TWisheshagi
Member
- May 2, 2020
- 14
- 209
UCHAGUZI wa mwaka huu unatakuwa ngumu na wenye mvuto mkali. Hii ni sawa na pambano lililosubiriwa kwa muda mrefu.
Mapambano kama haya yakitokea hulazimisha shughuli zingine zisimame ili kupisha mpambano mkali na wenye mvuto.
Hivi ndiyo ninavyoona uchaguzi wa mwaka huu. Siyo uchaguzi wa CCM VS CHADEMA. Ni uchaguzi Kati ya Tundu Antipus Lisu na John Pombe Magufuli.
Kwa sababu ya upekee huo, uchaguzi wa mwaka huu hautaamliwa kwa kushindanisha sera za wagombea, bali utaamliwa kwa kushindanisha sifa za wagombea.
Hapa Kuna aina mbili za wagombea. Yupo mgombea mwenye uchovu mwingi dhidi ya mgombea mwenye shauku nyingi.
Yupo mgombea mwenye kuitawala dhamiri yake mwenye dhidi ya mgombea mwenye kufungwa na dhamiri yake mwenyewe.
Yupo mgombea anayependa kuwatisha wenzake dhidi ya mgombea asiyezoea wala kuogopa kutishwa!
Yupo mgombea anayejua matatizo yetu hata kama hatujayasema dhidi ya mgombea anayependa kuahirisha matatizo yetu hata kama tumeyasema hadharani.
Yupo mgombea anayehisi na kuamini kwamba baya lolote likitokea ni hujuma za ndani au nje ya nchi dhidi ya mgombea anaye tambua kuwa makosa yetu ya kimfumo na kitaasisi ndicho chanzo kikuu cha mabaya tunayoyapata.
Yupo mgombea anayeamini hawezi kukosea, na akikosea husingizia wasaidizi wake au watangulizi wake dhidi ya mgombea anayeamini binadamu hatujakamilika, na kufanya makosa ni kuukamilisha utukufu wa MUNGU wetu aliye wema Sana.
Yupo mgombea anayeamini kuwa kila baya ni la watangulizi wake dhidi ya mgombea anayetambua mchango wa kila mtu katika ujenzi wa TAIFA letu. Uongozi ni pamoja na kurithi makosa ya wenzako.
Yupo mgombea mwenye uwezo wa kujenga nchi dhidi ya mgombea mwenye uwezo wa kujenga taifa.
Yaani ujenzi wa miundombinu mingi, sio ujenzi wa taifa. Kuna barabara zingine zinajengwa bila sababu. Nyingine zinaelekea makaburini.
Yupo mgombea anayechukia wakosoaji dhidi ya mgombea anayechukia makosa.
Yupo mgombea anayetenda anasema kila kitu dhidi ya mgombea anayetenda hasemi.
Yupo mgombea mwenye kumbukumbu nyingi kuliko ndoto dhidi ya mgombea mwenye ndoto na maono mengi kuliko kumbukumbu.
Yupo mgombea mwenye marafiki wengi wa kificho dhidi ya mgombea mwenye maadui wengi wa kificho!
Marafiki wa kificho ni wale wanakuunga mkono bila wewe kuwajua. Wapo tayari kulala njaa ili wewe ule na ushibe!
Maadui wa kificho, ni wale ambao wanakuunga mkono unapokuwepo na kuongoza mashambulizi ya aibu dhidi yako unapo wapa kisogo!
Hawa wapo wengi. Na wapo kila pahala. Wapo kwenye nyumba za ibada, wapo maofisini, wapo mtaa wa Lumumba, wapo kwenye vikao vyetu vya ndani!
Ndugu zangu, uchaguzi huu ni Kati ya nguvu ya maono dhidi ya nguvu za kufoka na kufokeana.
Uchaguzi huu utusaidie kutenganisha yafuatayo:
Ubabe sio ujasiri. Udhaifu sio busara wala hekima. Kufoka foka hovyo sio Uwajibikaji. Kujipendekeza sio uzalendo! Kupenda serikali sio kupenda nchi. Ujenzi wa nchi siyo ujenzi wa taifa.
Ndimi mkulima wa Bamia, bonde la mto Simiyu - Magu, Mwanza.
Mapambano kama haya yakitokea hulazimisha shughuli zingine zisimame ili kupisha mpambano mkali na wenye mvuto.
Hivi ndiyo ninavyoona uchaguzi wa mwaka huu. Siyo uchaguzi wa CCM VS CHADEMA. Ni uchaguzi Kati ya Tundu Antipus Lisu na John Pombe Magufuli.
Kwa sababu ya upekee huo, uchaguzi wa mwaka huu hautaamliwa kwa kushindanisha sera za wagombea, bali utaamliwa kwa kushindanisha sifa za wagombea.
Hapa Kuna aina mbili za wagombea. Yupo mgombea mwenye uchovu mwingi dhidi ya mgombea mwenye shauku nyingi.
Yupo mgombea mwenye kuitawala dhamiri yake mwenye dhidi ya mgombea mwenye kufungwa na dhamiri yake mwenyewe.
Yupo mgombea anayependa kuwatisha wenzake dhidi ya mgombea asiyezoea wala kuogopa kutishwa!
Yupo mgombea anayejua matatizo yetu hata kama hatujayasema dhidi ya mgombea anayependa kuahirisha matatizo yetu hata kama tumeyasema hadharani.
Yupo mgombea anayehisi na kuamini kwamba baya lolote likitokea ni hujuma za ndani au nje ya nchi dhidi ya mgombea anaye tambua kuwa makosa yetu ya kimfumo na kitaasisi ndicho chanzo kikuu cha mabaya tunayoyapata.
Yupo mgombea anayeamini hawezi kukosea, na akikosea husingizia wasaidizi wake au watangulizi wake dhidi ya mgombea anayeamini binadamu hatujakamilika, na kufanya makosa ni kuukamilisha utukufu wa MUNGU wetu aliye wema Sana.
Yupo mgombea anayeamini kuwa kila baya ni la watangulizi wake dhidi ya mgombea anayetambua mchango wa kila mtu katika ujenzi wa TAIFA letu. Uongozi ni pamoja na kurithi makosa ya wenzako.
Yupo mgombea mwenye uwezo wa kujenga nchi dhidi ya mgombea mwenye uwezo wa kujenga taifa.
Yaani ujenzi wa miundombinu mingi, sio ujenzi wa taifa. Kuna barabara zingine zinajengwa bila sababu. Nyingine zinaelekea makaburini.
Yupo mgombea anayechukia wakosoaji dhidi ya mgombea anayechukia makosa.
Yupo mgombea anayetenda anasema kila kitu dhidi ya mgombea anayetenda hasemi.
Yupo mgombea mwenye kumbukumbu nyingi kuliko ndoto dhidi ya mgombea mwenye ndoto na maono mengi kuliko kumbukumbu.
Yupo mgombea mwenye marafiki wengi wa kificho dhidi ya mgombea mwenye maadui wengi wa kificho!
Marafiki wa kificho ni wale wanakuunga mkono bila wewe kuwajua. Wapo tayari kulala njaa ili wewe ule na ushibe!
Maadui wa kificho, ni wale ambao wanakuunga mkono unapokuwepo na kuongoza mashambulizi ya aibu dhidi yako unapo wapa kisogo!
Hawa wapo wengi. Na wapo kila pahala. Wapo kwenye nyumba za ibada, wapo maofisini, wapo mtaa wa Lumumba, wapo kwenye vikao vyetu vya ndani!
Ndugu zangu, uchaguzi huu ni Kati ya nguvu ya maono dhidi ya nguvu za kufoka na kufokeana.
Uchaguzi huu utusaidie kutenganisha yafuatayo:
Ubabe sio ujasiri. Udhaifu sio busara wala hekima. Kufoka foka hovyo sio Uwajibikaji. Kujipendekeza sio uzalendo! Kupenda serikali sio kupenda nchi. Ujenzi wa nchi siyo ujenzi wa taifa.
Ndimi mkulima wa Bamia, bonde la mto Simiyu - Magu, Mwanza.