Uchaguzi 2020 Tundu Lissu (CHADEMA), aomba mdahalo na Dkt. Pombe Magufuli (CCM)

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu (CHADEMA), aomba mdahalo na Dkt. Pombe Magufuli (CCM)

Tundu Lissu si mwanasiasa ni mwanaharakati hilo wengi wanasema, wengi wape.

Nimewahi kusema humu kwamba namfahamu Tundu Lissu vizuri tu na ni mtu wa kawaida sana.

Ni kweli kapata tatizo la ulemavu ambao haijulikani mpaka leo wahusika shambulizi dhidi yake ni akina nani, hivyo mimi siwezi kuliongolea hilo.

Lakini baada ya uchaguzi October 28 Tundu Lissu ataendelea kuwa mwanaharakati wa kawaida akiwa Chadema.

Ila huko mbele atajifunza namna ya kufanya siasa akiwa Chadema.

..usiseme hujui waliomshambulia.

..hivi hujui chain of command ya aliyeondoa walinzi wa area D ili kuwapisha magaidi wakamshambulie Tundu Lissu?

..kweli hujui nani mwenye mamlaka ya kuondoa walinzi wale? Na mamlaka yake ni nidhamu huijui?
 
Ccm kumbukeni mwaka 2015 mliomba mdahalo baada ya kuona mgombea wa ukawa ni dhaifu,,Sasa mnaombwa mdahalo mnaanza kujinyata nyata inamaana Rais wetu anaogopa mdahalo wa kuelezea ilani na sera ya chama chake?mdahalo ni sehemu ya kufanya kampeni hofu ya nini?rais ni msomi tena degree tatu na amefanya presentation kibao ana uzoefu na pia kwa miaka 20 amekuwa waziri alikuwa anajibu maswali bungeni,akikataa mdahalo ataonesha ni dhaifu anastahili tumtumbue atakuwa na cheti feki,, haiwezekani PHD mzima uogope mdahalo.
 
Lissu anatafta kiki, ni kama anatafta umaarufu kupitia magufuli, na alivyo anaongea bila break au kutumia akili magufuli asiingie mtegon, maana kubishana na kichaa hua ni ngum sana
 
Ikishakuwa serikali ya majungu hayo ndiyo matokeo yake.

Kuna sheria kanuni na taratibu zilizotungwa kutoka kwenye katiba.

Sio kufanya kazi kwa hisia. Hata kama hupendi jambo lakini unabanwa kisheria ni wajibu wako kutekeleza.

Huu upuuzi ndiyo tunausikia eti mkichagua upinzani hampelekewi maendeleo.

Sasa sijui ukishachagua upinzani unakuwa nchi nyingine.
Siyo kweli kuwa ukichagua upinzani hupelekwei maendeleo kwenye jimbo lako, tatizo ni kuwa wabunge wa upinzani huwa hawapeleki mada zinazohusu majimbo yao bungeni bali wao huwa ni wanaharakati wa kupinga kila kitu cha serikali tu. Mpaka serikali ipitie mlango wa nyuma mikoani ndipo mambo ya majimbo husika yanapofika serikalini

Umewahi kumsikiliza Mbowe hapa?

 
Kwani kinachohofiwa kwenye mdahalo ni nini? Mbona mnahangaika hivi? Mnaelewa hapo kuwa mtu wenu hamuwezi Lissu kwa hoja, sasa mnajaribu kufunikafunika.

Usiseme mtu wenu, mtaje raisi alie madarakani ambae ni John Magufuli.

Na ndie mgombea wa sasa wa CCM.
 
..usiseme hujui waliomshambulia.

..hivi hujui chain of command ya aliyeondoa walinzi wa area D ili kuwapisha magaidi wakamshambulie Tundu Lissu?

..kweli hujui nani mwenye mamlaka ya kuondoa walinzi wale? Na mamlaka yake ni nidhamu hujui?

Usilazimishe mimi kuamini unachokiamini wewe.

Kila mtu ana haki na wajibu wa kutafakari shutuma za Tundu Lissu dhidi ya serikali.
 
Uraisi ni cheo cha heshima, mwenye cheo hicho hawezi kupoteza muda kufanya mdahalo na wapuuzi waropokaji
 
Inawezekana na wewe hujui kiingereza; unaweza kujua kuasiliana kwa kiingiereza bila kukijua vizuri kama Lissu na Magufuli walivyo.

Nimebahatika kusomea kwenye nchi inayoongea Kiingereza, naishi kwenye nchi inayoongea Kiingereza na mke na watoto wangu hawajui Kiswahili zaidi ya Kiingereza...
 


Akiwa mkoani Iringa leo tarehe 13 Septemba, Lissu amesema "Natoa rai kwa Mgombea Urais wa CCM na vyombo vyetu vya habari, kufanikisha mdahalo kuhusu mustakabali wa Taifa letu la Tanzania"

=====

LISSU IRINGA: MDAHALO NA MAGUFULI, MIKOPO ELIMU YA JUU NA HIFADHI YA JAMII KWA WOTE

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Mhe. Tundu Lissu ametoa wito kwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Mhe. John Magufuli, kuwa tayari kushiriki mdahalo utakaowakutanisha wagombea hao wawili ili waeleze na kuhojiwa kuhusu maono na mipango yao ya namna ya kutekeleza agenda zinazohusu Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watanzania, ikiwa ni sehemu ya wapiga kura kuwapima na kuwajua vyema washindani hao wakubwa katika nafasi ya juu ya uongozi wa nchi.

Mhe. Lissu amesema kuwa ushiriki wa midahalo kwa wagombea urais ni mojawapo ya kipimo muhimu kinachotumika kimataifa kujua uwezo wa wagombea urais na kwa hapa nchini, takriban wiki mbili tangu kuanza kwa mikutano ya kampeni za uchaguzi mkuu, Agosti 26, mwaka huu, haina shaka yoyote kuwa ushindani katika nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uko kati ya Mgombea wa Chadema na Mgombea wa CCM, ambapo amesisitiza wito huo kwa kuviomba vyombo vya habari vikubwa hususan vituo vya luninga, kuandaa mdahalo huo.

“Natoa rai kwa mgombea mwenzangu wa CCM, tukutane kwenye mdahalo. Ufanyike kwa lugha yoyote ile na uendeshwe na wataalam tutakaokubaliana. Ili tuwaeleze na tuhojiwe hadharani na kujibu hadharani mipango na maono yetu. Naamini mwenzagu ambaye ameshakuwa Rais kwa miaka mitano hatakuwa na hofu ya kushindana na mimi ambaye sijawahi kuwa Rais. Tukutane pamoja. Tuache haya mambo ya kuogopana na kuchengana. Nina imani hatakimbia mdahalo. Akiogopa tutahoji majigambo ya usomi wake,” amesema Mhe. Lissu.

Aidha, Mhe. Lissu amesema Serikali atakayoiunda chini ya chama Chadema, itaondoa mara moja masharti ya kibaguzi na utaratibu mbovu wa kisheria unaotumika katika mfumo wa sasa wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ambao umegeuka kuwa adha kubwa kwa wanafunzi na wazazi na badala yake, kanuni pekee itakayosimamia upatikanaji wa mikopo hiyo ni uhitaji wa mhusika.

Akisisitiza hoja hiyo, Mhe. Lissu amesema kuwa mfumo wa urejeshaji riba ya mikopo hiyo unaotumika sasa nao pia uko kinyume na utaratibu wa kisheria uliokuwa mwongozo kwa wanafunzi na wazazi kuingia makubaliano ya kukopeshwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu nchini (HESLB), ambapo Serikali imeingiza utaratibu mwingine kuwataka wanufaika kulipa riba ya asilimia 15 badala ya asilimia 3 ya awali, akiahidi kuwa Serikali ya Chadema itaufutilia mbali kwa sababu unawafilisi kiuchumi wanufaikaji wa mikopo hiyo.

Akihutubia mkutano wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020, uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi wa Mji wa Iringa na viunga vyake, uliofanyika leo katika Uwanja wa Mwembetogwa, Mhe. Lissu amesema mfumo unaotumika sasa umewekewa utaratibu ambao unawaumiza na kuwabagua wanafunzi na wazazzi hata wenye uhitaji wa mikopo hiyo ili waweze kujielimisha elimu ya juu kwa kadri ya uwezo wao.

Aidha, Mhe. Lissu akizungumzia umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa watu wote bila kubagua hali wala hadhi ya mtu, amesema kuwa kila mmoja katika wakati usiotarajiwa anaweza kuhitaji msaada wa kuhifadhiwa iwe kwa matibabu, ulemavu usiotarajiwa, umri wa uzeeni, kupoteza ajira au uhitaji wowote ule, hivyo Serikali atakayoiunda, akichaguliwa Oktoba 28, mwaka huu, itaweka utaratibu utakaohakikisha kila Mtanzania anapata hifadhi kadri ya ya mahitaji, ikiwemo bima ya afya, badala ya sasa wanaohudumiwa walioko kwenye ajira rasmi pekee.

“Iringa ni mahali sahihi kabisa kuzungumzia agenda ya hali ya elimu yetu na hususan elimu ya juu. Kuna tatizo katika mfumo wetu wa utoaji elimu nchini. Mtakumbuka wakati ule nilipokuja wakati wa kutafuta udhamini nilizungumza hili. Tunapaswa kuubadili ili uweze kuwapatia watoto wetu maarifa na uwezo wa kufikiria kutatua matatizo yao na kuajiriwa mahali popote duniani. Kwa sababu hilo nililisema wakati ule na mlinielewa, leo nataka nizungumzie hili la elimu ya juu na hususan elimu ya juu, chuo kikuu. Wale wa makamo yangu wanajua kuwa wakati wetu elimu tuliyosoma ililipwa na umma wa Watanzania. Katika zama za CCM wanaita ya kisasa, ili motto wako asome Chuo Kikuu lazima umlipie au akopeshwe na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, mikopo hiyo na utaratibu wa utoaji wake na urejeshaji wake, imegeuka kuwa adha kubwa mno kwa wazazi na wanafunzi wenyewe.

“Kumekuwa na masharti ya kibaguzi katika utoaji wa mikopo ya hiyo. Wanafunzi waliosoma shule za binafsi wamekuwa wakiambiwa hawastahili kupata mikopo. Wanafunzi wengine wengi wameshindwa kuendelea na masomo yao. Serikali ya Chadema, nitakayoiunda mkinichagua Oktoba 28, mwaka huu, itaweka utaratibu unaohakikisha kila mtoto anastahili kupata mkopo bila kujali alisoma wapi. Kanuni pekee itakayotuongoza ni, je anahitaji mkopo? Tutahakikisha pia wanufaikaji wote wanatendewa haki kwa kurejea kwenye sheria ya mwanzo iliyokuwa inaelekeza makato ya riba ya asilimia 3 badala ya sasa ambapo imefanywa kuwa asilimia 15 hali inayowafilisi kiuchumi,” amesema Mhe. Lissu.

Akitumia mkutano huo pia kuomba kura zake na kuwaombea kura wagombea ubunge na udiwani kwa tiketi ya Chadema katika Mkoa wa Iringa, Mhe. Lissu amezungumzia umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa watu wote, ambapo amesema kuwa mfumo uliopo sasa pamoja na kuwatenga watu wengine wasiokuwa kwenye ajira rasmi, pia umeshindwa kuwahudumia hata wahusika baada ya kutumiwa vibaya kwa matumizi yasiyokuwa na tija kwa wachangiaji, ambapo amesema fedha nyingi zimefujwa kiasi cha mifuko hiyo kushindwa kujiendesha na hatimae kufilisika.

Ameongeza kuwa tatizo la hifadhi ya jamii si uwingi au uchache wake, bali ni matumizi mabaya ya rasilimali zake, hivyo ameahidi kuwa Serikali atakayoiunda baada ya kuchaguliwa mwezi Oktoba, itahakikisha utaratibu mpya wa hifadhi ya jamii unawahusisha watu wote kwa ajili ya maendeleo yao na kuhakikisha inaendeshwa katika namna inayozingatia matumizi sahihi yenye tija kwa wahusika ambao watakuwa na uhuru wa kuamua.

“Tunazungumzia mfumo wa hifadhi ya jamii utakaoweza kuwahudumia watu wote, wastaafu wetu, wazee, wasiojiweza, bima ya afya. Tutahakikisha kila asiyejiweza anatunzwa na hifadhi ya jamii. Sisi wote hapa tutazeeka, tunaweza kuwa walemavu, tunaweza kupoteza ajira, tutaugua, tutahitaji kuhifadhiwa. Shida hapa kwetu si wingi wa mifuko, bali mifuko hiyo imefujwa. Walipoifilisi wakaleta masuala ya fao la kujitoa na ile kanuni mpya ya kikotoo, maana mifuko hiyo haina fedha tena,” amesema Mhe. Lissu.

Mhe. Lissu amesema kuwa utekelezaji wa mipango hiyo utahitaji vyanzo vya uhakika vya fedha, ambapo ametaja mapato yatakayotokana na uuzaji wa gesi asilia, ambayo uendelezaji wake ulianza wakati wa Serikali ya awamu ya nne, ulioibainisha Tanzania kuwa mojawapo ya nchi zenye utajiri mkubwa wa rasilimali hiyo, kabla haujatelekezwa katika awamu ya tano, itakuwa ni mojawapo ya vyanzo vya fedha ili kuhakikisha kila mtoto wa Kitanzania anapata elimu ya uhakika na Watanzania wote wanapewa haki ya hifadhi ya jamii.

Mhe. Lissu ametumia mikutano yake mitatu katika maeneo ya Migoli (Isimani), Ifunda (Kalenga) na Iringa mjini, kunadi agenda mbalimbali zilizomo katika Ilani ya Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020, inayozungumzia masuala yote katika muktadha wa Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu.

Imetolewa leo, Jumapili, Septemba 13, 2020 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano

Magufuli hahitaji kuongea ongea, magufuli siyo debe shinda (amejaa)! Magufuli ni maneno machache saana na ni mwingi wa vitendo.
Sote tumeona au kusikia - Lissu bado ana siasa za viongozi wa zamani! Siasa za maneno jukwaani na mvinyo! Kazi za kuonyesha hana na watu wake wanakufa kwa umasikini.
 
Usilazimishe mimi kuamini unachokiamini wewe.

Kila mtu ana haki na wajibu wa kutafakari shutuma za Tundu Lissu dhidi ya serikali.

..sasa wewe shutuma za kuwa walinzi waliondolewa area D umezichukuliaje?

..umeridhika na majibu ya serikali kuhusu shutuma hizo?

..umeridhika na jinsi jeshi la Polisi lilivyoshughulikia uchunguzi wa shambulizi lile?
 
Lissu ameshakutana na viongozi wa dunia ya kwanza na kuhojiwa na vyombo vyao vya habari ije kuwa Magufuli.
mu ignore tuu kama Magu anacheza mapanga na wakina Chege kweri anamuita Lissu muhuni? hawa marobot ya Lumumba wahanga wakukosa akiri kweri
 
Ikishakuwa serikali ya majungu hayo ndiyo matokeo yake.

Kuna sheria kanuni na taratibu zilizotungwa kutoka kwenye katiba.

Sio kufanya kazi kwa hisia. Hata kama hupendi jambo lakini unabanwa kisheria ni wajibu wako kutekeleza.

Huu upuuzi ndiyo tunausikia eti mkichagua upinzani hampelekewi maendeleo.

Sasa sijui ukishachagua upinzani unakuwa nchi nyingine.
Mkuu huyo uliyemnukuu unadhan haielwei hayo uliyoandika? Ni basi tu anaongozwa na mahaba jumlisha na unafiki.
 
Kwani kinachohofiwa kwenye mdahalo ni nini? Mbona mnahangaika hivi? Mnaelewa hapo kuwa mtu wenu hamuwezi Lissu kwa hoja, sasa mnajaribu kufunikafunika.
Mnachong'ang'ania kwenye mdahalo ni kipi hasa? Mmeona watanzania hawaelewi sera zenu mnaforce mdahalo. Magufuli yupo busy na kuongoza nchi na kufanya kampeni kwa wakati mmoja
 
Nimebahatika kusomea kwenye nchi inayoongea Kiingereza, naishi kwenye nchi inayoongea Kiingereza na mke na watoto wangu hawajui Kiswahili zaidi ya Kiingereza...
Unaweza kuwa na familia inayoongea kiingereza wakati mwenyewe unababaisha ila mnaelewana kimawasiliano tu! Nimeshakutana na familia nyingi za aina ambayo mke anakuwa ni face ya familia kwa sababu mwanamme hajui lugha vizuri. Binafsi watoto wangu wote hawajui kiswahili sawaswa ingawa mke wangu ni mtanzania ambaye siyo kabila langu na wala sijui lugha yao lakini siwezi kutumia leverage ya watoto wangu au mke wangu kujua lugha zao. Mimi nazungumzia lugha ya kiingereza kwa sababu ya nature ya kazi yangu, siyo kwa sababu ya mazingira ya familia yangu.
 
..usiseme hujui waliomshambulia.

..hivi hujui chain of command ya aliyeondoa walinzi wa area D ili kuwapisha magaidi wakamshambulie Tundu Lissu?

..kweli hujui nani mwenye mamlaka ya kuondoa walinzi wale? Na mamlaka yake ni nidhamu hujui?
Ikifika angle hii hua wanajitoa ufahamu, kuna mmoja hapo juu anadai baada ya shutuma nyingi za kuituhumu serikali, eti serikali nayo ikaacha kufuatilia. Ni kama vile imesusa wakati ni wajibu wao kuchunguza na kutoa ripoti ya uchunguzi na wahusika wawajibishwe!!
 
Sera zipo kwenye midahalo.

Tunataka mdahalo ili magufuli na Lisu watueleze sera zao.

Maana kusema kweli sera ya magufili siijui mpaka sasa. Huwa namsikia tu anasema ilani this ilani that, mara ndege sijui nini.

Tukipata mdahalo wa kumuhoji uso kwa uso itatusaidia kubaini maono yake.
Kama umeshindwa kujua lengo haswa la Magufuli kuinadi ilani makini ya ccm hata huo mdahalo hautakusaidia kitu comrade
 
Ikifika angle hii hua wanajitoa ufahamu, kuna mmoja hapo juu anadai baada ya shutuma nyingi za kuituhumu serikali, eti serikali nayo ikaacha kufuatilia. Ni kama vile imesusa wakati ni wajibu wao kuchunguza na kutoa ripoti ya uchunguzi na wahusika wawajibishwe!!

..wanawajua waliotaka kumuua Tundu Lissu.

..wangekuwa hawawajui wangewatafuta, maana kuna uwezekano wakashambulia na mwingine.

..lakini kwasababu wanawajua, na wanajua walitumwa kumuua Tundu Lissu na siyo mtu mwingine, basi ndio maana unaona wametulia tu.
 
Lissu kama kweli anataka mdahalo asubiri mgombea wa 2020 apatikane ndipo ajiandae.

Magufuli ni mtekelezaji wa ilani tangu 2015 hayupo katika hadhi sawa na Lissu kwa sasa.

Mwenye jukumu la kutekeleza malengo ya chama kwa vitendo hawezi kuwekwa jukwaa moja na yule mwenye ndoto za urais.
 
Back
Top Bottom