.

Madereva wengi hupoteza bodaboda kizembe sana hivyo ni bora muandikishiane namna atakavyo wajibika kuilipa iwapo itatokea upotevu wowote ule na kama hajiwezi kabisa basi awe na mdhamini wake. Kumkabidhi mtu pikipiki bila mkataba ni sawa na kutupa pesa chooni.

Binasfi niko mbioni kwenda kopa pesa kununua bodaboda ya biashara lakini kama nitakosa dereva wa uhakika wa kumkabidhi mimi mwenyewe nitaingia barabarani kama ufanisi wangu wa kazi nilikoajiliwa utadhorota kutokana na mimi kwenda kazini nimechoka poa tu sito jali hilo maadam nisipopambana na hali yangu hakuna wa kunisaidia dunia hii.
 
Eti mkuu kuna nyingine ipo FB wanajiita VICOBA FOCUS.

Wanatangaza unaweza kukopa kuanzia 5m-10m kupitia hiyo app yao kwa kujaza fomu inayopatikana FB na kutakiwa ulipe amana ambayo ni10% ya mkopo unaohitaji.

Naomba kuthibitishiwa huo mkopo kweli upo? Maana nina shida ya kuongeza mtaji kama 2m hivi.
Hao ni matapeli mkuu.
 
Mimi nilikopa mwaka jana NMB Mi. 9 kwa miaka mitano. Nikachukua pikipiki mbili. Moja ya bodaboda na nyingine ya kwangu kutembelea. Mil.4 nikachukua kiwanja na shamba kwa ajili ya kilimo. Laki 5 nikalimisha shmaba na kupanda mahindi na laki tano nikafanyia mambo yangu menginene. Mshahara nikabaki 247,000

Matokeo yake;

i)Bodaboda ilidumu miezi sita ikaibiwa.
ii) mahindi sikupata hata nusu gunia,kwa sababu ya ukame.
iii)mipango yangu ilikuwa mwaka huu nioe kama mambo yangeenda vizur kinyume chake nimeshindwa,mchumba wangu alipoona hali imekuwa tete akaanza visa kumbe kashaanza mahusiano na mwanaume mwingine,nikabaki mimi kama mimi.
iv)Baada ya bodi ya mkopo kuanza kukata 15% nikaanza kuchukua 197,000/= kwa mwezi
v) kwa sasa siwezi saidia chochote kwa mama na ndugu zangu kibaya zaidi mdogo wangu kachaguliwa chuo cha afya diploma ada mil.2. 5 sijaweza kumpa hata mia.

Sina bahati kabisa
Pole mkuu umenisikitisha ulivyomalizia hapo mwisho. Endelea kupambana
 
Yan habar hiyo isikie tu kwa mwenko
Kina jamaa alikuwa ughaibuni huko akawa anamtumia baba yake pesa amjengee nyumba na Raman akamtumia
Jamaa akarudi kumuulisa mshua nyumba iko WAP hamna nyumba ndio kwanza amechimba msingi na alishatafuna kama 75mls.

Sasa kama ndio ww utamfunga mzee wako au
Jamaa ucku ule ule aligeuka wakaenda kulala kwa hitel keshokesho yake hao Japan na mkewe
Kama yaliyonikuta dogo alilukuwa anaishi nikawa natuma hela za kula na kulipia fundi na vifaa ili nikienda nikute mjengo umekamilika.baada ya miaka 3 nikaenda kwa wife na watoto nikijua nafikia kwangu.sikukuta cha mjengo hata tofali moja.

Hasira nilizonazo nilimweka ndani dogo cha kushanganza mother akaja polisi na kuwaambia kwamba yeye ndio alimwambia dogo watumie hizo kwa matumizi mengine kwa sababu mie nakula raha mjini na Huyo mwanamke niliyenaye hivyo kama kuwekwa ndani awekwe yeye dogo atolewe.

Sikuwa na la ziada zaidi ya kuondoka ukizingatia hizo pesa tulikuwa tunachanga na wife wote tulikuwa wafanyakazi uamizi niliofanya ni kujenga ukweni ambao hawakuwa na mchezo mchafu kama wa kwetu SAA hizo kunibeza na kunilaumu nitajengaje ukweni inaonekana nimelishwa dawa
 
Mimi nilikopa mwaka jana NMB Mi. 9 kwa miaka mitano. Nikachukua pikipiki mbili. Moja ya bodaboda na nyingine ya kwangu kutembelea. Mil.4 nikachukua kiwanja na shamba kwa ajili ya kilimo. Laki 5 nikalimisha shmaba na kupanda mahindi na laki tano nikafanyia mambo yangu menginene. Mshahara nikabaki 247,000

Matokeo yake;

i)Bodaboda ilidumu miezi sita ikaibiwa.
ii) mahindi sikupata hata nusu gunia,kwa sababu ya ukame.
iii)mipango yangu ilikuwa mwaka huu nioe kama mambo yangeenda vizur kinyume chake nimeshindwa,mchumba wangu alipoona hali imekuwa tete akaanza visa kumbe kashaanza mahusiano na mwanaume mwingine,nikabaki mimi kama mimi.
iv)Baada ya bodi ya mkopo kuanza kukata 15% nikaanza kuchukua 197,000/= kwa mwezi
v) kwa sasa siwezi saidia chochote kwa mama na ndugu zangu kibaya zaidi mdogo wangu kachaguliwa chuo cha afya diploma ada mil.2. 5 sijaweza kumpa hata mia.

Sina bahati kabisa
Duuh pole sana kijana mwenzangu
 
Back
Top Bottom