Wanabodi
Msingi Mkuu wa kazi ya uandishi wa habari ni ukweli, kuwa mkweli kuusema ukweli na kuandika ukweli!.
Sisi waandishi wa habari wa zamani tulifundishwa na waalimu wazungu, mimi mpaka leo mpaka kesho nakumbuka kauli ya Mwalimu wangu mzungu pale TSJ, a Canadian, Patrick Walsh akitufundisha kuwa kazi uandishi wa habari, "journalism is to tell nothing but the truth"
Hivyo mimi kama mwandishi wa habari, I have been telling the truth, writing the truth, until nilipogundua ukiwa mkweli mno , haswa kwa kuusema ukweli mchungu ambao watu hawapendi kusikia, utachukiwa and sometimes ni hatari hata kwako na kwa maisha yako.
Tumeyashuhudia kwa waandishi wakweli kama kuna Stan Katabalo, Ben Saanane, Azory Gwanda and the like!.
Waandishi wa Habari na Kupotea/Vifo vya Kutatanisha, Toka Katabalo, Saanane, Gwanda, Mwangosi, Isango. Ni Ama Tuombe Mungu Atunusuru ama...
Uandishi wa habari ni sawa na kazi ya siasa, siasa za ukweli wa kuleta maendeleo ya kweli ni siasa za kweli na wanasiasa wanaosema ukweli ndio wanasiasa wa ukweli wa kuleta maendeleo ya kweli. JPM alikuwa ni mmoja wao, Tundu Lissu pia yumo!.
Kuna wengi wanadhani kazi ya siasa na wanasiasa ni kazi ya kupiga bla bla, kuwadanganya wananchi kwa ahadi hewa kam kem zisizotekelezeka!.
Hivyo ndivyo walivyo wengi wa wanasiasa wetu wakiwemo baadhi ya viongozi wetu hadi wakuu, sio wakweli daima, ni watu wa blah blah nyingi!.
Ukimuondoa Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa ni mkweli daima, Rais Mwnyi yeye alikuwa ni mkimya sio mtu wa blah blah. Mkapa pia alikuwa mkweli, JK naomba nisimzungumzie ila JPM alikuwa ni mtu mkweli mwenye ukweli sometimes kupitiliza hivyo kumfanya achukiwe!.
Ni ukweli wa JPM ndio uliomfanya aweze kuyatenda yale aliyoyatenda. Kuna wakweli wa type fulani ambao wao ni "hapa kazi tuu", wakitaka jambo lao liwe na lifanyike kwa haraka, kama katiba, sheria, taratibu na kanuni, ni vikwazo, then wataziweka pembeni na kulifanya jambo lao, na ndio maana JPM alikanyaga katiba ili mambo yaende na kiukweli yalikwenda!. Watu tulinyooka!, nchi ilinyooka, mafisadi, wazembe, walarushwa walinyooka na vyama vilikaza kweli kweli!.
Rais Magufuli ni Mkweli Daima!. Jee Tumuunge Mkono Rais Wetu Katika Kila Ukweli Wake, Hata Kama Uko Kinyume cha Katiba, Sera na Ilani?.
Mimi nimesoma sekondari Ilboru na Tundu Lissu, huyu jamaa Tundu Lissu ni mkweli na yuko bold tangu shuleni!. Kuna vitu vitatu Tundu Lissu anafanana sana na Magufuli, kimoja ni kwenye kuusema ukweli, Tundu Lissu ni mkweli kama JPM!, kwenye kuusema ukweli Lissu atausema no matter what!. Kitu cha pili ambacho Tundu Lissu ni kama Magufuli, naomba nisikitaje hapa kwasababu niliisha kitaja hapa, tena hicho cha pili Tundu Lissu ni zaidi ya Magufuli, hivyo hata ile 2020, mimi ni miongoni mwa tuliomchagiza Tundu Lissu agombee na Magufuli kwasababu Lissu ni zaidi ya Magufuli
Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli! ila kama mgombea wa CCM 2025, ni Mwanamke, simshauri Lissu kugombea!, maana kwa mwanamume jitu la miraba 4 kushindwa vibaya na mwanamke... itakuwa aibu!.
Jana nimetazama mahojiano ya Tundu Lissu kwenye kipindi cha Dakika 45 cha ITV na kumsikiliza kwa makini Tundu Lissu, nikafarijika sana kwa jinsi Tundu Lissu alivyokuwa mkweli.
Mimi kama mwandishi mkweli kazi yangu ni kuuliza, hivyo hili ni bandiko la kuuliza, kumbe Tundu Lissu yuko kama JPM, kwa mambo matatu, JPM ni mtu mkweli. Na Tundu Lissu ni mtu mkweli. Jana meusema ukweli wa jinsi kipengele cha ukomo wa uongozi kilivyoyeyuka toka ndani ya katiba ya Chadema!. Kumbe kipengele hicho haikuyeyuka, kiliyeyushwa kwa kunyofolewa, kimya kimya na ku vanish into thin air!.
Kipengele hicho, nimekuwa nakiulizia sana kwa muda mrefu toka kwa viongozi wa Chadema, kuhusu kipengele hicho cha ukomo wa uongozi ndani ya katiba ya Chadema, kilitowekaje?, kiliondolewa au kiliyeyuka tuu chenyewe?
Hoja ya kunyofolewa kwa kipengele hicho, niliibua hapa
Tuhuma Hii: CHADEMA kendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa
Angalia nilichojibiwa na Dr. Slaa
Jibu la Dr. Slaa linaonyesha, licha ya huyu kuwa ni mtendaji mkuu wa Chadema, alipaswa kuijua katiba ya Chadema kinyume nyume!, lakini Dr. Slaa kumbe haijui katiba ya Chadema wala hajui uwepo wa kipengele hicho hivyo yeye akasema hakijawahi kuwepo!.
Mtu wa pili kulijibia hili ni J.J Mnyika, yeye alijibu
Jibu hili la Mnyika linaonyesha kipengele hicho hakikujadiliwa popote, hivyo kiliachwa kwa kuwa redundant.
Sasa jana ndio Tundu Lissu amefichua ukweli, kumbe kuna watu wakikijadili kipengele hicho bila Dr.Slaa na Mnyika kujua na kuamua kiondolewe kimya kimya bila kuwasilishwa wala kujadiliwa!.
Kwa mujibu wa Tundu Lissu, sababu za kukiondoa ni changamoto ya kupata viongozi bora, kuwa kipindi cha miaka 10, hakitoshi kupika viongozi hivyo inapofika kipindi cha uchaguzi wa ndani, Chadema imekuwa ikipata changamoto ya kupata watu wa kujaza nafasi za viongozi waliotimiza umri wa miaka 10, hivyo wakaamua kukifuta kipengele hicho!.
Kiukweli kabisa kama chama hakina succession plan na hakuna grooming yoyote ya future leaders, na kipindi cha miaka 10 kinaonekana hakitoshi!, hii ni dalili ya incompetence ya aina fulani kwenye succession plan yao, na unaweza kukuta mpaka sasa ndani ya Chadema hakuna maandalizi yoyote ya succession plan ya Mwenyekiti wala hakuna grooming yoyote ya mtu yoyote wa kumpokea Mbowe uenyekiti!.
Lissu alipoulizwa kuhusu yeye kugombea urais 2025 alijibu kwanza katiba, alipobanwa sana akasema ndio atagombea!. That was a mistake!. Kwa vile Chadema bado hawajafanya kikao chochote cha kumteua mgombea wake wa urais wa 2025, hakuna ubaya wowote kwa mwana Chadema yeyote kuwa a wishful thinker kugombea urais 2025 lakini kutamka kwenye TV kuwa yes nitagombea wakati hakuna kikao chochote kilichomteua ni very dangerous!.
He who pays the piper, may call the tune!, whoever is paying the Chadema piper ndio may call the tune, nani agombee Chadema ili usimsumbue yule Malkia wetu, ikitokea sio Lissu, na huku Lissu ameisha tangaza kugombea, huko ndani kutakalika?.
Viongozi wasema ukweli wa type ya Lissu, ndio wanaolifaa taifa letu, na kwavile nilisema Lissu anafanana na Magufuli kwa mambo matatu, moja ni hili la ukweli, na hayo mawili yaliyobakia Lissu ni zaidi ya Magufuli, kama ikitokea Tundu Lissu akagombea tena urais na akachaguliwa kuwa rais wa JMT, then maendeleo ya Tanzania yatapaa maana Lissu ni zaidi ya Magufuli kwa hayo mengine mawili.
Hongera sana Tundu Lissu, jana umeongea vizuri kwenye ITV, hukutaja taja tena majina ya waliokushambulia.
Pia umesema dereva wao yuko Ubelgiji akihitajika kuhojiwa serikali inawaandikia serikali ya Belgium anarudishwa nchini kuhojiwa, kumbe Lissu hajui kuwa Tanzania hatuna mkataba wa extradition act na Belgium!.
Nimefurahi Lissu ameongea huku ametulia bila Jazba bila kutukana na au lugha ya maudhi.
Kilicho nifurahisha zaidi ni Tundu Lissu kuwa mkweli daima, keep on telling the truth and the truth will set you free!. Lissu akiendelea hivi, soon atakuwa like a real politician tena presidential material na sio mwanaharakati kama alivyo sasa!. Big up sana Bwana mdogo wangu wa Ilboru.
Paskali