Tundu Lissu: DCI Kingai kaniandikia barua ya wito wa kuripoti ofisini kwake. Nipo nje ya nchi, wiki ijayo narudi kumkabili

Tundu Lissu: DCI Kingai kaniandikia barua ya wito wa kuripoti ofisini kwake. Nipo nje ya nchi, wiki ijayo narudi kumkabili

Ofisi ya Upelelezi wa makosa ya jinai imemtaka Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Antiphas Mughwai Lissu kufika kwa Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya Jinai makao makuu Dar es Salaam kwa kosa la kutoa maneno yasiyo na staha kumjibu Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Hayo yamesemwa kupitia barua ya Ofisi hiyo kwa Lissu ikibainisha kuwa Ofisi inafanya uchunguzi kuhusiana na maneno ambayo Lissu aliyatumia ambayo hayana staha kumjibu Mh. Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kuanzia tarehe 15/07/2023.

“Ili tuweze kukamilisha uchunguzi wetu, ofisi hii inakutaka ufike ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Makao Makuu Ndogo Dar es Salaam siku ya alhamisi tarehe 20 Julai, 2023 saa 3:00 kamili asubuhi bila kukosa kwa ajili ya mahojiano.” imesema barua hiyo.
FB_IMG_1689719683536.jpg
 
Huu mwenge unatakiwa itupwe mbali ndio inafanya Watanzania watawaliwe na mazuzu..usikute ndio kimbola tunapigwa watanzani tunakosa umoja wa kusimamia mambo yetu.
Usikute? We hujui ili tutawalike lazima moto upitishwe kila wilaya? Na kafara kama zote🤔🤔
 
Kama Akina Lissu na Mbowe walikubali mimi na wewe ni nani tupinge?

Kama kwa maumivu na shida walizopata kujenga chama hadi mimi na wewe tukakipenda na ikafika mahali wakatafakari wakaona Lowasa anaweza kugombea sidhani kama kuna Mtu mwingine ana uhalali wa kupinga.

I stand to be corrected

Kwani hao hawawezi kufanya maamuzi kwa makosa? Au wakishaamua chochote kwako ww ni sawa? Huyo Lowassa leo bado yuko cdm?
 
Shame on it, yaani mkataba wa bandari ndio iwe kero wananchi kuanza kukamatwa kamatwa hovyo kwa kutoa maoni ya kupinga hicho kitu! Kama wananchi wenyewe hawautaki huo mkataba ya nini kuwanyamazisha kwa kitisho? Hao ni akina lissu wanaojulikana, wapo wasiojulikana ambao nao hawautaki huo mkataba wakikamatwa wote mahabusu zote nchini hazitatosha
 
Safi sana akamkabili, namshauri Kingai kitu cha kwanza ili kuisaidia mahakama ampeleke Lussu akapimwe wazimu.
 
Hoja gani Mzee? Matusi na kudhalilisha sio Demokrasia vinginevyo hata Shetani wenu atawashangaa View attachment 2692265
"Utu na heshima ya Rais Samia" itatokana na matendo ya uongozi wake. Kama matendo yake hayaendani na matakwa ya wananchi anaowaongoza, asitegemee kupewa hiyo heshima inayohimizwa..

Maajabu ya nchi yetu ndiyo haya. Mtu anatumia cheo chake kufanya ujambazi kwa watu wake, badala ya kumshutumu na kumtaka aachie ngazi, kuna watu bado wanataka jambazi huyo apewe heshima?

Samia wakati huu angetakiwa kuwa jela badala ya kudai apewe heshima.

Heshima haidaiwi, inatolewa tu kwa mtu yeyote kutokana na matendo yake katika jamii anayoishi
 
Baada ya mawakili Mwabukusi, Madeleka & Ruge Nshala, sasa ni zamu yangu. Leo DCI Kingai ametuma watu kuleta barua ya kuripoti ofisini kwake. Wamerudi nayo baada ya kujulishwa niko nje ya nchi. Nitarudi wiki ijayo kuwakabili. Madalali wa bandari zetu wasitutishe!

Rais anayesaini mikataba ya hovyo kuliko hata wa Chifu Mangungo; anayegawa bandari zetu zote na nia za usafirishaji kisirisiri kwa wageni; anayelazimisha Bunge kubariki uharamia huo, na anayenyang'anya watu wetu ardhi zao na kuwapa wageni, anastahili kukosolewa kwa staha gani?

Tundu Lissu
Julai 18, 2023

View attachment 2692285
Barua ya wito wa Polisi


====

Mnamo jana, Julai 17 Mdau wa JF alidokeza kuwa Lissu na Mbowe walikuwa wanasakwa DOKEZO - Lissu na Mbowe wanatafutwa kukamatwa lakini Lissu aliifahamisha JF "Sijazisikia tetesi hizo. Kama ni za kweli, itakuwa ni mara ya kwanza kwa mimi au Mwenyekiti kukamatwa?"
Huyo kingai ameshatibiwa ile fistula yake aliyopata wakati anawekwa mtukati na Kibatala?
 
...kila laheri
Hii "kila la heri" inamhusu nani, mkuu 'Proved'?

Maajabu ninayoyaona hapa ni kuwa mtu anayepanga mbinu za ujambazi kwa taifa lake, ndiye huyo huyo anayepambana kuwabana wanaotafuta njia za kumzuia jambazi huyo, hadi kutumia vifaa vinavyotakiwa kuzuia ujambazi huo, kama polisi.

Haya uliwahi kuyaona wapi?
 
ala, komandoo Kingai mzee wa Rau madukani bado upo baba !! umeshasahau lile kalinyekalinye la PGO 😀
 
Samahani bwana Red blood cells hivi akitumia lugha ya ustaha ni kwamba hatoeleweka ama naye ni wale wanaotafuta sifa mitandaoni?
Kama kiongozi ukiongea vitu vya kijinga na watu wakakuambia huo ulioongea ni upuuzi. Kuna shida gani? Kiongozi anapokusea na anakaza shingo, unataka wanaoongozwa wafanyaje?
 
Sa100 bhn badala ya kurekebisha makosa anaanza kuweka watu ndani.Kwamba mkimuweka TL ndani ndio itabadilisha mawazo ya watu?Juzi hapo mtoto wa Karume kawapa makavu live mkaishia kumtoa kwenye chama
 
Kamata hao weka kolokoloni wasote kabisa mpaka 2026. Mbowe na Lisu ni wahuni wahuni, walitutukania Dkt Magufuli mpaka wakafanya sherehe ya kifo chake na wameyakoroga tena kwa Mama, acha wakomeshwe!

Ningekuwa polisi ningehakikisha namrusha kichura chura lisu na mbowe halafu namtandika mbowe kirungu utosini huku analia anaruka kichura chura na lisu namchapa kirungu cha kwenye magoti namrusha kichura chura akome.
Utazikunya hizo hela ulizoongwa na Dp World🤣🤣
 
TUACHE KUCHANGANYA KWA MIHEMKO YA KISIASA NA PROPAGANDA ZA KIJINGA KWENYE TAALUMA YA SHERIA. MFANO HALISI NI HUU HAPA
SABABU ZA KUKAMATWA WAKILI PETER MADELEKA

Mnamo mwaka 2020 Wakili Peter Madeleka alikamatwa na kufunguliwa kesi ya Uhujumu Uchumi no. 40 (Economic case no 40/2020) katika mahakama ya Hakimu Mkazi ya Arusha. Katika kesi hiyo alishtakiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo kughushi (forgery) kinyume na Sheria ya Mwenendo wa Adhabu (Penal Code) kifungu cha 337 cha sheria hiyo. Pia alishtakiwa chini ya kifungu cha 12 cha Sheria ya Makosa ya Uhujumu Uchumu ( Anti Money laundering Act).

Wakati shauri lake linaendelea aliomba kufanya makubaliano na serikali ( Plea Bargaining) na taratibu zote za kufanya makubaliano zilifuatwa na ndipo aliachiwa huru.

Mara baada ya kuachiwa huru kupitia vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii Wakili Madeleka aliendelea kuchapisha habari kuwa alilazimishwa kukiri kosa na aliekuwa mkurugenzi wa mashtaka.

Baadae alifungua kesi katika mahakama kuu akipinga taratibu hizo lakini maombi hayo madogo yalitupwa nje kwa kuwa mahakama haikuwa na mamlaka ya kusikiliza shauri Hilo.

Ndipo alifungua shauri hilo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kupinga maamuzi hayo lakini mahakama ilitoa maamuzi kuwa taratibu zote za makubaliano ( plea bargaining )zilifanyika sawa.

Baada ya maamuzi hayo alikata rufaa tena na kuja na sababu tofauti ambapo mahakama ilisikiliza Hoja zake na kutoa amri kuwa taratibu za makubaliano hazikuzingatiwa hivyo kuamuru status ya kesi yake kurudi kama ilivyokuwa awali.

Baada ya maamuzi hayo Wakili Madeleka alikamatwa tena ili kuweza kuendelea na kesi yake ya msingi na kwa kuwa makosa anayoshtakiwa nayo hayana dhamana.

UPOTOSHAJI:

Jamii inapotoshwa na kuaminishwa kuwa mshtakiwa ameshikwa kutokana na kutoa maoni yake juu ya Mkataba wa DP world na Serikali ya JMT jambo ambalo si sahihi.

Ikumbukwe watu mbalimbali wametoa mawazo yao na hakuna yoyote alieshikwa.
Hata katika kesi iliyofunguliwa na mawakili yeye si miongoni Mwao.

Hivyo ifahamike na itambulike mshtakiwa ameshikwa kwa makosa yake aliyoyafanya huko nyuma ambapo yeye mwenyewe alikiri na sasa ameomba mahakama ifute maamuzi hayo hivyo kesi yake ya msingi inaendelea.
Upuuzi mtupu. Hizo kesi zote za kubambikia watu walisema wanazifuta. Sahizi kwa sababu mtu amewakosoa, wanazirudisha! Ni uwendawazimu wa madaraka kwa nia ya kukomoa watu.

Kama zingekuwa ni kesi halisia, ilishindikana vipi kwa zaidi ya mwaka mzima, serikali ishindwe kupata ushahidi?

Watu wajinga wanajifanya wana akili kuliko watu wenye akili. Wacha wenye mamlaka wajifariji kwa mbinu zao za kishetani kuwakomoa watu, lakini hawatashinda.

Wala hatutashangaa kuona watu wote walio mstari wa mbele katika kupinga wizi wa rasilimali za nchi unaofanywa na watawala kupitia uwekezaji magumashi, wakiwekwa mahabusu na wakibambikiwa kesi. Wamekwishaanza na Dr. Rugemeleza, Mwambukusi, Madeleka, Lisu, na bila shaka watafuata wengine. Lakini hawatafanikiwa. Shetani humpa mwanadamu ushindi wa muda ili kumpumbaza, lakini hawezi kumpa ushindi wa kudumu.
 
Back
Top Bottom