Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wapo wpUnawaza nenda commission of mediation and arbitration (CMA) wanaweza kukusaidia kupambana na hazi yako
Acha tu ila Mandonga ashawahi sema "Man never cry and sea never dry"Pole sana aisee maana nafeel unachokipitia
Umenena vyemaHapana. Hatuna elimu ya fedha. Tumepata fedha bila mpango
Tumeamini business partners au relatives
Wageni kwenye gemu husika.
Mambo ya kiroho
Tuambie ulikuaje, mwaka ukawa mbaya kwakoKufilisika jamani hili neno naliogopa, hata kulitamka tu natokwa na machozi. Mwaka 2021 ulikuwa mbaya sana kwangu.
Ni zaidi ya Legend, Nina mdogo wangu wa dizaini hii, Yeye ni Dar Combine.Huyo legend hahahah
Hujafilisika ila umewekeza.Huu uzi kweli kiboko! nilijua ni Mimi mwenyewe kumbe tupo wengi sana.
Nimemaliza chuo kikuu mwaka Jana Basi mzee akanipa M3, M1 nimsaidie kukarabati nyumba yake na zingine nione nafanyia nini, Sasa mimi kweli nyumba yake nikakarabati sasa hela iliyobaki nikawaza nijengee kijumba kwenye kiploti alichonipa nifanye masuala ya ujasiliamali hapo.
Mpaka sahizi lipo pagale lililoezekwa tu, na hela imekata sina ramani niponipo tu, lakini kila nikiangaliaga matofali yalivyopangika kwenye kijumba napata nguvu kwamba angalau sijaipoteza bure Kuna kitu nimefanya.
Mimi hapa nishapata wazo,Ahsante Mkuu, Ila unapowasoma wahusika na matukio mbalimbali yaliyowatokea ni exprience nzuri kuliko mawazo ya mtu mmoja yaliyowekwa kwenye kitabu,Mwandishi anaweza asipate exprience tofauti tofauti kama Live exprience toka kwa wahusika, Hii inavutia sana na wasio na uwezo wa kununua vitabu wanajifunza kwa gharama nafuu na uhalisia sana, wengi wamekuwa sio wachoyo kwenye kufunguka.
Ulikuwa private au governmentAsante mkuu, maana nimecheki akaunti yangu ya NSSF iko 0.0 maana walikuwa hawaweki kitu
Private mkuuUlikuwa private au government
Hii ishu imemtokea jamaa yangu mwezi huu yani ni hatari.Mwaka 2011 soko kuu mwanza nikiwa ninauza nafaka zikiwemo karanga, njugu, choroko,dengu,ufuta,ulezi,uwele,mtama,maharage na kunde.
Kamtaji kalivyokuwa nikawa naendea karanga tabora tani kadhaa nauza jumla. Nilipata pesa kwa njia hiyo. Basi kufkia December karanga zikawa chache Sokoni hivyo mwenye nazo alipiga pesa balaa.
January 2012 nikaingia poli kusaka karanga mpya ili niwahi bei sokoni. Basi nikapata kama gunia 30 (tani 3). Kufkisha Sokoni ziligombaniwa kama nyama. Nikaona pesa si hii apa. Nikazoa msingi wote around kama 22.8m. ili nikapige mkupuo mmoja nije nitulie.
Kuleta mzigo nafika Sokoni nakutana na fuso 6 zinashusha mzigo. Sasa kila mmoja ashajua ni dil acha bei ishuke. Nilijikuta karanga nimezinunua 2300 natakiwa niziuze 1600. Sasa nilipoharibu nikapiga mzigo stoo kwamba bei ikikaa sawa nitauza duh! Kumbe mzigo si haujakauka vizuri, nilikaa kama wiki nafungua stoo nakuta mzigo wote umevunda... Duh!
Bora usimuliwe tu usiombe ikukuteHii ishu imemtokea jamaa yangu mwezi huu yani ni hatari.
Ni raha ukisimuliwa omba iskukuteAseee yaan nataman nivae viatu vyako halafu naona vinanibana