huyu urais atausikia tu redioni watu wakiapishwa yeye aendelee kuropoka tu hana jipya fala huyo
*_KUHUSU NEMBO ZA TAIFA_*
1. National Flag - Bendera
2. National Animal - Twiga
3. Uhuru Torch - Mwenge
4. Coat of Arms - Ngao ya Bibi na Bwana
5. National Anthem - Wimbo wa Taifa
Hizi nembo zote (National Symbols) zinalindwa na sheria yaani (Protected by law) isipokuwa: wimbo wa Taifa pekee ambao haulindwi na sheria.
*_KWANINI IKO HIVI?;_*
Ili kitu kilindwe na Sheria ni lazima kiwe kinamilikiwa kwa asilimia 100. Tanzania haina Umiliki wa 100% wa Wimbo wa Taifa kwa sababu wimbo huu tumeukopa kutoka kwa jamii ya wa *XHOSA*
Baada ya kupata UHURU mwaka 1961, Tanganyika ilianza kuutumia wimbo huu kama *_Wimbo wa Taifa_"* lakini tayari ulikuwa unaimbwa na Jamii ya XHOSA iliyoko Afrika Kusini, na hata baada ya Muungano na Zanzibar, wimbo huu tumeendelea kuutumia. Sheria ya Nembo za Taifa ya mwaka 1971.
Ilitungwa ya kulinda *HAKI MILIKI* (Copyright) ya Nembo zetu za Taifa, haikujumuisha wimbo wa Taifa kwa sababu hatuumiliki kwa 100%, TUMEUKOPA.
Mpaka sasa, wimbo hui unaimbwa kwa lugha ya Kiswahili(Tanzania), Afrika ya Kusini (English) kama kipande cha wimbo wa Taifa lao, pia Zambia .
Wimbo huu ulitungwa na *ENOCH MANKAYI SONTONGA (24)* mwaka 1897 ukipewa jina la "Nkosi Sikelel' iAfrika" yaani, "MUNGU IBARIKI AFRIKA*" na ulitungwa uwe wimbo wa shule lakini ukapendwa na watu wengi na kupata umaarufu na kuwa wa wimbo wa TAIFA lao, kabla hatujaukopi.
Mpaka sasa, hakuna mwenye mamlaka kamili ya wimbo huu kwa sababu, kijana aliyeutunga alifariki mwaka 1905 na hakuna anayemiliki. Ndiyo maana unatumiwa na Nchi tatu(3) tofauti bila marumbano.