Ahsante ndugu,
Khadija binti Khuwaylid alikuwa mke wa kwanza na mfuasi wa kwanza wa nabii wa Kiislam Muhammad. Khadija alikuwa binti wa Khuwaylid ibn Asad, kiongozi wa kabila la Quraishi huko Makka, na mwanamke mfanyabiashara aliyefanikiwa kwa haki yake mwenyewe.
Khadija mara nyingi hujulikana na Waislamu kama "Mama wa Waumini". Yeye ni mmoja wa watu muhimu zaidi wa kike katika Uislamu.] Muhammad s.a.w alipofikisha miaka 25 ndio alimuoa Bi Khadija naye kwa mke mmoja kwa miaka 25, wakati huo Bi Khadija alikuwa na umri wa miaka 40. Na walizaa watoto sita akiwemo Qasim ibn Muhammad, Abdullah ibn Muhammad, Umm Kulthum, Ruqayyah, Zaynab, na Faṭmah.