Tuna cha kujifunza na Uchaguzi wa Marekani?

Tuna cha kujifunza na Uchaguzi wa Marekani?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana, elimu haina mwisho. Je, tuna cha kujifunza kutoka kwao waliotutangualia? Au ni yale yale ya ukichwa ngumu kama mawe kuwa tunajua kila kitu?

Mema waliyonayo wamarekani leo hayakuja kama mvua. Yalipiganiwa na hata damu kumwagika. Sembuse kukaa mahabusu au hata kufungwa jela?

Kwani kwao TISS, NEC, ZEC au police wa huko hawapo?

Kweli hatuwezi fanya uchaguzi tukauhitimisha kwa kupongezana? Kwamba hata CUF na hata NCCR nao wanalalamika na bado hatuna sababu za kujiuliza? Dhahiri tutakuwa na matatizo.

Madai ya haki katika chaguzi yanapaswa kuwa yetu sote wakiwamo Magufuli, na hata bwana Kaijage. Nani aijuaye kesho?

Kesho thabiti ni Ile inayotokana na leo thabiti kwa mujibu wa katiba na si vinginevyo.
 
Trump analalamika kuwa ni kama kuna namna fulani anataka kudhulumiwa kura. Sasa jiulize kwa teknolojia yao na ubobezi kwenye mambo ya kupiga kura, malalamiko haya yanatoa somo gani !?

 
Inaweza kuwa kwako better lakini uchaguzi popote duniani una sifa zinazofanana ukiondoa technology na level of democracy maturity

  • US wanalalamikia pia frauds
  • Jeshi lilisambazwa mitaani kuzuia vurugu wakati wa uchaguzi.
  • Usalama wako nyuma kusaidia wanayempenda, ama kuachia alina Russia kupitisha mikono yao nk.

Wametuzidi uwazi wa matokeo ila sijui huko ndani ma DED wao kama hawachakachui.
 
Waheshimiwa kabisa, Lissu, Maalim, Mbowe, Zitto na wote. Inajulikana kwenye kudai haki dhidi ya udhalimu tutakamatwa, tutauwawa, tutaumizwa na yote ya namna hiyo.

No easy walk to freedom. Haturudi nyuma.

Victoria acerta!
 
Inaweza kuwa kwako better lakini uchaguzi popote duniani una sifa zinazofanana....ukiondoa technology na level of democracy maturity

*US wanalalamikia pia frauds
*Jeshi lilisambazwa mitaani kuzuia vurugu wakati wa uchaguzi...
*Usalama wako nyuma kusaidia wanayempenda .. ama kuachia alina Russia kupitisha mikono yao nk.

Wametuzidi uwazi wa matokeo ila sijui huko ndani ma DED wao kama hawachakachui
👍🏽
 
Anaandika Dr. Christopher Cyrilo

Ulichofundishwa kwenye somo la uraia sio kweli. Kenge wewe!

Ulikuwa mwanafunzi bora darasani kuliko wengine, walimu wakakuita 'jiniasi'. Na wewe ukakenua meno na kuchekelea...utafikiri 'jiniasi' kweli!
Ulisoma kwa bidii zote, usiku na mchana - si kwa lengo la kuvuna maarifa bali kufaulu mitihani, ukafaulu bila maarifa. Sio kosa lako, ni mfumo wa elimu yetu unaomfanya mwanafunzi kuogopa mitihani zaidi kuliko kupenda kujifunza, anasema Mwl. Mabala.

Na sasa umekuwa mtu mzima, unashangaashangaa tu. Unachokishuhudia ni tofauti na kile ulichojaza kwenye mtihani wa Uraia uliyofaulu vema kuliko marafiki zako wengi.

Ulifundishwa eti Taifa linaundwa na mihimili mitatu, Serikali, Bunge na Mahakama, Uongo. Taifa linaundwa na Serikali, Serikali na Serikali. Spika wa bunge na jaji mkuu wote wanasujudu kwa kiongozi wa serikali, na wanaelekezwa cha kufanya na wao wanafuata bila hiyana. Wakikataa watakiona Cha mtemakuni. Kile ulichofundishwa eti mihimili mitatu inayojitegemea ni uongo mtupu.

Ukaambiwa eti viongozi wanachaguliwa na wapiga kura, Uongo.

Viongozi wanachaguliwa na wanaojumuisha mahesabu ya kura. Unapoacha shughuli zako kwenda kupanga foleni ya kupiga kura, sio kwamba ndio unachagua kiongozi - no - no - no, pale unawaongezea kazi wanaohesabu kura tu. Kura zikiwa nyingi ujue watachelewa kumtangaza mtu wanaomtaka wao. Hilo ulikuwa hujui? Wewe kweli ni pimbi.

Ukaambiwa Polisi ni walinzi wa raia na mali zao, na wewe ulivyo kilaza ukaamini kabisa! Kilaza mkubwa wewe!

Polisi ni walinzi wa viongozi wa nchi na matajiri dhidi ya masikini wasumbufu wanaojifanya kudai haki wakati hawana haki. Polisi ni ukuta unaotenganisha wananchi na 'WENYENCHI'. Na Kama hujui basi kuanzia leo ujue - masikini aliyekwapua kuku wa jirani anastahili adhabu kubwa hata kifo wakati tajiri aliyeibia serikali milioni 7 kwa kila dakika anasamehewa. Unakodoa macho?

Unasubiri mkuu mmoja wa mkoa atekwe - apotee uone jeshi la polisi litakavyohangaika? Sasa potea wewe! Watasema umejiteka au umekwenda kutembelea ndugu.

Halafu kuna lile suala la binadamu wote ni sawa! Na wewe uliamini kabisa?

Sikiliza, hata waasisi wa Taifa la Marekani, akina George Washington waliandika hivyo kwenye katiba yao, wakati huohuo wakiwa na mashamba makubwa yenye watumwa kibao wakiwafanyisha kazi za kitumwa. Bado unaamini binadamu wote ni sawa? Muone! wapo binadamu wengine ni sawa zaidi ya wengine - usipoelewa hapo sio tatizo langu.

Ndio maana kuna watu wanakunywa na kupikia tope huko Lindi kwa kukosa kisima cha Milioni 5, huku wengine wanapiga vigeregere mbele ya Dreamliner la Bilioni 500, na baadhi yao hawatalipanda hadi wazeeke wafe. Si binadamu wote ni sawa. Umeelewa we tumbili?

Elimu ni ufunguo wa maisha eti? He hee! Daah. Ungejua! Kuna profesa aliwahi kujizolewa umaarufu na kuonekana moja wa watu muhimu katika kuamua mustakabali wa nchi, leo ni mpumbavu mbele ya mtu aliyeghushi vyeti vya PhD! Unatoa macho? Jichunge na vumbi.

Elimu haiondoi ujinga, bali inampa mtu uwezo wa kuujua zaidi ujinga wake ili ajichunge, na hiyo haimaanishi kuwa elimu ni ufunguo wa maisha. Ujinga ndio ufunguo wa maisha na kadiri unavyokuwa mjinga ndivyo unavyofanikiwa zaidi- kama alivyosema mwandishi nguli wa zamani Mark Twain; "Ili ufanikiwe maishani unahitaji vitu viwili, Ujinga na kujiamini". Wajinga wengi wanaojiamini wametoka kwenye maisha kuliko wanaojifanya werevu... Ujinga ndio ufunguo wa maisha. Wewe endelea kujifanya mwerevu kwa sababu eti ulifaulu darasani! Faulu na maisha sasa! Ha haaa.

Tuache sisi wajinga tukomae na mapambio ya kusifu - kusifu - kusifu na kuabudu...na tukishateuliwa -nakwambia mtakoma. Mlijifanya sana kufaulu darasani sisi tukawa tunawachora tu... Eti wataalamu, utaalamu bongo!!! mapimbi wakubwa!
#JingaMimi
 
Trump analalamika kuwa ni kama kuna namna fulani anataka kudhulumiwa kura. Sasa jiulize kwa teknolojia yao na ubobezi kwenye mambo ya kupiga kura, malalamiko haya yanatoa somo gani !?


Tuna cha kujifunza? Kulalamika si hoja.

Hivi kwetu sitting president ana cha kulalamika hata mabegi ya kura yakiwa kwenye vituo vya kura?

Trump (sitting president) mwenye malalamiko kajibiwa je?

Je ana advantages zozote dhidi ya mgombea mwingine?
 
Kama unatoa alama uchaguzi wa marekani unatoa alama ngapi kwa huku kwetu ngapi?
 
Sina hakika kama kwao pia:

1. mitandao imezimwa.
2. TV zimedhibitiwa.
3. Hata waliojipigia kura zao hazitakuwapo kwenye matokeo.
4. Pana watu watakufa kwenye zoezi hili.
5. Pana watu wataishia kukamatwa kwenye zoezi hili.
6. Kuwa haijali kura kapigiwa nani au zimepigwa vipi kwa mujibu wa mama Samia.
7. Nk, nk.

Hayupo asiyetamani mazingira huru na ya haki kama ya hawa jamaa, labda tu kama ni parasite wa hii rotten system yetu.

Aluta continua!
 
Trump analalamika kuwa ni kama kuna namna fulani anataka kudhulumiwa kura. Sasa jiulize kwa teknolojia yao na ubobezi kwenye mambo ya kupiga kura, malalamiko haya yanatoa somo gani !?

Ana haki ya kulalamika....

Aende SUPREME COURT....watamsikiliza madai yake na kuamuru UCHUNGUZI UFANYIKE.
 
Dah! Umeanza na kumaliza Bro. Barikiwa sana

Majiniasi wamekuwa Mashetaniasi
 
Tanzania mwakani Dec tunafikisha miaka 60 ya Uhuru, basically mwaka huu tumetimiza miaka 28 toka kukubali kuwepo mfumo wa vyama vingi; huku ukiwa ni uchaguzi mkuu wa sita wa ku-exercise multiparty democracy.

Marekani Uchaguzi wa kwanza wamefanya 1788–1789 (kabla ya Berlin Conference kutaka kuligawa bara la Afrika)
Hawa jamaa wana demokrasia ya miaka 232 wamefanya chaguzi mara 58 kila baada ya miaka 4; huku kukiwa na mid term election kila baada ya miaka 2.

Pamoja na uzoefu huo, 2016 walilalamika mifumo yao ya uchaguzi kuingiliwa na Russia. Ndani ya Democrats kambi ya Hillary Clinton ilichakachua kura za Bernie Sanders ili asiweze kupata uteuzi wa chama.

Mwaka huu, Trump analalamika kuibiwa kura.

Kwa upande mwingine, shirika la Posta limegomea amri ya mahakama kutoa maelezo ya kura zilizopigwa kwa njia ya posta kuyeyukaaaa.



Balozi wa Marekani Tanzania Dr. Donald J. Wright na Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo inabidi atueleze wao wanawezaje kuona boriti kwa ile kuita "irregularities" kwetu; kumbe na wao nyumba yao chafu tu.
 

Attachments

  • 1604499626634.png
    1604499626634.png
    51.1 KB · Views: 2
Waheshimiwa kabisa, Lissu, Maalim, Mbowe, Zitto na wote. Inajulikana kwenye kudai haki dhidi ya udhalimu tutakamatwa, tutauwawa, tutaumizwa na yote ya namna hiyo.

No easy walk to freedom. Haturudi nyuma.

Victoria acerta!
Kwa kuandika to mko vizuri, ila ukweli mmedanganywa Sana na Lissu na shida ni kuletwa n Amsterdam Kama mwakilishi wa nchi ya Marekani
 
Waheshimiwa kabisa, Lissu, Maalim, Mbowe, Zitto na wote. Inajulikana kwenye kudai haki dhidi ya udhalimu tutakamatwa, tutauwawa, tutaumizwa na yote ya namna hiyo.

No easy walk to freedom. Haturudi nyuma.

Victoria acerta!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Hivi mmeandamania wapi? Twitter kama kawaida?
 
Inaweza kuwa kwako better lakini uchaguzi popote duniani una sifa zinazofanana....ukiondoa technology na level of democracy maturity...
Kabisa mkuu,

Bavicha huyu anafikiri ushindi unakuaja tu kama kuomba chips yai kwa muuzaji.
 
Back
Top Bottom