Tuliowahi kufukuzwa kwa watu/kwa ndugu tukumbushiane ilikuwaje

aisee, ulikua jasiri mnoo, safi sana
 
Kuna vitu Sisi wakaa kwa watu tunakosea sana, tabia za kununa na uvivu zinachangia kuchokwa haraka.
Kuna kisa kimoja hivi, ndugu wa mume akiwa kidato cha 3 alifikiaa kwa kaka yake, akawa hatoki ndani, yani asubuhi anaamka, anaoga, anarudi ndani, au sebuleni.. Yani yeye hana haya mtoto akilia sio jukumu lake, sawa watoto wako kwenye umri wa kujinyea sasa, mtoto akijinyea sebuleni yy anakimbilia chumbani( sasa km huwezi kumsaidia si umuite MTU!) Jamani muda wa kula anaenda kulala ukimtuma mtoto aende kumwamsha haamki. Hadi uende wewe!!! Sasa haya niliona kwa rafiki yangu.... Ila alijitahidi sana kuishi nae!!
 
BORA ulivyofukuzwa mkuu,ungeendelea kutegemea Ndugu ungekuwa masikini hata hela ya kununua bando ungekosa.
 
Hizo tabia zinakera sana mkuu
Sijui watu wa hivi huwa wana matatizo gani ya akili
Anatengeneza mazingira kama mnamnyanyasa.
Unakuta familia nzima mpo sebureni mnakula ila yeye yupo huko chumbani peke yake

Mara nyingi ni ndugu za sisi wanaume.
 
Aisee!!
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Umesema kweli mkuu, na ukifatilia hao wanaofanikiwa baada ya kulelewa/kusaidiwa na ndugu wengi wao hawanaga moyo wa kusaidia hata ndugu zao!
Kuna lijamaa na dada yake yalisomeshwa na mzee baba, ila saivi ukiliomba hata elfu kumi kuipata sio rahisi. Yani hua nawaangalia nashangaa sana ni wagumu balaa kusaidia ila wao walisaidiwa daaah
 
kwa niaba ya wale ambao hatujawahi kuishi kwa ndugu au kufukuzwa, nawapa pole wote mliowahi kukumbwa na kufukuzwa.
 
Kuna lijamaa na dada yake yalisomeshwa na mzee baba, ila saivi ukiliomba hata elfu kumi kuipata sio rahisi. Yani hua nawaangalia nashangaa sana ni wagumu balaa kusaidia ila wao walisaidiwa daaah
bora kusaidia wapita njia kuliko.ndugu
 
Kwahy mkuu umefurah uncle kutmulw kazi
 
Sie tupo wawili mimi ni mdogo wangu wakike mzee baada ya kuzaliwa tu miaka mitatu baadae akamtelekeza bumkubwa,siyo wa sabuni wala chupi,wakati huo bimkubwa akiwa hana nyumba wala kazi yoyote bali akiuza tu tuvitenge na shuka za kigoma,huku akiwa anaumwa ugonjwa wa sicle cell,ambao ilikuwa kila week lazma apigwe chupa za damu,the best moment ambayo sitaisahau katika maisha yangu ni kumbeba mama yangu mgongoni kwangu na kumpeleka hospitali hata usiku wa manane na kumrudisha enzi hizo ilikuwa gari mkoa mzima hazifiki hata 100 kwa idadi.vijibiashara vyake mwwnyewe akawa hivyo hvyo pamoja na kupata sent ndogo ndugu zake wakawa wanawaleta watoto zao akae nao na yeye alikuwa ni mtu wa watu akawa anaishi nao kama watoto zake nakumbuka hata nguo za skukuu walikuwa wanaanza kununuliwa wao the ndo sie tunafata,kimbembe kinaanza baada ya bumkubwa kufariki kwa sicle cell,hivyo kutufanya kulelewa na ndugu zake.nakumbuka wenyewe tuko shule ya msingi tunabebeshwa mgongoni wajukuu wa mtoto wa mama yangu mdogo mgongoni,kila wakija asubuhi na kuwarudisha nyumbani kwao jioni,kwenye chakula wao watakula chipsi kinachobakia(makombo ndo mnapewa nyinyi),na hata upande wa nguo ile nguo ambayo wameshaivaa na kuichoka ndizo ambazo huwa tulikuwa tunapewa.mme mtu alikuwa ni full kutufokea hata kama hakuna kosa tulikula msoto hadi pale nlipofika form 6 nikiwa nasubiria matokeo dogo akiwa form 5.wakati huo mme wa mamdogo akiwa na ugonjwa wa kisukari.basi akawa anaendelea na visa vya kila namna huku kunamda unamskia akimfokea mke wake atufukuze wakiwa chumbani wenyewe,but hakuwahi kutuambia face to face sababu alikuwa hana,inshort nlikuwa mpole mno na nisie na makuu japo wenzangu walisoma shule za bei ghali sie tukasoma kayumba,shule ambayo tulikuwa tunanunuliwa shati 2 kwa mwaka na suruali na sketi moja kwa mwenzangu.basi kuna siku nimechelewa kurudi mida kama ya saa 3,dah basi alinifokea na kunitukania mno mpka mama yangu,kiukweli moyo uliniuma kama unachomwa na moto wa koroboi maana nlikuwa naambiwa mpka kamtafute mama yako na baba yko,dah basi ilivyofika asubuhi nikaondoka,mungu alikuwa upande wangu kufika mida ya mchana bodi ya mkopo waktoa majina nami nkiwemo basi kuna dalali nlikuwa nafahimana nae nkamwelezea yote ikatafutwa nyumba nkàpta chumba na baraza kwa elf 30 wakati huo,yule mzee alinipa mwezi niwe nmeshalipa,basi sku hyo hyo nkahamia maana dalali alinkopa hela kidogo,then nkamfata ndugu yangu maisha yakaanzia hapo tukiwa tunalala kwenye vijigodoro mungu alitusaidia tukafungua vijiabishara vyetu mwisho wa siku tuko hapa now kila mtu na familia yake na kazi pia,japo mzee yule alikatwa mguu huwaga naendaga kumuona mara moja kwa miez mitatu hadi mi 4 na kila tukienda huwa analia mno kwa kujutia alotufanyia maana ni mengi mno japo mengne sikuyaelezea ,na ukiangalia wale watoto wenzetu walokuwa wanasoma international now wanashinda kwa kubeti tu mjini.
My advise kwa vijana unapokaa kwa mtu kaa kwa malengo ya mda mfupi uondoke usiseme unapokaa kwa mtu et kwenu hapana tafuta kwako mapema kwani ipo sik watakuchoka tu
Jerybanks
 
Dah...mie niko muwazi...ukifika geto kwangu kuna fomu maalum unazijaza...ukitaja sababu ya kuja..muda utakao kaa...na mchango wako wa kila siku kwenye bajeti.....Sheria za geto na adhabu zake nimebandika kila ukuta..ukivunja unajihukumu mwenyewe....sitaki shida[emoji41]
 
Kuna jitu flani lilisomeshwa na dingi kuanzia nursery school mpaka saivi limefikia ngazi ya uprofesa . Ni mmoja wa madean wa colleges pale udom , Kuna kipindi likawa linajifanya uzungu mwingi halitaki interaction na watu.. Lilikuja kupata pigo moja takatifu ikabidi limrudie dingi kumpigia magoti.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna lijamaa na dada yake yalisomeshwa na mzee baba, ila saivi ukiliomba hata elfu kumi kuipata sio rahisi. Yani hua nawaangalia nashangaa sana ni wagumu balaa kusaidia ila wao walisaidiwa daaah
Walikubalia kuwa kwa kusaidiwa na wenyewe waje wawasaidie?we komaa kivyako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…