Tuna cha kujifunza na Uchaguzi wa Marekani?

Tuna cha kujifunza na Uchaguzi wa Marekani?

Trump analalamika kuwa ni kama kuna namna fulani anataka kudhulumiwa kura. Sasa jiulize kwa teknolojia yao na ubobezi kwenye mambo ya kupiga kura, malalamiko haya yanatoa somo gani !?


..Trump ambaye ni Raisi aliyeko madarakani analalamika.

..anadai atakwenda kushitaki ktk mahakama kuu ya Marekani.

..sasa unajiuliza, kwanini hatumii vyombo vya DOLA wakati yeye ni Amiri Jeshi Mkuu?

..tatizo la hapa kwetu malalamiko ni ya upande mmoja tu, wakati upande mwingine ukichekelea na kufurahi siku zote.

cc tindo
 
Na huko wanaiba kura tu kama huku, hakuna cha democrasia wala nini ni yale yale tu
IMG-20201103-WA0083.jpg
 
Sitaki kusema mengi ila hii deomokrasia ya Marekani ni kiwango cha juu sana.

Ila yote kwa yote hakuna jambo muhimu kama kuheshimu mawazo ya watu 12M.

Uchaguzi umeisha sasa tuijenge nchi.

URT - JPM
SMZ - Mwinyi

CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Sina hakika kama kwao pia:

1. mitandao imezimwa.
2. TV zimedhibitiwa.
3. Hata waliojipigia kura zao hazitakuwapo kwenye matokeo.
4. Pana watu watakufa kwenye zoezi hili.
5. Pana watu wataishia kukamatwa kwenye zoezi hili.
6. Kuwa haijali kura kapigiwa nani au zimepigwa vipi kwa mujibu wa mama Samia.
7. Nk, nk.

Hayupo asiyetamani mazingira huru na ya haki kama ya hawa jamaa, labda tu kama ni parasite wa hii rotten system yetu.

Aluta continua!
 
Waheshimiwa kabisa, Lissu, Maalim, Mbowe, Zitto na wote. Inajulikana kwenye kudai haki dhidi ya udhalimu tutakamatwa, tutauwawa, tutaumizwa na yote ya namna hiyo.

No easy walk to freedom. Haturudi nyuma.

Victoria acerta!
We nu bingwa kwenye Keyboard tu
 
Sitaki kusema mengi ila hii deomokrasia ya Marekani ni kiwango cha juu sana.

Ila yote kwa yote hakuna jambo muhimu kama kuheshimu mawazo ya watu 12M.

Uchaguzi umeisha sasa tuijenge nchi.

URT - JPM
SMZ - Mwinyi

CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
Demokrasia ya kiwango cha juu na watu wanaiba kura
 
Mkuu ninayo katiba ya Marekani waliyoiandaa 1789 miaka michache baada ya kupata uhuru wao, katiba ile ni bora na inayotoa majibu mara 100 ziadi ya katiba yetu ya sasa. Cha kujiuliza ilikuaje watu watengeneze katiba 1790 na mpaka sasa wameifanyia marekebisho madogo sana lakini sisi tokea 1977 mpaka leo bado katiba yetu imeacha maswali mengi bila majibu?

Uchaguzi wa kwanza wa Marekani ulikua na matokeo mazuri na ya uwazi zaidi ya uchaguzi wetu wa leo 2020, miaka karibia 60+ tokea tupate uhuru. Je shida ni kua hatujifunzi mazuri kutoka kwa waliotangulia au akili zetu ndiyo finyu?
 
Kwa kuandika to mko vizuri, ila ukweli mmedanganywa Sana na Lissu na shida ni kuletwa n Amsterdam Kama mwakilishi wa nchi ya Marekani

Siyo kuandika tu. Tuyaandikayo hutoka mioyoni jombi.

Lissu aliyetudanganya ndiye huyu mliyetaka kumwua?

Huyu Amsterdam unayemwongelea naye ndiye huyu aliyewatia jamba jamba hadi mnapomsikia Lissu hadi mamboleo kaufyata?

Kwa mtaji huo si heri ya Amsterdam kuliko huyo mkoloni mweusi?
 
Unalialia kwenye keyboard ya smartphone kama mtu usie na akili. Kama binadamu akipata dhuluma unadhani atalazimishwa kuikomboa? Watanzania wanajua uchaguzi ulikuwa fair.

Juzi hata kwenye maandamano haukonekana. Ningekuona shujaa ungekuw kwenye list ya waliokamatwa.
 
..Trump ambaye ni Raisi aliyeko madarakani analalamika.

..anadai atakwenda kushitaki ktk mahakama kuu ya Marekani.

..sasa unajiuliza, kwanini hatumii vyombo vya DOLA wakati yeye ni Amiri Jeshi Mkuu?

..tatizo la hapa kwetu malalamiko ni ya upande mmoja tu, wakati upande mwingine ukichekelea na kufurahi siku zote.

cc tindo
Democrat na Republican, kwa maoni yangu nadhani wana"fake" uwepo wa demokrasia ya vyama vingi nchini humo. Ukichunguza kwa undani, Demo na Repa ni chama kimoja!!!( usishangae). Kwani historia ya vyama hivi viwili inavishitaki. Awali kilikuwa chama kimoja!!! Ni masuala haya haya ya uchaguzi yalisababisha kugawanyika chama hicho na kupatikana Demo na Repa, sina hakika ulikuwa mpango mahususi wanani kuturubuni namna hii !!!

Ufake wa vyama huo unatoka wapi!? Toka nizijue siasa za " kidemokrasia za Marekani " ni vyama hivi viwili tu ndivyo upokezana vijiti vya kuitawala Marekani. Naambiwa kuna vyama vingine vya siasa huko vipo static , kukua kwake ama kufifa kwa vyama hivyo hakujulikani!! Kwa nini!? Nigelesha kutupumbaza kuwa wana vyama vingi wakati Demo na Repa ni walewale!!

Trump analalamika kwa sababu chama chake DEMO-REPA anaona kina muhujumu!

Demokrasia inayosambazwa na nchi hizi haijawahi kuwanufaisha pakubwa wale waliopelekewa Demokrasia hiyo, mfano, Libya, Georgia, Iraq, Haiti, Afighanistan, Lebanon, Somalia, zitaje tu!!! Sana sana inatumika kujaza fujo nchini humo! Na uporaji wa kiana wa rasilimali za nchi husika ushamiri! Hata baadhi ya majirani zetu baadhi niwakutupia jicho namna demokrasia ilivyowasaidia!!

Nimepanua mjadala!!! Niko tayari kupingwa kwani haya ni maoni na siyo lazima msomaji ayaone ni facts!

Karibu.
 
Nilichojifunza ni kuwa wao wanagombania madaraka kuwasaidia wananchi kwa ujumla, sisi tunagombania madaraka ili familia zetu zisipate shida
 
Unalialia kwenye keyboard ya smartphone kama mtu usie na akili. Kama binadamu akipata dhuluma unadhani atalazimishwa kuikomboa? Watanzania wanajua uchaguzi ulikuwa fair.

Juzi hata kwenye maandamano haukonekana. Ningekuona shujaa ungekuw kwenye list ya waliokamatwa.

Fake ID ndiyo zinakuingiza mchecheto hivyo mburula were unayetumia VPN bado? Unadhani wapigania haki wana hata haja ya recognition.

Kwamba kuna brutal POLICEccm force inayokandamiza watu?

Nyie tegeni masikio kwani mbona hata mjusi joto ya jiwe hatimaye aliijua.
 
Fake ID ndiyo zinakuingiza mchecheto hivyo mburula were unayetumia VPN bado? Unadhani wapigania haki wa haha wana hata ya recognition.

Kwamba kuna brutal POLICEccm force inayokandamiza watu?

Nyie tegeni masikio kwani mbona hata mjusi joto ya jiwe hatimaye aliijua.
Hapa nilipo Segese nakula mtandao kama vile nakula bia. Uchaguzi ulikuwa wa huru na haki tuliza mnyeo.
 
Back
Top Bottom