Wadau walishauri kuwa ingelichaguliwa tume yenye mchanganyiko ulio sawa, pamoja na hao waliochaguliwa sasa, wangelikuwemo pia na watu kama Mbowe ama Wakili Madeleka na wafungwa waliofungwa hadi kumaliza vifungo kwa kesi za kubambikiziwa.
Wachunguze na TRAAkizungumza leo Jumanne Januari 31, 2023 Ikulu Chamwino, Dodoma wakati akizindua tume ya kuangalia jinsi ya kuboresha taasisi za haki jinai nchini, Rais Samia ameitaka tume hiyo kuichunguza ofisi hiyo juu ya utendaji kazi na uendeshaji ili kubaini kasoro zilizopo na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuiboresha iweze kutoa haki kwa wananchi.
Amesema mbali na ofisi hiyo ya mashtaka tume hiyo itakayoanza kazi Jumatano Februari 1, hadi Mei 30, 2023 itazifanyia tathmini taasisi za utoaji haki jinai nchini ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na kuibua manung’uniko kwa wananchi, ikiwamo Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Jeshi la Polisi, Magereza na Mahakama.
“Kutokana na ukubwa wa kazi tunawapa miezi minne kuanzia kesho hadi Mei 30 nendeni mkaangalie Ofisi ya Mashtaka kwenyewe kukoje na kuna kasoro zipi.
“Zamani ofisi hii kulikuwa na ngoma nzito inachezwa mpaka kukusanya fedha za plea bargaining nyingine zimeonekana na nyingine hazijaonekana ukifuatilia utaambiwa mara kuna akaunti China.
“Tutazame kuna nini haswa kilichoharibu hii taasisi, pia tuiangalie Takukuru kwa sababu kubadilisha tu mkuu wa taasisi haisaidii watamdanganya tu wafanye wanavyotaka.
“Jeshi la Magereza na kwenyewe tukalitazame, magereza zetu zikoje na zinatakiwa ziweje, mwendelezo wake na kama linafanya kazi ya msingi? Mamlaka ya Kuzuia Dawa za Kulevya nako kuna changamoto nyingi za kutegea watu dawa,” amesema Rais Samia.
Naye, Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amempongeza Rais kwa kuanzisha tume hiyo ili Watanzania waweze kupata haki kwani kumekuwa na manung’uniko mengi ya wananchi juu ya mfumo wa utoaji haki jinai nchini.
MWANANCHI
Nipe kwa kifupi Magoti alishauri nini?Hata hivyo Rais ameufanyia kazi Ushauri wa Tito Magoti
Utafute Uzi wa Tito magoti hapa upo.Nipe kwa kifupi Magoti alishauri nini?
Mkuu nimefuatilia na nimeusoma, ni madini matupu jamaa aliyatema.Utafute Uzi wa Tito magoti hapa upo.
Nashukuru sana. Nimeamini we ni Raia mwema sana na unajielewa. Hongera.Mkuu nimefuatilia na nimeusoma, ni madini matupu jamaa aliyatema.
Nikiri kuwa sikuwahi kuuona na kuusoma kabla.
Maudhui ya hiyo barua ya wazi yenye title " Barua ya wazi kwa Rais kuhusu haki jinai" imeeleza kwa kirefu sana na imegusa kila sehemu yenye "uozo"!
Nikiangalia na hotuba ya jana ambayo Rais aliitoa kwa hao wajumbe wa tume ya haki jinai, nina hakika ya 90% kuwa Rais aliisoma hiyo barua ya wazi iliyotumwa kwake na kuamua kuifanyia kazi.
Inauma sanaAkizungumza leo Jumanne Januari 31, 2023 Ikulu Chamwino, Dodoma wakati akizindua tume ya kuangalia jinsi ya kuboresha taasisi za haki jinai nchini, Rais Samia ameitaka tume hiyo kuichunguza ofisi hiyo juu ya utendaji kazi na uendeshaji ili kubaini kasoro zilizopo na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuiboresha iweze kutoa haki kwa wananchi.
Amesema mbali na ofisi hiyo ya mashtaka tume hiyo itakayoanza kazi Jumatano Februari 1, hadi Mei 30, 2023 itazifanyia tathmini taasisi za utoaji haki jinai nchini ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na kuibua manung’uniko kwa wananchi, ikiwamo Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Jeshi la Polisi, Magereza na Mahakama.
“Kutokana na ukubwa wa kazi tunawapa miezi minne kuanzia kesho hadi Mei 30 nendeni mkaangalie Ofisi ya Mashtaka kwenyewe kukoje na kuna kasoro zipi.
“Zamani ofisi hii kulikuwa na ngoma nzito inachezwa mpaka kukusanya fedha za plea bargaining nyingine zimeonekana na nyingine hazijaonekana ukifuatilia utaambiwa mara kuna akaunti China.
“Tutazame kuna nini haswa kilichoharibu hii taasisi, pia tuiangalie Takukuru kwa sababu kubadilisha tu mkuu wa taasisi haisaidii watamdanganya tu wafanye wanavyotaka.
“Jeshi la Magereza na kwenyewe tukalitazame, magereza zetu zikoje na zinatakiwa ziweje, mwendelezo wake na kama linafanya kazi ya msingi? Mamlaka ya Kuzuia Dawa za Kulevya nako kuna changamoto nyingi za kutegea watu dawa,” amesema Rais Samia.
Naye, Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amempongeza Rais kwa kuanzisha tume hiyo ili Watanzania waweze kupata haki kwani kumekuwa na manung’uniko mengi ya wananchi juu ya mfumo wa utoaji haki jinai nchini.
MWANANCHI
PerfectUtaratibu huu tayari ulikwishakukosolewa mapema kwamba, hao wote hawawezi kutenda ya maana kwa sababu mfumo huu wa hovyo wa haki jinai ndiyo walioukuta na ukawanufaisha
AbsolutelyWadau walishauri kuwa ingelichaguliwa tume yenye mchanganyiko ulio sawa, pamoja na hao waliochaguliwa sasa, wangelikuwemo pia na watu kama Mbowe ama Wakili Madeleka na wafungwa waliofungwa hadi kumaliza vifungo kwa kesi za kubambikiziwa
Hoja fikirishi🤔 Dhamira njema inashinda uovu ?Mapolisi, Jaji mkuu, Katibu mkuu, Mkurugenzi mkuu wa Takukuru na nani sijui shasahau, lakini wote hao walikuwa ni viongozi waandamizi wa taasisi hizo, kwa sasa ni wastaafu.
Utaratibu huu tayari ulikwishakukosolewa mapema kwamba, hao wote hawawezi kutenda ya maana kwa sababu mfumo huu wa hovyo wa haki jinai ndiyo walioukuta na ukawanufaisha.
Na hakuna hata mmoja wao katika historia ya maisha yake ambaye alikwishapata misukosuko ya kisheria na kutiwa ndani na akaonja joto ya jiwe kwa uharamia wa haki jinai.
Hivyo sasa, haidhaniwi kuwa tume hiyo wataweza kuleta mapendekezo ya maana na yenye tija.
Wadau walishauri kuwa ingelichaguliwa tume yenye mchanganyiko ulio sawa, pamoja na hao waliochaguliwa sasa, wangelikuwemo pia na watu kama Mbowe ama Wakili Madeleka na wafungwa waliofungwa hadi kumaliza vifungo kwa kesi za kubambikiziwa.
Hapo wangeweza kufukua vizuri makaburi bila kuacha mabaki ya mifupa.
Sasa ngoja tusubiri tuone tume hiyo kama itakidhi matakwa ya aliye wateua pamoja na wananchi kwa ujumla.
Ninaona dhamira njema ya kutoka moyoni ya Rais wetu Samia, lakini sina imani sana na viongozi wengi waliobebwa na mfumo huu mbovu wa ukandamizaji na uonevu wa haki jinai kwa watu.
Mtakwenda wapi ?2025 tunaenda na mama
Mimi ninavyoona, wakilindana kwa mambo ambayo yapo bayana nchi nzima watu wanayaelewa, kuanzi Rais mwenyewe aliyewateua mpaka kwa raia wa chini kabisa, basi ujue hakuna tena itakayokuja kuunda iaminike!tunachokiomba hii tume itende haki, waache tabia ya kulindana, penye uozo wauseme wazi kwa manufaa ya wananchi.
wafanye uchunhuzi wao kwa uhuru na kwa kujiamini, waache tabia ya kulindana
Maneno pasipo matendo, ni sifuri. Tuache unafiki wa kisiasa, kama hatutaki haya yajirudieYaani hata hivyo kwa Rais Samia kutambua kuwa hakuna haki huko ni nia njema.