Kuna mjadara unaendelea space kutoka kwa wataalam wa teknolojia bunifu ya akili bandia, nimejiunga kupata kitu na nimelegea kiakili zaidi baada ya kuona mambo yanayokuja.
Kwa mfano katika muundo unaokimbia sasa hivi ni Artificial Intelligence (AI) inaweza kufanya kitu unachowaza au kubuni kitu zaidi hata kuliko mtu aliyekaa kwenye kiti akiwa na computer akijenga picha na kuipa nakshi.
AI inaweza kukufanyia hiyo kazi kwa muda mfupi na kwa ubora mkubwa kuliko wako.
Kwanza angalia hizi picha hapa 👇🏾 ni kazi ya AI na ahkuna mkono wa mtu hapo.
View attachment 2580010
View attachment 2580013
Mpaka hapo nikawakumbuka jamaa zangu wapiga picha akiwepo jamaa yangu mmoja yupo Dodoma, kwamba itakuwaje kwa hali hii kama hatajiongeza kufikilia kuwa mkulima'?.
View attachment 2580018
View attachment 2580022
Kumbuka kila siku kabla jua alijachomoza kuna ujuzi mpya, wakati sisi tunafikilia kuomba msaada wa kujenga choo, wenzetu wanatumia AI aweze kufanya ujenzi wa tunnel la kuhifazia uchafu wako.
View attachment 2580030
Nilimaliziavkwa kusoma moja ya komenti ya mdau pale kwenye space akiuliza...
View attachment 2580044
Wataalam wetu sijui wako wapi? naishia hapa ila naiwaza kesho.
==============
Wakuu naongezea na hii sinema, ukiweza kuangalia hadi mwisho utaelewa, nimeiweka hapa kutokana na maswali kutoka kwa wadau.