Uchaguzi 2020 Tundu Lissu afanya mdahalo na Waandishi wa habari atoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali. Apangua hoja ya kutumika na mabeberu

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu afanya mdahalo na Waandishi wa habari atoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali. Apangua hoja ya kutumika na mabeberu

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628



"Tofauti ya Mrema, Slaa na Lowassa ni 'organization' wakati wa nyuma hakukuwa na 'organization' ila sasa tunayo, tunaweza kuweka mawakala nchi nzima"- @TunduALissu

#“Kutakua na Uhuru kamili wa vyombo vya Habari, katiba yetu haina neno ISIPOKUA, kutakua na Uhuru wa maoni, kutakua na Uhuru wa kutafuta habari, kumekua na ukiukwaji mkubwa wa Uhuru wa Habari, miaka mitano ya Magufuli imekua migumu kwa vyombo vya Habari”.@TunduALissu #Mwanza.

“Kumbe wakati mwingine polisi wanafanya kazi zao kwa weledi lkn wanakuwa victimized wanapokataa maagizo toka juu”. Tundu Lissu.

"Kuna vitu havihitaji utoe pesa ili upate pesa, kuna sehemu unahitaji akili tu"- @TunduALissu.

"Serikali yangu itakuwa na 'complete freedom' ili ku-stimulate uchumi mzima, ukishusha vifaa vya ujenzi watu wataweza kujenga nyumba zilizo bora"- Lissu.
===

Katika Mdahalo huo waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari wameuliza maswali mbalimbali ikiwamo namna gani atakavyouondoa ukoloni mambo leo? Umuhimu wa watu wengi kujaa kwenye mikutano, na auala la yeye kutumika na mabeberu.

Aidha alipoulizwa kuhusu serikali yake itapambana vipi kuundoa ukoloni mamboleo Lissu amefafanua kuwa suala la ukoloni mambo leo ni dhana iliyokuwa inabebwa zaidi na viongozi ambao walikuwa wanatawala kwa kufuata mfumo wa kijamaa ila kwa wakati huu dhana hii haipo tena maana hawa tunaowaita wakoloni mambo leo ndio ambao wamekuwa wakitusaidia na tukiwategemea katika kufadhili miradi mbalimbali.

Ameongeza kuwa hao tunaowaita mabeberu ndio wanatusaidia katika kila kitu hata katika vyombo vya usalama kama Polisi n.k. Pia wanatusaidia katika usafiri kama wa ndege na helikopta na wanatusaidia katika kutoa hela za miradi mikubwa mikubwa. Ameeleza kuwa ikitokea watu hao wametuzuia kidogo tu, tumekwisha. Hivyo amesisitiza kuwa watu waache kudanganyika na neno mabeberu na ukoloni mambo leo tutengeneze mahusiano mema na Dunia, kwa sababu dunia haitutegemei sisi isipokuwa sisi tunaitegemea dunia.

Sambamba na hilo, Tundu Lissu ameeleza nchi hii imeharibu uhusiano na nchi nyingine ndani ya miaka mitano iliyopita. Hivyo, wakipata ridhaa ya kuiongoza nchi watahakikisha wanajenga mahusiano mazuri na mataifa mengine ili kuleta maendeleo nchini.

Aidha, akijibu swali kwamba serikali yake itapata wapi pesa za fidia kuwalipa wakazi waliobomolewa nyumba zao, Tundu Lissu amefafanua kuwa kwa sheria ya nchi inasema kuwa pale serikali inapokosea au kubomoa nyumba za watu kimakosa inweza kushitakiwa na kulipa fidia. Hivyo, ukikosewa kwa namna yoyote ile na serikali unastahili kulipwa fidia. Hivyo, kwa namna yoyote Tundu Lissu amesema wakipata nafasi ya kuingia madarakani watatafuta namna ya kuwalipa fidia. Amesisitiza kuwa japo itakuwa bili kubwa ya kulipa fidia lakini itawalazimu watafute pesa hiyo ya kulipa watu fidia.

Aidha, kuhusu suala la watu kujaa kwenye mikutano, Lissu anasema kuwa katika siasa mtaji ni watu, ili kubaini kuwa Mwanasiasa ana nguvu kiasi gani kisiasa lazima uangalie anaungwa na watu kiasi gani. Ameweka bayana kuwa Chadema ya mwaka huu imejipanga zaidi na wana matawi mengi na kutengeneza Organization ya Chama inaitwa Chadema ni Mshindi.

Ama kuhusu uhuru wa vyombo vya habari, Tundu Lissu amesema kuwa serikali ya Chadema itavipa uhuru vyombo vyote vya habari na wataondoa vikwazo vyote mamlaka kama TCRA zitatumika kusajili tu vyombo na sio kuingilia maudhui yao.
 
... safi sana! Hii kitu waandishi waliikosa kwa miaka mitano iliyopita zaidi ya wale waimba sifa kana kwamba nchi hii ni yao na vizazi vyao wengine hawana haki nayo. Sasa enendeni mkatangaze habari hizi hadi miisho ya nchi kwamba Mungu amwemwinua kiongozi atakayeliongoza taifa lake na watu wake.
 
"Tofauti ya Mrema, Slaa na Lowassa ni 'organization' wakati wa nyuma hakukuwa na 'organization' ila sasa tunayo, tunaweza kuweka mawakala nchi nzima"- @TunduALissu

#LissuPress
#OktobaTutawezana
 
... safi sana! Hii kitu waandishi waliikosa kwa miaka mitano iliyopita zaidi ya wale waimba sifa kana kwamba nchi hii ni yao na vizazi vyao wengine hawana haki nayo. Sasa enendeni mkatangaze habari hizi hadi miisho ya nchi kwamba Mungu amwemwinua kiongozi atakayeliongoza taifa lake na watu wake.
Shida ya hawa waandishi hizi habari nzuri na njema kwa sisi watanzania huwa hawazitangazi.

Wakimaliza hapo Abbas anawaambia nin cha kuandika na nin sio.

Tulitegemea press kama hizi zitangazwe mpaka Chamwino pale wavurugwe.
 
Ninahakika hata wanahabari na wanamiliki wa vyombo vya habari watampigia kura Lissu.
Ni kweli watampigia,Unajua VYOMBO vingi vya habari vimefungiwa ukifungia chombo Cha habari maana yake umewanyima mapato,wafanyakazi kukosa Mishahara na familia zao kutaabika, VYOMBO vya habari Ni ajira na uwekezaji.
Watu siku hizi hawanunui magazeti kwa sababu yanaandika habari za CCM tu.
Hivyo VYOMBO vya habari vinajiendesha kwa hasara.
 
Back
Top Bottom