Tumshauri kijana huyu cha kufanya, muda bado upo

Good people? Africa? Are you serious?.... Muafrika hata uliyezaliwa naye wana matatizo sana kwenye kupata na kukosa. Yani usome kuliko mdogo wako usifiwe ukoo mzima kuwa una akili uko udsm, urudi home huna ajira alafu mdogo wako wakati unasifiwa kakmtumbua macho Leo awe good people?
 
kaka,naomba zingatia haya kwanza najua age yako huenda ikawa 33 na una shahada ina maana unakosa sifa kuwa talented na kuweza kumaintain katika kampuni weng wa hrs watakuona sio profitable coz soon unaingia uzeen na kampuni inataka vijana ambao watakaa muda mrefu kwenye industry...kw
 
Mnunulie sindano ya kushonea viatu,dawa ya viatu hata akianza rangi nyeusi, dark tan na neutral,kushungi cha kupakia dawa na brushes hata mbili ama tatu.

Vitambaa vya kufutia vumbi kwenye viatu ikiwezekana na chombo cha kuwekea maji na kipande kidoogo cha sabuni.

Msogeze maeneo yenye msongamano wa watu km vile nyumba zenye wapangaji wengi,wanapoishi wanafunzi wa vyuo,karibu na salon ya kike na ya kiume. Achukue pair mbili za viatu vyake akavianzie kabisa kupiga umasikini teke.

Kuna kingine unanidai?
 
pamoja chief
 
Maisha hayana extra time hapo sijui umemaanisha Nini!?
Ila sijaona shida ye aishi na kile alicho nacho aachane na kupambania kazi za maofisi maana hazina chochote zaidi ya kukupa pressure na sukari
Auze matunda maisha yaende
 
kama unaamin uwezo upo tafuta radio uombe watz weng wakarimu watakupa kazi au komaa kwenda dodoma kutafta ajira za serikali ila0kama options zote ngumu weka makaratas pemben jiambie wew ni mtafutaj na tafuta mkoa wenye viwanda,bahari (pirika) tafuta mtu mwenye pirika za ufund n.k muelezo matatzo utaunganishwa hapo ndo mwanzo wa kuyaendea mafanikio.
 
Akajiandikishe BBT kwa Bashe au Ulega.
 
Kama nakuona vle
 
Kivyovyote haijalishi ni chama gani ila jitahidi kuepuka kutugemea siasa kama njia ya ww kujikwamua, siasa kuwa na uelewa nayo tu siku mambo Yako yakikaa sawa basi jitose 🤔🤔yaani miaka 8 huna ajira mambo magumu biashara hauna afu unategemea ujitose ktk siasa?
 
Huko kwenye siasa ata ishia kuwa cahwa, mpaka ana zeeka
 
Kuna Kijiji mm nampeleka anasimamia ccm na wazee anawapa viroba vya unga kilo 10 tu anakula udiwani mwakani
 
good, simple and very positive idea and advice.
Kuna kitu kuchagua kazi, aibu na haya inasubumbua hapa..

ukikaa vijiweni ati hiyo ni kazi ya mtu alie choka, mzee asie na nguvu. Lakini ukicheki watu wanapata chochote kitu na jamaa ana shoe shines 5 au 7 maeneo tofauti tofauti ....

Aiseee...
 
Ukimaliza ngazi flan ya masomo usiweke muda wote kwenye kutafuta ajira tu ni muhimu kujifunza ujuzi mwingine hata kama ni gereji fanya kazi usione aibu ukifanya kazi unapata nafasi nyingi ya kukutana na watu wapya ambao wanaweza kukusaidia kuliko ukajifungia ndani kukikucha uende kuzungusha bahasha ya kaki kwenye maofisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…