Tumeachana lakini mwanamke hataki tulee mtoto pamoja; baadaye anataka aseme katelekezewa mtoto na hicho kitu mimi sikitaki

Tumeachana lakini mwanamke hataki tulee mtoto pamoja; baadaye anataka aseme katelekezewa mtoto na hicho kitu mimi sikitaki

Kuna mda wa huruma na ubinaadamu na kuna muda wa sheria nazan km unamtaka na unamuitaji mtoto wako fuata sheria nenda dawati nenda ustawi na ikibidi kbsa fungua kesi mahakamani

Wanasimba wanasema ubaya ubwera
 
Kama hujawai kukutana na huo mgogoro huwezi kuelewa.Hicho unachokisema kupambana hapo patazuka ugomvi mkubwa ambao hukuutarajia.Hawachelewi kukimbilia polisi kua umemtishia maisha na kama unavyojua wanasikilizwaga ata kama anayoyaongea ni ujinga.mwisho wa siku wewe mwanaume ndio unaonekana mkorofi na unaingia gharama.ndo maana wanaume wengi wanaamuaga kukaa kimya nakuendelea na harakati zingine.Wanawake waone hivyo hivyo ndugu.
Huyo hajui hakuna ugomvi mbaya kama wa kigombania mtoto.

Mhanga lazima awe baba
Na huyo baba asipokuwa makini anaweza kumdhuru huyo mama endapo akimshindwa.
 
Uislam siyi utsmaduni wa popote, ni universal.

Unajuwa hata AI Chat GPT amesilim?

Wewe Mbona unao huo utamaduni wa Mashariki ya kati? Utakikimbia kivuli chako?
Basi AI chat GPT kuslim ni heko Kwa waislam!! 😁 Umesahau na cr7 mpaka ukamfungulia na uzi
 
mkuu umejikita upande mmoja tu wa ke je wew unajua tatizo lako linalosababisha ukablokiwa kila pahala? Acha lawama nakushauli tafuta hela hakuna mwanamke anaemblok mwanaume anaejitambua na mwenye hela! toa kwanza boriti ndani ya jicho lako Acha lawama zisizo msingi.
Hahahaha..nimechoka sana aseh
 
Yaani umwache mwanao ukisubiri akue akutafute.

Sisi wanaume ni wabinafsi sana aisee,.

Kwanini asimpambanie mwanae, kugive up na kusubiri mtoto akue akutafute ni ubinafsi huo, yeye kwa sasa hana uwezo wa kumtafuta baba ila baba ana uwezo wa kumpata mtoto.

Kama mama yake anavyopambana kumhold ndivyo baba upambane kumpata.
Kwani kamzaa yeye ? mleta mada piga kimya achana nae huyo mtoto tafuta wawe wengi na usikae ukafikiri kwAmba utakuja kusaidiwa na huyo mtoto pambana huku ukimtanguliza mungu ukimsaidia kwa matarajio aje baadae akusaidie atakuliza na ukiendelea kumng'ang'ania utakuja kuambiwa huyo mtoto sio wako ndo itazidi kukuumiza zaidi.
 
Mpeleke ustawi wa jamii au panapohusika engine muandike hayo muweke sahihi zenu. Baada utakuwa na Amani.
 
Fuata sheria nenda ustawi au dawati kila kitu kiwe kimaandishi. Kuonana na mtoto sio lazima direct contact btn yako/yake. Mnaweza tumia hata ndugu. Mnafatana fatana mwisho mje kuuana bure.
 
Kwani kamzaa yeye ? mleta mada piga kimya achana nae huyo mtoto tafuta wawe wengi na usikae ukafikiri kwAmba utakuja kusaidiwa na huyo mtoto pambana huku ukimtanguliza mungu ukimsaidia kwa matarajio aje baadae akusaidie atakuliza na ukiendelea kumng'ang'ania utakuja kuambiwa huyo mtoto sio wako ndo itazidi kukuumiza zaidi.
Kama hutaki watoto unaacha kupiga mbupu, funga zipu..

Hamna mtoto aneomba kuzaliwa, ni starehe za wazazi wao wengi ndo zimewaleta duniani.
Sasa umeleta kiumbe kipya duniani kwa starehe zako halafu unataka ukikache..

Baba kumpambania mwanae kwa kila kitu ni wajibu wake mpaka huyo mtoto aingie kaburini maana yeye ndo kasababisha uwepo wake.
 
Kama hujawai kukutana na huo mgogoro huwezi kuelewa.Hicho unachokisema kupambana hapo patazuka ugomvi mkubwa ambao hukuutarajia.Hawachelewi kukimbilia polisi kua umemtishia maisha na kama unavyojua wanasikilizwaga ata kama anayoyaongea ni ujinga.mwisho wa siku wewe mwanaume ndio unaonekana mkorofi na unaingia gharama.ndo maana wanaume wengi wanaamuaga kukaa kimya nakuendelea na harakati zingine.Wanawake waone hivyo hivyo ndugu.
Niliambiwa na dada mmoja hivi!!
Si mkeo kaondoka na kwenda kupanga?
Nikamjibu ndio..
Akaniambia usimfuate we ishi maisha yako atarudi tu siku moja..
Nikamwambia pia nina muda wa yeye kurudi ukipita huo muda asitarajie tena.

Manzi akaniambia ukimfuata tu atakukatia RB na kukusingizia lolote baya.
Anaweza kusema hata kuwa ulitaka kumbakia binti yake..
Maana nilimkuta na mtoto wa kike wakati namuoa na mpaka anaondoka binti yake kafikisha miaka 17.
Akaniambia kaka yake aliwahi kushutumiwa hivyo na wifi yake tena kwa binti yake wa kumzaa kabisa je kwako ambae ni baba wa kambo utafanywa nini??
Nikabaki nalo moyoni..
Sasa ikaja siku nikamuita rafiki yake mke wangu waliokuwa wanaswampa pamoja
Nikamuonya kuhusu tabia yake ya kupenda kujipenyeza kwenye familia za watu na kuvunja ndoa aache atakuja kukutana na majanga..
Nikamwambia kwa aliyoyafanya sidhani kama nitamsamehe milele
Ila namuacha aende kwa kuwa sijapata cha kumfanya..
Akarusha mdomo sana na yuko ndqni kwangu na tuko wawili tu..
Shetani kwakuwa ni mshikaji wangu hakunituma vibaya siku hii aliniheshimu sana maana hata hasira nilikuwa nazitawala vyema.
Baadae akaenda wakayajenga na wife.
Sasa mimi nikiwa kijijini kwetu Mama akaniuliza hizi habari nikamueleza
Nikamuambia ngoja nimpigie simu na wewe usikie sauti kubwa.
Kwanza simu kupokelewa zikaanza shutuma oohoo umeanza kuwatishia marafiki zangu
Na maneno chungu nzima.
TUkajibizana pale mara akaniambia kwa taarifa yako nina RB yako usiwafuatilie marafiki zangu wala mimi.
NIkamuambia kama ni RB hata mimi naweza kukukatia fresh tu kama umefikia huko..
Akasema nimekukatia RB yaani unanifuatilia unataka kunibakia binti yangu??

Nikatabasamu kwa huzuni sana,, Mama alisikia akasema kajinga, Kashetani kabisa hako.
Nakupa miezi sita asiporudi tafuta mke mwingine oa.
Nikawaza miezi sita?
Mimi nishamaliza kupitia hiyo kauli tu,, Nilifanya kama alikufa tu na watoto nikampa ili siku nikioa niwashukie watoto wangu walipo kama Tai..

Ahsante Mungu naishi na mwingine, yeye amebaki kupiga simu tu na kusema wewe ishi na umtakae lakini kama Mungu alipanga uwe mume wangu utakuwa wangu tu.

Nasikitika tu rohoni mwangu..

Ile kauli itaishi ndani mwangu milele..
I wont find forgiveness for a such statement.

Yule dada nilipomueleza alisema, aliitarajia sana na shukurani ni kwamba sikumfuata pale alipohamia maana hiyo ndio silaha yao ya maangamizi wanayoitegemea kumuangushia mwanaume kwa madai ya huyu dada.
 
Na kesi kama yako kabisa. Hapa nawaza namna ya kudeal na huyu mwanamke.
 
Back
Top Bottom