Pre GE2025 Tundu Lissu, John Heche na viongozi wengine wapokelewa Ofisi za CHADEMA Makao Makuu. Wasisitizia No Reform, No Election

Pre GE2025 Tundu Lissu, John Heche na viongozi wengine wapokelewa Ofisi za CHADEMA Makao Makuu. Wasisitizia No Reform, No Election

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Lissu chadema.jpg
Nipo hapa Mikocheni opposite na CHADEMA HQ na ninashuhudia idadi kubwa ya Watu wakiwemo waandishi wa Habari ninaowafahamu wakiingia ofisi za Chadema

Wote wanasema wamekuja kupata Neno la Kwanza la Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Tundu Lissu na makamu wake Mh John Heche wakiwa rasmi ofisini

Ngoja tumsikie.


TUNDU LISSU
"Kwa sababu ya majukumu makubwa tuliyonayo mbele ya safari naomba mniruhusu nikaribishe wote ambao sio wanachama wetu wajiunge na CHADEMA tunahitaji nguvu kubwa tunahitaji jeshi kubwa zaidi mara dufu ya tulilonalo tunahitaji kila mtu alete karama, talanta zake kwenye hii kazi inayohitajika kufanyika kwa pamoja. Nikaribishe wote ambao kwa sababu mbalimbalo hawajawa bado wanachama wawe wanachama wetu.""Tuna uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba na kuna No reform no election(hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi).

Hayo mambo mawili hayaendi pamoja hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi sio hatutasusia uchaguzi tunaenda kujifungia tuijadili tuna chama haitakuwa uamuzi wa Tundu Lissu, itakuwa ni uamuzi wa chama tutakaa viongozi tutakaa na Sekretarieti tutakaa na Kamati Kuu, tutatoka na msimamo ukitoka msimamo utakuwa ni msimamo wa chama. Ninachoweza kusema tu ni kwamba sasa inabidi tuzungumze lugha pekee anayoweza kuielewa Rais Samia Suluhu Hassan.”


JOHN HECHE
“Nimememuona Mzee Wasira(Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara) amekuwa serikalini tangu akiwa na miaka 20 mimi sijazaliwa. Anataka atengeneze kama mabishano fulani na Mwenyekiti wetu wa taifa kwamba Wasira amshughulikia Lissu. Mzee Wasira Lissu atashughulika na Rais. Lissu anakuja kushughulika na Rais Samia hakuna nafasi ya Lissu kushughulika nawe. Wasira yule hawezi kuja na mawazo mapya kwa watu wamemaliza vyuo vikuu hawana ajira”

"Hakuna mtu atapata upendeleo kwa sababu alimuunga Lissu mkono na Heche tutachagua watu kutokana na uwezo, uwezo wako utakuweka kwenye nafasi tulihubiri mabadiliko na tutasimamia mabadiliko hakuna mtu ataonewa kwa sababu hakutuunga mkono kuweni na amani kabisa. Nataka niwaambieni wanachama wetu wanataka kutumia watu fulani hivi tupoteze muelekeo hiyo nafasi haipo. Tutawashughulikia sana, tutaacha kushughulika na CCM iwe tumekufa au tupo gerezani. Mtatunyamazisha tumekufa au tupo gerezani vinginevyo hakuna msalia mtume kwa hiyo msiwe na mashaka kwamba chama hakitaenda."
 
Nipo hapa Mikocheni opposite na CHADEMA HQ na ninashuhudia idadi kubwa ya Watu wakiwemo waandishi wa Habari ninaowafahamu wakiingia ofisi za Chadema

Wote wanasema wamekuja kupata Neno la Kwanza la Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Tundu Lissu na makamu wake Mh John Heche wakiwa rasmi ofisini

Ngoja tumsikie......
ataropoka tu kama kawaida yake. Mpuuzi mkubwa
sikiliza clip hiyo.....halafu umwamini mtu kama huyo...if you are a sensible man, you can no longer trust that person! kama Idd Amin!
 

Attachments

  • SINA MPANGO WA KUGOMBEA UENYEKITI LISU.mp4
    7.1 MB
Nipo hapa Mikocheni opposite na CHADEMA HQ na ninashuhudia idadi kubwa ya Watu wakiwemo waandishi wa Habari ninaowafahamu wakiingia ofisi za Chadema

Wote wanasema wamekuja kupata Neno la Kwanza la Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Tundu Lissu na makamu wake Mh John Heche wakiwa rasmi ofisini

Ngoja tumsikie......
Please 🙏 picha. Halafu muulize Lissu. Lini watamfukuza Mbowe Chadema? Maana walimtuhumu mlarushwa
 
Nipo hapa Mikocheni opposite na CHADEMA HQ na ninashuhudia idadi kubwa ya Watu wakiwemo waandishi wa Habari ninaowafahamu wakiingia ofisi za Chadema

Wote wanasema wamekuja kupata Neno la Kwanza la Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Tundu Lissu na makamu wake Mh John Heche wakiwa rasmi ofisini

Ngoja tumsikie......
CHADEMA kwa sasa ni habari ya mjini, ni hot news
 
Sema wanakuja kulalamika sio kuongea,maana walichotaka wamepata ila bado watalalamika.Shida ilikuwa Mbowe sasa hivi sijui shida itakuwa ni nani.
 
Back
Top Bottom