Tundu Lissu kuhitaji gari lake aliloshambuliwa nalo hapa kuna mtego mkubwa na hesabu kali inachezwa

Tundu Lissu kuhitaji gari lake aliloshambuliwa nalo hapa kuna mtego mkubwa na hesabu kali inachezwa

Dereva kabaki na mke wake kule Brussels ,Basi kama gari ni muhimu kurudishwa basi na dereva nae muhimu sana apatikane atoe his side of the story. Haiwezekani story ya Lissu ya upande mmoja ikajumuisha tukio lote na huyo dereva nae ni muhimu, na pia inatakiwa kuwapata wale wanaokuwaga walinzi pale waseme ni nani aliwaondoa siku ya tukio. eneo kama lile lina rota ya walinzi wa siku hio, waulizwe walinzi wa siku ile kwanini hawakua kazini na kwa amri ya nani?? Kitu kibaya zaidi Lissu anamsema Magufuli- rip kama yeye ndio aliefanya tukio , aseme ni serikali ya Tanzania ili iwe wazi na kuipeleka kortini kama serikali sio mtu binafsi. ni nini anaogopa kufanya hivyo???Maana kesi ikifanyika basi picha loote litajulikana. Kuna mengi kwenye hii issues sio hayo Tundu aliosema tu tena kwa upande wake.
 
Msimfanye Lissu ndo wa kwanza kusoma sheria hapa nchi. Sheria zipo wazi na taratibu za kufuata katika mazingira kama hayo zinajulikana.
Hivi unadhani tukio kama hilo lingetokea ndani ya nyumba polisi wangezuia hiyo nyumba isitumike tena kusubiri mwenendo wa uchunguzi?
Kuna issue hapo, kwanza hiyo gari ni kaa la moto!
 
Tukumbuke kuwa katika uchaguzi wa 2020, Lissu alikwenda pia polisi kudai gari lake ingawa sikumbuki kama alifanikiwa hata kuliona. Pia juzijuzi tu amesema Serikali haijamlipa madai yake ya pesa za matibabu na kiiuna mgongo na badala yake serikali imemlipia deni lake la gari kutoka katika pesa alizokuwa anawadai, yaani wameipiga juu kwa juu na balance bado wanapata kigugumizi kumpa. Kwa hiyo kama serikali imeona ni kipaumbele kulipa deni la gari ana haki ya kurudishiwa gari waliyokaa nalo kwa miaka yote hii. Wakidai wanalishikilia kwa ajili ya uchunguzi itabidi waseme uchunguzi umefikia wapi wakati yeye muathirika mkuu hajahojiwa mpaka sasa.
 
Halafu huwa najiuliza tu, siku ile dereva wa lissu angeweza kuchukua hata ushahidi wa risasi make naimani nyingi zilimkosa mlengwa make wale wajinga walikuwa wanazimimina kiboya sana kama kojo la mlevi.
Zile risasi zingesaidia kutambua kampuni zilikotengenezwa na ziliingizwa nchini na nani na kabla ya kutumiwa zilihifadhiwa wapi?
Mkuu, ile haikuwa movie, lilikuwa tukio halisi.
 
Gari lilichomwa moto ili kuficha ushahidi...na kwakuwa lissu ashapewa movie nzima ndio maana anakomaa ili awaumbue sukuma gang
Kama hivyo bado itabidi wajiibu lilitolewa polisi kwa utaratibu gani? Halikuondoka lenyewe!
 
Inawezekana anataarifa ya kwamba gari limekongoloka ndio mana cha kwanza anasema anataka kuliona then atafata taratibu ili aweze kukabidhiwa.
Kuwa judgemental kwa kilamjambo kunatufanya tuishi kwenye past na Future wakati maisha is prese t ou Nownow
 
atachukuaje gari hajatoa ushahidi polisi dereva hajatoa ushahidi kesi bado haijakamilika unataka gari vipi file lako bado halijafungwa
 
Haya Majiniasi ( Akili Kubwa ) wa JamiiForums hebu njooni mtupe Ujiniasi wenu katika hili Sisi Mangumbaru ( Akili Ndogo ) kwani wenye Akili Kubwa wanadai katika hili kuna mahala Tundu Lissu Kawatega lakini pia kuna Hesabu Kali mno inachezwa hapa ambayo ikikosewa tu Mzanzibari atadharaulika na hatoamini.
Si walisema wanamtaka aje ili ahojiwe? Sasa kaenda mwenyewe lakini hawakumhoji!
Lakini tusubiri labda anahojiwa.
 
Back
Top Bottom