Uchaguzi 2020 Tusemezane: Uhalisia wa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020

You wait..watakuja hapa kuanzia tarehe 29 na kuanza kulia lia tena.
 
Hakuna nayempigia debe!

Tatizo lenu nyie makamanda ni mko short-sighted sana.

Hamuwezi kuona hoja zaidi ya Magufuli.

Magufuli kwa sasa anazitawala fikra zenu.

Anaishi vichwani mwenu bure...halipi kodi ya pango wala nini.

Mtu akikosoa mfumo uliomuweka Magufuli madarakani, na ambao ndo uliwaweka Kikwete na Mkapa pia, nyie mnamwona Magufuli tu.

Na kama unadhani tatizo ni Magufuli na siyo mfumo mzima, basi subiri 2025 uone.
 
Niliona, ila sidhani kama Tanzania tutafikia huko. Hakuna lisilowezekana lakini sioni kama kuna uwezekano huo.
Mkuu mwenye kuepusha tusifike huko ni Magufuli na CCM yake, asiingilie utendaji wa Tume ya uchaguzi na asiibe kura. Ajinadi vizuri apewe kura halali basi, vinginevyo hayo mambo ya Misri au Sudan huwa yanahitaji mtu mmoja tuu kuleta hamasa na nchi ikaingia katika sintofahamu
 
Mkuu mgombe wa 2015 na huyu wa 2020 nitofauti kubwa Sana huyu wa Sasa Ni jeuri kiburi asieogopa kitisho chochote naomba tushauriane kujitokeza kupiga kura kwa wingi ili hata kuzilinda tuwe wengi ili hao walinda chama wakiona uwingi wa walinda kura kila kituo kila kitongoji kila Kijiji kila wilaya kila mkoa na hata nchi nzima hawawezi kuwa na mabomu ya machozi ya kumwagia nchi nzima Kama unakumbuka 2015 wengi tulisubiria kauli moja ya bwana Edo ili tukinukishe kukaa kwake kimya ndicho kilichofanya tuvunjike moyo ila kwa bwana huyu mwanasheria Hatakubali kuwa mjinga Kama kura zitamtosha,, naomba ujue kuwa chama tawala waliweka masikio pamba kuhusu tume ya uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi mpaka Waka kata rufaa baada ya mahakama kutengu wakutugenzi kusimamia uchaguzi yote hayo ni ili vyama vikuu vya upinzani wasusie uchaguzi wabakize vibaraka wao tu! Sasa mtego umegoma kufyatuka na wagombea wamepitishwa hofu iko kwao, mkuu nakuomba kwa mara nyingine waeleze wananchi na wanajukwaa faida ya kupiga kura na sio hasara ya kufirika,, mungu anasaidia mwenye juhudi tujiandaeni kupiga kura ki halali kabisa Ni wajibu wetu ,, ikiwa kweli tutapiga kura kwa moyo mmoja mwaka huu itakuwa mara ya kwanza magazeti kuandika habari za chama tawala kuibiwa kura, na lugha tutakayoitumia ni kuwa Mwizi analalamika kaibiwa
 
Ukweli mtupu

Teali tupo kwenye mtindo mbovu wa maisha na lazma tukubali tu hakuna linalotokea kwa bahati mbaya
 
Ndiyo mazingira tuliyomo, hatuwezi kuukataa ukweli.

Katiba haipo, tume huru pia haipo, lakini uchaguzi upo tufanyeje?!
Tujitokeze kwa wingi kuchagua viongozi tunaowataka halafu tusimame imara katika kutetea haki yetu viongozi ni wachache wananchi ni wengi mara dufu tuwe bega kwa bega kupata haki zetu kwa kusaidiana na viongozi wetu lissu amejiamini kwa sababu anaamini wananchi tupo tunaemkubali na kumuamini
 
Aisee wewe huijui Tanzania kabisa. Mie nakuambia sasa hivi Chadema iko imara sana mikoani kuliko ilivyokuwa awali pamoja na kuzuiwa kufanya siasa.
Ndio sababu ya hofu iliyonayo CCM kama chama.
 
Kila mmoja na mtizamo wake
 
Mmeanza kuweweseka sasa, tulieni dawa iwangieni vizuri dadeeeki
 
Jiandaeni kisaikolojia maana lissu ndiye ataapishwa baada ya October.

Wananchi wa Tanzania tegemeo lao ni mh Lissu.

Hutaki rudi kwenu Burundi.
Miezi miwili nyuma walikuwa na akili lakini ujuo wa Membe nyumba ile na ujio wa aliyekwenda kutibiwa ughaibuni umewatowa akili zitawaruxia baada ya october Magu atakapokuwa anaapishwa!
 
Hao Upinzani Uchwara wakijitahidi sana
Watapata 15%
Hiyo Wajione washindi
 
Mkuu hapo unapoteza nguvu zako kwa kumpigia mbuzi gitaa.

Hao unao waelimisha hawana chochote wajuacho zaidi ya kutetea, kuramba miguu na kupongeza.
 
Magufuli lazima ashinde
Hasiposhinda tutampa ushindi wa lazima halafu tunabadili katiba awe rais wa kudumu
 
Mbona husemi mlivyompiga mh Lissu pyuuuu pyuuuu?
 
Hakika mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…