Uchaguzi 2020 Tundu Lissu (CHADEMA), aomba mdahalo na Dkt. Pombe Magufuli (CCM)

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu (CHADEMA), aomba mdahalo na Dkt. Pombe Magufuli (CCM)

Anatapatapa sasa ameshindwa kuwa win watz! Hatuhitajj mdahalo sisi bali tunataka utuambie umefanya nini na utafanya nini tukikupa kura zetu! Hatuko kwenye mashindano ya mdahalo!
Sio kwamba hutaki mdaalo ni kwamba unajua uwezo duni alio nao mgombea wenu.
 
Lissu hajui ‘budgeting limitations factors’ wala actual cost za bima yake kila mtu achangie shilling ngapi. Let alone nikisema jambo kama hilo linataka uanze na hospital service costing kwanza, aina ya magonjwa tuliyonayo, idadi ya watu wanaogua magonjwa mbali mbali kila mwaka, hospita stay, hospital bed capacity etc before you even think of insurance cover ya nchi nzima kila mtu achangie kiasi gani.

Mtu anaropoka tu halafu anataka mdhahalo na raisi. Kukusaidia tu Lissu hana shida ya mdahalo kwa sababu ana hoja za msingi the bottom line kila mtu akiacha ushabiki wa siasa anachoongea Lissu ni upuuzi wa kuwahadaa wananchi wenye elimu ndogo.

Based on those facts kumpa mtu kama huyo mdhahalo sio kwamba unaenda jibizana nae kwa hoja zenye merit maana hana, bali kufanya ivyo ni ku entertain his mental issues; Tundu inabidi mumpe ukweli wake Magufuli ni raisi wa Tanzania na kwa katiba yetu he is very powerful aache kujiona yeye na Magufuli ni watu sawa.
Nimekuelewa!

Anachoongea Lissu umekipa rangi ya hadaa! Kuwa ana wahadaa raia wenye elimu ndogo na hana hoja ya msingi. Pia ukaweka ziada inambidi apewe ukweli wake Magufuli ni rais wa hii nchi. Vilevile ukaweka ziada kuwa kufanya mdahalo kwa Lissu ni kufurahisha sintofahamu zake za kichwani.

Lakini mazingira haya yametokea na yanatokea. Tumeshuhudia na imeshuhudiwa vijembe vikirushwa pande zote mbili, kwa Lissu Chadema na kwa Magufuli CCM. Si hivyo tu, bali mpaka wagombea Urais wenyewe wanarushiana vijembe.

Kwa hayo uliyoyaorodhesha kuhusu Lissu ni tunu kwa CCM. Kwa nini msiitumie hii fursa ya dhahabu ya mdahalo kumharibu na kuharibu carrier yake moja kwa moja kuliko ile ya kujibizana na mtu mwenye mental issues kwenye majukwaa?! Naamini hili likitendeka hamtampa tena sikio za kuhangaika naye kwenye vijembe. Kwani umma utakuwa umeshashuhudia.

Nafikiri ni muda wa muafaka wa Magufuli kumuonyesha fahari ni nani kwenye hili zizi. Njia pekee na sahihi ya kuwathibitishia hata kwa wale wenye elimu ndogo kuwa Lissu ana wahadaa ni mdahalo. Na si kitu kikubwa! Ni mdahalo tu!

Ruhusuni mdahalo.
 
Lisu anataka kutuletea mambo ya kisekondari sekondari. Eti Debate.

Nani anataka kudebate na mgombea wa chama kikuu cha wapangaji.

Wanapokea ruzuku wananywea konyagi badala ya kujenga ofisi.

Hivi kweli wanadhani w nani kuwa wanaweza kuleta maendeleo wakati kujisimamia wao tu hawawezi.
Wanataka debate ili wazungu wa Ulaya Wawaone na wajue kuwa pesa wanazowapa zinafanyiwa kazi.

Huwa nawaambia kuwa utendaji wa Magufuli ni mdahalo tosha kabisa.
 
Huyo mjamaa amekulia porini afu anajiona lugha ya kingereza ni kijijini kwao

Kufanya mjadala na mropkaji wa matusi nani atakubali?
Aende ubeligiji akafanye mjadala na robert
Lugha tu na Mzee kupangilia logical sequence ni issues msaidizi wake humprey aligonga zero HKL high school
 
Nimekuelewa!

Anachoongea Lissu umekipa rangi ya hadaa! Kuwa ana wahadaa raia wenye elimu ndogo na hana hoja ya msingi. Pia ukaweka ziada inambidi apewe ukweli wake Magufuli ni rais wa hii nchi. Vilevile ukaweka ziada kuwa kufanya mdahalo kwa Lissu ni kufurahisha sintofahamu zake za kichwani.

Lakini mazingira haya yametokea na yanatokea. Tumeshuhudia na imeshuhudiwa vijembe vikirushwa pande zote mbili, kwa Lissu Chadema na kwa Magufuli CCM. Si hivyo tu, bali mpaka wagombea Urais wenyewe wanarushiana vijembe.

Kwa hayo uliyoyaorodhesha kuhusu Lissu ni tunu kwa CCM. Kwa nini msiitumie hii fursa ya dhahabu ya mdahalo kumharibu na kuharibu carrier yake moja kwa moja kuliko ile ya kujibizana na mtu mwenye mental issues kwenye majukwaa?! Naamini hili likitendeka hamtampa tena sikio za kuhangaika naye kwenye vijembe. Kwani umma utakuwa umeshashuhudia.

Nafikiri ni muda wa muafaka wa Magufuli kumuonyesha fahari ni nani kwenye hili zizi. Njia pekee na sahihi ya kuwathibitishia hata kwa wale wenye elimu ndogo kuwa Lissu ana wahadaa ni mdahalo. Na si kitu kikubwa! Ni mdahalo tu!

Ruhusuni mdahalo.
Ni sawa na kusema raisi Magufuli aingie kwenye dimbwi na kucheza vita ya kurushiana matope just for the sake of entertaining Lissu niche crowd of supporters.

Tundu Lissu hana shida ya mdhahalo na wala hana hoja za msingi as yet zaidi ya porojo zisizo na kichwa wala muhimu, shida yake ni kujiweka on per na Magufuli and that line of reasoning is destroying is mental state.

Akuanza leo wala jana hiyo obsession ya kujilinganisha na Magufuli ata alipochaguliwa raisi wa ‘Tanganyika Law Society’ Lissu alikuwa analazimisha kwa nafasi yake akutanishwe na Magufuli na kila anachofanya Magu anapinga to the point of annoying the National security maana mambo mengine ni sentive kama ilivyokuwa kwenye renegotiation ya mikataba.

Deep down Tundu Lissu is just jealous of Magufuli presidency’s.

There is no point of entertaining such a person let his jealous yearn to be considered on equal per with Magu be the cause of his worsening mental state.
 
Ni sawa na kusema raisi Magufuli aingie kwenye dimbwi na kucheza vita ya kurushiana matope just for the sake of entertaining Lissu niche crowd of supporters.

Tundu Lissu hana shida ya mdhahalo na wala hana hoja za msingi as yet zaidi ya porojo zisizo na kichwa wala muhimu, shida yake ni kujiweka on per na Magufuli and that line of reasoning is destroying is mental state.

Akuanza leo wala jana hiyo obsession ya kujilinganisha na Magufuli ata alipochaguliwa raisi wa ‘Tanganyika Law Society’ Lissu alikuwa analazimisha kwa nafasi yake akutanishwe na Magufuli na kila anachofanya Magu anapinga to the point of annoying the National security maana mambo mengine ni sentive kama ilivyokuwa kwenye renegotiation ya mikataba.

Deep down Tundu Lissu is just jealous of Magufuli presidency’s.

There is no point of entertaining such a person let his jealous yearn to be considered on equal per with Magu be the cause of his worsening mental state.
Pamoja. Naheshimu mawazo yako.
 
Maendeleo gani unayasongelea?

ATCL?
Ukijiuluza kwa nini ATCL imehamishiwa kwenye Kasma ya Ikulu ambayo CAG haruhusiwi kukagua utagundua kuwa ununuzi wa madege hauna faida. Yamenunuliwa bila kufuata sheria ya PPRA ili kujipatia RUSHWA tu.

Juzi tarehe 11 jioni Bombardier ya Mwanza -DSM ya saa 10 ilikuwa na abiria 33. Just imagine hiyo ni ruti ya Mwanza kwa Bombardier. Kwa hiyo ma Airbus na Dreamliner ni LOSS tupu. Wananchi hawana hela hata za kusafiria hiyo ATCL.

FLYOVER?
Suala ni kipaumbele. Lipi lianze elimu na afya au daraja la juu la DSM? Ni vipi Mwananchi wa Kazuramimba au Nanjilinji anafaidika na hilo daraja la DSM wakati yeye hata barabara ya vumbi ya kusafirisha mazao yake haipo

Barabara?
Jili la barabara za lami hajaanza yeye. Alianza Benjamin Mkapa na Kikwete kaendeleza. Kama kuna mtu wa kumsifia kwa barabara ni Mkapa kwa kuanzisha Road Fund na TANROADS. Afanye kadri ya uwezo wake na wengine wataendeleza kama yeye alivyopokea.

SGR?
Cha ajabu nini hapa. Mjerumani mwaka 1890- 1915 alijenga Reli ya Kati na bado aliondolewa na Muingereza.

Nyerere alijenga TAZARA na akaachia madaraka. Acheni ushamba wa kuabudu matendo ya DIKTETA

STIGLER GORGE?
Huwezi ukaanzisha miradi ya nchi kwa mapenzi yako mwenyewe bila kuzingatia the economic viability zake ili tu kujitafutia cheap popularity. Unaweza ukamaliza kunenga Stigler Gorge electric dam lakini siyo lazima upate hizo 2100 MW
Tatizo unaandika kwa mihemko ya Kisiasa, hivi huoni DSM baada ya uboreshaji wa miundombinu ya Barabara foleni imepungua kwa kiwango kikubwa na watu wanafika kwa wakati maeneo yao ya kazi.
 
Sio kwamba hutaki mdaalo ni kwamba unajua uwezo duni alio nao mgombea wenu.
Kwahiyo unataka kusema Lowassa ambaye nae hakutaka mdahalo ile 2015 ni kutokana na uwezo mdogo alionao? na vp wapiga waliyompigia kura hawakuliona hilo?
 
Anatapatapa sasa ameshindwa kuwa win watz! Hatuhitajj mdahalo sisi bali tunataka utuambie umefanya nini na utafanya nini tukikupa kura zetu! Hatuko kwenye mashindano ya mdahalo!
hili utaliuliza kwenye mdahalo wala usijali
 
..jpm anaogopa mdahalo, kwa sababu ana uwezo mdogo sana wa kujenga hoja.

..hata huu utitiri wa wasanii ktk kampeni zake lengo ni kumlinda Jpm asizungumze kwa muda mrefu akatoa boko.

..hana uwezo wa kuzungumza moja kwa moja na wananchi akawashawishi, badala yake anatumia wasanii kuwahadaa.
 
Mi natamani kweli ufanyike mdahalo na sio lazima awepo Magufuli kama Magufuli hataki sio lazima hata 2015 yeye pamoja na Lowassa hawakutaka mdahalo na haikuwa issue. Mdahalo wagombea wengine wapo mdahalo unaweza kufanyika na tukaona huo uwezo wa Lissu.
 
Habari ya wakati huu wadau wa jukwaa hili pendwa.naombeni moderators msiunganishe thread hii na nyingine tafadhari. Jana nilibahatika kuhudhuria kwenye mkutano wa mgombea wa kiti cha urais kupitia Chadema mh. Tundu A. Lissu. Alianza kuhutubia kwa kuomba ufanyike mdaharo kati yake na mgombea wa nafasi ya uraisi kupitia ccm. Nanukuu kauli yake;

“Natoa rai kwa mgombea mwenzangu wa CCM, tukutane kwenye mdahalo. Ufanyike kwa lugha yoyote ile na uendeshwe na wataalam tutakaokubaliana. Ili tuwaeleze na tuhojiwe hadharani na kujibu hadharani mipango na maono yetu. Naamini mwenzagu ambaye ameshakuwa Rais kwa miaka mitano hatakuwa na hofu ya kushindana na mimi ambaye sijawahi kuwa Rais. Tukutane pamoja. Tuache haya mambo ya kuogopana na kuchengana. Nina imani hatakimbia mdahalo. Akiogopa tutahoji majigambo ya usomi wake”.

Neno ‘MDAHALO’ sio geni. Midahalo baina ya wagombea wa nafasi ya urais imekuwa ni jambo la kawaida sana duniani katika kipindi cha kampeni. Nchi zaidi ya 60 duniani wamekuwa na huu utaratibu, pia makundi mbalimbali ya kijamii yamekuwa yakishinikiza midahalo baina ya wagombea. Midahalo huwasaidia sana wapiga kura kuwa informed na kuwafanya wagombea kufocus na policy issues ambazo zipo kwenye ilani zao zaidi kuliko personal issuees. Lakini pia midahalo huchochea uvumilivu wa kisiasa (political torelance). Pia midahalo huwafanya wagombea kujikita kwenye issue za muhimu ambazo muda mwingine wameshindwa kuzieleza vizuri majukwaani wakati wa kampeni. Nakumbuka nchini marekani, mgombea wa chama cha Republican bwana Bob Dole mwaka 1996 alipohojiwa umuhimu wa mdahalo alisema “They force us to think”. Lakini pia hata Bill Clinton rais wa marekani 1993-2001 alisema
I am convinced that the debates I went through…..actually helped me to be a better president”.

nikirudi kwenye Hoja ya lissu. hoja hii imepokelewa katika mitazamo tofauti tofauti katika mitandao ya kijamii na hata katika mijadala kwenye makundi ya watu. Wapo wanaipokea hoja hii kwa mikono miwili wakiamini kwamba mdahalo ni muhimu sana kwa wagombea katika nafasi ya uraisi, lakini pia kuna baadhi ya watu wameonekana wakipinga hoja hii kwa,madai kwamba magufuri ni mtendaji na sio msemaji hivyo yeye anajikita kwenye kazi tu na sio porojo. Wengine wamesema Wananchi wanataka sera zinazo telelezeka sio mdahalo, Sera za majukuani ni zaidi ya mdahalo. Wengine wameenda mbali zaidi wakisema magufuri sio level ya kushindana kwenye mdahalo na lissu labda kibajaji au msukuma. Katika post ya polepole kwenye mtandao wa tweeter amesema

Screenshot_20200914-130053[1].jpg


Kutokana na hoja hizi nimeona ni vema tueleweshane hapa kwakujenga hoja za msingi bila kutumia lugha za matusi kwakujibu maswali haya

  • Je kwanini baadhi ya watu wanakataa mdahalo?ni athari zipi hujitokeza endapo taifa likiwa linapuuza midahalo?
  • Je hawa wanaopinga mdahalo hawana uelewa kuhusu umuhimu wa midahalo au wanaongozwa na hisia zaidi kuliko akili?
  • Je kuna mtu anaweza kuwa mtendaji bila kuwa mzungumzaji/ mjenga hoja?
  • Mheshimiwa Raisi ananafasi kubwa sana ya kuwin kwenye huu mdahalo kwasababu kuna mengi ameyafanya. Je hamuoni kama kuzuia mdahalo , mnamfanya asiyaeleze vema aliyoyafanya na wananchi wapate nafasi ya kuuliza maswali ili kujuzwa zaidi?
nawasilisha
 
Kwahiyo unataka kusema Lowassa ambaye nae hakutaka mdahalo ile 2015 ni kutokana na uwezo mdogo alionao? na vp wapiga waliyompigia kura hawakuliona hilo?
alifanyiwa interview na Zuhura Yunus wa BBC akaomba po! akasema unanioneaaa
 
Hii ni nzuri sana. Angalau sasa tuwe na issues ambazo tunaweza kupima/kulinganisha sera za vyama! Natamani sana media ingeweza kutusaidia wananchi kwa kutengeneza kitu kama matrix hivi......kwa mfano kwenye elimu (ccm wanasemaje, CDM, ACT?), kwenye mifuko ya jamii ? Kwenye afya? Etc.
 
Ila mdahalo hapana, watamtia aibu tu mgombea wetu......halafu msimu huu nimezimiss pushups ! Kulikoni?
 


Akiwa mkoani Iringa leo tarehe 13 Septemba, Lissu amesema "Natoa rai kwa Mgombea Urais wa CCM na vyombo vyetu vya habari, kufanikisha mdahalo kuhusu mustakabali wa Taifa letu la Tanzania"

=====

LISSU IRINGA: MDAHALO NA MAGUFULI, MIKOPO ELIMU YA JUU NA HIFADHI YA JAMII KWA WOTE

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Mhe. Tundu Lissu ametoa wito kwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Mhe. John Magufuli, kuwa tayari kushiriki mdahalo utakaowakutanisha wagombea hao wawili ili waeleze na kuhojiwa kuhusu maono na mipango yao ya namna ya kutekeleza agenda zinazohusu Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watanzania, ikiwa ni sehemu ya wapiga kura kuwapima na kuwajua vyema washindani hao wakubwa katika nafasi ya juu ya uongozi wa nchi.

Mhe. Lissu amesema kuwa ushiriki wa midahalo kwa wagombea urais ni mojawapo ya kipimo muhimu kinachotumika kimataifa kujua uwezo wa wagombea urais na kwa hapa nchini, takriban wiki mbili tangu kuanza kwa mikutano ya kampeni za uchaguzi mkuu, Agosti 26, mwaka huu, haina shaka yoyote kuwa ushindani katika nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uko kati ya Mgombea wa Chadema na Mgombea wa CCM, ambapo amesisitiza wito huo kwa kuviomba vyombo vya habari vikubwa hususan vituo vya luninga, kuandaa mdahalo huo.

“Natoa rai kwa mgombea mwenzangu wa CCM, tukutane kwenye mdahalo. Ufanyike kwa lugha yoyote ile na uendeshwe na wataalam tutakaokubaliana. Ili tuwaeleze na tuhojiwe hadharani na kujibu hadharani mipango na maono yetu. Naamini mwenzagu ambaye ameshakuwa Rais kwa miaka mitano hatakuwa na hofu ya kushindana na mimi ambaye sijawahi kuwa Rais. Tukutane pamoja. Tuache haya mambo ya kuogopana na kuchengana. Nina imani hatakimbia mdahalo. Akiogopa tutahoji majigambo ya usomi wake,” amesema Mhe. Lissu.

Aidha, Mhe. Lissu amesema Serikali atakayoiunda chini ya chama Chadema, itaondoa mara moja masharti ya kibaguzi na utaratibu mbovu wa kisheria unaotumika katika mfumo wa sasa wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ambao umegeuka kuwa adha kubwa kwa wanafunzi na wazazi na badala yake, kanuni pekee itakayosimamia upatikanaji wa mikopo hiyo ni uhitaji wa mhusika.

Akisisitiza hoja hiyo, Mhe. Lissu amesema kuwa mfumo wa urejeshaji riba ya mikopo hiyo unaotumika sasa nao pia uko kinyume na utaratibu wa kisheria uliokuwa mwongozo kwa wanafunzi na wazazi kuingia makubaliano ya kukopeshwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu nchini (HESLB), ambapo Serikali imeingiza utaratibu mwingine kuwataka wanufaika kulipa riba ya asilimia 15 badala ya asilimia 3 ya awali, akiahidi kuwa Serikali ya Chadema itaufutilia mbali kwa sababu unawafilisi kiuchumi wanufaikaji wa mikopo hiyo.

Akihutubia mkutano wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020, uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi wa Mji wa Iringa na viunga vyake, uliofanyika leo katika Uwanja wa Mwembetogwa, Mhe. Lissu amesema mfumo unaotumika sasa umewekewa utaratibu ambao unawaumiza na kuwabagua wanafunzi na wazazzi hata wenye uhitaji wa mikopo hiyo ili waweze kujielimisha elimu ya juu kwa kadri ya uwezo wao.

Aidha, Mhe. Lissu akizungumzia umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa watu wote bila kubagua hali wala hadhi ya mtu, amesema kuwa kila mmoja katika wakati usiotarajiwa anaweza kuhitaji msaada wa kuhifadhiwa iwe kwa matibabu, ulemavu usiotarajiwa, umri wa uzeeni, kupoteza ajira au uhitaji wowote ule, hivyo Serikali atakayoiunda, akichaguliwa Oktoba 28, mwaka huu, itaweka utaratibu utakaohakikisha kila Mtanzania anapata hifadhi kadri ya ya mahitaji, ikiwemo bima ya afya, badala ya sasa wanaohudumiwa walioko kwenye ajira rasmi pekee.

“Iringa ni mahali sahihi kabisa kuzungumzia agenda ya hali ya elimu yetu na hususan elimu ya juu. Kuna tatizo katika mfumo wetu wa utoaji elimu nchini. Mtakumbuka wakati ule nilipokuja wakati wa kutafuta udhamini nilizungumza hili. Tunapaswa kuubadili ili uweze kuwapatia watoto wetu maarifa na uwezo wa kufikiria kutatua matatizo yao na kuajiriwa mahali popote duniani. Kwa sababu hilo nililisema wakati ule na mlinielewa, leo nataka nizungumzie hili la elimu ya juu na hususan elimu ya juu, chuo kikuu. Wale wa makamo yangu wanajua kuwa wakati wetu elimu tuliyosoma ililipwa na umma wa Watanzania. Katika zama za CCM wanaita ya kisasa, ili motto wako asome Chuo Kikuu lazima umlipie au akopeshwe na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, mikopo hiyo na utaratibu wa utoaji wake na urejeshaji wake, imegeuka kuwa adha kubwa mno kwa wazazi na wanafunzi wenyewe.

“Kumekuwa na masharti ya kibaguzi katika utoaji wa mikopo ya hiyo. Wanafunzi waliosoma shule za binafsi wamekuwa wakiambiwa hawastahili kupata mikopo. Wanafunzi wengine wengi wameshindwa kuendelea na masomo yao. Serikali ya Chadema, nitakayoiunda mkinichagua Oktoba 28, mwaka huu, itaweka utaratibu unaohakikisha kila mtoto anastahili kupata mkopo bila kujali alisoma wapi. Kanuni pekee itakayotuongoza ni, je anahitaji mkopo? Tutahakikisha pia wanufaikaji wote wanatendewa haki kwa kurejea kwenye sheria ya mwanzo iliyokuwa inaelekeza makato ya riba ya asilimia 3 badala ya sasa ambapo imefanywa kuwa asilimia 15 hali inayowafilisi kiuchumi,” amesema Mhe. Lissu.

Akitumia mkutano huo pia kuomba kura zake na kuwaombea kura wagombea ubunge na udiwani kwa tiketi ya Chadema katika Mkoa wa Iringa, Mhe. Lissu amezungumzia umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa watu wote, ambapo amesema kuwa mfumo uliopo sasa pamoja na kuwatenga watu wengine wasiokuwa kwenye ajira rasmi, pia umeshindwa kuwahudumia hata wahusika baada ya kutumiwa vibaya kwa matumizi yasiyokuwa na tija kwa wachangiaji, ambapo amesema fedha nyingi zimefujwa kiasi cha mifuko hiyo kushindwa kujiendesha na hatimae kufilisika.

Ameongeza kuwa tatizo la hifadhi ya jamii si uwingi au uchache wake, bali ni matumizi mabaya ya rasilimali zake, hivyo ameahidi kuwa Serikali atakayoiunda baada ya kuchaguliwa mwezi Oktoba, itahakikisha utaratibu mpya wa hifadhi ya jamii unawahusisha watu wote kwa ajili ya maendeleo yao na kuhakikisha inaendeshwa katika namna inayozingatia matumizi sahihi yenye tija kwa wahusika ambao watakuwa na uhuru wa kuamua.

“Tunazungumzia mfumo wa hifadhi ya jamii utakaoweza kuwahudumia watu wote, wastaafu wetu, wazee, wasiojiweza, bima ya afya. Tutahakikisha kila asiyejiweza anatunzwa na hifadhi ya jamii. Sisi wote hapa tutazeeka, tunaweza kuwa walemavu, tunaweza kupoteza ajira, tutaugua, tutahitaji kuhifadhiwa. Shida hapa kwetu si wingi wa mifuko, bali mifuko hiyo imefujwa. Walipoifilisi wakaleta masuala ya fao la kujitoa na ile kanuni mpya ya kikotoo, maana mifuko hiyo haina fedha tena,” amesema Mhe. Lissu.

Mhe. Lissu amesema kuwa utekelezaji wa mipango hiyo utahitaji vyanzo vya uhakika vya fedha, ambapo ametaja mapato yatakayotokana na uuzaji wa gesi asilia, ambayo uendelezaji wake ulianza wakati wa Serikali ya awamu ya nne, ulioibainisha Tanzania kuwa mojawapo ya nchi zenye utajiri mkubwa wa rasilimali hiyo, kabla haujatelekezwa katika awamu ya tano, itakuwa ni mojawapo ya vyanzo vya fedha ili kuhakikisha kila mtoto wa Kitanzania anapata elimu ya uhakika na Watanzania wote wanapewa haki ya hifadhi ya jamii.

Mhe. Lissu ametumia mikutano yake mitatu katika maeneo ya Migoli (Isimani), Ifunda (Kalenga) na Iringa mjini, kunadi agenda mbalimbali zilizomo katika Ilani ya Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020, inayozungumzia masuala yote katika muktadha wa Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu.

Imetolewa leo, Jumapili, Septemba 13, 2020 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano

Ukweli ni huu hapa...

Magufuli ni Rais JMT...ni raia namba moja wa Tanzania huwezi kumkalisha meza moja ya mdahalo na Wahuni.

Lisu kwanini asiombe mdahalo na wenzake wanaoitaka Ofisi kuu kwa mara ya kwanza? Aombe mdahalo na Membe, Sipunda na Lipumba!! Period
 
Habari ya wakati huu wadau wa jukwaa hili pendwa.naombeni moderators msiunganishe thread hii na nyingine tafadhari. Jana nilibahatika kuhudhuria kwenye mkutano wa mgombea wa kiti cha urais kupitia Chadema mh. Tundu A. Lissu. Alianza kuhutubia kwa kuomba ufanyike mdaharo kati yake na mgombea wa nafasi ya uraisi kupitia ccm. Nanukuu kauli yake;

“Natoa rai kwa mgombea mwenzangu wa CCM, tukutane kwenye mdahalo. Ufanyike kwa lugha yoyote ile na uendeshwe na wataalam tutakaokubaliana. Ili tuwaeleze na tuhojiwe hadharani na kujibu hadharani mipango na maono yetu. Naamini mwenzagu ambaye ameshakuwa Rais kwa miaka mitano hatakuwa na hofu ya kushindana na mimi ambaye sijawahi kuwa Rais. Tukutane pamoja. Tuache haya mambo ya kuogopana na kuchengana. Nina imani hatakimbia mdahalo. Akiogopa tutahoji majigambo ya usomi wake”.

Neno ‘MDAHALO’ sio geni. Midahalo baina ya wagombea wa nafasi ya urais imekuwa ni jambo la kawaida sana duniani katika kipindi cha kampeni. Nchi zaidi ya 60 duniani wamekuwa na huu utaratibu, pia makundi mbalimbali ya kijamii yamekuwa yakishinikiza midahalo baina ya wagombea. Midahalo huwasaidia sana wapiga kura kuwa informed na kuwafanya wagombea kufocus na policy issues ambazo zipo kwenye ilani zao zaidi kuliko personal issuees. Lakini pia midahalo huchochea uvumilivu wa kisiasa (political torelance). Pia midahalo huwafanya wagombea kujikita kwenye issue za muhimu ambazo muda mwingine wameshindwa kuzieleza vizuri majukwaani wakati wa kampeni. Nakumbuka nchini marekani, mgombea wa chama cha Republican bwana Bob Dole mwaka 1996 alipohojiwa umuhimu wa mdahalo alisema “They force us to think”. Lakini pia hata Bill Clinton rais wa marekani 1993-2001 alisema
I am convinced that the debates I went through…..actually helped me to be a better president”.

nikirudi kwenye Hoja ya lissu. hoja hii imepokelewa katika mitazamo tofauti tofauti katika mitandao ya kijamii na hata katika mijadala kwenye makundi ya watu. Wapo wanaipokea hoja hii kwa mikono miwili wakiamini kwamba mdahalo ni muhimu sana kwa wagombea katika nafasi ya uraisi, lakini pia kuna baadhi ya watu wameonekana wakipinga hoja hii kwa,madai kwamba magufuri ni mtendaji na sio msemaji hivyo yeye anajikita kwenye kazi tu na sio porojo. Wengine wamesema Wananchi wanataka sera zinazo telelezeka sio mdahalo, Sera za majukuani ni zaidi ya mdahalo. Wengine wameenda mbali zaidi wakisema magufuri sio level ya kushindana kwenye mdahalo na lissu labda kibajaji au msukuma. Katika post ya polepole kwenye mtandao wa tweeter amesema

View attachment 1569505

Kutokana na hoja hizi nimeona ni vema tueleweshane hapa kwakujenga hoja za msingi bila kutumia lugha za matusi kwakujibu maswali haya

  • Je kwanini baadhi ya watu wanakataa mdahalo?ni athari zipi hujitokeza endapo taifa likiwa linapuuza midahalo?
  • Je hawa wanaopinga mdahalo hawana uelewa kuhusu umuhimu wa midahalo au wanaongozwa na hisia zaidi kuliko akili?
  • Je kuna mtu anaweza kuwa mtendaji bila kuwa mzungumzaji/ mjenga hoja?
  • Mheshimiwa Raisi ananafasi kubwa sana ya kuwin kwenye huu mdahalo kwasababu kuna mengi ameyafanya. Je hamuoni kama kuzuia mdahalo , mnamfanya asiyaeleze vema aliyoyafanya na wananchi wapate nafasi ya kuuliza maswali ili kujuzwa zaidi?
nawasilisha
Wananchi wenyewe hawaoni umuhimu wa mdahalo,na ndio maana 2015 wagombea wa urais wa hivyo vyama(ccm na chadema) wote walikataa mdahalo na hakukuwa na tabu na wao ndio walishika nafasi ya kwanza na ya pili na kuwaacha mbali hata wale wagombea waliyoshiriki mdahalo.
 
Back
Top Bottom