Uchaguzi 2020 Tundu Lissu anajitutumua kuitumia Corona kisiasa lakini wapi!

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu anajitutumua kuitumia Corona kisiasa lakini wapi!

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Leo akiwa huko Muheza ‘kwenye kampeni zake za urais’, Tundu Lissu kazungumzia tena suala la Corona.

Japo kalizungumzia kidogo tu, lakini kaligusia kwa kumkosoa tena Rais Magufuli na jinsi alivyoamua kukabiliana nayo.

Kamkosoa Magufuli kwa kuwaambia watu wasivae barakoa, ‘kwanza zinafanana na sidiria za wanawake’.

Sijui ni lini na wapi Rais alisema hivyo. Mnaojua mtanifahamisha.

Ila kwa Tundu Lissu kusimama mbele ya watu ambao hawana ‘time’ na Corona, ambao wamesimama kwa kurundikana bila kuacha nafasi, na ambao wala hawajavaa barakoa, akiwemo yeye mwenyewe, ni unafiki wa daraja la kwanza.

Kila siasa huwa ni za mahali pake. Kwa Tanzania hii, suala la Corona si hoja yenye mashiko, na kwa mtaji huo, si hoja ya ushindi.

Mbaya zaidi ni kutokitenda kile ambacho unakihubiri.

Huyo Tundu Lissu yeye anachukua tahadhari gani dhidi ya Corona tokea aje?

Ile barakoa yake aliyoivaa kwa dakika chache ile siku aliporudi, iko wapi?

Huyu jamaa ni kama vile yuko nje ya mguso na mambo ambayo Watanzania wanayajali.

Hebu mtazame hapa kuanzia dakika ya 6:30.....

 
Lissu yuko vizuri anazungumzia kuhusu utawala mbovu wa Magufuli na umuhimu wa kuung'oa madarakani ili kusimika utawala unaheshimu katiba, sheria za nchi wenye kufuata misingi ya utawala bora, usiotesa raia, kuwabambikia kesi na kubambikizia wafanyabiashara kodi!

Lissu anatetea maslahi ya watumishi wa umma, anataka wapate nyongeza za mishahara zilizoko kwa mujibu wa sheria na pia anapinga kauli za kinyanyasaji na zisizo na staha hasa kwa wanawake waliogeuzwa kuwa wanasesere wa mizaha kwenye utawala huu!.

Lissu katolea mfano wa kauli ya kukejeli barakoa baada ya Jiwe siku moja kuifananisha na sidiria, infact Jiwe aliifananisha na Titi moja la mtu lililokatwa!!. Maneno gani sasa yale kutoka kwa mtu mwenye hadhi ya ukuu wa kaya kuyatamka mbele ya hadhara?, Ni aibu!

Kiufupi Lissu anafaa kuwa raisi, na akipata atakuwa rais bora kuliko Magufuli
 
Lissu yuko vizuri anazungumzia kuhusu utawala mbovu wa Magufuli na umuhimu wa kuung'oa madarakani ili kusimika utawala unaheshimu katiba, sheria za nchi wenye kufuata misingi ya utawala bora, usiotesa raia, kuwabambikia kesi na kubambikizia wafanyabiashara kodi!

Lissu anatetea maslahi ya watumishi wa umma.

Kiufupi Lissu anafaa kuwa raisi, na akipata atakuwa rais bora kuliko Magufuli
Katika kuzungumza huko naye anaonyesha ubovu wake kama mwanasiasa.

Yeye ni mwanaharakati tu.

Siasa haziwezi.
 
Mkuu Nyani Ngabu, hapo alikuwa akirejea kipindi cha mtanziko wakati maeneo mbalimbali ya dunia yakihaha kukabiliana na janga la COVID-19. Kauli yake ilikuwa "retrospective" kwa mazingira ya tishio halisi lilivyoripotiwa kupitia takwimu zilizokuwepo kwa wakati huo, na kauli za serikali zilivyotolewa.
 
Mkuu Nyani Ngabu, hapo alikuwa akirejea kipindi cha mtanziko wakati maeneo mbalimbali ya dunia yakihaha kukabiliana na janga la COVID-19. Kauli yake ilikuwa "retrospective" kwa mazingira ya tishio halisi lilivyoripotiwa kupitia takwimu zilizokuwepo kwa wakati huo, na kauli za serikali zilivyotolewa.
Sasa kuna haja gani kurejea yaliyopita kama yashaonekana hayana lolote?

Wewe upo ‘rockdown’? Unavaa barakoa?
 
Kisiasa au anaongea kilichopo/ facts kajititimua kipi hapo[emoji23][emoji23]
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Sina hoja lakini kila niandikapo hukosi kupita na kutema nyongo zako!

Dizaini nakupa kiungulia cha moyo kila unionapo maana washindwa kujizuia!!!!

Pole.
Tukikuacha utadhani wote hatujitambui kama wewe, hivyo unapotaka kujiona mjuaji kuliko wote tuanakupa makavu yako. Mara nyingi unataka kujifanya mmiliki wa fikra zetu, hata sisi tunaona na kusikia, na tulikuwa watu wazima tangu sakata la Korona limeanza hadi leo., hivyo tunajua mbivu na mbichi usitipangie. Tunajua wapi serikali imefanya vizuri wapi imeboronga.
 
Alichoongea Lissu na wewe ulichoelewa ni tofauti
20200816_183217.jpg

Shubamittttttttt
 
Hahahaha kinacho muuma zaidi Lissu ni kutojibiwa hilo linamtesa sana!


Angekuwa timamu au nagekuwa sawa kisaikolojia angeachana na swala la corona maana sidhani kama kuna mtanzania au mwanachadema yeyote anaweza kumuelewa kabisa!

Na hili la Corona ndilo linazidi kumfanya watanzania wasithubutu kumpigia kura kwani wengi wameshaogopa kuwekwa karantini!
 
Hahahaha kinacho muuma zaidi Lissu ni kutojibiwa hilo linamtesa sana!


Angekuwa timamu au nagekuwa sawa kisaikolojia angeachana na swala la corona maana sidhani kama kuna mtanzania au mwanachadema yeyote anaweza kumuelewa kabisa!

Na hili la Corona ndilo linazidi kumfanya watanzania wasithubutu kumpigia kura kwani wengi wameshaogopa kuwekwa karantini!
Yeye mwenyewe hajielewi!

Anapozungumzia barakoa, yeye anakuwa kaivaa?
 
Anaongelea tahadhari za Corona kwa watu ambao hawana ‘time’ na Corona, akiwemo yeye mwenyewe!

Amezungumzia historia ya utendaji wa Magufuli katika miaka yake mitano, hajazungumzia korona tu.

Kazungumzia:

1.kauli za Magufuli kipindi cha tetemeko Kagera
2. kauli za Magufuli kipindi cha ukame wa njaa
3. kauli za Magufuli kipindi cha Korona
4. Kauli za Magufuli wananchi wanapomdai nyongeza za mishahara

Yote haya ameyazungumza kuwaonyesha na kuwakumbusha Watanzania aina ya kiongozi tuliye naye na umuhimu wa kumbadilisha ili tuweke mwingine atakayewasaidia wananchi kipindi cha majanga na atakayekuwa na kauli za staha na heshima kwa wananchi!
 
Anawatemea mate wananchi waliokusanyika halafu anakosoa hatua zilizochukuliwa
 
Anaongelea tahadhari za Corona kwa watu ambao hawana ‘time’ na Corona, akiwemo yeye mwenyewe!

Mimi uncle wangu juzi kafariki singida kwa Corona yaani anazikwa juma nne. Wajinga wachache wanasababisha ndugu zetu kufa kwa ushabiki wa Siasa. Ngoja upoteze mtu ndiyo utajua Corona ipo
 
Lissu yuko vizuri anazungumzia kuhusu utawala mbovu wa Magufuli na umuhimu wa kuung'oa madarakani ili kusimika utawala unaheshimu katiba, sheria za nchi wenye kufuata misingi ya utawala bora, usiotesa raia, kuwabambikia kesi na kubambikizia wafanyabiashara kodi!

Lissu anatetea maslahi ya watumishi wa umma, anataka wapate nyongeza za mishahara zilizoko kwa mujibu wa sheria na pia anapinga kauli za kinyanyasaji na zisizo na staha hasa kwa wanawake waliogeuzwa kuwa wanasesere wa mizaha kwenye utawala huu!.

Lissu katolea mfano wa kauli ya kukejeli barakoa baada ya Jiwe siku moja kuifananisha na sidiria, infact Jiwe aliifananisha na Titi moja la mwanamke lililokatwa!!. Maneno gani sasa yale kutoka kwa mtu mwenye hadhi ya ukuu wa kaya kuyatamka mbele ya hadhara?, Ni aibu!

Kiufupi Lissu anafaa kuwa raisi, na akipata atakuwa rais bora kuliko Magufuli
Labda kung'oa jino
 
Back
Top Bottom