Tumebakisha siku 4 kuadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.a.w): Niulize chochote kuhusu Mtume Muhammad (S.A.W.) Nitakujibu

Tumebakisha siku 4 kuadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.a.w): Niulize chochote kuhusu Mtume Muhammad (S.A.W.) Nitakujibu

Zitaje,upingaji wangu na upingajia wako ni ardhi na mbingu hatufanani hata chembe.

Sasa usitafute kichaka,nasubiri jibu la hizo sifa. Usipoteze muda kijana. Huu mjadala wa kielimu usilete utoto na kukinbia maswali.
as log as unapinga haibadili maana kua kwa namna moja au nyingine unavikubali
 
Sasa nijue mara ngapi ? Hujaona nilipo kwambia kama unauliza maswali ya kijinga maswali ambayo laiti kama ungekuwa unatafakari au kufanya utafiti hata wa kiwango kidogo sana usingeuliza maswali kama unayo uliza.

Yaani unaleta habari za makatuni unakuja kujengea hoja katika uhalisia ?

Hivi hukuwahi kusoma somo la "Adabu za kujadiliana na kufanya utafiti" ?
makatuni gani?
 
Ukweli ni kwamba hakuna ushahidi kuwa baba yake na Muhammad alikuwa muislamu
yule mzee Alikua mpagani Kama wapagani wengine wa pale Makka enzi hizo Jamii za wakuraish walikua wanaabudu jiwe jeusi maarufu Kama Kaaba na wapagani wengi walikua wanaenda Kila mwaka kuhiji
Hijja haijaanza na Waislam ilianza kitambo enzi za Giza huko Mohammed alikopi tu Kwa Babu zake ukisoma historia IPO wazi ila Hawa ndugu zetu hua hawaupendi ukweli asilani!
 
Kwanini mnaadhimisha Maulidi (Mazazi) ya Mtume ?

40.HUKMU YA MAWLID​

Written by Said Al Habsy


KHALFAN SALIM from
Kenya
--------------------------------------
Swali:
asalam alaikum warrahamatu Allah wabarakatu je maulid (mazazi ya mtume) yako katika dini yetu ya kiisilamu.
JAWABU:
Walaykum Salaam warahmatullah wabarakatuh.
Maulidi haikuwepo katika zama za Mtume s.a.w. wala masahaba wala wafuasi
wao. Ni kitu kimeanzishwa baada ya muda kupita kama uanzishaji wa vingine
kama mashindano ya Quran, kuweka Maquba msikitini, n.k.
Na kuhusu nani muanzishaji wake kuna khilafu baina ya wanachuoni, na kumjua au kutomjua si muhimu kwani kinachotazamwa ni kuwafikiana na sheria.
Hukmu ya Maulid itategemea malengo na namna ya kuyafanya hayo maulid yenyewe. Ikifanywa vizuri itakuwa nzuri na kinyume chake ndio ubaya wake.
Maulid zinazofanywa katika nchi zetu za Kiafrika na Asia, nyingi zinakuwa na mambo yasiyokubalika kisheria mengi na kuleta madhara hasa katika
kufanyika kwake usiku, kutoka kwa mabinti wa kiislam wari, kuenea kwa
zina, n.k.
Hivyo yakirekebishwa hayo na yakafanyika maulid kwa namna bora kama
kukutana msikitini kukatolewa historia ya Mtume au mawaidha na anasheed za
bila kuruka na kurukaruka, bila madufu, na bila ya kuchanganyika wanaume
na wanawake hakuna dhambi katika hilo bali watapata thawabu.
Na kwa hivyo ametoa fat wa Sheikh wetu Shaban Albattashi - Allah mtukufu amuhifadhi- kuhusu uharam wa maulid hizo zenye hayo makosa tuloeleza.
Na ametazama Sheikh wetu Ahmed Alkhalili - Allah amuhifadhi - uzuri wa yapatikanayo katika maulid zenye nidhamu, na taratibu nzuri akatoa fat wa ya kujuzu kwake, pamoja na kuelekeza kuwa iwe ni msimu wa kujipima kimaendeleo, na njia ya kuelekea katika mapenzi ya vitendo na kumuiga yeye Mtume s.a.w.
Amesema Allah mtukufu:
Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu. 3:31
Pia Amesema Allah mtukufu:
"Hakika nyinyi mnayo ruwaza njema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa anaye mtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na akamkumbuka Mwenyezi Mungu sana." 33:61
Wallahu aalamu.
Abu Muslim Alghammawi
Khamis.alghamawi@ibadhi.com
 
Lengo ni kuongeza mapenzi yetu kwa Mtume, Mtume (saw) alisema, "Hakuna hata mmoja wenu atakayekuwa na imani mpaka anipende mimi kuliko baba yake, watoto wake na wanadamu wote. .

Kulingana na mila ya Kiislamu, wanyama, miti na hata vitu visivyo na uhai kama milima vilionyesha upendo kwa Nabii Muhammad (saw), na pia aliwaonyesha upendo pia. Kwa hivyo, kuongeza upendo wetu kwake na kuionyesha ni sawa na maumbile yote na hutuunganisha na nishati ya kiroho ya ulimwengu.

40.HUKMU YA MAWLID​

Written by Said Al Habsy


KHALFAN SALIM from
Kenya
--------------------------------------
Swali:
asalam alaikum warrahamatu Allah wabarakatu je maulid (mazazi ya mtume) yako katika dini yetu ya kiisilamu.
JAWABU:
Walaykum Salaam warahmatullah wabarakatuh.
Maulidi haikuwepo katika zama za Mtume s.a.w. wala masahaba wala wafuasi
wao. Ni kitu kimeanzishwa baada ya muda kupita kama uanzishaji wa vingine
kama mashindano ya Quran, kuweka Maquba msikitini, n.k.
Na kuhusu nani muanzishaji wake kuna khilafu baina ya wanachuoni, na kumjua au kutomjua si muhimu kwani kinachotazamwa ni kuwafikiana na sheria.
Hukmu ya Maulid itategemea malengo na namna ya kuyafanya hayo maulid yenyewe. Ikifanywa vizuri itakuwa nzuri na kinyume chake ndio ubaya wake.
Maulid zinazofanywa katika nchi zetu za Kiafrika na Asia, nyingi zinakuwa na mambo yasiyokubalika kisheria mengi na kuleta madhara hasa katika
kufanyika kwake usiku, kutoka kwa mabinti wa kiislam wari, kuenea kwa
zina, n.k.
Hivyo yakirekebishwa hayo na yakafanyika maulid kwa namna bora kama
kukutana msikitini kukatolewa historia ya Mtume au mawaidha na anasheed za
bila kuruka na kurukaruka, bila madufu, na bila ya kuchanganyika wanaume
na wanawake hakuna dhambi katika hilo bali watapata thawabu.
Na kwa hivyo ametoa fat wa Sheikh wetu Shaban Albattashi - Allah mtukufu amuhifadhi- kuhusu uharam wa maulid hizo zenye hayo makosa tuloeleza.
Na ametazama Sheikh wetu Ahmed Alkhalili - Allah amuhifadhi - uzuri wa yapatikanayo katika maulid zenye nidhamu, na taratibu nzuri akatoa fat wa ya kujuzu kwake, pamoja na kuelekeza kuwa iwe ni msimu wa kujipima kimaendeleo, na njia ya kuelekea katika mapenzi ya vitendo na kumuiga yeye Mtume s.a.w.
Amesema Allah mtukufu:
Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu. 3:31
Pia Amesema Allah mtukufu:
"Hakika nyinyi mnayo ruwaza njema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa anaye mtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na akamkumbuka Mwenyezi Mungu sana." 33:61
Wallahu aalamu.
Abu Muslim Alghammawi
Khamis.alghamawi@ibadhi.com
 
Ufunuo wa kwanza wa Muhammad lilikuwa tukio lililoelezewa katika mila ya Kiisilamu kama ilifanyika mnamo AD 610, wakati ambapo nabii wa Kiislam, Muhammad alitembelewa na malaika Jibrīl, anayejulikana kama Gabrieli kwa Kiingereza, ambaye alimfunulia mwanzo wa kkitabu cha Qur.'an. Hafla hiyo ilifanyika katika pango liitwalo Hijra, lililoko kwenye mlima Jabal an-Nour, karibu na Makka. Ilikuwa Jumatatu, tarehe 21 ya Ramadhani kabla tu ya jua kuchomoza, yaani Agosti 10, 610 - wakati Muhammad alikuwa na miaka 40. Baada ya hapo aya za kitabu kitukufu zilikuwa zikishuka kulingana na matukio husika nasio mapangano.

.............
Abu Lahab alikuwa mjomba wa mtume Muhammad, ndiye mtu pekee kutoka kwa maadui wa Uislamu ambaye amelaaniwa kwa jina lake katika Qur'an Tukufu. Baada ya mtume kutangaza kuwa yeye ni mjumbe wa MUNGU Watu walitawanyika wakinung'unika kimya kimya, lakini Abu Lahab, ambaye kila wakati alimpenda mpwa wake Mohammed (S.A.W.), alimpinga vikali kwa sababu aliona ujumbe huo kuwa changamoto kwa uongozi wake.

Wakati Mtume Muhammad (SAW) alikuwa akitoa hotuba yake ya kwanza hadharani wakati akiwaalika watu wa kabila la Quraishi kwenye Uislam kwa mara ya kwanza hadharani, hakuna mtu aliyemtukana Nabii Mohammed (s.a.w) ispokuwa mjomba wake Abu Lahab mwenyewe, Nabii Mohammed (s.a.w) alitumia kimya kujibu tusi la Mjomba wake lakini Mwenyezi Mungu (SWT) hakufanya hivyo na akafunua ufunuo wa kumlani Abu lahab. Hivyo basi alimpinga mtume kwa kuhofia uwongozi wake.
Asante kiongozi Mimi ni mkristu navutiwa na watu wenyemajibu mirua matamu Kama wewe hakika wewe ndye muislamu
MUNGU akubariki Sana.
 
Ahsante mtoa mada kwa maelezo,ujuzi na ufafanuzi kuhusu maswali mbalimbali yanayoulizwa na wachangiaji tofauti. Pia nakusifu kwa uvumilivu wa kuulizwa maswali ya kitoto na kejeli nadharau. Huo ndiyo ukomavu!!!
Maelezo:Mtume alipofariki ,kabla hajazikwa kulitokea sintofahamu ya nani anapaswa kumrithi kati ya wafuasi wa Abu Bakr (Baba Mkwe na Rafiki kipenzi wa mtume) na Ali ibn Abi Talib (Binamu na mkwe wa mtume)( Naomba kusamehewa kama nimekosea vyote hapo juu)

Swali 1: Kwanini Mtume aliacha hali hii itokee?? Hakuona??Hakuota??Hakuwaza mbele ??

Swali 2: Huoni yeye ndiye chanzo cha madhehebu makuu ya Sunni (Wafuasi wa Abu Bakr na Shia (Wafuasi wa Ali)???

Swali 3: Uislamu baada ya kifo cha mtume kwa kiasi kikubwa ulienezwa kwa kutumia nguvu kubwa( Ncha ya upanga) kuliko ushawishi.Nini sababu?

Swali 4: Baada ya kifo cha mtume wengi wao kama siyo wote waliomfuatia walikufa kwa ugomvi mkubwa wa kugombea madaraka.Walikosea wapi??Kipi kilisababisha??Mungu alikuwa wapi wakati haya yote yanatokea???
Swali la 5: Ukijitoa kwenye vazi la udini, huoni yote yaliyotokea ni hali ya kawaida ya kibinaadamu kwenye kugombea madaraka usipowekwa msingi mzuri wa kurithi na kuna makosa yalitokea??

Nb: Samahani sana kama nimekukosea na kukejeli .
 
yule mzee Alikua mpagani Kama wapagani wengine wa pale Makka enzi hizo Jamii za wakuraish walikua wanaabudu jiwe jeusi maarufu Kama Kaaba na wapagani wengi walikua wanaenda Kila mwaka kuhiji
Hijja haijaanza na Waislam ilianza kitambo enzi za Giza huko Mohammed alikopi tu Kwa Babu zake ukisoma historia IPO wazi ila Hawa ndugu zetu hua hawaupendi ukweli asilani!
Nani kasema Alkaaba kaianzisha Muhammad (s.a.w)?
 
Kwanini asiitwe marehemu mtume ? Maana haidaiwi kuwa alikimbia kaburi kama yule mwingine
Ahsante ndugu. Kwasababu sisi waisilamu tunamaamini kwamba Mtume yupo hai, japokuwa alifariki lakini bado yupo hai katika nyoyo zetu
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Ila watu ,Hapana hakuvaa nguo za kike na katika Uislam mwanaume kuvaa nguo za kike hairuhusiwi vilevile mwanmke kuvaa nguo za kiume
Ni Kweli alikuwa anavaa nguo Za kike kama magauni ya Aisha??
 
Ni Kweli alikuwa anavaa nguo Za kike kama magauni ya Aisha??
Hapana sio kweli, huo ni uwongo wenye kumdhihaki mtume, hakuna hadithi wala chanzo chochote cha kuaminika kunako habari hiyo. Ikiwa hata leo unavutiwa kusoma kwa moyo wazi wasifu wake na usiamini upotoshaji huo, hakuna chochote hasi cha nabii wetu utacho kutana nacho. Alikuwa ni mwenye tabia safi kabisa.
 
Kwanza kwa ushahid wa Quran wenyewe

Mwenyezi Mungu (s.w) ameikusudia Qur-an iwe kitabu hata kabla ya kuumbwa chochote katika maumbile yake aliyo yaumba.Kama inavyoashiriwa katika aya mbali mbali kwamba Qur-an ilikuwako kwenye Lawhil Mahfudh hata kabla ya kuteremshwa kwa Mtume (s.a.w) kulingana na matukio mbali mbali yalivyotokea:

“Bila shaka hiki (mnacho somewa) ni kitabu kilichokusanya kila yanayohitajiwa na chenye heshima. Kimetolewa katika hicho kitabu kilicho hifadhiwa kweli kweli."
(Qur-an 56:77-78).


"Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uongozi kwa wamchao Mwenyezi Mungu."
(Qur'an 2:2).

vile rejea Qur-an 3:3, 7; 7:2; 10:1; 13:1; 14:1, n.k

Kutokana na marejeo hayo haiwezekani kuwa pawe hapana kitu cha aina hiyo lakini bado Mwenyezi Mungu arudie namna hiyo neno "kitab" linatumika kwa vitu mbali mbali vilivyoandikwa kama mikataba au hata barua lakini bado katika Qur-an neno hili limetumika kurudia kitabu katika maana halisi hasa ya kitabu.

Hivyo Allah(s.w) alipotaja neno Al-Kitab kwa kuirudia Qur-an alikuwa na maana hiyo .

Ushahidi wa kihistoria

Katika hadithi maarufu sana iliyo pokelewa na Imam Muslim toka kwa Ibnu Mas-'ud, Mtume amesema katika Hijja yake ya kuaga kuwa:

"Na nimewaachieni vitu wili ambavyo mkishikamana navyo hamtapotea kamwe baada yangu - Kitabu cha Allah na Sunnah yangu." (Musilim)

Hadith hii kiakili haiashirii kitu ambacho hakijulikani kilipo na chenye ugumu kupatikana kama alivyoeleza Zaid (r.a) bali ni kitu ambacho kila mmoja anatarajiwa kukifikia pasipo na ugumu wowote. Wala Hadith hii haishirii kitu ambacho kimetawanyika katika mawe na mifupa ambayo pa kupatikana hapafahamiki bali ni kitu kilichokusanywa na kuhifadhiwa mahala
maalumu.Mtume(s.a.w) asingelisema hivyo kama kitabu hicho hakikuwepo

Ukiacha hadithi hiyo, kuna hadithi nyingine ambayo ameipokea mwenyewe Imamu Bukhari ambayo inasema wazi kabisa kuwa Mtume ameacha Msahafu:

'Abdul'-Aziz bin Rufai(ra) ameeleza kuwa: "Mimi na Shaddad bin Ma'aqil tuliingia kwa Ibnu "Abbas. Shaddad akamuuliza:
Je Mtume (s.a.w) ameacha chochote?" akajibu (Ibn 'Abbas) "Hakuacha chochote isipokuwa (hiki) kilichopo baina ya magamba mawili (ya Qur-an)." Baadaye tulimtembelea Muhammad bin Al-Hanafiyya na akamuuliza suala (lile lile). Akajibu (Al-Hanafiyya), Mtume hakuacha kitu isipokuwa (hiki) kilichopo baina ya magamba mawili (ya Qur-an)."

Hadithi hii, kwanza, inaisadikisha Qur-an kuwa ni kitabu (mas-hafu) ambacho kimeandikwa katika kurasa na kuwekewa magamba (bindings or covers) ili kihifad hike.

Pili, Hadithi hii inaisadikisha Hadith tuliyoirejea juu miongoni mwa vitu ambavyo Mtume ameviacha. Hapa tunaambiwa alichoacha ni kile kilicho baina ya magamba mawili - la mwanzo na mwisho - yaliyokuwa yamehifadhi Qur-an ambayo hapana shaka ilikuwa ndani ya karatasi za aina yake
Nashukuru kwa kuchukua muda kujibu.
Nadhani swali langu hujalielewa. Wewe unaamini Mungu aliishusha Quran na hilo linatosha. Ila kwangu qmbaye siamini, hupaswi kuanzia hapo. Kwa sababu kabla ya kuamini shahada lazima niwe na uhakika kweli aliwahi kuishi mtu anayeitwa Muhammad, ambaye ndiye aliyeshushiwa Quran na Allah na kuwa hadith na sira ni za kuaminika.

Sasa kwa sababu kwa maelezo ya Quran, Sira na Hadith ni kuwa Muhammad aliishi katika historia ya mwanadamu, alikuwa kiongozi wa kiroho na kijeshi na utawala wake ulikuwa na eneo sio dogo mpaka kifo chake, basi tunatarajia kukuta angalau taarifa juu yake katika vyanzo vya nje ya Quran hadith na sira.

Tunatarajia kukuta majina ya miji kama Maka, Madina, n.k. majina angalau ya Ma Khalifa waliomfuata kama Uthman na Abu Bakr.

Kwa utafiti niliofanya hizi taarifa hazipo. Hata Quran, Hadith na Sira zimeandikwa miaka mingi sana baadaye, na watu ambao hawakuwahi kushuhudia chochote kwa macho yao.

Ndii nikamuuliza mtoa mada na yeyote anayeweza kunisaidia, kuna historia yoyote anayoifahamu, historia toka karne ya 7, au iliyoandikwa na mashuhuda? Mimi sijaweza kuipata, lakini haimaanishi haipo.

Naamini umenielewa!
 
Unataka kumaanisha nini ndugu? kuna hoja yoyote unataka kuiweka ? Qur'an Iliandaliwa chini ya swahaba aitwae Uthman miaka ishirini baada ya kifo cha Mtume Muhammad s.a.w.
Ninachomaanisha ni hiki nikichoandika ndugu yangu. Sina maana nyingine. Ninatafuta vyanzo vya kihistoria kuhusu uislam vinavyotoka karne ya 7. Ni kawaida tu mtu anapotaka kujua historia ya kitu huenda kuangalia ndani ya karne mambo yalitendeka.

Hii ya Quran kundaliwa na Khalif Uthman, ni inatoka kwenye hadith (sina hakika kama kwenye sira imeandikwa pia). Ila nimejaribu kuangalia waandishi wa hadith kama Muslim, al Bukhari, n.k. wanaandika miaka mingi sana baadaye.

Kwa hiyo kwa mtu anayetafiti, hii inakuwa haimfai, kwa sababu kihistoria hawa hawakuwahi kushuhudia walichokiandika na wala hawakuandika kipindi wale mashuhuda wakiwa hai, ili kama wamepunguza ama kuongeza wawakosoe.

Natumaini swali langu nimeliweka kwa uwazi zaidi, na naomba nilirudie: Unaweza nisaidia vyanzo vya historia na matukio ya Uislam, vya karne ya 7 au vilivyoqndikwa na shuhuda?
Ahsante
 
Ahsante mtoa mada kwa maelezo,ujuzi na ufafanuzi kuhusu maswali mbalimbali yanayoulizwa na wachangiaji tofauti. Pia nakusifu kwa uvumilivu wa kuulizwa maswali ya kitoto na kejeli nadharau. Huo ndiyo ukomavu!!!
Maelezo:Mtume alipofariki ,kabla hajazikwa kulitokea sintofahamu ya nani anapaswa kumrithi kati ya wafuasi wa Abu Bakr (Baba Mkwe na Rafiki kipenzi wa mtume) na Ali ibn Abi Talib (Binamu na mkwe wa mtume)( Naomba kusamehewa kama nimekosea vyote hapo juu)

Swali 1: Kwanini Mtume aliacha hali hii itokee?? Hakuona??Hakuota??Hakuwaza mbele ??

Swali 2: Huoni yeye ndiye chanzo cha madhehebu makuu ya Sunni (Wafuasi wa Abu Bakr na Shia (Wafuasi wa Ali)???

Swali 3: Uislamu baada ya kifo cha mtume kwa kiasi kikubwa ulienezwa kwa kutumia nguvu kubwa( Ncha ya upanga) kuliko ushawishi.Nini sababu?

Swali 4: Baada ya kifo cha mtume wengi wao kama siyo wote waliomfuatia walikufa kwa ugomvi mkubwa wa kugombea madaraka.Walikosea wapi??Kipi kilisababisha??Mungu alikuwa wapi wakati haya yote yanatokea???
Swali la 5: Ukijitoa kwenye vazi la udini, huoni yote yaliyotokea ni hali ya kawaida ya kibinaadamu kwenye kugombea madaraka usipowekwa msingi mzuri wa kurithi na kuna makosa yalitokea??

Nb: Samahani sana kama nimekukosea na kukejeli .
Ahsante ndugu.

------1
Wasunni wanaamini kwamba Mtume hakuwa ameteua mrithi na badala yake alikuwa amekusudia jamii ya Waislamu kuchagua kiongozi kati yao. Wanakubali utawala wa Abu Bakr, ambaye alichaguliwa huko eneo la Bani Saqifah, na ule wa warithi wake, ambao wote wanajulikana kama Makhalifa wa Rashidun.

Swala la Mrithi wa Muhammad ni jambo kuu ambalo liligawanya jamii ya Waislamu katika mafungu kadhaa katika karne ya kwanza ya historia ya Kiisilamu, na kutokea madhehebu ya Shia na Sunni. Uislamu wa Shia unashikilia kwamba Ali ibn Abi Talib ndiye mrithi aliyeteuliwa wa nabii wa Kiislamu baada ya Muhammad kama mkuu wa jamii. Uislamu wa Kisuni unashikilia Abu Bakr kuwa kiongozi wa kwanza baada ya Muhammad kwa msingi wa uchaguzi.

Kwa upande mwingine, Shia wanaamini kwamba Ali alikuwa ameteuliwa na Mtume kuwa mrithi baada yake, haswa wakati wa hafla ya Ghadir Khumm. Kwa maoni ya Shia, warithi halali wa Muhammad ni Ali na Maimamu kumi na wawili wa ukoo wake, ambao wanaonekana kama walioteuliwa na Mungu. Na wa mwisho katika hao Maimamu 12, anaitwa Mahdi, ambaye ujio wake unangojewa na kukubalika na Shia na Sunni kwa pamoja.
Kwa hivyo, mtume alichagua uwongozi baada yake na alimchagua Ali ibn Abi Talib kwenye hadhara ya maelfu ya maswahaba kulingana na ushahidi mbalimbali, lakini baada ya kufa Mtume, waliokuwepo hawakufuata hayo maagizo. Nadhani ni mtihani ambao MUNGU aliwapima ili kutimiza kauli ya Mtume s.a.w aliyosema kwamba umati wangu utagawanyika makundi 73.

--------2
Mtume siyo chanzo cha madhehebu japokuwa mwenyewe aliacha ametabiri kwamba umati wake utagawanyika makundi 73

------3,4
Hakika baada ya kufa mtume watu walisambaratika sana, na waisilamu waliuwana wenyewe kwa wenyewe kwa kugombania maslahi ya uwongozi, na pia baadhi ya watu waliingiza mila zao katika dini. Huu wote ni mtihani bado ili kupima imani zao, nasisi kutupa juhudi ya kuupambania ukweli.

-----5
Misingi ilikuwa imara lakini watu walikengeuka, kumbuka mtume alipigana vita mbili, moja ni kupigana na wasio waisilamu lakini pili ni kupigana na wanafiqi ambao walijivika vazi la uwislamu. Wanafiqi ni maadui ambao unakuwa nao pamoja bila ya wewe kuwafahamu. Hii yote ni mitihani. Lau kama kila kitu kingelikuwa sawa kusingekuwa na juhudi za watu kupembua mambo, ndio maana MUNGU aliacha hili litokee.
 
Je, Mtume alisema siku ya kiyama tutapewa mabikira 70?
Je, kama ndivyo tutatumia mkongo au alkasusu?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom