Uchaguzi 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi ina upendeleo wa wazi kwa CCM na mgombea wake dhidi ya CHADEMA na Tundu Lissu

Wewe una picha halisi za Karatu?
Yaani kushinda nyinyi ni ndoto ya mchana. Leo nimehakikisha kabisa kuwa mnaedit picha leo nilikuwepo Karatu hakukuwa na watu kama mnavyoonyesha picha.
 
Mbona ulisema Leo Ndio umeamini?
Kua picha zina fanyiwa editing
Pole Sana
Ndiyo nimeona picha zinazotembea hapa JF siyo za kweli nilikuwepo Karatu hakukuwa na watu wengi hivyo kama inavyoonyeshwa kwenye picha hizo.
 
Ndiyo nimeona picha zinazotembea hapa JF siyo za kweli nilikuwepo Karatu hakukuwa na watu wengi hivyo kama inavyoonyeshwa kwenye picha hizo.
Labda na ile ya jiwe kupiga magoti ni ya uongo
 
Maisha yetu yanatudai uaminifu,kuaminika.
Yàani ikiwa unasimamia maslahi ya watu,ufanye hivyo kwa uaminifu na watu wenyewe wakuamini.
Ikiwa mtu mwenye hadhi yake na akili zake akawa anafanya kazi kwenye taasisi kubwa na yenye dhamana ya kusimamia uchaguzi mkuu wa nchi na inakosa kuaminika na wananchi,bila shaka hana budi kuacha hiyo kazi.
Watu wetu ambao tunawaheshimu na kuwaona wasomi,hii leo wanafanya kazi katika tume ya uchaguzi inayokosa kuaminika na wananchi walio wengi,hivyo na wao viongozi wa tume wanakosa kuaminika na kwa kweli SI WAAMINIFU.
Tunadhani huko vyuoni waliokwenda kusoma basi watakuwa walienda kusomea UJINGA.
Tunaona sasa ni muda muafaka wa kuacha kuiongozea jamii yetu na kurudi kwenye kazi zao za siasa waliozoea ili waweze kujijengea uaminifu kwa wananchi.
 
Hiyo siyo uongo ni heshima ya wananjombe kumbe hujui na mila za wananjombe?
Heshima
Kaanza lini kua good boy?
Mimi najua sifa zake
Muuaji
Kiburi
Haambiliki
Mtekaji
Asiekua na huruma
Katili
Mdini
Mkabila
Mkanda
Mlipa visasi
Anasifa zote za farao
Baada ya uchaguzi utamuona
Wana Njombe watalipa goti Hilo
 
Mifumo na taasisi zetu ziko weak Sana kutusaidia kuwa na maendeleo na maisha yenye Haki

Kuna wakati huwa nasema kwa mifumo hii ni Kama tumaamua kutawaliwa na wachache
 
Asante kwa kuyaweka haya pamoja. Tume hii ya Mahera ni mbaya kuliko ZEC ya Jecha. Jecha aliweka makucha yake ndani mpaka uchaguzi ulipofanyika. Huyu Mahera bila aibu kabisa anapigia CCM kampeni. Hawezi kabisa kumtangaza TL mshindi. Wananchi tujitayarishe kulinda ushindi wetu kwa jasho na damu.
 
Mifumo na taasisi zetu ziko weak Sana kutusaidia kuwa na maendeleo na maisha yenye Haki

Kuna wakati huwa nasema kwa mifumo hii ni Kama tumaamua kutawaliwa na wachache

Tunahitaji overhaul ya mfumo mzima wa utawala nchini, huu mfumo tulionao ni mfumo wa enzi za chama kushika hatamu, haukidhi tena mahitaji ya wananchi!. Just imagine kada wa wazi wa CCM eti ndiye mkurugenzi wa NEC. Huu ni utani mbaya sana kwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!
 
Huna jipya. Tume, CCM na Serikali wameshatukanwa sana na mgombea wenu na nyie vibaraka wa mkoloni. Ila izi ngebe zenu mwisho 28 Oktoba 2020. Akili zitawakaa sawa tu.
 
Hii lialia yenu sio bure. Design mmeshaona kabisa kwamba hamtoboi, hamtoboiiiii in Bwegez voiz, yani hamtoboi, sasa njia na option pekee mliyobaki nayo ni kujenga chuki, kuchochea vurugu, ila juzi nimemcheck mgombea wenu kule Nyamongo mabomu ya machozi tu alipoteana na walinzi wake. Fanyeni kampeni kistaarabu fujo hamziwezi waoga wakubwa nyie.
 
Katiba mpya ni muhimu sana kikawaida mtu ukiwa na rasilimali nyingi unaweza kuzitumia hovyo hovyo kwahiyo lazima uchorewe mstari
 
Mimi Naweza kusema kuwa wewe huzijui Sheria vyema, unasoma upande mmoja tu. Labda niseme Sheria inasomwa Kama ambavyo inasonga ugali, katu huwezi songs ugali kwa mkono mmoja.

Lakini hivi umesahau kuwa ni Mbowe na Lissu ndio waliobifukuza hivyo vyombo vya umma? Hivi unajua kua sio kila vipindi ni vya bure katika vituo vya habari vya umma. Kuna vingine wanalipwa hasa hizo live.

Unalia na Lissu tu hatndewi Haki, vipi Lipumba, Rungwe, Membe, na wagombea wengine 10 waliobaki je wanapewa huduma hiyo.

Tume inamkemeaje wakala wa kampeni wa Mgombea fulani. Majaliwa ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Chama chake kimemteua kuwa wakala wa Mgombea wao kimnadi. Anatimiza majukwaa ya wagombea Ubunge na ratiba zao hayupo kwenye ratiba ya tume. Hata Lissu Kama Mnyika anaweza kufanya hivyo anaweza Mbona Zitto Kabwe alikuwa anazunguka Mikoani kuwanadi wagombea wa Chama chake na hamsemi Time imkemee? Abdull Nondo wa ACT alikuwa anazunguka Mikoani kunadi wagombea Mbona hamkusema kuhusu hilo? Toeni boriti jichoni kwenu kabla ya kibanzi kwa mwenzio.
Kauli ya Magufuli na Wakurugenzi aliitoa lini na wapi? Je mnaweza ipeleka Kamati ya Maadili?. USIKURUPUKE.

Hivi kumbe kuna vyama Ilani zao ni matusi, kuhimiza vurugu na kutishiana na si kumleta maendeleo kwa wapigakura wao. Hivi ni cha gani ambacho kikishinda, Miundominu ya Barabara, afaya, Elimu, umeme, mawasiliano hakitafanya? Mimi Kama Mwananchi nataka Sana Chama kitakacho hakikisha huduma bora za kijamii, mkulima nayafikia masoko kwa kua na Barbara nzuri, watoto wanasema vizuri na huduma za afya zinakuja Bora zaidi ya Sasa. JIPANGE NDUGU.
 
Pombe kesho piga magoti
Kesho ataanza kuomba msamaha
Kwa muda mrefu watanzania tulikua tunasema
We can't breathe
Lakini Sasa jiwe ndo linasema
I can't breathe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…