Tumeachana lakini mwanamke hataki tulee mtoto pamoja; baadaye anataka aseme katelekezewa mtoto na hicho kitu mimi sikitaki

Tumeachana lakini mwanamke hataki tulee mtoto pamoja; baadaye anataka aseme katelekezewa mtoto na hicho kitu mimi sikitaki

Baada ya kupata nini cha kufanya,matunzo yote yapitie benk,unaweza ukamfungulia account.
Mzazi mwenzio bado anahasira ya kuachwa
 
Kiislam huyo ni mtoto wa mama.

Sijuwi imani yenu.

Ushauri wa ndoa ni mgumu Sanaa maana mkikalishwa chini mkaelewana ushauri wetu itakuwa hauna maana..
Na umesema mpare lazima itakuwa chini yake tu labda Kama utakaza kutorudiana nae
Wee fanya ujanja wako mkatie mtoto bima ya Afya tu.
Mengine akigoma we tulia kimya watafata tu matumizi hata ustawi watakufata.
Ila ndio ukiona mama mkwe Ana power mzee mpaka unakufa hutopata amani labda mkeo awe zimo kichwani sawa sawa ndo atatulia
Shukrani kwa ushauri
 
Una uhakika huyo mtoto ni wako?
Autowe wapi?

Tanzania hii watoto wa ndani ya ndoa na watu wanabambikiwa, itakuwa wa nje ya ndoa?

Usikute huyo mtoto, masikini ya Mungu, kila mwanamme anayeingia kwao anaambiwa *mwamkie babako".

Na mwanamke ukute anachukuwa huduma ya mtoto kwa wanaume hata watano tofauti.

Uasherati na uzinzi ni uchafu. Msiukaribie.
 
Dunia ya leo ke wengi wanatumia watoto kama silaha ya kutuchapia sisi!

Ukijenga nyumba na mkeo na mna watoto kiburi humpanda na kutaka abaki na Mali na watoto wewe uende ukaanze upya!

Watoto hawana faida Tena kwa sisi me zaidi ya kurithi majina tu!

We tulia tu mkuu!akikua atakutafuta mwenyewe na mtapiga stori inatosha,punguza matarajio yoyote Kwa watoto ambao mliachana na mama zao!!

Mama zao huwajaza watoto wao ujinga wa kutosha ambao Huwa mwiba kwetu baadae!!

Jihesabu kama hujazaa vile!
Ahsante kaka
 
Kisheria mtoto bado mdogo hivyo ana hali ya kukaa na mama yake..

Kisheria una haki ya wewe kama baba mtoto wako anaishi wapi, anakula nini na mazingira anayoishi kama yako salama.

Una haki ya kuonana na mwanao katika utaratibu ambao hautaleta vikwazo kwenu wawili.

Una haki na wajibu wa kumhudumia mwanao pia.

Hivyo mueleze haya mzazi mwenzio.

Akitia kichwa ngumu mpeleke ustawi wa jamii mkayajengee huko.

All in all usiache kutuma muamala wa matumizi kila mwezi na risiti utunze.
Ahsante kwa ushauri
 
Autowe wapi?

Tanzania hii watoto wa ndani ya ndoa na watu wanabambikiwa, itakuwa wa nje ya ndoa?

Usikute huyo mtoto, masikini ya Mungu, kila mwanamme anayeingia kwao anaambiwa *mwamkie babako".

Na mwanamke ukute anachukuwa huduma ya mtoto kwa wanaume hata watano tofauti.

Uasherati na uzinzi ni uchafu. Msiukaribie.
Mtoto ni wangu copy&paste hadi DNA
 
Wewe tuliza akili, yatamshinda tu, atakutafuta kuomba msaada wa mtoto! Acha tu mtoto akikua atakutafuta mwenyewe!

Kingine? Dah, hunamove on, inshort bado unampenda huyo mwanamke ni vile tu ana kiburi akakuacha! Uchumi umekaa aje?
Uchumi upo wastani kaka na maisha yalikua yanaenda fresh tu baada ya mtoto kuwa mkubwa kidgo ndo matatizo yakaanza
 
Uchumi wako upoje ? Unapesa ? Au bado umepanga? Unabiashara yeyote ya maana?/ni ngumu sana kwa alienapesa apewe block call zake
 
Yaani umwache mwanao ukisubiri akue akutafute.

Sisi wanaume ni wabinafsi sana aisee,.

Kwanini asimpambanie mwanae, kugive up na kusubiri mtoto akue akutafute ni ubinafsi huo, yeye kwa sasa hana uwezo wa kumtafuta baba ila baba ana uwezo wa kumpata mtoto.

Kama mama yake anavyopambana kumhold ndivyo baba upambane kumpata.
Hakika kaka hakuna kukata tamaa
 
Yaani umwache mwanao ukisubiri akue akutafute.

Sisi wanaume ni wabinafsi sana aisee,.

Kwanini asimpambanie mwanae, kugive up na kusubiri mtoto akue akutafute ni ubinafsi huo, yeye kwa sasa hana uwezo wa kumtafuta baba ila baba ana uwezo wa kumpata mtoto.

Kama mama yake anavyopambana kumhold ndivyo baba upambane kumpata.
Kama hujawai kukutana na huo mgogoro huwezi kuelewa.Hicho unachokisema kupambana hapo patazuka ugomvi mkubwa ambao hukuutarajia.Hawachelewi kukimbilia polisi kua umemtishia maisha na kama unavyojua wanasikilizwaga ata kama anayoyaongea ni ujinga.mwisho wa siku wewe mwanaume ndio unaonekana mkorofi na unaingia gharama.ndo maana wanaume wengi wanaamuaga kukaa kimya nakuendelea na harakati zingine.Wanawake waone hivyo hivyo ndugu.
 
Kiislam huyo ni mtoto wa mama.

Sijuwi imani yenu.
😅😅🤣🤣😂 niwe mkweli sister; nyuzi zako almost zote huaga naziruka, sisomi hasa kule jukwaa la kimataifa, sababu yangu huaga ni moja tu, popote lazima upenyeze utamaduni wa middle east..., sasa uzi hu nilipoona sura yako, fasta nikaona nipitie kidogo, shit, same shits again.😂 sorry.
 
😅😅🤣🤣😂 niwe mkweli sister; nyuzi zako almost zote huaga naziruka, sisomi hasa kule jukwaa la kimataifa, sababu yangu huaga ni moja tu, popote lazima upenyeze utamaduni wa middle east..., sasa uzi hu nilipoona sura yako, fasta nikaona nipitie kidogo, shit, same shits.😂 sorry.
Uislam siyi utsmaduni wa popote, ni universal.

Unajuwa hata AI Chat GPT amesilim?

Wewe Mbona unao huo utamaduni wa Mashariki ya kati? Utakikimbia kivuli chako?
 
Je, unajua ni kwa nini hasa huyo Mwanamke hataki wewe umhudumie huyo mtoto wake? Sababu za yeye kufanya hivyo unazijua?? Fanya utafiti kwanza juu ya suala hili.

Aidha, siku hizi Kesi za Paternity Fraud (akina baba kubambikiziwa watoto wasiokuwa wao kiuhalisia) ni nyingi Sana, hivyo uchukue tahadhari mapema kuhusu suala hili pia. If possible, make sure that you undergo a DNA Test to confirm your paternity to that child. Yawezekana huenda huyo Mwanamke tayari ameshagundua jambo fulani kuhusu suala lako wewe binafsi kuhusika na ubaba-mzazi wa huyo mtoto wake, hivyo, anachukua hatua za tahadhari mapema ya kutokukuhusisha na gharama za malezi ya huyo mtoto kiasi kwamba hata utakapokuja kugundua kuwa wewe ni baba mlezi tu Basi isikuletee maumivu makali Sana hapo baadaye, maumivu ambayo yanaweza kusababisha maafa kwa huyo mwanamke na mtoto wake.

Kumbuka: Visa vya mauaji kwa wanawake na watoto wao vitokanavyo na janga hili la Paternity Fraud ni vingi Sana siku hizi, siyo kwa hapa Tanzania tu peke yake, Bali ni kwa dunia yote kabisa kwa ujumla wake. Tafakari na Chukua Hatua mapema!
Umeusoma uzi vizuri? Is like mwanamke anataka warudiane na mwamba hataki ndio sasa mwanamke nae kakaza. Halafu iko hivi, kwa sisi wanaume kama mtoto sio wako wala huaga hatuhitaji DNA test, huaga tunajua tu kama hapa nilipigwa, majority ukiona kaamua kwenda kupima, ujue anatafuta tu ushahidi but jibu alikua analo siku nyingi; kuna njia nyingi sana nje ya sayansi hi ya kisasa kujua kama umepigwa au vipi; kwa maandishi ya huyu mwamba, is like ana uhakika, mtoto ni wake. Trust me, wanawake huaga wanatumia watoto/mtoto kwenye mahusiano.
 
Kama hujawai kukutana na huo mgogoro huwezi kuelewa.Hicho unachokisema kupambana hapo patazuka ugomvi mkubwa ambao hukuutarajia.Hawachelewi kukimbilia polisi kua umemtishia maisha na kama unavyojua wanasikilizwaga ata kama anayoyaongea ni ujinga.mwisho wa siku wewe mwanaume ndio unaonekana mkorofi na unaingia gharama.ndo maana wanaume wengi wanaamuaga kukaa kimya nakuendelea na harakati zingine.Wanawake waone hivyo hivyo ndugu.
Baba hivyo nikikua nakukataa
 
Habari zenu wakuu,

Kuna jambo moja natak kushare na nyie, nilikuwa katika mahusiano na mwanamke mmoja tukafanikiwa kupata mtoto mmoja tuishi pamoja toka 2021 tumekuja kutengana mwez wa sita mwaka huu na sababu iliyofanya kutengana ni mke wangu kuanza kubadilika ana kiburi kupita kiasi, ameanz dharau sana ana jambo anavyoamua yeye in short kama vile anatak kunicontrol tukiwaita wazazi

Tuongelee wazazi wake kama vile wako upande wake, wanahisi mtoto wao anaonewa nikaona isiwe kesi tukaamua kila afate maisha yake, baada ya muda ya kama mwezi mmoja hivi nikawa najaribu kuwasilian naye ili me niwe naendelea kumlea mtoto wangu kama vile mahitaji ya mtoto. Lakin cha ajabu akawa hatk kupokea simu zangu kaniblock kila mahali nikasema frsh.

Baad ya yeye kukaa kimya kwa muda kuna siku akanitafuta turudishe mahusiano lakini me nikamwambia tulishatengan sabab niliona hajabalika chochot tabia ni zile zile.

Point yangu ni nn hapa, kila mimi nikimwambia tuweke utaratibu mzur wa kumlea huyo mtoto yye hatak kabisa, kabila lake ni Mpare me nataka niwe naendelea kumtunza mtoto wangu lakini mama yake hataki?

Anataka amlee mwenyew ili badae aje aseme ametelekezewa mtoto na mtoto wang nimehangaika nae kuanzia ana mwezi mmoja tumbon mpk kafikisha miaka miwili na nusu leo mama ake hataki nimlee mtoto wang naombeni ushauri wenu.
Nenda ustawi wa Jamii. Ukifika nitafute nikusaidie kutatua shida yako pronto.
 
Back
Top Bottom