Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

Namkumbuka mkuu wa shule Kaishozi wa DODOMA SECONDARY miaka ya 92-96 sita msahau kwa wale waliosoma DOM SEC natumaini watamkumbuka alikuwa kama anapasha kwanza weed then ndiyo anaingia kazini.

Mwaka jana nienda Dodoma kuna rafiki yangu alikuwa anaenda kutoa mahari wakati tunahangaika kupata mshenga ghafla aliingia kwenye kikao na akapendekezwa kuwa mshenga ambapo alikubali alichokifanya alipiga konyagi ndogo 2 na akaenda kuchukuwa kanzu yake tayari kwa kazi ya kuwa mshenga ajabu tukiwa ukweni wakati wsjumbe wengine wanaongea yeye alikuwa anauchapa usingizi haha haaaa nilicheka sana ilipofika wakati wake akakurupuka na kuanza kuongea watu si vicheko kwani inaonekana hakujua yanayoendelea hata huvyo baadaye mambo yalienda sawa.

Tulipopata fursa ya kusalimiana nilimkumbusha hasa siku aliponipa adhabu ya kukata bonge la mti then nikate viapande vya kuni nikaakataa so talifurahi sana.
 
Karigita dah huyu ticha wa loyola ni mnoko sana alinifanyia unoko sana
 
Ma maan the emperor Chief@ Ilboru...mmoja wa wanaume waliokuwa wakinipa uoga..
I feared my grandpa..but that dude..he terrified me..alinipiga makofi mjini tena mbele ya umati.
I wont forget that day..!!!
I heard he passed away..RIP Mr Losujak!!
 
Yaani nimesikitika sana uzi unakaribia kufungwa bila Mwalimu Ntauka wa Ndanda Secondari ya Masasi kutajwa kama mwalimu mnoko kuliko wote kwa kanda ya Lindi na Mtwara, na ambaye pia anastahili kuchukua nafasi za juu sana katika ngazi ya kitaifa kwa unoko, ukuda, na tabia zinazofanana na hizo. Huyu Mwalimu alikuwa Discipline Master na baadaye second master lkn ni kama shule yote ilikuwa mikononi mwake

Yaani ulikuwa ukikamatwa na Ntauka kwa kosa lolote hata la kupiga kelele darasani basi utakuwa maarufu shule nzima kuanzia siku hiyo. Atakuburuza hadi kwenye paredi, na kulisoma jina lako na kukuponda (kukudhalilisha) kwa mbwembe zilizopindukia kisha bakora. Watu mliosoma Ndanda mwishoni mwa miaka ya tisini hadi miaka ya katikati ya elfu mbili mpo mtoe ushuhuda zaidi?
 
Mwl Tugawane. Alikuwa anapenda ligi sana. Yaani akikutwa unaadhibiwa na ticha mwingine naye anaomba collabo.
 
Mwalimu Mchwampaka alikuwa ana makengeza, alikuwa balaa akikukamata haujachomekea hata ukiwa Kariakoo. Kuna siku alinikamata natoroka kupitia geti dogo la Jangwani nilikula mbata, sitasahau hiyo siku.Mungu ailaze roho ya marehemu Mchwampaka mahali pema peponi.Amina
 
old moshi ticha anaitwa kinunda asee kwanza akiingia tu class unahisi kampuni ya fegi imeungua. Ila yuko deep sana kwenye math.

Kinunda kanifundisha pia Adv Math pale majengo second.. Mitiani yake ilikua haisogei halafu akiwa anapiga pindi anawapa swali moja ambalo haliendi halafu anaenda nje kwanza kupiga fegi
 
Huyu Mwalimu si ndo yule tulimpachika jina la Mwalimu "Sapa" make alikwua hawezi kutamka "Saba" badala yake anatamka "Sapa" Mwisho wa siku likashika hilo jina Mwalimu Sapa!!!!!!!!! :evil: :evil:

Hahahahahaha! Ndio yeye...
 
Hahahaha! Yaani hata sipati picha jinsi huyo mwalimu alivyokuwa akiwabutua hayo amateke!

Umenikumbusha Mwalimu Pius wa shukleni kwetu Mara Sekondari enzi zile za 1990's. Mwanafunzi ukifanya kosa, alikuwa hana haja ya kukukimbiza--yeye alikuwa akiokota fungu la mawe na kuanza kukutungua nayo--jitihada zako za kuyakwepa ndio 'msalie mtume' wako--ukikosea kukwepa, ngeo zinakuhusu! Yaani full movie nikikumbuka enzi zile. hahahahaha!

huyo ticha noma alikuwa anapenda biashara katu charge mia mbili badae katu geuka yani hyo miteke aliyo tu pga ni hatari
 
Ruaha University college Iringa, kuna mwalimu mmoja hivi mlemavu wa miguu anaitwa Kitinya, jamaa ni zaidi ya mkuda aisee..
 
Katika shule/chuo hakosekani mwalimu msumbufu na ambaye huwafuatilia sana wanafunzi hata ktk mambo madogo madogo na kuwapa adhabu za ajabu ajabu.

Leo nataka tuwakumbuke walimu hawa pamoja na kujikumbusha vituko walivyowahi kuvifanya.

Mimi shuleni kwetu Mara Sekondari kulikuwa na mwalimu mmoja aliyeitwa Jigge. Basi siku moja kuna wanafunzi walitoroka kwenda mjini bila ruhusa. Na kibaya zaidi, walipokuwa huko mjini wakafanya fujo na kuharibu mali za wananchi. Taarifa zao zikafika shuleni. Ilikuwa jioni na kiza kilikuwa kimeanza kukolea. Mwalimu Jigge akapiga kengere. Wanafunzi wote tuliokuwepo shuleni tukakusanyika bwaloni na akaanza kuchuka roll call.

Ili kumkomesha mwalimu huyu, pamoja na kuwanusuru wale wanafunzi 'wahalifu' waliokuwa wamefanya tukio mjini, wanafunzi wakapanga kuzima umeme main switch na kumpopoa kwa mawe. Ghafla tu, umeme ulipozimika, mwalimu alichomoka kama mshale na kutokomea kizani. Wanafunzi walimtupia mawe lakini, kwa ile speed aliyochomoka, hakuna jiwe lililompata. Ana bahati sana.

Namkumbuja Credo Celestine IFM, Mtaalamu wa Quantitative Techniques
 
mwl donge mwenge high xul,mwl kitoko tarime high xul,mwl malilika korogwe primary xul kahama,mwl doto old shy

hapo mwenge huyo donge alikuwa pimbi sana hasa ikiwa zamu yake kumi na moja yupo mabwenini mkakimbie mchakamchaka na kuna f.a.l.a. mwingine alikuwa anajiita horsepower
 
Namkumbuka mkuu wa shule Kaishozi wa DODOMA SECONDARY miaka ya 92-96 sita msahau kwa wale waliosoma DOM SEC natumaini watamkumbuka alikuwa kama anapasha kwanza weed then ndiyo anaingia kazini.

Mwaka jana nienda Dodoma kuna rafiki yangu alikuwa anaenda kutoa mahari wakati tunahangaika kupata mshenga ghafla aliingia kwenye kikao na akapendekezwa kuwa mshenga ambapo alikubali alichokifanya alipiga konyagi ndogo 2 na akaenda kuchukuwa kanzu yake tayari kwa kazi ya kuwa mshenga ajabu tukiwa ukweni wakati wsjumbe wengine wanaongea yeye alikuwa anauchapa usingizi haha haaaa nilicheka sana ilipofika wakati wake akakurupuka na kuanza kuongea watu si vicheko kwani inaonekana hakujua yanayoendelea hata huvyo baadaye mambo yalienda sawa.

Tulipopata fursa ya kusalimiana nilimkumbusha hasa siku aliponipa adhabu ya kukata bonge la mti then nikate viapande vya kuni nikaakataa so talifurahi sana.

Du, miserable but interesting countdown memories!
 
Back
Top Bottom