Tuna cha kujifunza na Uchaguzi wa Marekani?

Tuna cha kujifunza na Uchaguzi wa Marekani?

Cha kujifunza ni kwamba kule Marekani mgombea anayeona hajatendewa haki anakimbilia mahakamani sio kuandamana.
Hujaona wale waandamanaji wa TRUMP wa 'count all votes! Na kwingine 'stop the count!?
 
Trump alijua mapema kuwa kushinda mwaka huu itakuwa ni kazi nzito!

Hivyo akaanza kujihami mapema kwa kumteua mkuu mpya wa shirika la Posta. Mkuu huyu badala ya kuboresha huduma za shirika yeye akaziharibu ili kuzorotesha upigaji wa kura kwa njia ya barua.( Wengi wa wapiga kura hizi ni wale wa rangi ya blue).

Mapema kabla ya uchaguzi alianza kujihami kuwa hatokuwa tayali kutoka WH kwani Demo’ wameshaiba kura kwa njia ya barua.

Usiku wa kupiga kura akajitangaza kuwa kashinda uchaguzi.

Na sasa anakwenda Mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi!

Hii yote inatufundisha nini?
 
Marekani incumbency may not help you!
Africa huku hiko ni kichaka
Trump anazo hizo power kama walizonazo marais wa afrika? Kwa sababu marais wa afrika wanafanya hayo wanayoyafanya kwa sababu wanazo power za kufanya hivyo iwe ndani ya katiba au nje ya katiba,je Trump akiamua kufanya kama marais wa afrika atafanikiwa?anao uwezo huo?
 
Trump alijua mapema kuwa kushinda mwaka huu itakuwa ni kazi nzito!

Hivyo akaanza kujihami mapema kwa kumteua mkuu mpya wa shirika la Posta. Mkuu huyu badala ya kuboresha huduma za shirika yeye akaziharibu ili kuzorotesha upigaji wa kura kwa njia ya barua.( Wengi wa wapiga kura hizi ni wale wa rangi ya blue).

Mapema kabla ya uchaguzi alianza kujihami kuwa hatokuwa tayali kutoka WH kwani Demo’ wameshaiba kura kwa njia ya barua.

Usiku wa kupiga kura akajitangaza kuwa kashinda uchaguzi.

Na sasa anakwenda Mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi!

Hii yote inatufundisha nini?
Tunajifunza kwamba sio afrika tu ndio kuwa watu hupenda madaraka bali hata huko watu hupenda madaraka,hivyo na huko nako kungekuwa na mazingira kama ya huku afrika basi nao wangefanya kama viongozi wetu huku afrika.
 
Hatuna cha kujifunza maana nako anaeshindwa hakubali analalamika kuibiwa kura sawa na wagombea wetu tu
 
Kwahiyo Trump anazo power kama walizonazo marais wa africa ila hazitumii?

..ninachoelewa ni kwamba Trump ni Amiri Jeshi Mkuu kama walivyo hawa wa kwetu huku Afrika.

..sasa sielewi kwamba hatumii vyombo vyake kutokana na kutokuwa na mamlaka, au kutokana na tabia yake, maadili yake, pamoja na malezi.

..kwasababu hata katika nchi za Kiafrika sheria, kanuni, na taratibu, zipo kama ilivyo kwenye nchi za wenzetu.
 
Trump anazo hizo power kama walizonazo marais wa afrika? Kwa sababu marais wa afrika wanafanya hayo wanayoyafanya kwa sababu wanazo power za kufanya hivyo iwe ndani ya katiba au nje ya katiba,je Trump akiamua kufanya kama marais wa afrika atafanikiwa?anao uwezo huo?
I dont think so
US Mifumo na Taasisi iko imara/independent
 
Hatuna cha kujifunza maana nako anaeshindwa hakubali analalamika kuibiwa kura sawa na wagombea wetu tu
Kwanza Trump hata akishindwa bado ana miezi mitatu madarakani kabla Rais mpya hajaapishwa. Kwa namna hiyo muda upo wa kutosha kabisa kushughulikia malalamiko yoyote kama yapo kwa njia mbali mbali ikiwa ni pamoja na mahakama. Marekani hawakimbilii kumwapisha rais harakaharaka kama tunavyofanya hapa kwetu hata kama malalamiko ya msingi yapo.

La pili, Rais kulalamika kwamba kaibiwa kura hapa Afrika ni ndoto isiyowezekana kwani kwa Afrika Rais ni mungu mtu. Rais ndiye anaamua mgombea gani ashinde, kura ziibwe wapi na kwa njia gani, vyombo vya dola vitumike vipi kuwezesha ushindi wake na kila aina ya dhulma ina baraka zake. Kama hapa huoni chochote cha kujifunza basi sisi ni watu wa ajabu sana.

La tatu, huko nyuma Wamarekani wamepitia hali tete kuliko hii tunayoishuhudia leo lakini wakavuka salama. Ziko chaguzi zilikuwa na sintofahamu na tata kuzidi hii na watu wasioifahamu Marekani walikuwa na wasi wasi kuwa labda Marekani itasambaratika lakini haikutokea hivyo. Wanayo misingi imara isiyoyumbishwa na isiyoyumbika hovyo kwa matukio kama haya.
 
Kwanza Trump hata akishindwa bado ana miezi mitatu madarakani kabla Rais mpya hajaapishwa. Kwa namna hiyo muda upo wa kutosha kabisa kushughulikia malalamiko yoyote kama yapo kwa njia mbali mbali ikiwa ni pamoja na mahakama. Marekani hawakimbilii kumwapisha rais harakaharaka kama tunavyofanya hapa kwetu hata kama malalamiko ya msingi yapo.

La pili, Rais kulalamika kwamba kaibiwa kura hapa Afrika ni ndoto isiyowezekana kwani kwa Afrika Rais ni mungu mtu. Rais ndiye anaamua mgombea gani ashinde, kura ziibwe wapi na kwa njia gani, vyombo vya dola vitumike vipi kuwezesha ushindi wake na kila aina ya dhulma ina baraka zake. Kama hapa huoni chochote cha kujifunza basi sisi ni watu wa ajabu sana.

La tatu, huko nyuma Wamarekani wamepitia hali tete kuliko hii tunayoishuhudia leo lakini wakavuka salama. Ziko chaguzi zilikuwa na sintofahamu na tata kuzidi hii na watu wasioifahamu Marekani walikuwa na wasi wasi kuwa labda Marekani itasambaratika lakini haikutokea hivyo. Wanayo misingi imara isiyoyumbishwa na isiyoyumbika hovyo kwa matukio kama haya.
Sawa mmarekani wa mtandaoni, kwahiyo?
 
Back
Top Bottom