KERO Tumekwama ndani ya Treni ya SGR hapa Ngerengere kwa saa tatu sasa, tunaambiwa kuna suala la kiufundi

KERO Tumekwama ndani ya Treni ya SGR hapa Ngerengere kwa saa tatu sasa, tunaambiwa kuna suala la kiufundi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Treni 6

Tatu kutoka Dom - Dar moja ilikua inatoka Moro, na tatu nyingine Dar - Moro - Dom


Treni iliyotoka saa nane mchana haijafika Dar
Mbn niliona taarifa ya TRC wakiomba radhi kwa tatizo husika,

Ina maana hawajafika walipokuwa wanaelekea mpaka sasa ?
 
Treni zinazofanya kazi kwa siku ni 4 tu , hiyo idadi uliyotaja Haina uhalisia.
Treni ya kwanza ni ya Dom _dar ya asubuhi 11.00 ambayo ndo inakuja kubeba abiria wa sa Tatu kutoka dar _ dodoma na kurudi kutoka dar saa 17.00 jion

Ya pili dar_ Dom saa 12.00 asubuhi inakuja beba abiria wa dom_dar saa 14.10 na kurudi dodoma tena kutokea dar saa 18.00
Treni ya Tatu ni royal ambayo inapiga go and return kwa siku na ni moja nyerere.
Yaa nne ni Ile ya moro dar ambayo inapiga trip ya jion kwenda moro saa 16.00
Kwa ujumla Kuna treni nne tu mbili zinapiga trip Tatu kwa siku na mbili zinapiga go and return.
Hizo treni 6 umezitolea wapi?
 
Mbn niliona taarifa ya TRC wakiomba radhi kwa tatizo husika,

Ina maana hawajafika walipokuwa wanaelekea mpaka sasa ?
Leo kumekuwepo na mvua sana tena zenye radi, nahisi zimeleta madhara hiyo ni kawaida kwa treni za umeme inatakiwa tuwe na vichwa vya diesel kwa dharura kama ya leo
 
Mbn niliona taarifa ya TRC wakiomba radhi kwa tatizo husika,

Ina maana hawajafika walipokuwa wanaelekea mpaka sasa ?
Morogoro ziko mbili zimepaki

Njian ziko mbili zimepaki

Kutoka Dar mbili, tumesikia hazijatoka
 
kwanza hao trc ni wababaishaiji sana aisee! wameongeza nauli kimya kimya ya train kwa safari za express za asubuh kutoka Dar saa 12:00 na kutoka Dodoma saa 11:15 asubuhi. kama latra ameshirikishwa basi na wao ni wahuni tu kwa sababu ilipaswa consumers watangaziwe. Nauli imepanda kutoka 40k to 50k kinyemela
 
Leo kumekuwepo na mvua sana tena zenye radi, nahisi zimeleta madhara hiyo ni kawaida kwa treni za umeme inatakiwa tuwe na vichwa vya diesel kwa dharura kama ya leo
Aseeh poleni sana wazee, hasa kipindi Cha mvua safari zinakuwa zenye changamoto.... Ila mpo salama ?
 
Morogoro ziko mbili zimepaki

Njian ziko mbili zimepaki

Kutoka Dar mbili, tumesikia hazijatoka
Hao wa njian watalala humo humo au inakuaje? Na ukute watu wanasafiri kwa mambo yanayowahitaji kwa haraka...... Aseeh poleni wazee kwa changamoto hiyo.....
Pengine hata mabasi kwa kipindi hiki ni Bora zaidi kuliko hizo sgr! nimejaribu tu kuwaza.
 
kwanza hao trc ni wababaishaiji sana aisee! wameongeza nauli kimya kimya ya train kwa safari za express za asubuh kutoka Dar saa 12:00 na kutoka Dodoma saa 11:15 asubuhi. kama latra ameshirikishwa basi na wao ni wahuni tu kwa sababu ilipaswa consumers watangaziwe. Nauli imepanda kutoka 40k to 50k kinyemela
Kweli aisee duuuh huu ni wizi latra kimyaa
 
Serikali na biashara Umesikia wapi....We umesikia wapi
Kweli kwa nchi masikini ni shida sana ila kwa wenzetu ni sawa tu
Uingereza walibinafsisha mashirika ya Reli miaka ila sasa wameona makampuni yanasuasua na leo wametangaza kuwa Serikali inarudisha mpira kwapani hakuna cha reli binafsi kuanzia mwakani
Mikataba ikiisha basi
Ila wenzetu Serikali inamudu haya na ajira zitaongezeka
Sisi kila cha Serikali ni shamba la bibi
 
Halafu muda huu wanafunzi wanaenda likizo!
Kwenye mabasi nauli kky kwenye sgr nauli poa...
 
Baada ya Treni ya SGR kukwama awali asubuhi ya leo, Desemba 4, 2024, mimi ni mmoja kati ya abiria ambao walikuwemo kwenye treni hiyo, nikaona JamiiForums imeripoti kuhusu tukio hilo.

Mpaka muda huu naandika hapa saa Tatu usiku huu ni kwamba tumekwama kwenye kituo cha Ngerengere tukiwa tunatokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam.

Tangu saa Kumi na Moja jioni mpaka muda huu Treni imesimama hapa, maafisa wa humu ndani ya Treni wanatuambiwa kuwa kuna ishu ya kiufundi ndio tatizo.

Soma
~
Treni ya SGR kutoka Dar kwenda Dodoma yadaiwa kukwama tena baada ya Umeme kukatika Stesheni ya Kilosa
~ TRC: Treni za SGR zilisimama maeneo matatu tofauti kutokana na hitilafu ya umeme katika Gridi ya Taifa
1741155343767.png
 
Back
Top Bottom