Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Vumilia tu. Huyo ndo Raisi wako kuanzia October 2020 hadi October 2025Huyu jamaa hafai kua rais wa JMT. Labda chadema waanzishe cheo kipya cha rais wa mpe lissu lakini kwa JMT hawezi kabisaàaa.
Kwa nn alinyimwa matibabu na stahiki zake kama mbunge na hatimaye kuvuliwa UbungeSijawahi kusikia serikali yenye wahalifu wapumbavu kama Tanzania. Inawezekana Magufuli alikuwa hajui kinachpkwenda kutokea, lakini wahuni wakachomeka kwenye hotuba yake ili aonekane alikuwa anajua shambulizi lile na hivi hata yeye uwezo wa kuchuja maneno ni below 0, basi akalipuka nalo.
Sera utazisikiliza kampeni zikianza rasmi. Saivi tulieni muelezwe ushetani wenuTunataka sera atasaidiaje wakulima, machinga, wasomi, wajiriwa,viwanda,uchumi,siasa ,elimu ,aachane na mambo ya risasi
Not only a terrorist, He is a monster if not a devil!Mtu haitaji hata elimu ya chekechea kujua kwamba jiwe ndiye mastermind wa lile shambulizi. This guy is a terrorist
Evidence!,.... those are propagandasNot only a terrorist, He is a monster if not a devil!
Magufuli ndiye mhusika mkuu wala hilo halina kificho na ni aibu kubwa sana kwake!Ni nyie nyie chadema ndo mlimpiga Lissu risasi. ipo siku itajulikana. Tubuni
Ohooo.. mie simo!Mgombea Urais wa Chadema katika uchaguzi mkuu ujao mwishoni mwa mwaka huu, ametoa madai mazito mjini Njombe jana katika ziara zake za kutafuta wadhamini, akimuhususisha Rais, kuhusu jaribio la kuuawa kwake, lililofanyika September 7 mwaka 2017
Akihutubia umati wa wananchi, alikumbushia historia ya tukio lake la kumiminiwa risasi, ambapo aliponea chupuchupu kuuawa na kukimbizwa nchi za nje kwa matibabu.
Akisimulia mkasa huo alieleza kuwa kuna "connection" kati ya hotuba aliyoitoa Rais Magufuli, ya uzinduzi wa ripoti ya tume ya madini, masaa takribani mawili, kabla ya kupigwa kwake risasi, aliyotoa akiwa Ikulu, jijini Dar-es-Salaam.
Aliendelea kueleza kuwa katika hotuba hiyo aliyotoa Rais Magufuli, ambayo alidai ipo ndani ya YouTube, alimnukuu Rais akiyatamka maneno yafuatayo "Katika mapambano ya kijeshi, huwa wana kawaida ya kumwua, askari yeyote ambaye anawasiliti katika mapambano yao, vile vile katika vita ya kiuchumi ambayo nchi yetu inapigana hivi sasa, hatuwezi kuruhusu ku-survive kwa mtu mmoja, ambaye imebainika amekuwa akiwasiliana mwanasheria wa kampuni hiyo ya madini, Deo Mwanyika, ili kumwibia taarifa mbalimbali nyeti, katika lengo lao wakishirikana na mabeberu katika kutuhujumu malipo yetu ya madini, hastahili kabisa ku-survive" mwisho wa kunukuu.
Tunajua kuwa katika tukio hilo la kupigwa kwake risasi mwaka 2017, Tundu Lissu, Jeshi la Polsi limekuwa likutaaminisha kuwa uchunguzi wa tukio hilo unakwamishwa na Tundu Lissu, muhanga mkubwa wa tukio hilo, pamoja na Dereva wake, ambao wote walikuwa wameenda nchi za nje kwa matibabu.
Hivi sasa Tundu Lissu amesharudi nchini na amewapa "hints" ya kilichompata siku ile ya kutisha sana, ambapo "watu wasiojulikana" walimpiga risasi mfululizo 16 mwlini mwake katika jaribio la kutaka kumwua na ameeleza mwenyewe nini kilimtokea siku ile, ambapo Jeshi letu la Polisi, limekuwa likidai kuwa limekwamishwa kuendelea na uchunguzi wake, kutokana na kukosekana ushahidi huo wa Tundu Lissu
Kwa hiyo nadhani Jeshi la Polisi lingeanza kufanyia uchunguzi wa tukio lile sasa, kwa "hints" alizozitoa yeye mwenyewe muathirika wa tukio lile Tundu Lissu.
one needs not to substantiate the obvious. Common sense is enough evidence on this matter. However, common sense is not that common. Therefore, you are excused.Evidence!,.... those are propagandas
Chuki tu ndo zimewajaa, mbowe na genge lake wamefanya mambo.Magufuli ndiye mhusika mkuu wala hilo halina kificho na ni aibu kubwa sana kwake!
Maoni yangu ni kwamba huyu jamaa anaweza kuwa hakujua chochote, lakini kwa vile ni mtu wa visasi akakubali hata mambo ambayo yanamchonganisha na jamii.Kwa nn alinyimwa matibabu na stahiki zake kama mbunge na hatimaye kuvuliwa Ubunge
We Kama nani?Atatwangwa mamako sio lissu na yeyote atakaye mgusa mim nikotayar nice ila aliemgusa nimuue pia
Huyo Deo Mwanyika wa Barrick Gold aliyesema anavujisha siri za nchi kwa Tundu Lissu na kumfunga detention miaka kadhaa na kisha kumwachia I hope sio huyo huyo waliyempitisha leo kuwa mgombea ubunge wa CCM Njombe Mjini.hatuwezi kuruhusu ku-survive kwa mtu mmoja, ambaye imebainika amekuwa akiwasiliana mwanasheria wa kampuni hiyo ya madini, Deo Mwanyika, ili kumwibia taarifa mbalimbali nyeti
Polisi wameshaweka mpira kwapani ndio maana wapo kimya mpaka sasa.Ndiyo hivyo tena...........
Huyo Tundu Lissu ana "guts" hadi anadiriki kutoa tuhuma nzito kiasi hicho kwa mkuu wa nchi!........
Amewaachia mpira huo waucheze Jeshi letu la Polisi, waliokuwa wanadai kwa muda mrefu kuwa uchunguzi wao utaendelea pale Tundu Lissu atakaporejea nchini na ndiyo hivyo kesharejea na ameamua kuyaweka hadharani mambo yote yaliyomtokea!