Tuongee Kifamilia leo, kama unataka kuoa au kuolewa na mna imani za dini tofauti jitafakari upya

Tuongee Kifamilia leo, kama unataka kuoa au kuolewa na mna imani za dini tofauti jitafakari upya

Nitaandika kwa kifupi tu, kuna case nimeshindwa kuipa suluhu nimeitwa kuleta amani kwenye nyumba ya hao wana ndoa.

Wewe ni mwanamke muislamu olewa na mwislamu mwenzako, na kama wewe mwanaume ni Mkristo owa Mkristo mwenzako.

Issue ni ngumu, Mkristo kaka mwanamke muislamu kipindi mahaba ndindindi, Sasa ndoa imejibu Watoto Wawili, mwanamke wote anadai ni Watoto wake na wote wanapenda madrasa za kiislamu.

Sasa sitaki mada hii iwe ni mihadhara au jukwaa la kukashifu dini nyingine, nimeweka hii mada ili kuitwa ushauri wa bure.

Ikiwa mwanamke na mwanaume mmekubaliana kuweka dini zenu pembeni na mfunge ndoa bomani basi jitahidini na swala Watoto mkubaliane wakizaliwa wafuate imani gani au mgawane vipi urithi wa imani kwa Watoto na kwa hali ya Sasa muandikishiane kisheria ili lisilete tabu baadaye.

Nawapenda sana Mama zangu na Dada zangu lakini ukweli uko wazi wao ndio tatizo, wanaume huwa hawana ligi za kijinga.

Nimewashauri acheni Watoto wakiwa adult wachaguwe imani wanayotaka ila mke wa ndoa anasema Watoto ni wake, ila kimoja kipengele cha school fees mke ndio anatambuwa kama Watoto wana baba.

Nimehairisha hii case namuomba Mungu anipe busara sijui muhafaka utapatikana vipi? Inasikitisha sana Watoto wadogo kuwaharibu kisaikolojia kurithi dini za wakoloni.

Kwakweli mnaotegemea kuowa au kuolewa na watu wa dini tofauti msilipuuze hili muandikishiane kwa Wakili kama mlivyofunga mkataba wa ndoa serikalini.

Wacha nipate kwanza lager zinipe hekima kulimaliza.
Kamuulize mwanamke na hawa watoto ni kabila gani? Akikujibu kamuulize mwanamke hawa watoto ni kabila gani? Na kwa nini? Akikujibu maliza kesi.
Nitaandika kwa kifupi tu, kuna case nimeshindwa kuipa suluhu nimeitwa kuleta amani kwenye nyumba ya hao wana ndoa.

Wewe ni mwanamke muislamu olewa na mwislamu mwenzako, na kama wewe mwanaume ni Mkristo owa Mkristo mwenzako.

Issue ni ngumu, Mkristo kaka mwanamke muislamu kipindi mahaba ndindindi, Sasa ndoa imejibu Watoto Wawili, mwanamke wote anadai ni Watoto wake na wote wanapenda madrasa za kiislamu.

Sasa sitaki mada hii iwe ni mihadhara au jukwaa la kukashifu dini nyingine, nimeweka hii mada ili kuitwa ushauri wa bure.

Ikiwa mwanamke na mwanaume mmekubaliana kuweka dini zenu pembeni na mfunge ndoa bomani basi jitahidini na swala Watoto mkubaliane wakizaliwa wafuate imani gani au mgawane vipi urithi wa imani kwa Watoto na kwa hali ya Sasa muandikishiane kisheria ili lisilete tabu baadaye.

Nawapenda sana Mama zangu na Dada zangu lakini ukweli uko wazi wao ndio tatizo, wanaume huwa hawana ligi za kijinga.

Nimewashauri acheni Watoto wakiwa adult wachaguwe imani wanayotaka ila mke wa ndoa anasema Watoto ni wake, ila kimoja kipengele cha school fees mke ndio anatambuwa kama Watoto wana baba.

Nimehairisha hii case namuomba Mungu anipe busara sijui muhafaka utapatikana vipi? Inasikitisha sana Watoto wadogo kuwaharibu kisaikolojia kurithi dini za wakoloni.

Kwakweli mnaotegemea kuowa au kuolewa na watu wa dini tofauti msilipuuze hili muandikishiane kwa Wakili kama mlivyofunga mkataba wa ndoa serikalini.

Wacha nipate kwanza lager zinipe hekima kulimaliza.
 
Katika dini mwanamke hufuata upande wa mwanaume akikaidi ni uzembe wa mwanaume husika,
Hakuna hiyo kitu, kwa waislamu kwanza hapo hakuna ndoa haitambuliki kidini na watoto wanakuwa wa mwanamke.

Pili mwanamke ndiyo anakaa na watoto kipindi kirefu kwa hivyo by default watoto watakuwa wanafuata dini ya mwanamke (awe muislamu au mkristo).
 
sio hivyo,kwa jamii zetu za ki tz ni ngumu kukwepa kwa jinsi tulivyojichanganya,mapenzi ni upofu,hayaoni kesho...
Nilipo-bold

Hapo ndiyo penye tatizo,mkuu mimi naishi mji wenye imani tofauti tofauti kabla sijaowa nilikuwa na mahusiano na wanawake wa imani tofauti na walinifurahisha ila lilipokuja suala la kuanzisha familia kwanza niliizingatia sana imani yangu hata mke nilitafuta wa Imani yangu kwa sababu najua na naamini ndiyo ipo sahihi kutuongoza ktk maisha.

Haya mambo ya kusema mapenzi upofu yanaumiza na yanayumbisha sana familia iwe ni kwenye imani au kwenye mambo ya kawaida ya kimaisha hii kauli ni ya kuikemea siyo ya kuiendekeza.
 
Mheshimiwa ,
Hapo kunaonekana Kuna udhaifu upande wa mume kwa sababu ubini mzima (kabila & dini ) lazima zitokea kwa baba ....Kuna sababu kadhaa zinaweza kuchangia akachua kwa mama mfano mtoto alitelekezwa au hawakufunga ndoa (mwanamke hajaolewa alizalishwa tu)

Kwa hapo mwanaume ana madhaifu kwa vile alitamkiwa kumconfess huyo mke afuate kila kitu na imani yake tangu mwanzo .Hiyo ndo maana halisi ya kichwa cha familia
 
Asante mnoo kwa mleta mada.
Bahati mbaya sana kuna wachangiaji wengi hapa wa hii mada wameshindwa kumuelewa mleta mada. Hoja kuu hapo ya mleta ni namna gani ilipaswa huo mkwamo utatuliwe kwa kuepukwa kabla ya ndoa kufungwa. Nami nitachambua hapa.

1. Hata kama hao wanandoa wangeweka mambo yao kisheria wakati wa kuoana (kusema watoto wafuate dini fulani) bado huenda isingekuwa suluhisho kamili kwa kuwa, dini ni suala la moyoni unaotokana na utashi, na kwa mtoto hujifunza imani kama tabia za kuiga kutoka kwa mzazi/wazazi. Kama wazazi ni wafuasi wa dini tofauti, kwa mtoto kinakuwa kitendawili kigumu. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.

2. Ni hatari kuwaza kuwa, watoto walelewe kibagani (bila kufuata dini yoyote) ili wakiwa wakubwa wachague dini watakayoitaka! Samaki mkunje angali mbichi.

Suluhisho la hayo matatizo ni nini? Ndoa za dini tofauti hazifai kwa malezi ya mtoto kiimani, ziepukwe.
 
Kama ulifata dini ya mama yako ni uzembe wa baba yako,

Fatilia wanaume waliobadili dini kufata wanawake wanavyoonekana katika jamii
Anaeingia kwenye familia ya mwenzie ni ke, zamani hata ubini wa majina ya wanawake yalibadilika na kuwa ya waume zao,
Mfano mwingine

Me;Samweli
Ke;Grace

Ke ataitwa Mrs samweli kwanini isiwe Mrs Grace?
Mkuu, naomba nikuongeze uwe jiko dogo maana sio kwa nondo hizo...😂
 
Nitaandika kwa kifupi tu, kuna case nimeshindwa kuipa suluhu nimeitwa kuleta amani kwenye nyumba ya hao wana ndoa.

Wewe ni mwanamke muislamu olewa na mwislamu mwenzako, na kama wewe mwanaume ni Mkristo owa Mkristo mwenzako.

Issue ni ngumu, Mkristo kaka mwanamke muislamu kipindi mahaba ndindindi, Sasa ndoa imejibu Watoto Wawili, mwanamke wote anadai ni Watoto wake na wote wanapenda madrasa za kiislamu.

Sasa sitaki mada hii iwe ni mihadhara au jukwaa la kukashifu dini nyingine, nimeweka hii mada ili kuitwa ushauri wa bure.

Ikiwa mwanamke na mwanaume mmekubaliana kuweka dini zenu pembeni na mfunge ndoa bomani basi jitahidini na swala Watoto mkubaliane wakizaliwa wafuate imani gani au mgawane vipi urithi wa imani kwa Watoto na kwa hali ya Sasa muandikishiane kisheria ili lisilete tabu baadaye.

Nawapenda sana Mama zangu na Dada zangu lakini ukweli uko wazi wao ndio tatizo, wanaume huwa hawana ligi za kijinga.

Nimewashauri acheni Watoto wakiwa adult wachaguwe imani wanayotaka ila mke wa ndoa anasema Watoto ni wake, ila kimoja kipengele cha school fees mke ndio anatambuwa kama Watoto wana baba.

Nimehairisha hii case namuomba Mungu anipe busara sijui muhafaka utapatikana vipi? Inasikitisha sana Watoto wadogo kuwaharibu kisaikolojia kurithi dini za wakoloni.

Kwakweli mnaotegemea kuowa au kuolewa na watu wa dini tofauti msilipuuze hili muandikishiane kwa Wakili kama mlivyofunga mkataba wa ndoa serikalini.

Wacha nipate kwanza lager zinipe hekima kulimaliza.
Kwa watu wasio wasomi, wenye Elimu ya chini, wasio na exposure, au upeo mkubwa wa uelewa, mambo ya ndoa na tofauti za dini, huwapa shida sana.

Mke wa Khasim Majaliwa, PM wa sasa ni mkristo na hakuna shida, mkuu wa mkoa wa zamani wa Kagera, Abdulaman Babu, alikuwa Mkristo, jamaa alikua anamleta kanisani kila Jumapili, wewe unaoa mtu sio dini, kwanza Kuna unafki mwingi sana, unakuta wote ni dini moja, lakini mnamaliza hata mwaka bila kwenda kanisani au masjid, sasa dini ya nini.

Kila mtu aabudu kivyake, ubovu wa Waafrika, dini inapewa nafasi kubwa kwenye mausiano na familia!!
Uchumi ndio iwe kiapumbele, katika kutafuta pesa, hakuna dini, tafuta pesa saidia wasiojiweza huo ndio Uislam, Ukristo mzuri!! Sio unaaacha msichana mzuri kisa dini yake??!!!!
 
Huo mtihani unawakuta familia nyingi sana tangu enzi na enzi ila hawajifunzi sababu ya mapenzi pale mwanzoni yakinoga,

Suluhu yake, Watoto wasomeshwe dini zote mbili, madrasa waende na sunday school waende, wakikua watachagua upande wenyewe hakuna haja ya kugombana wazazi.
Maji ya chumvi na baridi huwa hayachanganyiki kwenye mkondo bahari mmoja..
 
hakuna hiyo kitu, kwa waislamu kwanza hapo hakuna ndoa haitambuliki kidini na watoto wanakuwa wa mwanamke.

Pili mwanamke ndiyo anakaa na watoto kipindi kirefu kwa hivyo by default watoto watakuwa wanafuata dini ya mwanamke (awe muislamu au mkristo).
Narudia tena mwanamke(wa dini yoyote) kukaidi kufata dini ya mwanaume ni uzembe wa mwanaume, short loud and clear,

Kwa huo mfano wako watoto wanatumia ubini upi?
 
Narudia tena mwanamke(wa dini yoyote) kukaidi kufata dini ya mwanaume ni uzembe wa mwanaume, short loud and clear,

kwahuo mfano wako watoto wanatumia ubini upi?
Hata wakitumia ubini so what? Imani ni kitu tafauti kabisa
 
Hiyo ligi kuisha mpka mmoja afe
Hata wafe wote bado haitasaidia.

Kumbuka kuna mmoja ambaye ndiye kwa asili tunaamini alipaswa awarithishe kile aliamini ni sahihi kwao (baba) na sasa ameshindwa wahusika wameshaenda anakoamini hakuwafai that's why tupo hapa tunajadili.
 
Back
Top Bottom