Dah! Umeongea point... Hii ndiyo inafanya Tanzania tuwe na siasa za ubabaishaji uongo mwingiiiii.... Iwe upinzani iwe ccmMkuu, kwa idadi ya wajinga nchini anaweza kupata. Umewahi kujiuliza kwanini mtu wa ovyo kama lowasa alipata mamilioni ya kura?!
Tunayo mamilioni ya raia wasioweza kufikiri, wanasubiri viongozi wao watoe matamko wao watekeleze.
Acha kufananisha bata na vitu vya kipumbavuYaani wewe ndio Bata kabisa
Kabudi si anacheza na upepo unavyokwenda? Maza kajitanabaisha kama mtu asiyependa kutibua maji yaliyotulia kwenye glass, hataki kuwavuruga "wakubwa" ndiyo maana anacheza appeasement game. Walio chini yake lazima watakuwa bendera fata upepo. I don't like that type of people, by the way, wasio na misingi yao binafsi. So tuichukulie toba ya Kabudi for what it is, appeasement game...hakutumia njia sahihi ndio maana Prof.Kabudi amejitokeza na kukiri kwamba madai dhidi ya acacia yalikuwa sio sahihi/ uongo, na wengine wameita kanyaboya.
..kwa msingi huo huwezi kusema Magufuli alikuwa anatetea maslahi ya nchi. Huwezi kumuita mzalendo kwasababu nchi haitetewi kwa njia za uongo, hila, na ulaghai.
..Lissu ni Mtanzania wa kwanza aliyekuwa na ujasiri wa kusema ukweli kuhusu ripoti na madai ya Magufuli. Prof.Kabudi amepata ujasiri wa kutubu na kusema ukweli 5 yrs later.
..sakata zima la makinikia lilikuwa na lengo la kuwalaghai wananchi na kujiongezea umaarufu wa kisiasa.
..Kama Magufuli alikuwa serious na mwenye uchungu kuhusu rasilimali zetu angechukua hatua kali dhidi ya vigogo waliotumia madaraka yao vibaya kuliingiza taifa ktk mikataba ilitusababishia hasara.
..Vilevile asingemteua Deo Mwanyika, ambaye aliwahi kuwa Mtendaji Mkuu wa Acacia hapa nchini kuwa mgombea ubunge wa Ccm.
Mimi hapo nawaona hovyo wote wawili, mwizi au aliyemficha mwizi, usimuonee Lowassa peke yake.Kwangu mimi lowasa ni miongoni mwa watanzania wa ovyo.
Amewahi kuchunguzwa na serious fraud office ya Uingereza kuhusiana na jumba alilonunua London, akakingiwa kifua na wahujumu wenzake ndani ya CCM.
Wewe unamuona mtu wa maana?!
Hahahaaaa punguza mahaba niue!.Unaonekana una njaa sana, kila issue muhimu inapoongelewa unawaza kula tu.
Tuambieni ninyi chadema mnamuitaje?Kwanini unamuita Lowassa mtu wa hovyo?
Ulaia?Lisu huwenda akawa mhamiaji wa maisha huko Brazos! Na pengine tayari ana ulaia wa huko!
Na ili aje huku, Chadema wananjia moja tu ya kumfanya aje!
Ni kumruhusu agombee nafasi ya Urais, na hili lijulikane pia, akishiriki kugombea nafasi hiyo, ikitokea ameshindwa! Hawezi ishi nchini kamwe!
Na huo ndio uchaguzi wake Kwa sasa!
Tusitaniane bajameni, Ulaya ni Ulaya tuu, Africa itabaki kuwa Africa tu
Ole wa mtu mweusi aonje maisha ya ulaya tena Kwa kibali cha huko, na akapata walau ajira!!! Hawezi kumbuka home!
Waulizeni wazenji, wako tayari familia wauze nyumba na viwanja ili tu mmoja kati yao wa familia hiyo, azamie ulaya, na akizamia, atahakikisha anatuma pesa nyumbani ili kuijenga tena familia hiyo!
Na Zanzibar inajengwa Kwa njia hiyo, na wahamiaji wa ulaya Zanzibar huenda Kwa nia hiyo!
Nani anayebeza maisha ya Ulaya?
Na ndiyo maana hata marais wa nchi za Ki Africa, huwekeza huko ulaya, na wanaishi tu huku Kwa shingo upande ila mioyo yao, iko ulaya
Africa itajengwa na watu wa kawaida saana, wenye kudharauliwa saana na kubezwa na watu weupe na siyo wanaosifiwa na wazungu,
Kwa sababu wote wansosifiwa na wazungu, kuna mawili, either wameuza utu wao, na labda mzungu ana miadi na nchi yake!
Tanzania nakupenda!
Kuna USD 300m+ ambayo kuna pahala umeiita kishika uchumba, nayo tulilaghaiwa? Kwamba hakuna ahadi kama hiyo iliyotolewa na acacia?
Kama ahadi ilitolewa, kwanini kampuni kubwa kama acacia itoe ahadi ya kulipa kiasi hicho kikubwa cha pesa kwenye madai ya kilaghai/kitapeli?!