DOKEZO Tumevunjiwa maeneo yetu ya biashara Tungi Mnadani - Kigamboni bila taarifa, tunaomba msaada wa Serikali

DOKEZO Tumevunjiwa maeneo yetu ya biashara Tungi Mnadani - Kigamboni bila taarifa, tunaomba msaada wa Serikali

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Si mmeshamaliza kuwachagua wandugu? Mlitegemea ile petipeti itaendelea! Mnaposikia kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe mnafikiri ni mbinguni? No ni hapahapa wazee
 
Hii ndio serikali ya CHURA.watanganyika tutateseka MNO! Chini ya uyo znz.
All the best
 
Sa mnataka mlipwe fidia halafu eneo la azizi kawaeka Kwa hisan?
Mmejenga na kuwekeza kwenye eneo la mtu mwingine.mnalipwaje fidia.?
Hameni hapo katafuteni eneo jingine,mwacheni Aziz apambane na Wo.wakiyaweka sawa na muafaka uukifikiwa ndo mtajua mnarudi au la.
 
Poleni sana kwa yaliyowakuta. Mimi ningewashauri wafanyabiashara ndogondogo, badala ya kutumiwa na wanaiasa, hasa ccm, mitano tena, sijui mama anaweza n.k

Ni bora muungane, muombe maeneo salama, yanayokidhi biashara zenu mtulie. Serikali haikosi maeneo ya wazi ya kuwapa kufanya biashara, wakawa wanachukua ushuru.

Na uchaguzi wa mwakani ukiisha, mtakuwa na hali ngumu sana. Wa Kariakoo watatolewa, na nyote mliovamia maeneo ya wazi mtatolewa pia, sababu mtakuwa mmetumiwa, hamna kazi tena. Mjipange.
 
Aisee watu mnapenda kukurupuka sana, hivi we Kwa akili Yako unahisi mtu aende avamie sehemu hajui ya nani aanze kufanya biashara Tena ya pesa kubwa?????
Hii sehemu ni ya ROSTAM AZIZI.
NA kama mmesoma vizuri hapo hatimiliki ni jina la ROSTAM AZIZI, na sisi yeye ROSTAM ndio alikabidhi hii sehemu kwetu. Baadae jirani na sehemu hii ya ROSTAM ambapo ndio tunafanyia biashara akawa amenunua World Oil. Mara ghafla akaja anatwambia hii sehemu tulipo pia ni ya kwakwe, swali hii sehemu inakuwaje ya kwakwe wakati alietukabidhi hapa ni ROSTAM AZIZI?????
Kuja kufuatilia tukaambiwa ROSTAM na world Oil wana mvutano, na ndo maana Huyu MMILIKI WA WORD OIL anasema hii sehemu ni yake tuondoke.

Sasa na sisi kama wafanyabiashara hatukutaka kero tukakubaliana nae atulipe fidia tuondoke yeye akamalizane na ROSTAM Sasa inakuwaje badala ya kutulipa yeye anatuma watu wabomoe?????
Siku nyingine muwe mnasoma na kuelewa sio mnakimbilia kusema msoyajua
ommytk
chiembe
Msigazi Mkulu
Yoda
Na wengine punguzeni ujuaji
Maandishi ya Rostam kuwapa hiyo ardhi yapo? Mna transfer documents ? Zilipita wizara ya ardhi? Ardhi huwezi kupewa kama unavyopewa pipi, hasa iliyopimwa.

Mlipewa kama mtu mmoja mmoja? Mlifanya sub division ya viwanja? Mna kibali hicho? Nyaraka za kulipia kodi zinamtaja nani? Mlifanya search Wizara ya ardhi mkajua aliyewapa ni lake au kawaachia jumba bovu mjikinge mvua, na sasa limewadondokea?
 
Nikiwapa pole nitakuwa mnafki, ukweli ni kwamba eneo wanalo lalamika kubomolewa nila serikali? Je walikaa hapo na kufanya biashara kwa ruhusa ya nani? Waki itwa wavamizi ni sawa? Wanalipa pango?
Conclusion nikiwa kama Mtanzania najuwa matatizo ya watanzania wenzangu tuna penda kulalamika na kuonewa huruma sana kwa kisingizio wao ni maskini. Ukweli ni kwamba walivamia eneo wamejenga vibanda kimya kimya wamefanya biashara mwisho wakaona kama ni haki yao kuwa hapo,je hawa kujuwa kuwa walipo sio eneo la wazi, na hata kama ni eneo la wazi kuna utaratibu wa kwenda kufanya biashara eneo hilo. Wanapo taka fidia wao wanatoa fidia gani kwa kutumia eneo la mwenyewe kwa miaka miwili? tusipende sana kuwa watu wa kulalamika wakati ukweli upo wao ni wavamizi wasijitete kwa mgongo wa mikopo ndio mana kuna hasara sheria ikifwata mkondo na wao walipe fidia kuvamia eneo na kufanya biashara. Kuto kulizwa kwanini wamefanya biashara kwenye eneo miaka miwili hapa wapi nafasi wao kuona ni haki kufanya biashara ni eneo la watu watabaki kuwa wavamizi wa maeneo ya watu.
Mawazo yangu na niko tayari kurekebishwa
 
Aisee watu mnapenda kukurupuka sana, hivi we Kwa akili Yako unahisi mtu aende avamie sehemu hajui ya nani aanze kufanya biashara Tena ya pesa kubwa?????
Hii sehemu ni ya ROSTAM AZIZI.
NA kama mmesoma vizuri hapo hatimiliki ni jina la ROSTAM AZIZI, na sisi yeye ROSTAM ndio alikabidhi hii sehemu kwetu. Baadae jirani na sehemu hii ya ROSTAM ambapo ndio tunafanyia biashara akawa amenunua World Oil. Mara ghafla akaja anatwambia hii sehemu tulipo pia ni ya kwakwe, swali hii sehemu inakuwaje ya kwakwe wakati alietukabidhi hapa ni ROSTAM AZIZI?????
Kuja kufuatilia tukaambiwa ROSTAM na world Oil wana mvutano, na ndo maana Huyu MMILIKI WA WORD OIL anasema hii sehemu ni yake tuondoke.

Sasa na sisi kama wafanyabiashara hatukutaka kero tukakubaliana nae atulipe fidia tuondoke yeye akamalizane na ROSTAM Sasa inakuwaje badala ya kutulipa yeye anatuma watu wabomoe?????
Siku nyingine muwe mnasoma na kuelewa sio mnakimbilia kusema msoyajua
ommytk
chiembe
Msigazi Mkulu
Yoda
Na wengine punguzeni ujuaji
Mnakiri wazi eneo sio lenu.afu mna taka mlipwe fidia ? Amjui kama jamaa akikaza nyie ndo mta takiwa kumlipa fidia kwa kufanya uharibifu na ku trespass
 
Aliyekuwa RC wa Simiyu, Dkt Nawanda ashinda kesi ya “kumlawiti Mwanafunzi”, asema anamuachia Mungu
 
Basi wangetumia busara, siku 1 kabla ya kubomoa, wangewapa taarifa.
Wangetumia utu wa kibinadamu.
huwajui waswahili wewe, huoni hata huyu eneo sio lake walala la bibi yake lakini kashajimilikisha eti anataka fidia
 
Sisi Wafanyabiashara wadogowadogo tuliokuwa tukifanya shughuli zetu za biashara katika eneo lililopo jirani na ofisi za World Oil eneo la Tungi Mnadani, Kigamboni hapa Dar es Salaam.

Tulianza kufanya biashara kwa takribani miaka miwili iliyoputa na tukajenga vibanda vyetu eneo hilo, tulitumia biashara hiyo kuendesha familia zetu kwa kipato ambacho tulikipata hapo.

Miezi ya hivi karibuni kukatokea mvutano baina ya pande mbili ambazo zote zilijitambulisha kuwa zinamiliki eneo hilo.

Upande wa kwanza ni Ofisi ya World Oil ambao walitutaka tuhame eneo hilo wakidai ni la kwao, tuliwapinga na tukawasilisha malalamiko yetu kwa Ofisi ya Katibu Tawala Kigamboni, akawaandikia barua ya wito ili kujadili suala hilo.

Mazungumzo yakafanyika kati yetu Wafanyabiashara na World Oil tukakubaliana nao kuwa watatulipa fidia ili kuondoka eneo hilo, japokuwa kulikuwa na upande wa pili wa mmiliki mwingine ambaye ni mfanyabaishara maarufu naye alidai lile eneo ni lake.

Wakati tunasubiri kujua hatma ya eneo hilo, tumekuta miundombinu ya biashara zetu yote imebomelewa usiku, hatujui aliyebomoa lakini taarifa tulizopewa ni kuwa World Oil ndio wamehusika kubomoa maeneo yetu.

Tunaomba Serikali itusaidie kwani, kama ni mgogoro ulikuwa unaendelea kutafutiwa utatuzi ila kuna Wahuni wamejitokeza na kuvunja, wameharibu mitaji yetu, tumebaki na majuto.

Huyu ni nani ambaye ana nguvu kiasi cha kubomoa bila kibali na bila taarifa huku vitu vyetu vingi vikiwa ndani, kuna hasara kubwa imepatikana, tunaomba msaada wa Serikali Kuu inaonekana aliyefunja ana nguvu kuliko hata mamlaka za Serikali nyingine zilizowekwa huku Kigamboni.

Mbona hadi leo naona vitu vyenu bado viko pale huku vinanyeshewa na mvua,mmevisusa au mna kesi Mahakamani hamtaki kuharibu ushahidi!!??
 
Back
Top Bottom