Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Nikiibiwa kura nitawaingiza Wananchi barabarani

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Nikiibiwa kura nitawaingiza Wananchi barabarani

Hiyo ndio Kauli ya Mh Tundu Lissu iwapo ikitokea ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu mwezi October 2020. Ataingiza watanzania barabarani ikiwa ataibiwa kura zake.

View attachment 1526711

My take: Ni mapema Sana kwa mgombea urais kutoa kauli Kama hii si kiashiria kizuri. Anataka kutuaminisha kuwa hata ikitokea ameshindwa kihalali tuamini kuwa kaibiwa kura ili atimize azima yake.

Uongozi wa CHADEMA umshauri huyu mgombea kauli hizi hazifai kwa usalama wa nchi yetu.
Hao watu wa kuingia barabarani, Ni barabara hizi za kwetu hapa Tanzania, au Ubelgiji?

Na atakayeongoza hao watu ni yeye na wale watoto wake na familia yake, au Wabelgiji na Wajerumani?

Huyu alikwisha fahamika kuwa Ni mtu asiye na vision yoyote wala hana agenda ya maendeleo katika Nchi hii.

Huyu anachohitaji ni jukwaa la kueneza uchochezi , chuki, fitina ili Nchi hii iingie kwenye machafuko na kila kitu kizuri kilichoanzishwa kiharibike tukose wote, kwa sababu yeye na hao waliomtuma wanafahamu fika kwamba anatumika tu, hawezi kuchaguliwa kuwa Rais kwa sababu hana chochote cha ku_deliver.

Kwa hiyo, hili halitowezekana kwa sababu tunataka kuendelea kuona watoto wetu wakiwa wanaongozana kila siku asubuhi wakielekea shule huku wakiwa katika hali ya utulivu Kama ilivyo sasa, tunataka kuendelea kuona watoto wetu wakisubiri mabasi ya shule vituoni na kwenye "junctions" wakiwa wanacheka kwa furaha kama ilivyo hivi sasa bila kuhofu milipuko.

Tunataka kuona rasilimali za Nchi hii zikiendelea kulindwa na kuinufaisha Nchi hii na Wananchi wake.

Haya yote, pamoja na masuala mengine muhimu kwa Nchi hii na raia wake, tayari yameshawekewa misingi thabiti, na misingi hii lazima ilindwe kwa gharama yoyote dhidi ya mtu/ kikundi chochote wenye lengo ovu la kuivunja na kuisababishia Nchi kuingia kwenye vurugu kwa sababu za kutumika tu.
 
Dawa ya kumzuia Lisu asiingize watu barabarani ni rahisi sana, UCHAGUZI HURU NA HAKI! Watu waachwe wafanye maamuzi ndani ya box la kura, basi!
 
Sisi ambao tumefuatilia siasa za Tanzania tokea awamu ya kwanza tumewahi shuhudia watanzania wakiasi nchi na kutaka hadi kumuua Baba wa Taifa zaidi ya mara moja. Kaa ukikumbuka kwamba huyu Baba wa Taifa ndiye Raisi ambaye aliwahi kupendwa kuliko maraisi wote Tanzania na alilindwa sana na vyombo vya usalama. Lakini miaka yake ya mwisho ilikuwa imejaa vimbwanga vingi kutoka kwa watanzania hadi ikampelekea ang'atuke kwa amani.

Sasa sembuse utawala wa awamu ya tano kweli ??? Hivi nyie wandungu mmepeleka akili zenu likizo hadi kuzisahau siasa za Tanzania kipindi cha funga mkanda. Nadhani wewe ni shabiki na una utoto mwingi sana, lakini kama ungekuwa ni mtu mzima nadhani ungefahamu kwamba Tanzania inapita katika kipindi kigumu kuliko wakati wowote ule. Kama hatutakuwa makini basi tutakuja kuikumbuka hii miaka kwa masikitiko sana huko mbeleni.
Achana na Lumumba hawa. Hawajui hata historia ya hii nchi kazi kukaririshwa tu eti Nyerere alikuwa hivi alikuwa vile. Hawajui kuwa Nyerere alipona mapinduzi mengi kuliko raisi yeyote yule Tanzania. Awashukuru vijana wa enzi hizo kina Mahiga na col Apson Mwang’onda.

Magu hawezi shinda bila kuiba kura na mwaka huu ndo mwisho wake kufanya udhalimu kwa watanzania.

Namuunga Mkono Lissu haiwezekani maamuzi ya wananchi yakachezewa. Tutaingia tu barabarani wakiiba kura
 
Kwa ninavyomjua Magufuli... Dunia itamlaumu tu! Atawabutua wote.. barabara zitajaa mavi yalimwagika.
Natamani nishuhudie hii mbinde.
Haiwezi kutokea kitu Kama hicho mkuu watanzania sio wajinga kiasi hicho, huyu Lissu anataka tu kutengeneza attention ili apate huruma kwa wanachi atakaposhindwa uchaguzi apate Cha kusema kuwa kaibiwa kura.

Hapa anaanza kuandaa mazingira mapema ili apate kisingizio lakini uzuri watanzania wanaona kwa macho yao hakuna mtu atakae muunga mkono kwenye huo ujinga.

Ninachosema mimi hizi kauli anazozitoa kila siku si ishara nzuri inaonyesha ana nia ovu huyu ama labda tegemeo lake la kukamatwa pindi aliporudi mchini lilipofel anaona awe anatoa kauli Kama hizi ili kuvuta jicho la Wana usalama wamkamate kumhoji ili apate kiki ya kisiasa wakati huu ambao jato la uchaguzi limekuwa kubwa sana.

Kwa maana hii bado tutegemee kauli nyingi za ovyo kutoka kwake ili atimize azma yake. CHADEMA wana wajibu wa kumshauri huyu mgombea aachane na huu mwenendo wake wa kisiasa. Pia vyombo vya usalama viwe makini visikubali kuingia kwenye mtego wake.
 
..wewe umechukizwa na alichokisema TL?
Bila shaka, sababu anatumia dhana na si hakika.
..amesema akiibiwa kura ata...
Sasa anatakiwa asubiri mpaka atakapo ibiwa hizo kura.
..sasa hebu tueleze mgombea Uraisi wa Tz aliyeibiwa kura anapaswa kuchukua hatua gani?
Anatakiwa afanye kama sheria zinavyo elekeza mgombea akiibiwa kura anatakiwa afanye nini, au mambo yenu huwa hamyaendeshi kisheria ?
..at least kwenye ubunge tunajua anaweza kwenda mahakamani, kwenye Uraisi mgombea aliyeibiwa kura tunamtetea na kumsaidia vipi?
Hili sina elimu nalo, waulize wajuzi wa hili, kwamba ikitokea mtu anaibiwa kura anatakiwa achukue hatua, je kuhamasisha vurugu au kufata sheria ?

Hivi kuwatoa watu kuwapeleka barabarani, ni jambo la kisheria au mihemko na ujinga ?
..siyo kweli kwamba watu wanajenga dhana tu.
Kama siyo dhana mbona ushahidi hutuwekei ? Usahihi wa mambo siyo kila unalo sikia uliseme au kila unalo wazia uliseme.

Unatakiwa ufanye uchunguzi na uwe na ithibati, kwanini tunashindwa kutumia akili zetu vizuri ?
..Tanzania kuna wizi wa kura, na dhuluma nyingi ktk uchaguzi, na ushahidi ni kesi mbalimbali zilizoamuliwa na mahakama zetu.
Hili hata mimi huwa nalisia ila sina ushahidi kwahiyo siwezi kuliongelea.
 
Haiwezi kutokea kitu Kama hicho mkuu watanzania sio wajinga kiasi hicho, huyu Lissu anataka tu kutengeneza attention ili apate huruma kwa wanachi atakaposhindwa uchaguzi apate Cha kusema kuwa kaibiwa kura.

Hapa anaanza kuandaa mazingira mapema ili apate kisingizio lakini uzuri watanzania wanaona kwa macho yao hakuna mtu atakae muunga mkono kwenye huo ujinga.

Ninachosema mimi hizi kauli anazozitoa kila siku si ishara nzuri inaonyesha ana nia ovu huyu ama labda tegemeo lake la kukamatwa pindi aliporudi mchini lilipofel anaona awe anatoa kauli Kama hizi ili kuvuta jicho la Wana usalama wamkamate kumhoji ili apate kiki ya kisiasa wakati huu ambao jato la uchaguzi limekuwa kubwa sana.

Kwa maana hii bado tutegemee kauli nyingi za ovyo kutoka kwake ili atimize azma yake. CHADEMA wana wajibu wa kumshauri huyu mgombea aachane na huu mwenendo wake wa kisiasa. Pia vyombo vya usalama viwe makini visikubali kuingia kwenye mtego wake.
Suala hapa ni hakuna kuiba kura. Hata anayeiba kura au mwenye mipango hiyo, vyombo vya usalama ndo vinapaswa kuanza nae
 
Hao watu wa kuingia barabarani, Ni barabara hizi za kwetu hapa Tanzania, au Ubelgiji?

Na atakayeongoza hao watu ni yeye na wale watoto wake na familia yake, au Wabelgiji na Wajerumani?

Huyu alikwisha fahamika kuwa Ni mtu asiye na vision yoyote wala hana agenda ya maendeleo katika Nchi hii.

Huyu anachohitaji ni jukwaa la kueneza uchochezi , chuki, fitina ili Nchi hii iingie kwenye machafuko na kila kitu kizuri kilichoanzishwa kiharibike tukose wote, kwa sababu yeye na hao waliomtuma wanafahamu fika kwamba anatumika tu, hawezi kuchaguliwa kuwa Rais kwa sababu hana chochote cha ku_deliver.

Kwa hiyo, hili halitowezekana kwa sababu tunataka kuendelea kuona watoto wetu wakiwa wanaongozana kila siku asubuhi wakielekea shule huku wakiwa katika hali ya utulivu Kama ilivyo sasa, tunataka kuendelea kuona watoto wetu wakisubiri mabasi ya shule vituoni na kwenye "junctions" wakiwa wanacheka kwa furaha kama ilivyo hivi sasa bila kuhofu milipuko.

Tunataka kuona rasilimali za Nchi hii zikiendelea kulindwa na kuinufaisha Nchi hii na Wananchi wake.

Haya yote, pamoja na masuala mengine muhimu kwa Nchi hii na raia wake, tayari yameshawekewa misingi thabiti, na misingi hii lazima ilindwe kwa gharama yoyote dhidi ya mtu/ kikundi chochote wenye lengo ovu la kuivunja na kuisababishia Nchi kuingia kwenye vurugu kwa sababu za kutumika tu.
Yes, upo vizuri, Lisu azingatie hilo, naomba upande wa pili wadumishe amani kwa kutuachia wananchi tuchague tumtakaye! Kama kuna ushindi utoke kwenye box tu, siyo polisi au tume, ama wizi. Tuanze na fair play, kabla vitusho kamaya kama njia ya kuzuia machafuko! #SASABASI!
 
Hiyo ndio Kauli ya Mh Tundu Lissu iwapo ikitokea ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu mwezi October 2020. Ataingiza watanzania barabarani ikiwa ataibiwa kura zake.

View attachment 1526711

My take: Ni mapema Sana kwa mgombea urais kutoa kauli Kama hii si kiashiria kizuri. Anataka kutuaminisha kuwa hata ikitokea ameshindwa kihalali tuamini kuwa kaibiwa kura ili atimize azima yake.

Uongozi wa CHADEMA umshauri huyu mgombea kauli hizi hazifai kwa usalama wa nchi yetu.
Ajaribu kuwaingiza wakione cha mtema kuni. Huyu anatapatapa kama mfa maji. Asituletee balaa nchini kwetu.
 
Twitter siyo ya Lissu na haiko accurate alichokisema Lissu na hiyo Twitter tofauti ni kama usiku na mchana.,
Sasa lete alicho kisema yeye tuone Kama havina mahusiano na hiyo Twitter hapo, mbona simple tu mkuu.
 
Thubutu yenu. Ya Malawi lazima yatokee Tanzania mwaka huu
We jamaa tangu Jana unatokwa na povu, huyo jamaa yako hapati hata thelusi ya kura za JPM.

Kama unabisha subiri tarehe 28/10/2020 uone jinsi mtakavyotembezewa kipigo cha Mbwa mwizi.
 
Nilipoona jana wanabadili Tunu yetu ya taifa, utambulisho wetu wa Taifa yaani wanageuza maneno ya Wimbo wa Taifa kwa kuweka maneno ya chama chao, nikajua hapa hawa hawana nia njema na watanzania. Wana ushari. Na wanachokitafuta watakipata.

Hakuna mtanzania anaweza kukubali chama kumpitisha mgombea ambaye aliitakia mabaya Tanzania awe huyo huyo kuwaongoza kelekea barabarani. Lissu ni mwanaharakati si mtu wa kusimamia mfumo wa uongozi wa nchi. Hili nililisema muda mrefu sana. Hapa watu wataanza kunielewa.

Na kwa kosa la jana nadhani wanatafuta sababu ya kujitoa uchaguzi kukwepa aibu kushindwa vibaya sana hapo October, 2020.
Chadema haishindwi uchaguzi wa mwaka huu ndugu. Amini maneno yangu. CCM imechokwa, inatosha kwa jinsi walivyowafanya watanzania mafukara. Inatosha kwa walivyoiharibu Tanzania
 
We jamaa tangu Jana unatokwa na povu, huyo jamaa yako hapati hata thelusi ya kura za JPM.

Kama unabisha subiri tarehe 28/10/2020 uone jinsi mtakavyotembezewa kipigo cha Mbwa mwizi.
Tukutane October 2020
 
Sasa anatakiwa asubiri mpaka atakapo ibiwa hizo kura.

Anatakiwa afanye kama sheria zinavyo elekeza mgombea akiibiwa kura anatakiwa afanye nini, au mambo yenu huwa hamyaendeshi kisheria ?

..wewe una CHUKI binafsi.

..TL amesema ikiwa ataibiwa kura ata...

..maana yake ni kwamba atasubiri mpaka atakapoibiwa kura kama ambavyo unapendekeza.

..sheria zetu zinaruhusu mgombea ubunge aliyeibiwa kura apeleke shauri mahakamani.

..lakini sheria zetu hazitoi mwanya huo kwa mgombea Uraisi, lakini sheria zetu zimetoa mwanya wa kufanya maandamano ilimradi yawe ya amani. hivyo utaona basi mgombea Uraisi aliyeibiwa kura anaweza kutumia option ya maandamano kuelezea hisia zake kuhusu uchaguzi.
 
Back
Top Bottom