Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Nimefuatilia post za wadau hapa kuna kitu kimoja nimekiona ambacho kwa nafasi kubwa ndicho kilichosababisha washindwe kuidhibiti shilingi iliyopita mikononi mwao,nacho ni kupenda kuiona cash,kwamba bank account yangu inasoma 12mill au 20mill basi hata nikenda nikatoa mill1 nikanunua hiki mtabaki na balance yakutosha na shida ya pesa ukiishakuwa nayo na ukawa na uhuru nayo inakuwa rahisi sana kuitumia,pia kushindwa kuiheshimu na kusahau tulipotoka.

Obviously wengi tumetoka ktk familia maskini hata kutoa toa msaada maana sio kila aliefilisika hela alihonga hapana mwingine ndugu alimfuata bwana nipe kiasi fulani cha pesa nitarudisha baada ya muda fulani then anazingua kumshtaki unashindwa inabidi ukubali.binafsi nimeshika hela nikiwa mdogo sana{masuala ya elimu tusiulizane wakuu}ila hela yangu ikikaa tu ndani sikuiweka bank nikiwa aged 21 nikanunua kiwanja kwa Tsh3,150,000/= nikiwa 23 nikanunua kingine kwa thamani zaidi ya hiyo kidogo nikiwa aged 25 nikaanza ujenzi.

Kwanini nilifanya hivi,sikutaka kukaa na hela inizoee na hata nikifuatwa na ndugu kukopa nilikuwa najifanya masikini wa mwisho sometimes huko kwenye kununua assets nilikuwa nabaki na deni ila sio kiasi kikubwa na hii imenijenga sana kuithamini shilingi.na tunapozungumzia asset hatuzungumzii kumiliki gari,kwa imani yangu asset nzuri kwa sisi ambao tunadunduliza dunduliza ni kile kitu ambacho hakitakufanya utoe hela yako nyengine mfukoni kukihudumia labda kukiboresha tu kwa manufaa yako ya muda mrefu.
 
Ukiwa nazo za kukinga.
Rafiki yako mkubwa ATM. Ukiingia pale una bofya tu. Mpunga unatoka. Zingine mpyaaaa. Alafu zina ubaridi ubaridi wa air condition. Ngoja siku ziishe. ATM utaipitia kwa mbaaali. Uingie ukafanye nini.?
Nimeyamiss haya maisha kwa kweli.
Oya mbavu zetu.

Unapopita maeneo yenye ATM Machine, unaangalia upande mwingine huku ukfyonza ''mfyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyuuuuuu''
 
Watu wengi wanapenda kujifunza kwa waliofanikiwa tu, wanasahau kuwa kuna mengi ya kujifunza kwa walioshindwapia, Nimejifunza kitu kupitia uzi huu.
Tafuta kitabu kinachoitwa ''The anatomy of failure'' cha Praise George. Utajifunza mengi sana mle. Soma piakingine cha The Law of Success by Napoleon.
Utagundua why people fail.
 
Tatizo akili inarudi pale receipt inaposoma salio lako ni laki mbili [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] ndio unajiuliza hii niiiinunuliee halafu jibu linakujia pale pale haitoshi baada ya siku mbili unaenda toa laki na nusu halafu hukanyagi tena bank na ukipita karibu ni upande wa pili wa Barabara [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
[emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] dah... Sio kwakunichekesha huku mkuu
 
Nakumbuka miaka hiyo nimemaliza advance najiandaa kwenda chuo kikuu, tukauza nyumba ya urithi ya mzee tukagawana mil50 kila mtu tulikuwa watatu.
Baada ya kuzipata zile milioni 50

Nilitafuta mjengo kabla sijaenda chuo Mwanza, baada ya kununua hiyo nyumba for approximately 25mil. Remaining balance nikaenda nayo chuo but kiukweli mpaka Leo huwa najiuliza ile pesa iliishaje? Note sikua mtu wa tungi sana wala totoz. But hela zilikuwa zinaisha tu bila kujielewa naweza kuwa na elfu 50 mfukoni nikienda kula hata lunch tu nikija kucheki kwenye wallet nina kama 20k tu.

But hela zilivyokaribia kukata ikabidi nimfuate bi. Mkubwa kuongea nae baada ya kutembea tembea kwa wataalam jibu tulilopewa ni kwamba kuna ndugu alinitupia chuma ulete ili pesa nisiifanyie jambo la maana ikawa inapotea katika mazingira ambayo wew hujitambui.

Nachoshukuru nilinunua nyumba otherwise ningekua sina pakukimbilia.
 
Jamanii Pesaa ya BUMUU sio pesaa.. yaani unapewa kilaki 6 ndani ya week hujahonga hata.. Pesaa hunaa...!! Unaanza kushindiaa mikatee..Ivii mshahara unawezaje kutosha..!??? Discipline ya helaa wanayo wachache snaa
 
Mi nashukuru nilishtuka toka mwezi June baada ya kuona masanga ndio yanapeleka mambo yangu wrong sikuamua kuacha ila nimejiwekea utaratibu ambao ndio nautumia mpaka leo hii nikitoka kazini napita liquor store nachukua konyagi kubwa jibapa la 9000 naenda kunywea home nashukuru nilirudi kwenye dira na hela naiona zaidi baada ya kuacha pombe za kampani.

"Pesa mfano wa puto zinazopepea starehe ndio sindano"
 
Hujawahi kufilisika mkuu. Wewe uliingia hasara, ingekuwa umepoteza mtaji wa milioni 100 sawa. Hizo za milioni 2,3 mpaka 10 tumeshapoteza wengi sana ni hela ya kawaida kuingia loss kwa sisi watafutaji.

Ikitokea unasikitika kidogo, unajitathmini wapi ulipokosea, unajipanga unarudi vitani.
 
Back
Top Bottom