Tundu Lissu kama JPM, ni mtu mkweli. Asema ukweli jinsi ukomo wa uongozi ulivyoyeyuka CHADEMA

Tundu Lissu kama JPM, ni mtu mkweli. Asema ukweli jinsi ukomo wa uongozi ulivyoyeyuka CHADEMA

Huwa najiuliza kwanini watu huwa wanamsema Pasco kuwa anatafuta teuzi? Lakini pia najiuliza hivi huwa anaandika akijua ni yeye tu anayejua? Hivi kila akionacho yeye kuwa ni 'kweli' kinakuwa kweli kwa wote? Huwa sipati majibu ila naigundua tofauti kati ya P huyu na P yule wa zamani
kwenye Tv
 
Acha kuchanganya mambo, Zito alitaka kugombea urais akiwa CDM? Lisu yuko sahihi kusema atagombea, suala la kupitishwa na chama chake yeye sio muamuzi. Hivi karibuni kwenye mikutano ya hadhara, Mnyika amesema mwanachama yoyote anayetaka kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CDM aanze kuonyesha nia. Je Lisu amefanya kosa gani kuonyesha nia?
Kilichomkuta Zito ni nia yake ya kugombea uenyekiti na sio urais..na huyu lissu ndo alishiriki kikamirifu kumuondoa Zito pale CDM
 
Kiukweli leo ndo najua chadema Wana viongozi Wa Maisha haijawahi kutajwa hii kwamba waliondoa kipengele cha ukomo Wa viongozi wao nadhani hapa mlengwa alikua ni mweneyekiti mbowe aendelee kusalia kwenye kiti kwa kisingizio hawana mtu wa kushika wadhfa huo inasikitisha na kufikirisha sana nadhani hao viongozi wengine wamewekwa kama geresha flani hivi lengo ni mwenyekiti adumu milele..
 
NotaBene

1.Pasco alistaafu ya uandishi wa Habari.

2.Pasco ni kada wa chama Cha mapinduzi aka mambuzi.

Kwa namba yeyote Ile andiko la Pasco Kaa Sasa litakuwa na chembechembe za propaganda sababu ule uandishi habari halisi alisema kastaafu.

Kuwa makini sana na soma between lines utagundua kapenyeza propaganda.

Andika hili sidhani kama Lina lengo kusifia ukweli wa TAL ila nahisi Lina lengo la kumfarakanisha Lissu na wanachama wenzake.

Kuweni makini n

NotaBene

1.Pasco alistaafu ya uandishi wa Habari.

2.Pasco ni kada wa chama Cha mapinduzi aka mambuzi.

Kwa namba yeyote Ile andiko la Pasco Kaa Sasa litakuwa na chembechembe za propaganda sababu ule uandishi habari halisi alisema kastaafu.

Kuwa makini sana na soma between lines utagundua kapenyeza propaganda.

Andika hili sidhani kama Lina lengo kusifia ukweli wa TAL ila nahisi Lina lengo la kumfarakanisha Lissu na wanachama wenzake.

Kuweni makini nae.
Pasko kakosea nn sasa hapo yeye kamsifia lissu kua mkweli kuhusu mwwnyekiti Wa maisha mwamba ni kweli kipengele kiliondolewa ili tu mbowe aendelee na walifanya hivo ili kuua Fikra kama za kina Zitto kabwe za kuutamani uenyekiti
 
Zito alikuwa haaminiki.
Zito alikua haaminiki !? Kutokuaminika kwa Zitto kuna uhusiano gani na kunyofoa kioengele cha ukomo wa mwenyekiti....na hayo Ndo maneno waliolishwa wanaCDM Kipindi kile ili tu kumuondoa zito na mwenyekiti aendelee milele..na wakafika mbali wakanyofoa kipengele cha ukomo Wa mwenyekiti..
 
Zito alikua haaminiki !? Kutokuaminika kwa Zitto kuna uhusiano gani na kunyofoa kioengele cha ukomo wa mwenyekiti....na hayo Ndo maneno waliolishwa wanaCDM Kipindi kile ili tu kumuondoa zito na mwenyekiti aendelee milele..na wakafika mbali wakanyofoa kipengele cha ukomo Wa mwenyekiti..

Hoja yako ni ipi hapa? Mbona ni kama umepanick?!
 
Wanabodi

Jana nimetazama mahojiano ya Tundu Lissu kwenye kipindi cha Dakika 45 cha ITV na kumsikiliza kwa makini Tundu Lissu, nikafarijika sana kwa jinsi Tundu Lissu alivyokuwa mkweli.

Paskali

Nimeona hii habari huko Twitter. Inasema kuwa Mbowe alikuwa mwenyekiti wa CDM mwaka 2004. Wakati huo katiba ya chama ilikuwa imezungumza kuwa kutakuwa na ukomo wa miaka kumi kwa mwenyekiti.
Mkuu Wakili wa shetani, hapo juu Lissu amekujibu ila ni kweli Mbowe alipoingia kuwa Mwenyekiti wa Chadema, katiba ya Chadema ilikuwa na ukomo wa uongozi mwisho ni vipindi 2 vya miaka 5 jumla ni miaka 10.
Mwaka 2006 yalifanyika mabadiliko ya katiba. Lakini suala la ukomo wa uongozi halikuzungumzwa kwenye mkutano.
Ni kweli 2006 Chadema walifanya mabadiliko ya katiba na ni kweli kipengele hicho hakikujadiliwa.
Inasema kuwa katiba ilipoendwa kuchapwa, Mbowe akaondoa kipengele cha ukomo wa uongozi kinyemela. Hii ndiyo hadi leo mwaka wa 20 bado ni mwenyekiti.

Madai haya yanaukweli wowote?
Ni kweli katiba ilipoenda kuchapwa, hicho kipengele hakikuwepo, kiliyeyuka ila aliyekiyeyusha sio lazima awe ni Mbowe.

Hili jambo tuliisha lijadili humu kwa kirefu, Tuhuma Hii: CHADEMA kendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa
Dr. Slaa alikuwa KM na alichangia Tuhuma Hii: CHADEMA kendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa

na JJ Mnyika akiwa Mkurugenzi wa Habari wa Chadema pia alichangia Tuhuma Hii: CHADEMA kendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa
Nyuzi nyingine zinazohisiana na hili ni hizi Hatma ya Freeman Mbowe CHADEMA Elections 2015 - CHADEMA ikipewa Nchi, Oktoba 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu! ila juzi kati hapa hili jambo Lissu kalifafanua vizuri kabisa Tundu Lissu kama JPM, ni mtu mkweli. Asema ukweli jinsi ukomo wa uongozi ulivyoyeyuka CHADEMA

P
 
Wanabodi
Msingi Mkuu wa kazi ya uandishi wa habari ni ukweli, kuwa mkweli kuusema ukweli na kuandika ukweli!.

Sisi waandishi wa habari wa zamani tulifundishwa na waalimu wazungu, mimi mpaka leo mpaka kesho nakumbuka kauli ya Mwalimu wangu mzungu pale TSJ, a Canadian, Patrick Walsh akitufundisha kuwa kazi uandishi wa habari, "journalism is to tell nothing but the truth"

Hivyo mimi kama mwandishi wa habari, I have been telling the truth, writing the truth, until nilipogundua ukiwa mkweli mno , haswa kwa kuusema ukweli mchungu ambao watu hawapendi kusikia, utachukiwa and sometimes ni hatari hata kwako na kwa maisha yako.
Tumeyashuhudia kwa waandishi wakweli kama kuna Stan Katabalo, Ben Saanane, Azory Gwanda and the like!. Waandishi wa Habari na Kupotea/Vifo vya Kutatanisha, Toka Katabalo, Saanane, Gwanda, Mwangosi, Isango. Ni Ama Tuombe Mungu Atunusuru ama...

Uandishi wa habari ni sawa na kazi ya siasa, siasa za ukweli wa kuleta maendeleo ya kweli ni siasa za kweli na wanasiasa wanaosema ukweli ndio wanasiasa wa ukweli wa kuleta maendeleo ya kweli. JPM alikuwa ni mmoja wao, Tundu Lissu pia yumo!.

Kuna wengi wanadhani kazi ya siasa na wanasiasa ni kazi ya kupiga bla bla, kuwadanganya wananchi kwa ahadi hewa kam kem zisizotekelezeka!.

Hivyo ndivyo walivyo wengi wa wanasiasa wetu wakiwemo baadhi ya viongozi wetu hadi wakuu, sio wakweli daima, ni watu wa blah blah nyingi!.

Ukimuondoa Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa ni mkweli daima, Rais Mwnyi yeye alikuwa ni mkimya sio mtu wa blah blah. Mkapa pia alikuwa mkweli, JK naomba nisimzungumzie ila JPM alikuwa ni mtu mkweli mwenye ukweli sometimes kupitiliza hivyo kumfanya achukiwe!.

Ni ukweli wa JPM ndio uliomfanya aweze kuyatenda yale aliyoyatenda. Kuna wakweli wa type fulani ambao wao ni "hapa kazi tuu", wakitaka jambo lao liwe na lifanyike kwa haraka, kama katiba, sheria, taratibu na kanuni, ni vikwazo, then wataziweka pembeni na kulifanya jambo lao, na ndio maana JPM alikanyaga katiba ili mambo yaende na kiukweli yalikwenda!. Watu tulinyooka!, nchi ilinyooka, mafisadi, wazembe, walarushwa walinyooka na vyama vilikaza kweli kweli!. Rais Magufuli ni Mkweli Daima!. Jee Tumuunge Mkono Rais Wetu Katika Kila Ukweli Wake, Hata Kama Uko Kinyume cha Katiba, Sera na Ilani?.

Mimi nimesoma sekondari Ilboru na Tundu Lissu, huyu jamaa Tundu Lissu ni mkweli na yuko bold tangu shuleni!. Kuna vitu vitatu Tundu Lissu anafanana sana na Magufuli, kimoja ni kwenye kuusema ukweli, Tundu Lissu ni mkweli kama JPM!, kwenye kuusema ukweli Lissu atausema no matter what!. Kitu cha pili ambacho Tundu Lissu ni kama Magufuli, naomba nisikitaje hapa kwasababu niliisha kitaja hapa, tena hicho cha pili Tundu Lissu ni zaidi ya Magufuli, hivyo hata ile 2020, mimi ni miongoni mwa tuliomchagiza Tundu Lissu agombee na Magufuli kwasababu Lissu ni zaidi ya Magufuli Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli! ila kama mgombea wa CCM 2025, ni Mwanamke, simshauri Lissu kugombea!, maana kwa mwanamume jitu la miraba 4 kushindwa vibaya na mwanamke... itakuwa aibu!.

Jana nimetazama mahojiano ya Tundu Lissu kwenye kipindi cha Dakika 45 cha ITV na kumsikiliza kwa makini Tundu Lissu, nikafarijika sana kwa jinsi Tundu Lissu alivyokuwa mkweli.

Mimi kama mwandishi mkweli kazi yangu ni kuuliza, hivyo hili ni bandiko la kuuliza, kumbe Tundu Lissu yuko kama JPM, kwa mambo matatu, JPM ni mtu mkweli. Na Tundu Lissu ni mtu mkweli. Jana meusema ukweli wa jinsi kipengele cha ukomo wa uongozi kilivyoyeyuka toka ndani ya katiba ya Chadema!. Kumbe kipengele hicho haikuyeyuka, kiliyeyushwa kwa kunyofolewa, kimya kimya na ku vanish into thin air!.

Kipengele hicho, nimekuwa nakiulizia sana kwa muda mrefu toka kwa viongozi wa Chadema, kuhusu kipengele hicho cha ukomo wa uongozi ndani ya katiba ya Chadema, kilitowekaje?, kiliondolewa au kiliyeyuka tuu chenyewe?

Hoja ya kunyofolewa kwa kipengele hicho, niliibua hapa Tuhuma Hii: CHADEMA kendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa

Angalia nilichojibiwa na Dr. Slaa


Jibu la Dr. Slaa linaonyesha, licha ya huyu kuwa ni mtendaji mkuu wa Chadema, alipaswa kuijua katiba ya Chadema kinyume nyume!, lakini Dr. Slaa kumbe haijui katiba ya Chadema wala hajui uwepo wa kipengele hicho hivyo yeye akasema hakijawahi kuwepo!.

Mtu wa pili kulijibia hili ni J.J Mnyika, yeye alijibu

Jibu hili la Mnyika linaonyesha kipengele hicho hakikujadiliwa popote, hivyo kiliachwa kwa kuwa redundant.

Sasa jana ndio Tundu Lissu amefichua ukweli, kumbe kuna watu wakikijadili kipengele hicho bila Dr.Slaa na Mnyika kujua na kuamua kiondolewe kimya kimya bila kuwasilishwa wala kujadiliwa!.

Kwa mujibu wa Tundu Lissu, sababu za kukiondoa ni changamoto ya kupata viongozi bora, kuwa kipindi cha miaka 10, hakitoshi kupika viongozi hivyo inapofika kipindi cha uchaguzi wa ndani, Chadema imekuwa ikipata changamoto ya kupata watu wa kujaza nafasi za viongozi waliotimiza umri wa miaka 10, hivyo wakaamua kukifuta kipengele hicho!.

Kiukweli kabisa kama chama hakina succession plan na hakuna grooming yoyote ya future leaders, na kipindi cha miaka 10 kinaonekana hakitoshi!, hii ni dalili ya incompetence ya aina fulani kwenye succession plan yao, na unaweza kukuta mpaka sasa ndani ya Chadema hakuna maandalizi yoyote ya succession plan ya Mwenyekiti wala hakuna grooming yoyote ya mtu yoyote wa kumpokea Mbowe uenyekiti!.

Lissu alipoulizwa kuhusu yeye kugombea urais 2025 alijibu kwanza katiba, alipobanwa sana akasema ndio atagombea!. That was a mistake!. Kwa vile Chadema bado hawajafanya kikao chochote cha kumteua mgombea wake wa urais wa 2025, hakuna ubaya wowote kwa mwana Chadema yeyote kuwa a wishful thinker kugombea urais 2025 lakini kutamka kwenye TV kuwa yes nitagombea wakati hakuna kikao chochote kilichomteua ni very dangerous!.

He who pays the piper, may call the tune!, whoever is paying the Chadema piper ndio may call the tune, nani agombee Chadema ili usimsumbue yule Malkia wetu, ikitokea sio Lissu, na huku Lissu ameisha tangaza kugombea, huko ndani kutakalika?.

Viongozi wasema ukweli wa type ya Lissu, ndio wanaolifaa taifa letu, na kwavile nilisema Lissu anafanana na Magufuli kwa mambo matatu, moja ni hili la ukweli, na hayo mawili yaliyobakia Lissu ni zaidi ya Magufuli, kama ikitokea Tundu Lissu akagombea tena urais na akachaguliwa kuwa rais wa JMT, then maendeleo ya Tanzania yatapaa maana Lissu ni zaidi ya Magufuli kwa hayo mengine mawili.

Hongera sana Tundu Lissu, jana umeongea vizuri kwenye ITV, hukutaja taja tena majina ya waliokushambulia.

Pia umesema dereva wao yuko Ubelgiji akihitajika kuhojiwa serikali inawaandikia serikali ya Belgium anarudishwa nchini kuhojiwa, kumbe Lissu hajui kuwa Tanzania hatuna mkataba wa extradition act na Belgium!.

Nimefurahi Lissu ameongea huku ametulia bila Jazba bila kutukana na au lugha ya maudhi.

Kilicho nifurahisha zaidi ni Tundu Lissu kuwa mkweli daima, keep on telling the truth and the truth will set you free!. Lissu akiendelea hivi, soon atakuwa like a real politician tena presidential material na sio mwanaharakati kama alivyo sasa!. Big up sana Bwana mdogo wangu wa Ilboru.

Paskali
Stan Katabalo, Azory Gwanda, Mwangosi, Steven Ulimboka (si mwandishi lkn ni binadamu nae) Saed Kubenea, Jamal Kashogi, Julian Asange na list inaendelea.
Msioneshe tu watu waliopata madhara kipindi cha JPM ili kumchafua! Hata USA yanatokea. Tutoe mifano kimataifa pia. Juzi kuna mtangazaji UK anaitwa Gary Lineker amefukuzwa kazi kwa kutoa maoni kuhusu sera mbaya ya uhamiaji!
 
Stan Katabalo, Azory Gwanda, Mwangosi, Steven Ulimboka (si mwandishi lkn ni binadamu nae) Saed Kubenea, Jamal Kashogi, Julian Asange na list inaendelea.
Msioneshe tu watu waliopata madhara kipindi cha JPM ili kumchafua! Hata USA yanatokea. Tutoe mifano kimataifa pia. Juzi kuna mtangazaji UK anaitwa Gary Lineker amefukuzwa kazi kwa kutoa maoni kuhusu sera mbaya ya uhamiaji!
Acha ushabiki mandazi!
 
Hata ndani ya vyama wanagombea

Cc johnthebaptist
Ndani ya vyama ni kugombea kuteuliwa, ukiisha shinda uteuzi wa ndani ya chama ndipo sasa unagombea uongozi.

Hata CCM, japo ina utaratibu wa rais aliyemadarakani hapingwi mid term hivyo mgombea wa urais wa CCM kwa uchaguzi wa 2025 ni mmoja tuu, Samia Suluhu Hassan, lakini kamwe huwezi kumsikia Samia akisema ni yeye atagombea urais 2025, bali wakati utakapofika, Samia ataomba kuteuliwa na CCM, akiishateuliwa sasa ndio anakuwa mgombea.

Wanachadema kubalini kataeni kitendo cha Tundu Lissu kusema ni yeye atagombea urais 2025 kwa tiketi ya Chadema, it's a mistake!. Unaweza kutangaza nia ya kugombea lakini sio kusema atagombea!.

Kosa kama hili la Lissu, Zitto alilifanya na alishughulikiwa ipasavyo nikiwemo mimi Urais wa ZZK 2015: Ngoma Ikivuma Sana...!.

Kitendo cha Tundu Lissu kutangaza expressly kuwa atagombea urais wa 2025 kupitia Chadema, tangazo hilo litawafanya presidential hopefuls wengine wote wa Chadema wasithubutu kumpinga Lissu.

Hii tabia ya viongozi wa Chadema waliogombea nafasi fulani kujimilikisha kugombea tena ndicho kilichomtoa Dr. Slaa Chadema baada ya kumpokea Edward Lowassa na kumfanya ni mgombea wake Ujio wa Lowassa CHADEMA: Kuna kundi wamesusa, wanapanga kurejea CCM!

Hivyo ikitokea Chadema ikapata mgombea bora zaidi wa urais 2025 kuliko Lissu, Jee Lissu atakubali?.
P
 
Wanabodi
Msingi Mkuu wa kazi ya uandishi wa habari ni ukweli, kuwa mkweli kuusema ukweli na kuandika ukweli!.

Sisi waandishi wa habari wa zamani tulifundishwa na waalimu wazungu, mimi mpaka leo mpaka kesho nakumbuka kauli ya Mwalimu wangu mzungu pale TSJ, a Canadian, Patrick Walsh akitufundisha kuwa kazi uandishi wa habari, "journalism is to tell nothing but the truth"

Hivyo mimi kama mwandishi wa habari, I have been telling the truth, writing the truth, until nilipogundua ukiwa mkweli mno , haswa kwa kuusema ukweli mchungu ambao watu hawapendi kusikia, utachukiwa and sometimes ni hatari hata kwako na kwa maisha yako.
Tumeyashuhudia kwa waandishi wakweli kama kuna Stan Katabalo, Ben Saanane, Azory Gwanda and the like!. Waandishi wa Habari na Kupotea/Vifo vya Kutatanisha, Toka Katabalo, Saanane, Gwanda, Mwangosi, Isango. Ni Ama Tuombe Mungu Atunusuru ama...

Uandishi wa habari ni sawa na kazi ya siasa, siasa za ukweli wa kuleta maendeleo ya kweli ni siasa za kweli na wanasiasa wanaosema ukweli ndio wanasiasa wa ukweli wa kuleta maendeleo ya kweli. JPM alikuwa ni mmoja wao, Tundu Lissu pia yumo!.

Kuna wengi wanadhani kazi ya siasa na wanasiasa ni kazi ya kupiga bla bla, kuwadanganya wananchi kwa ahadi hewa kam kem zisizotekelezeka!.

Hivyo ndivyo walivyo wengi wa wanasiasa wetu wakiwemo baadhi ya viongozi wetu hadi wakuu, sio wakweli daima, ni watu wa blah blah nyingi!.

Ukimuondoa Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa ni mkweli daima, Rais Mwnyi yeye alikuwa ni mkimya sio mtu wa blah blah. Mkapa pia alikuwa mkweli, JK naomba nisimzungumzie ila JPM alikuwa ni mtu mkweli mwenye ukweli sometimes kupitiliza hivyo kumfanya achukiwe!.

Ni ukweli wa JPM ndio uliomfanya aweze kuyatenda yale aliyoyatenda. Kuna wakweli wa type fulani ambao wao ni "hapa kazi tuu", wakitaka jambo lao liwe na lifanyike kwa haraka, kama katiba, sheria, taratibu na kanuni, ni vikwazo, then wataziweka pembeni na kulifanya jambo lao, na ndio maana JPM alikanyaga katiba ili mambo yaende na kiukweli yalikwenda!. Watu tulinyooka!, nchi ilinyooka, mafisadi, wazembe, walarushwa walinyooka na vyama vilikaza kweli kweli!. Rais Magufuli ni Mkweli Daima!. Jee Tumuunge Mkono Rais Wetu Katika Kila Ukweli Wake, Hata Kama Uko Kinyume cha Katiba, Sera na Ilani?.

Mimi nimesoma sekondari Ilboru na Tundu Lissu, huyu jamaa Tundu Lissu ni mkweli na yuko bold tangu shuleni!. Kuna vitu vitatu Tundu Lissu anafanana sana na Magufuli, kimoja ni kwenye kuusema ukweli, Tundu Lissu ni mkweli kama JPM!, kwenye kuusema ukweli Lissu atausema no matter what!. Kitu cha pili ambacho Tundu Lissu ni kama Magufuli, naomba nisikitaje hapa kwasababu niliisha kitaja hapa, tena hicho cha pili Tundu Lissu ni zaidi ya Magufuli, hivyo hata ile 2020, mimi ni miongoni mwa tuliomchagiza Tundu Lissu agombee na Magufuli kwasababu Lissu ni zaidi ya Magufuli Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli! ila kama mgombea wa CCM 2025, ni Mwanamke, simshauri Lissu kugombea!, maana kwa mwanamume jitu la miraba 4 kushindwa vibaya na mwanamke... itakuwa aibu!.

Jana nimetazama mahojiano ya Tundu Lissu kwenye kipindi cha Dakika 45 cha ITV na kumsikiliza kwa makini Tundu Lissu, nikafarijika sana kwa jinsi Tundu Lissu alivyokuwa mkweli.

Mimi kama mwandishi mkweli kazi yangu ni kuuliza, hivyo hili ni bandiko la kuuliza, kumbe Tundu Lissu yuko kama JPM, kwa mambo matatu, JPM ni mtu mkweli. Na Tundu Lissu ni mtu mkweli. Jana meusema ukweli wa jinsi kipengele cha ukomo wa uongozi kilivyoyeyuka toka ndani ya katiba ya Chadema!. Kumbe kipengele hicho haikuyeyuka, kiliyeyushwa kwa kunyofolewa, kimya kimya na ku vanish into thin air!.

Kipengele hicho, nimekuwa nakiulizia sana kwa muda mrefu toka kwa viongozi wa Chadema, kuhusu kipengele hicho cha ukomo wa uongozi ndani ya katiba ya Chadema, kilitowekaje?, kiliondolewa au kiliyeyuka tuu chenyewe?

Hoja ya kunyofolewa kwa kipengele hicho, niliibua hapa Tuhuma Hii: CHADEMA kendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa

Angalia nilichojibiwa na Dr. Slaa


Jibu la Dr. Slaa linaonyesha, licha ya huyu kuwa ni mtendaji mkuu wa Chadema, alipaswa kuijua katiba ya Chadema kinyume nyume!, lakini Dr. Slaa kumbe haijui katiba ya Chadema wala hajui uwepo wa kipengele hicho hivyo yeye akasema hakijawahi kuwepo!.

Mtu wa pili kulijibia hili ni J.J Mnyika, yeye alijibu

Jibu hili la Mnyika linaonyesha kipengele hicho hakikujadiliwa popote, hivyo kiliachwa kwa kuwa redundant.

Sasa jana ndio Tundu Lissu amefichua ukweli, kumbe kuna watu wakikijadili kipengele hicho bila Dr.Slaa na Mnyika kujua na kuamua kiondolewe kimya kimya bila kuwasilishwa wala kujadiliwa!.

Kwa mujibu wa Tundu Lissu, sababu za kukiondoa ni changamoto ya kupata viongozi bora, kuwa kipindi cha miaka 10, hakitoshi kupika viongozi hivyo inapofika kipindi cha uchaguzi wa ndani, Chadema imekuwa ikipata changamoto ya kupata watu wa kujaza nafasi za viongozi waliotimiza umri wa miaka 10, hivyo wakaamua kukifuta kipengele hicho!.

Kiukweli kabisa kama chama hakina succession plan na hakuna grooming yoyote ya future leaders, na kipindi cha miaka 10 kinaonekana hakitoshi!, hii ni dalili ya incompetence ya aina fulani kwenye succession plan yao, na unaweza kukuta mpaka sasa ndani ya Chadema hakuna maandalizi yoyote ya succession plan ya Mwenyekiti wala hakuna grooming yoyote ya mtu yoyote wa kumpokea Mbowe uenyekiti!.

Lissu alipoulizwa kuhusu yeye kugombea urais 2025 alijibu kwanza katiba, alipobanwa sana akasema ndio atagombea!. That was a mistake!. Kwa vile Chadema bado hawajafanya kikao chochote cha kumteua mgombea wake wa urais wa 2025, hakuna ubaya wowote kwa mwana Chadema yeyote kuwa a wishful thinker kugombea urais 2025 lakini kutamka kwenye TV kuwa yes nitagombea wakati hakuna kikao chochote kilichomteua ni very dangerous!.

He who pays the piper, may call the tune!, whoever is paying the Chadema piper ndio may call the tune, nani agombee Chadema ili usimsumbue yule Malkia wetu, ikitokea sio Lissu, na huku Lissu ameisha tangaza kugombea, huko ndani kutakalika?.

Viongozi wasema ukweli wa type ya Lissu, ndio wanaolifaa taifa letu, na kwavile nilisema Lissu anafanana na Magufuli kwa mambo matatu, moja ni hili la ukweli, na hayo mawili yaliyobakia Lissu ni zaidi ya Magufuli, kama ikitokea Tundu Lissu akagombea tena urais na akachaguliwa kuwa rais wa JMT, then maendeleo ya Tanzania yatapaa maana Lissu ni zaidi ya Magufuli kwa hayo mengine mawili.

Hongera sana Tundu Lissu, jana umeongea vizuri kwenye ITV, hukutaja taja tena majina ya waliokushambulia.

Pia umesema dereva wao yuko Ubelgiji akihitajika kuhojiwa serikali inawaandikia serikali ya Belgium anarudishwa nchini kuhojiwa, kumbe Lissu hajui kuwa Tanzania hatuna mkataba wa extradition act na Belgium!.

Nimefurahi Lissu ameongea huku ametulia bila Jazba bila kutukana na au lugha ya maudhi.

Kilicho nifurahisha zaidi ni Tundu Lissu kuwa mkweli daima, keep on telling the truth and the truth will set you free!. Lissu akiendelea hivi, soon atakuwa like a real politician tena presidential material na sio mwanaharakati kama alivyo sasa!. Big up sana Bwana mdogo wangu wa Ilboru.

Paskali

facts, CHADEMA ni wanadamu tu kama walivyo TLP, CUF na chama cha waasi wa CCM yani CCK.
 
Wanabodi
Jana nimetazama mahojiano ya Tundu Lissu kwenye kipindi cha Dakika 45 cha ITV na kumsikiliza kwa makini Tundu Lissu, nikafarijika sana kwa jinsi Tundu Lissu alivyokuwa mkweli.

Mimi kama mwandishi mkweli kazi yangu ni kuuliza, hivyo hili ni bandiko la kuuliza, kumbe Tundu Lissu yuko kama JPM, kwa mambo matatu, JPM ni mtu mkweli. Na Tundu Lissu ni mtu mkweli. Jana meusema ukweli wa jinsi kipengele cha ukomo wa uongozi kilivyoyeyuka toka ndani ya katiba ya Chadema!. Kumbe kipengele hicho haikuyeyuka, kiliyeyushwa kwa kunyofolewa, kimya kimya na ku vanish into thin air!.

Kipengele hicho, nimekuwa nakiulizia sana kwa muda mrefu toka kwa viongozi wa Chadema, kuhusu kipengele hicho cha ukomo wa uongozi ndani ya katiba ya Chadema, kilitowekaje?, kiliondolewa au kiliyeyuka tuu chenyewe?

Hoja ya kunyofolewa kwa kipengele hicho, niliibua hapa Tuhuma Hii: CHADEMA kendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa

Angalia nilichojibiwa na Dr. Slaa


Jibu la Dr. Slaa linaonyesha, licha ya huyu kuwa ni mtendaji mkuu wa Chadema, alipaswa kuijua katiba ya Chadema kinyume nyume!, lakini Dr. Slaa kumbe haijui katiba ya Chadema wala hajui uwepo wa kipengele hicho hivyo yeye akasema hakijawahi kuwepo!.

Mtu wa pili kulijibia hili ni J.J Mnyika, yeye alijibu

Jibu hili la Mnyika linaonyesha kipengele hicho hakikujadiliwa popote, hivyo kiliachwa kwa kuwa redundant.

Sasa jana ndio Tundu Lissu amefichua ukweli, kumbe kuna watu wakikijadili kipengele hicho kimya kimya bila Dr.Slaa na Mnyika kujua na kuamua kukinyofoa kimya kimya bila kuwasilishwa wala kujadiliwa!.
Kipengele chenyewe ni hiki View attachment 2845558

Kwa mujibu wa Tundu Lissu, sababu za kukiondoa ni changamoto ya kupata viongozi bora, kuwa kipindi cha miaka 10, hakitoshi kupika viongozi hivyo inapofika kipindi cha uchaguzi wa ndani, Chadema imekuwa ikipata changamoto ya kupata watu wa kujaza nafasi za viongozi waliotimiza umri wa miaka 10, hivyo wakaamua kukifuta kipengele hicho!.

Kiukweli kabisa kama chama hakina succession plan na hakuna grooming yoyote ya future leaders, na kipindi cha miaka 10 kinaonekana hakitoshi!, hii ni dalili ya incompetence ya aina fulani kwenye succession plan yao, na unaweza kukuta mpaka sasa ndani ya Chadema hakuna maandalizi yoyote ya succession plan ya Mwenyekiti wala hakuna grooming yoyote ya mtu yoyote wa kumpokea Mbowe uenyekiti!.

Lissu alipoulizwa kuhusu yeye kugombea urais 2025 alijibu kwanza katiba, alipobanwa sana akasema ndio atagombea!. That was a mistake!. Kwa vile Chadema bado hawajafanya kikao chochote cha kumteua mgombea wake wa urais wa 2025, hakuna ubaya wowote kwa mwana Chadema yeyote kuwa a wishful thinker kugombea urais 2025 lakini kutamka kwenye TV kuwa yes nitagombea wakati hakuna kikao chochote kilichomteua ni very dangerous!.

He who pays the piper, may call the tune!, whoever is paying the Chadema piper ndio may call the tune, nani agombee Chadema ili usimsumbue yule Malkia wetu, ikitokea sio Lissu, na huku Lissu ameisha tangaza kugombea, huko ndani kutakalika?.

Viongozi wasema ukweli wa type ya Lissu, ndio wanaolifaa taifa letu, na kwavile nilisema Lissu anafanana na Magufuli kwa mambo matatu, moja ni hili la ukweli, na hayo mawili yaliyobakia Lissu ni zaidi ya Magufuli, kama ikitokea Tundu Lissu akagombea tena urais na akachaguliwa kuwa rais wa JMT, then maendeleo ya Tanzania yatapaa maana Lissu ni zaidi ya Magufuli kwa hayo mengine mawili.

Hongera sana Tundu Lissu, jana umeongea vizuri kwenye ITV, hukutaja taja tena majina ya waliokushambulia.

Pia umesema dereva wao yuko Ubelgiji akihitajika kuhojiwa serikali inawaandikia serikali ya Belgium anarudishwa nchini kuhojiwa, kumbe Lissu hajui kuwa Tanzania hatuna mkataba wa extradition act na Belgium!.

Nimefurahi Lissu ameongea huku ametulia bila Jazba bila kutukana na au lugha ya maudhi.

Kilicho nifurahisha zaidi ni Tundu Lissu kuwa mkweli daima, keep on telling the truth and the truth will set you free!. Lissu akiendelea hivi, soon atakuwa like a real politician tena presidential material na sio mwanaharakati kama alivyo sasa!. Big up sana Bwana mdogo wangu wa Ilboru.

Paskali


Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Tundu Lissu wakati akitangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa CHADEMA Taifa amesema CHADEMA haina budi kurudisha utaratibu wa ukomo wa Madaraka kwani utaondoa uwezekano wa Viongozi kung'angania madaraka na kuandaa Viongozi wapya, kupatikana kwa mawazo mapya na itapunguza upambe na uchawa ulioshamiri pale kiongozi anang'ang'ania madaraka pale ambapo hakuna ukomo wa madaraka
Afadhali leo ndio TL amelizungumzia hili, anashangiliwa, kama hakuna ukomo, then hakuna kung'ang'ania madaraka,hili neno kung'ang'ania madaraka ni kumsema mtu kwa mlango wa nyuma!。

Msikilize TL hapa Tundu Lissu kama JPM, ni mtu mkweli. Asema ukweli jinsi ukomo wa uongozi ulivyoyeyuka CHADEMA

Siku nilipoibua hii issue ya ukomo wa madaraka, KM wa wakati huo, Dr Slaa, aliruka kimanga na kuniparua Tuhuma Hii: CHADEMA kuendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa

Nilipolisema hili, niliparuliwa, sasa leo TL kayasema, nasubiria kuona kama je na yeye ataparuliwa?。
P
 
Afadhali leo ndio TL amelizungumzia hili, anashangiliwa, kama hakuna ukomo, then hakuna kung'ang'ania madaraka,hili neno kung'ang'ania madaraka ni kumsema mtu kwa mlango wa nyuma!。

Msikilize TL hapa Tundu Lissu kama JPM, ni mtu mkweli. Asema ukweli jinsi ukomo wa uongozi ulivyoyeyuka CHADEMA

Siku nilipoibua hii issue ya ukomo wa madaraka, KM wa wakati huo, Dr Slaa, aliruka kimanga na kuniparua Tuhuma Hii: CHADEMA kuendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa

Haya sasa leo TL kayasema, nasubiria kama ataparuliwa!。
P
Pasco, natumai utahusika sana kwenye siasa za 2025 kama katiba mpya na tume zitapatikana.
 
Afadhali leo ndio TL amelizungumzia hili, anashangiliwa, kama hakuna ukomo, then hakuna kung'ang'ania madaraka,hili neno kung'ang'ania madaraka ni kumsema mtu kwa mlango wa nyuma!。

Msikilize TL hapa Tundu Lissu kama JPM, ni mtu mkweli. Asema ukweli jinsi ukomo wa uongozi ulivyoyeyuka CHADEMA

Siku nilipoibua hii issue ya ukomo wa madaraka, KM wa wakati huo, Dr Slaa, aliruka kimanga na kuniparua Tuhuma Hii: CHADEMA kuendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa

Haya sasa leo TL kayasema, nasubiria kama ataparuliwa!。
P
P huwa adui anaombewa njaa kwani TL adui yako?Inakuwaje umwoombee kuparuliwa.
 
Anafuata falsafa za Cromwell kwamba watu waachiane madaraka na si kuganda tu.Ametoa mfano wa wenyeviti wa kwanza wa Chadema Mzee Mtei na W Amani walitumikia kipindi kimoja kimoja.
Hivyo Mbowe nae aachie kijiti kwa wengine.
It is not over until it is over.
 
Back
Top Bottom