DOKEZO Tumevunjiwa maeneo yetu ya biashara Tungi Mnadani - Kigamboni bila taarifa, tunaomba msaada wa Serikali

DOKEZO Tumevunjiwa maeneo yetu ya biashara Tungi Mnadani - Kigamboni bila taarifa, tunaomba msaada wa Serikali

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
photo_2024-11-19_17-23-11.jpg

photo_2024-11-19_17-23-09.jpg
Sisi Wafanyabiashara wadogowadogo tuliokuwa tukifanya shughuli zetu za biashara katika eneo lililopo jirani na ofisi za World Oil eneo la Tungi Mnadani, Kigamboni hapa Dar es Salaam.

Tulianza kufanya biashara kwa takribani miaka miwili iliyoputa na tukajenga vibanda vyetu eneo hilo, tulitumia biashara hiyo kuendesha familia zetu kwa kipato ambacho tulikipata hapo.

Miezi ya hivi karibuni kukatokea mvutano baina ya pande mbili ambazo zote zilijitambulisha kuwa zinamiliki eneo hilo.

Upande wa kwanza ni Ofisi ya World Oil ambao walitutaka tuhame eneo hilo wakidai ni la kwao, tuliwapinga na tukawasilisha malalamiko yetu kwa Ofisi ya Katibu Tawala Kigamboni, akawaandikia barua ya wito ili kujadili suala hilo.

Mazungumzo yakafanyika kati yetu Wafanyabiashara na World Oil tukakubaliana nao kuwa watatulipa fidia ili kuondoka eneo hilo, japokuwa kulikuwa na upande wa pili wa mmiliki mwingine ambaye ni mfanyabaishara maarufu naye alidai lile eneo ni lake.

Wakati tunasubiri kujua hatma ya eneo hilo, tumekuta miundombinu ya biashara zetu yote imebomelewa usiku, hatujui aliyebomoa lakini taarifa tulizopewa ni kuwa World Oil ndio wamehusika kubomoa maeneo yetu.

Tunaomba Serikali itusaidie kwani, kama ni mgogoro ulikuwa unaendelea kutafutiwa utatuzi ila kuna Wahuni wamejitokeza na kuvunja, wameharibu mitaji yetu, tumebaki na majuto.

Huyu ni nani ambaye ana nguvu kiasi cha kubomoa bila kibali na bila taarifa huku vitu vyetu vingi vikiwa ndani, kuna hasara kubwa imepatikana, tunaomba msaada wa Serikali Kuu inaonekana aliyefunja ana nguvu kuliko hata mamlaka za Serikali nyingine zilizowekwa huku Kigamboni.


photo_2024-11-19_17-22-53.jpg

photo_2024-11-19_17-22-58.jpg

photo_2024-11-19_17-23-01.jpg

photo_2024-11-19_17-23-06.jpg

photo_2024-11-19_17-23-03.jpg
 
Yaani ni majonzi makubwa.
Ukizingatia hizi biashara zilikiwa na mikopo mingi tu lakini mpaka Sasa hatujui hatima ni nini
Wenye pesa Tanzania wana nguvu sana kuweni makini sana na uhai wenu,maana kama wameweza kuwafanyia hivyo kwenye biashara zenu basi mjuwe hawashindwi kutoa uhai wenu pia wakitaka!!
 
Wenye pesa Tanzania wana nguvu sana kuweni makini sana na uhai wenu,maana kama wameweza kuwafanyia hivyo kwenye biashara zenu basi mjuwe hawashindwi kutoa uhai wenu pia wakitaka!!
😟😟😟😟😟, biashara zetu je
 
Kutokana na maelezo yako ya awali,inaonekana mlivamiya eneo la wazi bila kujuwa ni la nani, kwa kutumia wingi wenu mkadhani kwamba mtakuwa na kinga kisheria,msichojuwa hizo mali na miundombinu mnayodai mliweka,yote ni ya mwenye eneo hilo.
 
Sisi Wafanyabiashara wadogowadogo tuliokuwa tukifanya shughuli zetu za biashara katika eneo lililopo jirani na ofisi za World Oil eneo la Tungi Mnadani, Kigamboni hapa Dar es Salaam.

Tulianza kufanya biashara kwa takribani miaka miwili iliyoputa na tukajenga vibanda vyetu eneo hilo, tulitumia biashara hiyo kuendesha familia zetu kwa kipato ambacho tulikipata hapo.
Mlianza kufanya biashara katika hilo eneo kwa kibali cha nani?
Mlikodishiwa na nani?
Mlikuwa mnalipa kodi ya eneo kwa nani?
 
Yaani nyie wafanya bihashara wadogo mliambiwa mhame mkakataa madam mpaka mlipe fidia? Sasa hapo ndo sijaelewa, mlitaka kulipwa fidia ya nini wakati eneo sio la kwenu ni kama vile mlivamia au kama serikali ndo iliwaelekeza mfanyie biashara hapo basi ni halal kuomba msaada.
 
Back
Top Bottom