Tumsadie Lijualikali na wengine kuzijua Katiba za Vyama vya Siasa

Tumsadie Lijualikali na wengine kuzijua Katiba za Vyama vya Siasa

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
Hii ni katiba ya CHADEMA kila anayejiunga na chama hiki nikuwa amesoma ameikubali, na unapochukua fomu ya kugombea uongozi ni lazima unakuwa uneikubali kwanza Katiba ya Chama.

Sasa kelele za Lijualikali hazina maana zaidi ni propaganda za waliomrubuni asaliti chama tu na mkumbuke Lijualikali alianza jeuri na kupingana na Chadema baada tu ya kumuoa binti wa Job Ndugai, Yaani huyu ni mkwe halisi wa Spika wa Bunge, Nimshauri tu bado ni kijana mdogo, awe na akiba ya maneno, haijui kesho! Na kama amejiunga na ccm bila kusoma katiba ya chama hicho atajikuta mikononi mwa wasiojulikana siku za usoni kwakuwa huko huruhusiwa hata kujaribu tu kufikiria juu ya kumkosoa mwenyekiti au vyovyote vile ambavyo ndani ya Chdema unauhuru navyo. Sisi tunaipenda Katiba ya Chadema kwakuwa inatujali vijana tunapotaka kugombea ubunge, udiwani ambapo chama kinatoa support, Lakini chama chetu kinaweza kujiendesha vizuri hata ikiwa hakitakuwa na ruzuku ya kutosha.

Kwakumsaidia Lijualikali na wanaccm wengine, Ripoti ya CAG 2018/19 imetoa HATI SAFI kwa Chadema, hii inamaana kwamba hakuna huo upotevu wa bilioni 8 anaousema. Chama cha upinzani kupewa hati safi ndani ya utawala huu ni jambo linalitakiwa chama hicho kisiwe na kwere hata ya punje ya mchere, Sasa muulizeni Lijualikali na CAG nani anaakili? Zingatia mwaka huu wa hesabu za CAG chama anachokwenda Lijualikali cha CCM kimepewa HATI CHAFU.

Iko hoja inajirudiarudia mara kadhaa, na hata Lijualikali leo kaizungumza, kwamba hakupewa nafasi ya kusikilizwa, ama kujitetea kabla ya kufukuzwa. Hili Lijualikali na wabunge hawa wanapotosha umma, na wengi wa wananchi hawasomi katiba ya Chadema. Yeye Lijualikali na wenzake 8 chama kimewapa nafasi ya kujitetea, Wabunge wanne Rwakatare, Silinde, Komu, na Selasini ndio wamefukuzwa direct kwakutumia kifungu cha katiba kinachotoa mamlaka kwa CC kufukuzwa bila kusubiri waangushe Chama. Atekeleze agizo la chama kujitetea asilete uongo.

Chadema inaendeshwa kwa misingi ya katiba, si Mbowe, Lissu, Mnyika wala yoyote kwamba ndie mwenye uamuzi. Uamuzi wowote katika taasisi hii ni uamuzi wa kikatiba.

Wasome Katiba ya Chadema ya 2006 Toleo la 2019, Ibara ya 6.5.1(d) kuhusu mamlaka ya Kamati Kuu kuamua jambo la dharura kwa maslahi ya chama.

Jambo la dharula linaamliwa bila kusubiri mtu anayehatarisha maslahi ya chama asikilizwe.

Niwakumbushe wabunge hawa, walipoamua kurubunika walitakiwa kujiridhisha kuwa wanakinga madhubuti. Taasisi ni kubwa kuliko mtu yoyote.

Na Yericko Nyerere
IMG-20200518-WA0150.jpg

FB_IMG_1589828954801.jpg
 
Yeriko huyu achana kujibizana naye. Hawa lililo kichwani mwao ni kuwa yale ya uchaguzi wa serikali za mitaa yatajirudia na hivyo wataiba kura etc kama ilivyofanyika na hivyo kuwa na uhakika wa kurudi bungeni. Achana nao work on how you will fight that hooliganism by serikali and CCM
 
Peter akiwa Diwani kule Ifakara aliniambia nia yake ya kugombea Ubunge.Nikamuuliza unataka Ubunge unaijua njia?Unaweza kwenda kumbe wenzio wanarudi.

Siasa ya Bongo ni Kama watu wako location wanadondosha episode moja moja.Leo my friend unalia? Siku ukiijua njia utajua unakokwenda.
 
Siasa ni mchezo mchafu kila mtu anajaribu kuvutia upande wake bwana yerico ameandika anachoona yeye ni sahihi na bwana lijua kali ametoa ya moyoni aliyaona ni ukweli basi tafran
 
Kwa wanasiasa wakitanzania wala haihitaji akiba ya maneno....kesho anaweza rudi mkamsifia kama Yesu alivyopanda mwanapunda kuelekea Galilaya.

Kama Lowasa alipondwa kiwango Cha kutobolewa ngozi na baadae akawa malaika Gabriel wacha wengine waongee tu.

Mi siasa za bongo zilishanichosha, ai chadema wala CCM wote wachumia tumbo tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Peter akiwa Diwani kule Ifakara aliniambia nia yake ya kugombea Ubunge.Nikamuuliza unataka Ubunge unaijua njia?Unaweza kwenda kumbe wenzio wanarudi.Siasa ya Bongo ni Kama watu wako location wanadondosha episode moja moja.Leo my friend unalia? Siku ukiijua njia utajua unakokwenda.

Kulia huyu ni kawaida yake....machozi ya wasanii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa najiuliza, wakati huu wa mchafuko wa hali ya hewa Chadema huyu mtu yupo wapi? Anyway naona umejitokeza na unaongelea katiba ambayo MMM alisha itolea maelezo alibadilishwa kinyemela na akina Mnyika ikaondoa na ukomo wa uenyekiti bila wajumbe kujijua.

Report ya mahesabu iliyopelekwa kwa CAG haikuandikwa na wanachama, wabunge wala madiwani ni mchakato wa kiutawala, sasa wenye pesa zao wanauliza zimetumikaje?

Wapeni report mliyopeleka kwa CAG Waijadili jinsi mlivyomdanganya. Vinginevyo umetumia jukwaa hili kutangaza biashara😂😂
 
Watu wengi hawajumuelewa Lijuakali!!!hoja yake ya msingi hizo fedha zinazokatwa kutoka kwa Wabunge wa CHADEMA ziko wapi???zimefanya kazi gani???je zimepelekwa kuliko kusudiwa???

Sasa naona Kila mtu analeta hiyo ibara ya katiba bila kujibu kiini Cha mlalamikaji!!!

Anyway Mimi sio mtabiri lakini niliwahi andika humu 2020 wabunge wa CHADEMA hawatazidi watatu bungeni!!!tunahitaji vyama vyenye adabu!!!
 
Lakini CDM mfikiri zaidi namna ya chama kufanya kazi na wabunge wake, suala la mwenyekiti wa chama kuwa pia KUB nadhani linaleta mkanganyiko wa kuadmnister cacus ya chama
 
Back
Top Bottom