Maeneo muhimu ya kuzingatia ni pamoja na:
1. Usawa wa kijinsia na kuimarisha uwakilishi wa kijinsia:
- Kuanzisha mipango maalum ya kuongeza ushiriki wa wanawake katika maamuzi ya kisiasa na kiuchumi.
- Kuboresha sera na sheria zinazolinda haki za wanawake na kuhakikisha utekelezaji wake.
- Kuhamasisha ajira na fursa sawa za kimaendeleo kwa wanawake.
2. Kukabiliana na ubaguzi na dhuluma dhidi ya makundi maalum:
- Kujenga ufahamu wa jamii kuhusu haki za binadamu na kupambana na mitazamo duni.
- Kuimarisha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa makundi yenye mahitaji maalum.
- Kuongeza ushiriki na uwakilisho wa makundi haya katika ngazi zote za uongozi.
3. Kuimarisha elimu na ujuzi:
- Kuhakikisha upatikanaji wa elimu bure na ya ubora kwa wote bila ubaguzi.
- Kuhamasisha ushiriki wa wanawake na makundi maalum katika fani za sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati.
- Kuongeza uwezo wa walimu na wataalamu katika kushughulikia masuala ya usawa na ukweli.
4. Kukuza utamaduni wa haki na usawa:
- Kuendeleza kampeni za mawasiliano ya jamii kuhusu usawa na haki za binadamu.
- Kuhamasisha ushiriki wa jamii katika kuleta mabadiliko ya kimtazamo na desturi.
- Kujenga uwezo wa taasisi za kiraia katika kulinda na kutetea haki.
Ushirikiano baina ya serikali, sekta binafsi, asasi za kiraia na jamii kwa ujumla ni muhimu sana katika kutekeleza mikakati hii.
Heri ya Pasaka wana JamiiForums,
Mimi ni Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Wenye Makundi Maalum.
Ninayo furaha kujiunga nanyi katika mtandao huu. Nimekuwepo hapa tangu 2015 kama msomaji zaidi lakini sasa rasmi nitakuwa active member.
Naamini JF itakuwa sehemu nzuri ya kupokea maswali, maoni na mawazo yenu kuhusu namna tunavyoweza kuboresha maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake, na watu wenye makundi maalum nchini Tanzania.
Hivyo, ninawakaribisha nyote kushiriki kwenye majadiliano haya na mimi niko tayari kujibu maswali yenu na kusikiliza maoni yenu na hata kuyafanyia kazi haraka pale inapobidi.
Unaweza kutoa maoni yako kwenye mjadala huu au kupitia ujumbe wa faragha (PM).
Karib