Mwenyekiti Mpya wa CHADEMA, Tundu Lissu akiwa kwenye Mkutano wa Baraza Kuu la Chama ambalo limekutana leo Jumatano, Januari 22, 2025 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, ameanza kupanga safu yake ya uongozi kwa Kuteua Katibu Mkuu, Manaibu Katibu Wakuu pamoja na wajumbe wa Kamati Kuu.
Mh. Tundu Lissu amefanya uteuzi kama ifuatavyo
Katibu Mkuu
1. John John Mnyika
Manaibu Katibu Mkuu
1. Aman Golugwa - Naibu Katibu Mkuu Tanganyika (Tanzania Bara)
2. Wakili Ally Ibrahim Juma - Naibu Katibu Mkuu Zanzibar
Uteuzi wa Wajumbe wa Kamati Kuu
1. Godbless Lema
2. Dkt. Rugemeleza Nshala - Mwanasheria Mkuu wa Chama
3. Rose Mayemba
4. Salma Musa Kasanzu
5. Hafidh Ally Salehe
View: https://www.youtube.com/live/n57Tc7XtINo