Uchaguzi 2020 Tundu Lissu ahusisha kauli ya Rais Magufuli na kupigwa kwake risasi

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu ahusisha kauli ya Rais Magufuli na kupigwa kwake risasi

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057

Mgombea Urais wa Chadema katika uchaguzi mkuu ujao mwishoni mwa mwaka huu, Tundu Lissu, ametoa madai mazito mjini Njombe jana katika ziara zake za kutafuta wadhamini, akimuhususisha Rais, kuhusu jaribio la kuuawa kwake, lililofanyika September 7 mwaka 2017.

Akihutubia umati wa wananchi, alikumbushia historia ya tukio lake la kumiminiwa risasi, ambapo aliponea chupuchupu kuuawa na kukimbizwa nchi za nje kwa matibabu.

Akisimulia mkasa huo alieleza kuwa kuna "connection" kati ya hotuba aliyoitoa Rais Magufuli, ya uzinduzi wa ripoti ya tume ya madini, masaa takribani mawili, kabla ya kupigwa kwake risasi, aliyotoa akiwa Ikulu, jijini Dar-es-Salaam.

Aliendelea kueleza kuwa katika hotuba hiyo aliyotoa Rais Magufuli, ambayo alidai ipo ndani ya YouTube, alimnukuu Rais akiyatamka maneno yafuatayo "Katika mapambano ya kijeshi, huwa wana kawaida ya kumwua, askari yeyote ambaye anawasiliti katika mapambano yao, vile vile katika vita ya kiuchumi ambayo nchi yetu inapigana hivi sasa, hatuwezi kuruhusu ku-survive kwa mtu mmoja, ambaye imebainika amekuwa akiwasiliana na mwanasheria wa kampuni hiyo ya madini, Deo Mwanyika, ili kumwibia taarifa mbalimbali nyeti, katika lengo lao wakishirikiana na mabeberu kutoka nje ya nchi, katika kutuhujumu malipo yetu ya madini, huyo mtu hastahili kabisa ku-survive" mwisho wa kunukuu.

Tunajua kuwa katika tukio hilo la kupigwa kwake risasi mwaka 2017, Tundu Lissu, Jeshi la Polisi limekuwa likutaaminisha kuwa uchunguzi wa tukio hilo unakwamishwa na Tundu Lissu, muhanga mkubwa wa tukio hilo, pamoja na Dereva wake, ambao wote walikuwa wameenda nchi za nje kwa matibabu.

Hivi sasa Tundu Lissu amesharudi nchini na amewapa "hints" ya kilichompata siku ile ya kutisha sana, ambapo "watu wasiojulikana" walimpiga risasi mfululizo 16 mwlini mwake katika jaribio la kutaka kumwua na ameeleza mwenyewe nini kilimtokea siku ile, ambapo Jeshi letu la Polisi, limekuwa likidai kuwa limekwamishwa kuendelea na uchunguzi wake, kutokana na kukosekana ushahidi huo wa Tundu Lissu

Kwa hiyo nadhani Jeshi la Polisi lingeanza kufanyia uchunguzi wa tukio lile sasa, kwa "hints" alizozitoa yeye mwenyewe muathirika wa tukio lile Tundu Lissu.
 
Aisee 🙄
Ndiyo hivyo tena...

Huyo Tundu Lissu ana "guts" hadi anadiriki kutoa tuhuma nzito kiasi hicho kwa mkuu wa nchi!........

Amewaachia mpira huo waucheze Jeshi letu la Polisi, waliokuwa wanadai kwa muda mrefu kuwa uchunguzi wao utaendelea pale Tundu Lissu atakaporejea nchini na ndiyo hivyo kesharejea na ameamua kuyaweka hadharani mambo yote yaliyomtokea!
 
Ukiunganisha "dots" hapo unapata jawabu

Mbunge ananyimwa haki yake ya kutibiwa ambayo ni haki yake kisheria.

Mbunge ananyimwa mshahara wake pasipo sababu za msingi.

Hatimaye mbunge anavuliwa kabisa ubunge wake kwa madai kuwa Bunge hilo halijui alipo Mbunge huyo, wakati dunia nzima inajua kuwa mbunge huyo anatibiwa nje ya nchi, baada ya kumimiwa risasi mfululizo!
 
Kunwaendewa Tanzania anayeweza kuchunguza hilo tukio?.


Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
Wenyewe si ndiyo waliosema kuwa wanamsubiri Tundu Lissu ili waendelee na uchunguzi wa tukio lake?

Sasa keshawasili nchini na keshatoa ushahidi wake, kwa hiyo kazi kwao Jeshi letu la Polisi, liuchukue ushahidi huo na kuufanyia kazi
 
Ukiunganisha "dots" hapo unapata jawabu

Mbunge ananyimwa haki yake ya kutibiwa ambayo ni haki yake kisheria...
Tatizo taratibu zipo lakini hutaki kuzirejea, matibabu ya nje ya nchi yana taratibu zake mbona hapo unakwepa kueleza? Kama unajiamulia kuondoka nchini kwenda kutibiwa nje ya nchi bila kufuata taratibu, gharamikia matibabu mwenyewe usitafute watu wa kulaumu kwa kulazimisha utaratibu usiokuwepo
 
Sijawahi kusikia serikali yenye wahalifu wapumbavu kama Tanzania. Inawezekana Magufuli alikuwa hajui kinachpkwenda kutokea, lakini wahuni wakachomeka kwenye hotuba yake ili aonekane alikuwa anajua shambulizi lile na hivi hata yeye uwezo wa kuchuja maneno ni below 0, basi akalipuka nalo.
 
Tatizo taratibu zipo lakini hutaki kuzirejea, matibabu ya nje ya nchi yana taratibu zake mbona hapo unakwepa kueleza? Kama unajiamulia kuondoka nchini kwenda kutibiwa nje ya nchi bila kufuata taratibu, gharamikia matibabu mwenyewe usitafute watu wa kulaumu kwa kulazimisha utaratibu usiokuwepo
alijiondokeaje?
 
Hakuna polisi atakayeweza kuchunguza hilo tukio.
Ni kupoteza muda kuamini hilo jambo.
Wenyewe si ndiyo waliosema kuwa wanamsubiri Tundu Lissu ili waendelee na uchunguzi wa tukio lake?

Sasa keshawasili nchini na keshatoa ushahidi wake, kwa hiyo kazi kwao Jeshi letu la Polisi, liuchukue ushahidi huo na kuufanyia kazi

Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
 
Ni nyie nyie chadema ndo mlimpiga Lissu risasi. ipo siku itajulikana. Tubuni
 
Back
Top Bottom